Jihadhari kukopesha ndugu fedha

Tape measure

JF-Expert Member
Nov 26, 2015
1,972
3,511
Habarini wanajukwaa natumaini mpo salama,

Najua wengi watajiuliza kwanini nasema ujihadhari kukopesha ndugu fedha! Wengine watahisi kuwa mimi nina roho mbaya na kuanza kunipa majina lukuki mara nitakua mangi, msambaa mpare na kadhalika.

Mpaka naandika huu uzi nimepitia mengi sana. Kwanza kabisa kuna siku rafiki yangu alikuja getto kwangu jioni na kunieleza kuwa amepata kazi katika ofisi mpya hivyo basi anaomba nimkopeshe Tsh 600,000. Ili aweze kuhama nyumbani kwa wazazi wake alipokua anaishi na kuweza kupangisha chumba maeneo jirani na sehemu ya kazi alikopata.Aliahidi mwisho wa mwezi angenirejeshea fedha zangu sikua na hiyana kwani zilikua zimebakia siku chache tu mwisho wa mwezi kufika.

Nilikua nina akiba ya Tsh 8,000,000. Nikampatia laki 6 akaanza maandalizi ya kuhama nyumbani. Mwezi ukaisha nikamuuliza vipi deni langu jamaa ananiambia nisubiri tarehe 15 ya mwezi mwingine atanipa, tarehe 15 nayo ikapita nikamuuliza tena ndugu vipi nahitaji 600,000 yangu nimekwama.
Jamaa akazidi kunipiga tarehe Mara nivumilie mwezi ujao nitakupa angalau nusu, nikaendelea kua mvumilivu Mara mwezi wa 3 ukaisha hela yangu sipewi nazidi kupewa story mpya kila kukichaa.

Ikafikia kipindi nikimpigia simu hapokei wala message hajibu, Mara aniambie nitakutumia siku fulani then siku hiyo ikifika anazima simu hata siku 2 mfululizo.


Ikawa mchezo ndio huo nikimfuata kwake basi ni story tu za matatizo ananisimulia yanii mpaka nikashindwa kumuelewa kwani inafika kipindi naona kama tunashindana kuelezeana shida kwani na mimi nilikua nina shida tena nyingi na kubwa kuliko yeye.

Kiukweli alinikwamisha sana kwani malengo yangu yalikua ni kudunduliza Tsh 1,000,000. Ili niweze kuanza kufanya biashara na ilikua imekasoro Tsh laki 2 tu malengo yangu yatimie.

Tukio jingine alikuja jamaa mmoja ambaye pia ni mpangaji wa nyumba tuliokua tunaishi, yeye alikua ni mtumishi wa serikali pia anajihusisha na kilimo, Hivyo aliniomba nimkopeshe Tsh laki 3 ili akanunue mbegu na kuahidi atanirejeshea mwisho wa mwezi. Nilimjibu hiko kiasi sina ila ninaweza kumkopesha laki 2, ambayo ndio ilibaki nilipomkopesha jamaa wa kwanza laki 6.

Sikua na wasiwasi naye kwani tupo nyumba 1. Mwisho wa mwezi ukafika deni langu hakunilipa. Mbaya zaidi huyu jamaa akaanza kuwa na life style ya tofauti yaani anadamka sa 11 asubuhi kwenda kazini na akawa anarud usiku mnene kusudi tu tusionane. Kiukweli nilishindwa kuelewa kuwa tatizo ni deni langu tu?? Kufua akawa anafua usiku asubuhi mnakuta kaanika nguo kwenye kamba.

Dunia ina mengi kwani nikawa naambiwa nikisafiri tu kwenda mikoani jamaa ndio huwa anaonekana nyumbani kwani ata siku za wkend ilikua haonekani na haikua kawaida yake, siku akirud sa 7 usiku ukimgongea mlango haitiki anajidai hakusikii.

