Jihadhari na matapeli

majebsmafuru

JF-Expert Member
May 1, 2017
453
628
Kuna matapeli wameingia na kuwatapeli wakina mama ntilie, saloon, restaurant, kushona n.k. n.k.
Aidha watajifanya kuna tender ya kusuka watoto, kulisha watoto, kulisha shule, kulisha mkutano, kushona nguo za shule, kusambaza kuku wa nyama. n.k. n.k.
Wanakuja na zao kwamba wanataka kukupa tenda, wataomba uwatumie hela ya fomu, baadaye wataomba hela ya kuwahonga ili upate hiyo tenda na mwisho watataka tena hela kwa kusema haijatosha kuhonga upate tenda....
WATAKUJA NA LAFUDHI YA KICHAGA, TUJIHADHARI HASA WAKINA MAMA WAHANGAIKAJI, KUNA WATU HAWANA HURUMA MNAVYOUMIA KUTAFUTA, MASHETANI HAWA HAWANA HATA AIBU KUWAIBIA MAMA NA DADA ZETU...
MMEJULISHWA WAKUU....
 
Masikini kuna mama mmoja alitapeliwa hivo ni mama lishe, ana kimgahawa kidogo mtaji wa chapati kilo 1, akaja jamaa eti kumpa tenda ya kulisha mafundi site, maza kakopa huko kapika michapati ya kufa mtu kumbe hakuna hata cha tenda.... Alilia siku hiyo kama mtoto.
 
Masikini kuna mama mmoja alitapeliwa hivo niama lishe, ana kimgahawa kidogo mtaji wa chapati kilo 1, akaja jamaa eti kumpa tenda ya kulisha mafundi site, maza kakopa huko kapika michapati ya kufa mtu kumbe hakuna hata cha tenda.... Alilia siku hiyo kama mtoto.
Na hukumsaidia? BTW Ngano 1 Kg inatoa chapati ngapi?
 
Wajinga ni malisho ya Wajanja, wacha samaki wanaemudu kula wengine wafanye hivyo maana ni juhudi yao.
 
Back
Top Bottom