KWA ENEO NA GHARAMA KIDOGO FUGA SAMAKI WENGI NA BILA KULAZIMIKA KUCHIMBA ARDHI
1.Tunaelimisha jamii kuhusu teknolojia mpya za ufugaji samaki kisasa
2.Tunawajengea wateja wetu mabwawa yakisasa ya ufugaji samaki yanayojengwa kutumia mabanzi au yale ya kuhamishika ambayo mara nyingi tunatumia chuma na turubali maalum
3.Tunawauzia wafugaji wa samaki kila wanachohitaji kufanikisha ufugaji wa samaki kisasa, ikiwemo vyakula, na mabwawa yaliyotayari na mbegu bora ya samaki kwa gharama nafuu.
4.Tunatoa huduma za ushauri wa kitaalam zaidi kwa wale wafugaji walioanza ufugaji samaki kisasa kwa kujengewa nasi kwa teknolojia tunazowajengea au kuwauzia.
5.Tunatoa ushauri wa kuhusiana na upatikanaji wa soko la samaki haswa kwa wafugaji walioanza kufuga kwa msaada wetu.
6.Malengo yetu nikufanya ufugaji samaki kuwa rahisi kadiri iwezekanavyo, utumie eneo dogo kwa uzalishaji mkubwa, hii tunafanya kwa kutumia ubunifu na kuchanganya teknolojia yetu na ya ufugaji samaki kwenye mataifa yaliyoendelea iwe rahisi kufanyika kwa mazingira yetu.
7.Tuna malengo yakuzalisha minofu ya samaki na na bidhaa nyingine zitokanazo na samaki kwa soko la ndani na la nje, hivyo mbeleni tutafanya ufugaji wa kimkataba na wafugaji wa samaki waliokwishabobea kwenye ufugaji huu wa kisasa chini ya uangalizi wetu nakuwaakikishia soko la samaki watakaozalisha.
UFUGAJI SAMAKI
Kwa miaka mingi imekuwa kawaida kwa watu wanapotajiwa ufugaji wa samaki moja kwa moja hupata picha au kuanza kufikiria mchakato wakupata makatapila au mtaji mkubwa kuchimba mabwawa.
Positive eye Co. Ltd inakuwa kampuni ya kwanza kabisa kutambulisha Tanzania ufugaji wa samaki kisasa na kibiashara katika mabwawa yasiyochimbwa ardhini ambayo yamekuwa yakitumika katika nchi nyingine mbalimbali ikiwemo Kenya kwa kitambo sasa, na hata sasa kampuni hii imeweza kubuni na inaendelea na tafiti zakibunifu za aina nyingine ya mabwawa ambayo hufaa kuamishika kwa wafugaji wanaokaa eneo lisilokuwa lakudumu au nyumba yakupangishwa kunufaika na ufugaji samaki.
Katika teknolojia hii ya ufugaji samaki kisasa, tofauti na inavyofaamika kitaalamu na ilivyosomwa na wataalam wetu wa kilimo kwa miaka mingi kuwa utaweza kufuga samaki 3-4 tu kwa eneo la mita moja mraba. Kwenye ufugaji huu teknolojia na uwezo wakuthubutu kujiongeza kijasiriamali vimebadilisha mambo, kwani utahitaji eneo la mita 4 urefu, mita 2 upana na mita 1 kina kuwezakufuga samaki 1000 aina ya kambale au wastani wa tilapia 300-400 na kulazimika kubadili maji nusu ya ujazo mara moja tu kwa wiki.
Kutengenezewa mabwawa haya utahitaji kuwa na mirunda kidogo na mabanzi ambayo yatatumika kutengeneza umbo la bwawa la samaki kwa kuinua juu bila kulazimika kuchimba chini na baada ya hapo yatawekewa karatasi maaalum yakuhifadhi maji(tazama picha hapo chini kwa uelewa zaidi). Karatasi hizi ziko za aina tofauti zikitofautiana kwa ubora na muda wakudumu, Japo wengi huanza mradi huu kulingana na uwezo wakimtaji wa mhusika lakini sisi tunashauri aina bora ya karatasi ambayo ni gharama juu kidogo kuinunua lakini inawezakudumu kwa wastani wa miaka hadi 30 endapo itatunzwa vyema
Katika ufugaji huu wa samaki kisasa samaki aina ya kambale watawezakufikia kuvunwa yaani uzito wa kati ya 1-1.5kg ndani ya kipindi cha miezi 6-8 tu, kutegemeana na sababu mbalimbali ikiwemo upatikanaji wa chakula bora ,hali joto ya wastani mzuri ambavyo huchangia ukuaji wa haraka wa samaki na maji.