Tisa kumi hii ndio ilikua kituko ambacho sitokaa nisahau kwani nilimuekea mtego. Hiyo siku nikaamua kukaa jikoni nimsubirie mpaka atakaporudi nimkamate anilipe pesa zangu.

Maajabu ya mtume ilipofika sa 5 usiku nikaona mtu anakuja kwa kunyata nikashtuka kulikoni huyu atakua ni kibaka ama! Alipokaribia karibu kumbe ndio yule mdeni wangu, nikaendelea kujibanza alipokua anakaribia kwa mlango wake ile anaanza kufungua tu kufuli la mlango wake basi nikatokea nikamwita kwa jina..mambo vipi jamaa kugeuka na kukuta ni mimi huwezi amini alifungua kufuli kwa kasi akaingia ndani upesi alafu akajifungia kumwita haitiki utazani kazimia nilitamani nikeshe mlangoni mpaka sa 11 amke nipambane naye nikaona mbu watanifaidi tu nitulize hasira nikalale yaishe.

Huu ni mwaka wa 3 sijalimpwa hata senti na wote 2 niliowakopesha. Ulifika pahali nikahisi ni majaribu kulikoni mtaji wangu umetoweka katika mazingira ya kutatanisha hivyo.

Nilichojifunza;
1. Kamwe usimkopeshe mtu fedha ambayo una mpango wa kuitumia hata kama ni miezi 3 baadae.
Yaani hata aje mtu akuambie ATM sijui Tigo pesa imegoma nitakurudishia baadae usimwamini kabisa ata kama ni boss wako.
2. Kutoa ni moyo sio utajiri lakini kamwe usimsaidie yeyote fedha yako uliotenga kwa ajili ya dharura ama matumizi mengine.
3. Kukopesha watu sio zambi lakini usijijengee tabia ya kukopesha watu fedha wakati mwingine deni lako laweza kuwa sababu tosha ya wewe kupoteza uhai wako.
4. Ni vema mtu anaetaka kukopa ukamwelekeza kwenye vikundi au mashirika yanayotoa mkopo kwa riba kuliko kumzamini wewe.
5. Kopesha mtu kiasi ambacho hata asipokirudisha hakitaweza kuharibu mipango yako ya maisha.

Nikikumbukaga huwa nacheka sana.
 
umeongea point kubwa sana japo kwenye tarakimu umeshindwa tofautisha milion na laki...


mimi mwenyewe nina uchungu sana.

kuna hawa wanajifanyaga wachukua tenda za serikali.. nina ndugu yangu mmoja aliniazima laki tisa mwaka jana mwezi wa tatu na akahaidi kunilipa wiki moja tu inayofata maana ana malipo anafatilia alifanya tenda halmashauri sijui nzega..

hapo mkewe alikuwa amejifungua na yeye hana kitu.

mimi nikamwazima laki tisa hiyo tena nilimkopea saccoss ofisini...

mpaka leo umepita mwaka mzima hajanilipa..

ameongea uongo mpaka ukamwisha na ikabidi aanze kunikwepa na kutopokea simu..

laki tisa tu imemtoa ubinadamu...

amenidanganya hajalipwa hiyo tenda hadi akaamua kunidhulumu kabisa
 
Kumkopesha mtu pesa ni sawa na kufanya biashara ya matunda.....
 
Unachoongea ni sahihi...kuna rafiki yangu tulikuwa Na kawaida ya kuazimana hela kimzunguko wa biashara, Mara ya mwisho aliniazima milioni nne bahati mbaya mambo yake yakaenda kombo mpaka leo mwaka wa Tatu hajanilipa Na mbaya zaidi hatukuandikishana popote hata njia za kumdai nashindwa.

Tena kuna mdogo wangu kabisa alikuwa Na kawaida ya kuchukua mzigo ofisini kwangu anaenda kuuza analeta hela, lakini Mara ya mwisho zaidi ya miezi nane iliyopita alichukua kama mzigo wa laki Tisa mpaka sasa sijui atanipa lini hiyo hela .


