Jihadhari na Mfuko wa Plastic (Rambo) Barabarani

Karibu sana, Ila tu mimi si Kaka ni Dada, nimekusamehe bila malipo

Nashukuru kwa taarifa mkuu lakini kwenye post yako umesema kati ya waliopatwa na hili tatizo ni mke wako na hapa unasema wewe nidada umenichanganya
 

asante mkuu,sasa ni vizuri na wewe ungetoa msaada jinsi ya kujilinda.
 
Tunashukuru kwa taarifa mkuu lakini hii mifuko ya Rambo inakazi nyingi mno! kuna maeneo fulani ya uswazi (Uswahilini) huwa wao wanaiita ni selfconteiner yaani wanaitumia kwaajili yakuendea haja, alfajiri na mapema we damka uone watu wanavyopishana na mifuko ya Malboro kwenda kutupa vinyesi.
 
asante mkuu hata huku kwetu nimeona vimejaa barabarani ,sikujali kwani huwa siku zote navikwepa
 
Asante kwa taarifa muhimu. Kwa njia hii pia tunaweza kuimarisha ulinzi shirikishi kwa kupeana taarifa za kuzuia halifu.
 
Intelijensia iko wapi? Waambieni wapande plaiveti ka na vyuma vya moto, wapitie mitaa ya hizo rambo zenu wapate pancha zenu hizo. Kibaka na bange zake akijipendekeza atenguliwe nyonga, kiuno au hata ugoko. Maumivu yakizidi apelekwe kwa daktari. Tuna mambo ya kuhangaika nayo ebo! Asante anyway kwa info mkuu.
 
kwa kawaida unapokuwa barabarani unashauriwa usikanyage kitu kigeni barabarani.
 
Inaonyesha kuwa ni habari muhimu ya ki_umbea umbea asante kwa tahadhari hii ya muhimu dume jike
 

Usimwamini muongo hata kama anasema ukweli
 
Kweli mkuu, unajua niliposoma huu uzi nimeshangaa kuwa kuna 'dereva' anayetahadharishwa asikanyage hivyo vitu kama vile ni kawaida wa madereva kuvikanyaga! Lakini umenikumbusha kuwa kuna wale wa vyuo vya kata!!!
 
Haahaaahaaaa! Asante mkuu kwa kunivunja mbavu.. Tatizo ni kuwa ili hiyo operation iwepo lazima wakubwa wao wakae kama kwa siku mbili 'kupanga' hiyo 'mikakati', walipane posho ya kukaa, ndo waidhinishe hiyo kitu...
 
Asante kwa taarifa muhimu sana@ Amavubi... Ila watu wameconcentrate kwenye jambo ambalo,uhalisia wake unaujua wewe mwenyewe... Kama Amavubi ni F au ni M...na ama Mrembo ni F au M...na ama hao wawili ni mtu mmoja mwenye ID mbili tofauti,na tena jinsia ni siri yake..
 
Pamoja mkuu....imeandikwa.....waacheni watoto wadogo waje kwangu.......................
 
Haahaaahaaaa! Asante mkuu kwa kunivunja mbavu.. Tatizo ni kuwa ili hiyo operation iwepo lazima wakubwa wao wakae kama kwa siku mbili 'kupanga' hiyo 'mikakati', walipane posho ya kukaa, ndo waidhinishe hiyo kitu...

Umeona tabu hiyo mkuu?
 

He he daktari kagoma mkuu,maumivu yakizidi aende kwa mganga wa kienyeji
 

Karibu sana, Ila tu mimi si Kaka ni Dada, nimekusamehe bila malipo


Mkuu umesema waliopata pancha ni pamoja na mke wako, halafu unasema wewe si kaka ni dada, pamekaaje hapo?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…