Jihadhari kukopesha ndugu fedha

Jihadhari kukopesha ndugu fedha

Mkopo ni kiumbe mbaya sana nakumbuka kuna mama mmoja miaka michache iliyopita alikopa pesa kwenye taasisi moja ya fedha akawa hajalipa kwa mda unaotakiwa, wale jamaa wa benki walimtafuta nyumbani kwake hawampati mwisho wa siku wakaelezwa na majirani zake kwamba yule mama anashinda na kulala kanisani kwa kakobe Mwenge, basi bwana si wakaja kanisani kumtafuta walipofika getini wakajieleza vizuri yule mama kweli alikuwepo akaitwa na wahudumu getini ile kufika na kuwaona wadeni wake hiiiiiiiiiiiiiiiii hakujali kama yeye ni mama mlokole aisee acha weee kilichotokea ni kwamba mama yule alikurupuka na kuruka ukuta kurukia upande wa pili asikamatwe na wadeni wake nakwambia watu hawakuamini kilichotokea mbele ya macho yao, mama yule akapotea bila kuwekwa mikononi mwa wadeni wake, kwa hiyo ndugu yangu deni ni mzigo mzito sana unaondoa utu na hata thamani yako.
haijalishi wewe ni mlokole, tajiri, mchungaji, sheikhe au nani kama huwezi kurudisha mkopo acha kukopa vinginevyo fedheha na aibu itakupata ndugu!
 
Sikuizi kukopesha imezidi kua mbaya, kuna kipindi hua nacheka nikiona wadada wanadaiana hela za vikoba sijui mara imekuja mkokoteni unabeba vitu,mara imetoka Tv mara wamekodi watu,sasa wewe kudai hujui mkuu kukopesha unajua,
manake watu wa uswahilini mahodari wakudai,kwanza hiyo aibu yake atakavyo kuadhiri lazima hela yake urejeshe..
 
Mim elf 20 tu nilimkopa dogo mmoja analia alipe bili ya maji na umeme yan tang mwk jana mpk leo nkimdai anasema hela ndog iyo ndg yang unaidai km nin kuna mda naishiwa kat sent sin ndan nkimdai hapokei cm wana la sms hajibu apo aliomba 50 nkampa 20 ngempa 50 ngeumia zaida hela ya kutafuta mwenyew inauma sana hata km buku ni yako na jasho lako
 
kweli kabisa
kukopesha ni kujichimbia kaburi, tena mtaishia kugombana bure
bora umpe mtu ela ambayo hata asiporudisha,haitakukwamisha kitu
 
Jirani yetu nilimkopesha laki 400,000/= akawa ananizungusha ikapita miezi kama minne nikajiuliza pesa ya mwanaume hailiki bila jasho nikamvutia muda miezi mitatu tena kimya siku moja nikasubiri mwisho wa mwezi nikaenda nyumbani kwake nimevaa koti refu na sime kiunoni akanikaribisha ndani tukaongea akaanza kunizungusha mimi nikamwambia jamaa yangu pesa ya mwanaume mwenzio huwezi kuila bila kuitolea jasho sasa basi leo tunamalizana nikachomoa sime langu akahamaki akasema jirani tusifikie hatua ya kutoleana silaha pesa yako nakupa akazama ndani akanipa pesa yangu nikatoka hapo nikaenda polisi kuchukua RB kuwa kuna mtu ananitishia maisha maana nilijua nimeshalianzisha mpaka leo hii nikimkopa hela huwa anarudisha bila shuruti
 
Nimepoteza Mil 2 na lake Moja na kumi Alipewa ancle ili nikasome chuo kikuu huria badae Jina langu litatokea nikapata mkopo wa serikali ilikuwa 2009 wakati naondoka kwenda chuo nikamwambia naomba hela. Akaniambia atanilipa amekombolea gari bandarini hadi leo sijapata pesa na nimesamehe tu Sina namna
 
sasa wote mkikataa kukopesha sisi tutakopa wapi....hata wew unaekataa kukopesha kuna siku utataka kukopa...cha msingi ni kuweka mazingira rafiki ya kuipata pesa yako andikishiana na mtu ikizidi milioni awe na kitu ukishike kadi ya gar, pikipik or kiwanja ukifanya hivyo hela yako itaipata tu
 