Ndugu ndio wanafanya familia nyingi za Kiafrika ziwe maskini sababu ya kujuana Na utegemezi wa kuumizana.
 
Usini kumbushie MACHUNGU...
Iliku mwaka jana.. kuna jurani yangu alikuja kunikopa kwa gia ya ATM hakuna network na alikua na shida ya laki4 ya fasta nimsaidie thn kesho yake asubuhi angenipatia.... Huwezi amini ile pesa yangu ndio imenifanya tuwe maadui.... ni bora umsaidie mtu kuliko ahadi ya kukopeshana... hizo ni presha
 
Usini kumbushie MACHUNGU...
Iliku mwaka jana.. kuna jurani yangu alikuja kunikopa kwa gia ya ATM hakuna network na alikua na shida ya laki4 ya fasta nimsaidie thn kesho yake asubuhi angenipatia.... Huwezi amini ile pesa yangu ndio imenifanya tuwe maadui.... ni bora umsaidie mtu kuliko ahadi ya kukopeshana... hizo ni presha

Ungemjibu kuwa naww hela ipo benki hapo ulipo una buku tano tu ya matumizi ya kununua mboga.hela ina haribu urafiki na undugu pia huwa haijengi urafiki bali ni kuvunja
 
Habarini wanajukwaa natumaini mpo salama

Najua wengi watajiuliza kwa nini nasema ujihadhari kukopesha ndugu fedha!! Wengine watahisi kuwa mim nina roho mbaya na kuanza kunipa majina lukuki mara nitakua mangi, msambaa mpare na kadhalika.

Mpaka naandika huu uzi nimepitia mengi sana. Kwanza kabisa kuna siku rafiki yangu alikuja getto kwangu jioni na kunieleza kuwa amepata kazi katika ofisi mpya hivyo basi anaomba nimkopeshe Tsh 600,000. Ili aweze kuhama nyumbani kwa wazazi wake alipokua anaishi na kuweza kupangisha chumba maeneo jirani na sehemu ya kazi alikopata.
Aliahidi mwisho wa mwezi angenirejeshea fedha zangu sikua na hiyana kwani zilikua zimebakia siku chache tu mwisho wa mwezi kufika.

Nilikua Nina akiba ya Tsh 8,000,000. Nikampatia laki 6 akaanza maandalizi ya kuhama nyumbani. Mwezi ukaisha nikamuuliza vipi deni langu jamaa ananiambia nisubiri tarehe 15 ya mwez mwingine atanipa , tarehe 15 nayo ikapita nikamuuliza tena ndugu vipi nahitaji 600,000 yangu nimekwama.
Jamaa akazidi kunipiga tarehe Mara nivumilie mwezi ujao nitakupa angalau nusu, nikaendelea kua mvumilivu Mara mwezi wa 3 ukaisha hela yangu sipewi nazidi kupewa story Mpya kila kukichaa.

Ikafikia kipindi nikimpigia simu hapokei wala message hajibu, Mara aniambie nitakutumia siku fulani then siku hiyo ikifika anazima simu hata siku 2 mfululizo.


Ikawa mchezo ndio huo nikimfuata kwake basi ni story tu za matatizo ananisimulia yanii mpaka nikashindwa kumuelewa kwani inafika kipindi naona kama tunashindana kuelezeana shida kwani na mimi nilikua nina shida tena nyingi na kubwa kuliko yeye.

Kiukweli alinikwamisha sana kwani malengo yangu yalikua ni kudunduliza Tsh 1,000,000. Ili niweze kuanza kufanya biashara na ilikua imekasoro Tsh laki 2 tu malengo yangu yatimie.

Tukio jingine alikuja jamaa mmoja ambaye pia ni mpangaji wa nyumba tuliokua tunaishi, yeye alikua ni mtumishi wa serikali pia anajihusisha na kilimo, Hivyo aliniomba nimkopeshe Tsh laki 3 ili akanunue mbegu na kuahidi atanirejeshea mwisho wa mwezi. Nilimjibu hiko kiasi sina ila ninaweza kumkopesha laki 2, ambayo ndio ilibaki nilipomkopesha jamaa wa kwanza laki 6.

