Hapana mkuu nilikua nina laki 8 tu akanikopa laki 6 .mwingine akaja nikamkopesha laki 2 hivyo akiba yangu ikaisha na ndoto za kudunduliza 1M zikapotea.Dah, Ni ndugu umemsaidia.... Potezea bwana.... Sio ndugu wote wako hivyo.... Mi mtu akichelewa nilipa lakini anaonyesha concern namwelewa, mambo yanakuwaga tight wakati mwingine tunasaidiana. Dah ulikuwa una 8m, hiyo laki Sita Ni Fanya Ni malumbuko ukilalama hivi utakosa pesa na baraka
Ni kweli mkuu tabia ya kukopesha sio nzuri hasa unapomkopesha mtu pesa nyingi kama 5M kuendelea.Jamaa yangu alikwenda kudai pesa zake na hakupewa na aliporudi nyumbani akaugua ugwanjwa wa ajabu na akafa watu wakaseama amelogwa. Kuna mwandishi mmoja alikuwa anatafuta habari na akaenda kwa mganga kujifanya ana shida na akakutana na watu wamekuja kwa mganga kwa ajili ya kuloga watu waliowakopesha pesa zao. Nimeshawakopesha wengi na cha kusikitisha ni mmoja alikuwa akijiita mchungaji na ameishia na pesa zangu. Inakuwa vigumu saa nyingine kumnyima maana anakuwa ni rafiki yako lakini akishapata anaishia. Kwa ujumla ukikopesha jiambie mwenyewe umemsaidia.
Hahahah... et nilie kwanza!Mkuu ngoja nilie kwanza nitarudi.....
Wengine waaminifu... Mpe tu!!Basi nimeahirisha kuna jamaa hapa alikuwa anahitaji 300k simkopeshi tenaaah!!
Daah mkuu me sijui ntamuaminije maana jamaa alianza job mwezi uliopita ninapofanya, sasa sijazoeana naye kivile na sijui huko alikotoka yupoje, halafu kwenye job huwa jamaa ana tabia ya kuchomoka chomoka na siku nyingine haji tena hata taarifa hatoi! Sasa aliambia juzi hadi leo ananikomalia kama yake, kafuata wengine wakamtolea nje...Wengine waaminifu... Mpe tu!!
Hapana mkuu nilikua nina laki 8 tu akanikopa laki 6 .mwingine akaja nikamkopesha laki 2 hivyo akiba yangu ikaisha na ndoto za kudunduliza 1M zikapotea.