TATHMINI YA UZALISHAJI, SOKO/UHITAJI WA SAMAKI DUNIANI
Imethibitika upatikanaji wa samaki kwenye vyanzo vya asili umekuwa ukiendelea kuporomoka kutokana na uvuvi haramu, uchafuzi wa maji na kemikali toka viwandani, n.k,huku uhitaji wa nyama nyeupe umekuwa ukiendelea kuongezeka kwa kasi siku hadi siku. Tathmini inaonyesha miaka ya 1970 ni wastani wa 5% tu ya samaki walioliwa duniani walitoka kufugwa, Hivi leo nusu ya kiwango cha samaki wanaoliwa duniani ni wakufugwa, na baadhi ya wanasayansi wametabiri hadi ifikapo mwaka 2048 hazina ya samaki wote wapatikanao kwenye vyanzo vya asili itakuwa imekwisha hivyo kulazimisha uhitaji wote wa samaki duniani kutoshelezwa kwa samaki wafugwao kibiashara mashambani mwetu, hivyo kuthibitisha fursa ya kuzalisha samaki kulisha dunia na idadi kubwa ya watu inayoongezeka kwa kasi kuliko uzalishaji wa chakula kinachohitajika mwanadamu kuishi vyema.
Tembelea:
All seafood will run out in 2050, say scientists
Kanuni ya uhitaji na uzalishaji (demand & supply principle)
Kanuni ya kiuchumi ya uzalishaji na uhitaji inasema “mara zote kunapokuwa na uhitaji mkubwa wa bidhaa yeyote sokoni kuliko kiwango cha uzalishaji au upatikanaji wake basi bei itakuwa juu” na vivyo hivyo uzalishaji ukiwa mkubwa kuliko uhitaji bei ya bidhaa hiyo itakuwa chini. Kwa kutumia kanuni hiyo fanya ufuatiliaji utagundua nyama ya samaki inauzwa ghali kiasi cha watu wengi wa kipato cha chini na kati kutomudu kuitumia kadiri wapendavyo. Na hiyo ni ishara yakuwa soko lake lipo ni kubwa.
KWA UJUMLA BISHARA YAKUZALISHA CHAKULA NI BISHARA AMBAYO SOKO LAKE LIPO SIKU ZOTE AU KAMA NI LAKUTAFUATA AU KULITENGENEZA NI RAHISI SANA SABABU MWANADAMU KABLA YA MAMBO MENGINE YOTE KULA NI SUALA LA LAZIMA ILI AWEZE KUISHI.
GHARAMA ZA KUANZA MRADI WA UFUGAJI SAMAKI KISASA
S/N
MAELEZO
KIASI
MARADI WA BWAWA 1
KIASI
MRADI WA MABWAWA 2
1
Ujenzi wa shamba kitalu (green house) la kufugia samaki na bwawa bora ndani yake,Malighafi zake zote zenye ubora unaoshauriwa na kampuni,gharama za ufundi na utaalamu wa teknologia hii, na ushauri wa kitaalam pamoja nakutembelewa mara moja kwa mwezi wa kwanza wa mradi kuanza.
1,193,700
2,048,700
2
Mbegu bora ya samaki aina ya kambale(Hybrid Catfish -mono sex)
1000
450,000
2,000
900,000
3
Chakula bora cha samaki
400,000
800,000
Jumla kuu gharama yakuanza mradi kisasa
2,043,700
3,748,700
S/N
MAUZO KADIRIWA/SALES FORECAST
KIASI
MARADI WA BWAWA 1
KIASI
MRADI WA MABWAWA 2
1
Mauzo kwa makisio ya bei chini Tshs 5,000/= kwa 1kg
1000
5,000,000
2000
10,000,000
Toa (-)
1
Ngarama za ulishaji hadi kuuza
(400,000)
(800,000)
2
Maji upatikanaji kama unalipia ya bomba makisio ya juu
(600,000)
(1,200,000)
3
Mbegu ya samaki
(400,000)
(800,000)
4
Dharura nyingine yeyote ile inayowezakujitokeza
(1,000,000)
(2,000,000)
FAIDA (BAADA YAKUTOA GHARAMA ZAUENDESHAJI)
2,600,000
5,200,000
ndo hawa? maelezo mazuuri kumbe ni matapeli asante ngoja nikamtie mabovu hukohuko kwenye kablog kake