Sikua na wasiwasi naye kwani tupo nyumba 1. Mwisho wa mwezi ukafika deni langu hakunilipa. Mbaya zaidi huyu jamaa akaanza kuwa na life style ya tofauti yaani anadamka sa 11 asubuhi kwenda kazini na akawa anarud usiku mnene kusudi tu tusionane. Kiukweli nilishindwa kuelewa kuwa tatizo ni deni langu tu?? Kufua akawa anafua usiku asubuhi mnakuta kaanika nguo kwenye kamba.

Dunia ina mengi kwani nikawa naambiwa nikisafiri tu kwenda mikoani jamaa ndio huwa anaonekana nyumbani kwani ata siku za wkend ilikua haonekani na haikua kawaida yake, siku akirud sa 7 usiku ukimgongea mlango haitiki anajidai hakusikii.

Tisa kumi hii ndio ilikua kituko ambacho sitokaa nisahau kwani nilimuekea mtego. Hiyo siku nikaamua kukaa jikoni nimsubirie mpaka atakaporudi nimkamate anilipe pesa zangu.

Maajabu ya mtume ilipofika sa 5 usiku nikaona mtu anakuja kwa kunyata nikashtuka kulikoni huyu atakua ni kibaka ama! Alipokaribia karibu kumbe ndio yule mdeni wangu, nikaendelea kujibanza alipokua anakaribia kwa mlango wake ile anaanza kufungua tu kufuli la mlango wake basi nikatokea nikamwita kwa jina ....Mambo vipi jamaa kugeuka na kukuta ni mimi huwezi amini alifungua kufuli kwa kasi akaingia ndani upesi alafu akajifungia kumwita haitiki utazani kazimia nilitamani nikeshe mlangoni mpaka sa 11 amke nipambane naye nikaona mbuu watanifaidi tu nitulize hasira nikalale yaishee.

Huu ni mwaka wa 3 sijalimpwa hata senti na wote 2 niliowakopesha. Ulifika pahali nikahisi ni majaribu kulikoni mtaji Wang umetoweka katika mazingira ya kutatanisha ivooo.

Nilichojifunza
1. Kamwe usimkopeshe mtu fedha ambayo una mpango wa kuitumia hata kama ni miezi 3 baadae.
Yaani hata aje MTU akuambie ATM sijui Tigo pesa imegoma nitakurudishia baadae usimwamini kabisa ata kama ni boss wako.
2. Kutoa ni moyo sio utajiri lakini kamwe usimsaidie yeyote fedha yako uliotenga kwa ajili ya dharura ama matumizi mengine.
3. Kukopesha watu sio zambi lakini usijijengee tabia ya kukopesha watu fedha wakati mwingine deni lako laweza kua sababu tosha ya wewe kupoteza uhai wako.
4. Ni vema mtu anaetaka kukopa ukamwelekeza kwenye vikundi au mashirika yanayotoa mkopo kwa riba kuliko kumzamini wewe.
5. Kopesha MTU kiasi ambacho hata asipokirudisha hakitaweza kuharibu mipango yako ya maisha.

Nikikumbukaga Huwa nacheka Sanaaa.
umenitonesha milioni tano yangu nilomkopesha mtu hadileo ingekua fixed account ningeshapata faida nusu,,ni laana yaani sinaga hamu,,,mtu akija na shida ooh niazime elfu kumi Nampa tano namwambie ndo niliyonayo akirudisha poa akisepa poa,,
 
Yani cku hizi ukimkopesha mtu hela lazma ulie na ujutie mana kurudisha ni ngumu
Mtu akiwa na shida anakua na uso unatia huruma ukianza kudai chako anaanza maneno
Mi cku hz mtu akija kunikopa naanza kueleza shda zangu na mm ili tuwe ngoma droo.
 
Back
Top Bottom