Jamaa yangu alikwenda kudai pesa zake na hakupewa na aliporudi nyumbani akaugua ugwanjwa wa ajabu na akafa watu wakaseama amelogwa. Kuna mwandishi mmoja alikuwa anatafuta habari na akaenda kwa mganga kujifanya ana shida na akakutana na watu wamekuja kwa mganga kwa ajili ya kuloga watu waliowakopesha pesa zao. Nimeshawakopesha wengi na cha kusikitisha ni mmoja alikuwa akijiita mchungaji na ameishia na pesa zangu. Inakuwa vigumu saa nyingine kumnyima maana anakuwa ni rafiki yako lakini akishapata anaishia. Kwa ujumla ukikopesha jiambie mwenyewe umemsaidia.
 
jombaaa iyo kitu nouma xana deni linakera watu wakishasolve shida zao bac asivi akija mtu anataka mkopo mwambie aende bank uko
 
Habarini wanajukwaa natumaini mpo salama,

Najua wengi watajiuliza kwanini nasema ujihadhari kukopesha ndugu fedha! Wengine watahisi kuwa mimi nina roho mbaya na kuanza kunipa majina lukuki mara nitakua mangi, msambaa mpare na kadhalika.

Mpaka naandika huu uzi nimepitia mengi sana. Kwanza kabisa kuna siku rafiki yangu alikuja getto kwangu jioni na kunieleza kuwa amepata kazi katika ofisi mpya hivyo basi anaomba nimkopeshe Tsh 600,000. Ili aweze kuhama nyumbani kwa wazazi wake alipokua anaishi na kuweza kupangisha chumba maeneo jirani na sehemu ya kazi alikopata.Aliahidi mwisho wa mwezi angenirejeshea fedha zangu sikua na hiyana kwani zilikua zimebakia siku chache tu mwisho wa mwezi kufika.

Nilikua nina akiba ya Tsh 8,000,000. Nikampatia laki 6 akaanza maandalizi ya kuhama nyumbani. Mwezi ukaisha nikamuuliza vipi deni langu jamaa ananiambia nisubiri tarehe 15 ya mwezi mwingine atanipa, tarehe 15 nayo ikapita nikamuuliza tena ndugu vipi nahitaji 600,000 yangu nimekwama.
Jamaa akazidi kunipiga tarehe Mara nivumilie mwezi ujao nitakupa angalau nusu, nikaendelea kua mvumilivu Mara mwezi wa 3 ukaisha hela yangu sipewi nazidi kupewa story mpya kila kukichaa.

Ikafikia kipindi nikimpigia simu hapokei wala message hajibu, Mara aniambie nitakutumia siku fulani then siku hiyo ikifika anazima simu hata siku 2 mfululizo.


Ikawa mchezo ndio huo nikimfuata kwake basi ni story tu za matatizo ananisimulia yanii mpaka nikashindwa kumuelewa kwani inafika kipindi naona kama tunashindana kuelezeana shida kwani na mimi nilikua nina shida tena nyingi na kubwa kuliko yeye.

Kiukweli alinikwamisha sana kwani malengo yangu yalikua ni kudunduliza Tsh 1,000,000. Ili niweze kuanza kufanya biashara na ilikua imekasoro Tsh laki 2 tu malengo yangu yatimie.

Tukio jingine alikuja jamaa mmoja ambaye pia ni mpangaji wa nyumba tuliokua tunaishi, yeye alikua ni mtumishi wa serikali pia anajihusisha na kilimo, Hivyo aliniomba nimkopeshe Tsh laki 3 ili akanunue mbegu na kuahidi atanirejeshea mwisho wa mwezi. Nilimjibu hiko kiasi sina ila ninaweza kumkopesha laki 2, ambayo ndio ilibaki nilipomkopesha jamaa wa kwanza laki 6.

Sikua na wasiwasi naye kwani tupo nyumba 1. Mwisho wa mwezi ukafika deni langu hakunilipa. Mbaya zaidi huyu jamaa akaanza kuwa na life style ya tofauti yaani anadamka sa 11 asubuhi kwenda kazini na akawa anarud usiku mnene kusudi tu tusionane. Kiukweli nilishindwa kuelewa kuwa tatizo ni deni langu tu?? Kufua akawa anafua usiku asubuhi mnakuta kaanika nguo kwenye kamba.

Dunia ina mengi kwani nikawa naambiwa nikisafiri tu kwenda mikoani jamaa ndio huwa anaonekana nyumbani kwani ata siku za wkend ilikua haonekani na haikua kawaida yake, siku akirud sa 7 usiku ukimgongea mlango haitiki anajidai hakusikii.

Tisa kumi hii ndio ilikua kituko ambacho sitokaa nisahau kwani nilimuekea mtego. Hiyo siku nikaamua kukaa jikoni nimsubirie mpaka atakaporudi nimkamate anilipe pesa zangu.

Maajabu ya mtume ilipofika sa 5 usiku nikaona mtu anakuja kwa kunyata nikashtuka kulikoni huyu atakua ni kibaka ama! Alipokaribia karibu kumbe ndio yule mdeni wangu, nikaendelea kujibanza alipokua anakaribia kwa mlango wake ile anaanza kufungua tu kufuli la mlango wake basi nikatokea nikamwita kwa jina..mambo vipi jamaa kugeuka na kukuta ni mimi huwezi amini alifungua kufuli kwa kasi akaingia ndani upesi alafu akajifungia kumwita haitiki utazani kazimia nilitamani nikeshe mlangoni mpaka sa 11 amke nipambane naye nikaona mbu watanifaidi tu nitulize hasira nikalale yaishe.

Huu ni mwaka wa 3 sijalimpwa hata senti na wote 2 niliowakopesha. Ulifika pahali nikahisi ni majaribu kulikoni mtaji wangu umetoweka katika mazingira ya kutatanisha hivyo.

Nilichojifunza;
1. Kamwe usimkopeshe mtu fedha ambayo una mpango wa kuitumia hata kama ni miezi 3 baadae.
Yaani hata aje mtu akuambie ATM sijui Tigo pesa imegoma nitakurudishia baadae usimwamini kabisa ata kama ni boss wako.
2. Kutoa ni moyo sio utajiri lakini kamwe usimsaidie yeyote fedha yako uliotenga kwa ajili ya dharura ama matumizi mengine.
3. Kukopesha watu sio zambi lakini usijijengee tabia ya kukopesha watu fedha wakati mwingine deni lako laweza kuwa sababu tosha ya wewe kupoteza uhai wako.
4. Ni vema mtu anaetaka kukopa ukamwelekeza kwenye vikundi au mashirika yanayotoa mkopo kwa riba kuliko kumzamini wewe.
5. Kopesha mtu kiasi ambacho hata asipokirudisha hakitaweza kuharibu mipango yako ya maisha.

Nikikumbukaga huwa nacheka sana.

Dah, Ni ndugu umemsaidia.... Potezea bwana.... Sio ndugu wote wako hivyo.... Mi mtu akichelewa nilipa lakini anaonyesha concern namwelewa, mambo yanakuwaga tight wakati mwingine tunasaidiana. Dah ulikuwa una 8m, hiyo laki Sita Ni Fanya Ni malumbuko ukilalama hivi utakosa pesa na baraka
 
Pesa ya mwanaume hailiki bila kuitolea jasho nikikukopesha zangu utazirudisha tu
 
Pesa ya mwanaume hailiki bila kuitolea jasho nikikukopesha zangu utazirudisha tu
 
Nenda kwenye taasisi za mikopo,utaratibu huu wa kukopesha kishikaji ni Africa tu
sasa wote mkikataa kukopesha sisi tutakopa wapi....hata wew unaekataa kukopesha kuna siku utataka kukopa...cha msingi ni kuweka mazingira rafiki ya kuipata pesa yako andikishiana na mtu ikizidi milioni awe na kitu ukishike kadi ya gar, pikipik or kiwanja ukifanya hivyo hela yako itaipata tu
 
Habarini wanajukwaa natumaini mpo salama,

Najua wengi watajiuliza kwanini nasema ujihadhari kukopesha ndugu fedha! Wengine watahisi kuwa mimi nina roho mbaya na kuanza kunipa majina lukuki mara nitakua mangi, msambaa mpare na kadhalika.

Mpaka naandika huu uzi nimepitia mengi sana. Kwanza kabisa kuna siku rafiki yangu alikuja getto kwangu jioni na kunieleza kuwa amepata kazi katika ofisi mpya hivyo basi anaomba nimkopeshe Tsh 600,000. Ili aweze kuhama nyumbani kwa wazazi wake alipokua anaishi na kuweza kupangisha chumba maeneo jirani na sehemu ya kazi alikopata.Aliahidi mwisho wa mwezi angenirejeshea fedha zangu sikua na hiyana kwani zilikua zimebakia siku chache tu mwisho wa mwezi kufika.

Nilikua nina akiba ya Tsh 8,000,000. Nikampatia laki 6 akaanza maandalizi ya kuhama nyumbani. Mwezi ukaisha nikamuuliza vipi deni langu jamaa ananiambia nisubiri tarehe 15 ya mwezi mwingine atanipa, tarehe 15 nayo ikapita nikamuuliza tena ndugu vipi nahitaji 600,000 yangu nimekwama.
Jamaa akazidi kunipiga tarehe Mara nivumilie mwezi ujao nitakupa angalau nusu, nikaendelea kua mvumilivu Mara mwezi wa 3 ukaisha hela yangu sipewi nazidi kupewa story mpya kila kukichaa.

Ikafikia kipindi nikimpigia simu hapokei wala message hajibu, Mara aniambie nitakutumia siku fulani then siku hiyo ikifika anazima simu hata siku 2 mfululizo.


Ikawa mchezo ndio huo nikimfuata kwake basi ni story tu za matatizo ananisimulia yanii mpaka nikashindwa kumuelewa kwani inafika kipindi naona kama tunashindana kuelezeana shida kwani na mimi nilikua nina shida tena nyingi na kubwa kuliko yeye.

Kiukweli alinikwamisha sana kwani malengo yangu yalikua ni kudunduliza Tsh 1,000,000. Ili niweze kuanza kufanya biashara na ilikua imekasoro Tsh laki 2 tu malengo yangu yatimie.

Tukio jingine alikuja jamaa mmoja ambaye pia ni mpangaji wa nyumba tuliokua tunaishi, yeye alikua ni mtumishi wa serikali pia anajihusisha na kilimo, Hivyo aliniomba nimkopeshe Tsh laki 3 ili akanunue mbegu na kuahidi atanirejeshea mwisho wa mwezi. Nilimjibu hiko kiasi sina ila ninaweza kumkopesha laki 2, ambayo ndio ilibaki nilipomkopesha jamaa wa kwanza laki 6.

Sikua na wasiwasi naye kwani tupo nyumba 1. Mwisho wa mwezi ukafika deni langu hakunilipa. Mbaya zaidi huyu jamaa akaanza kuwa na life style ya tofauti yaani anadamka sa 11 asubuhi kwenda kazini na akawa anarud usiku mnene kusudi tu tusionane. Kiukweli nilishindwa kuelewa kuwa tatizo ni deni langu tu?? Kufua akawa anafua usiku asubuhi mnakuta kaanika nguo kwenye kamba.

Dunia ina mengi kwani nikawa naambiwa nikisafiri tu kwenda mikoani jamaa ndio huwa anaonekana nyumbani kwani ata siku za wkend ilikua haonekani na haikua kawaida yake, siku akirud sa 7 usiku ukimgongea mlango haitiki anajidai hakusikii.

Tisa kumi hii ndio ilikua kituko ambacho sitokaa nisahau kwani nilimuekea mtego. Hiyo siku nikaamua kukaa jikoni nimsubirie mpaka atakaporudi nimkamate anilipe pesa zangu.

Maajabu ya mtume ilipofika sa 5 usiku nikaona mtu anakuja kwa kunyata nikashtuka kulikoni huyu atakua ni kibaka ama! Alipokaribia karibu kumbe ndio yule mdeni wangu, nikaendelea kujibanza alipokua anakaribia kwa mlango wake ile anaanza kufungua tu kufuli la mlango wake basi nikatokea nikamwita kwa jina..mambo vipi jamaa kugeuka na kukuta ni mimi huwezi amini alifungua kufuli kwa kasi akaingia ndani upesi alafu akajifungia kumwita haitiki utazani kazimia nilitamani nikeshe mlangoni mpaka sa 11 amke nipambane naye nikaona mbu watanifaidi tu nitulize hasira nikalale yaishe.

Huu ni mwaka wa 3 sijalimpwa hata senti na wote 2 niliowakopesha. Ulifika pahali nikahisi ni majaribu kulikoni mtaji wangu umetoweka katika mazingira ya kutatanisha hivyo.

Nilichojifunza;
1. Kamwe usimkopeshe mtu fedha ambayo una mpango wa kuitumia hata kama ni miezi 3 baadae.
Yaani hata aje mtu akuambie ATM sijui Tigo pesa imegoma nitakurudishia baadae usimwamini kabisa ata kama ni boss wako.
2. Kutoa ni moyo sio utajiri lakini kamwe usimsaidie yeyote fedha yako uliotenga kwa ajili ya dharura ama matumizi mengine.
3. Kukopesha watu sio zambi lakini usijijengee tabia ya kukopesha watu fedha wakati mwingine deni lako laweza kuwa sababu tosha ya wewe kupoteza uhai wako.
4. Ni vema mtu anaetaka kukopa ukamwelekeza kwenye vikundi au mashirika yanayotoa mkopo kwa riba kuliko kumzamini wewe.
5. Kopesha mtu kiasi ambacho hata asipokirudisha hakitaweza kuharibu mipango yako ya maisha.

Nikikumbukaga huwa nacheka sana.
 
Back
Top Bottom