Jifunzeni kutoka kwangu

Jifunzeni kutoka kwangu

koba lee

JF-Expert Member
Joined
Sep 29, 2016
Posts
982
Reaction score
1,610
Mimi sio mwandishi mzuri tuvumiliane lakini natumaini tutaelewana tu wakuu, ngoja niwape story kidogo ya yaliyonikuta na yanayoendelea kunikuta katika maisha .

Huyu mwanamke mwaka jana kategeshea nimepata mshahara na ilitakiwa tulipe kodi ya nyumba kasepa na hela yote pamoja na kila kitu ndani na vijisenti nilivyokua navyo.

Ilikua hivi nyumba kwa mwezi tunalipa laki na 70 nikamkabidhi ya miezi mitatu, tulikua tumepanga mwezi huohuo asafiri aende mkoa ampeleke mtoto kwa bibi yake,kwahiyo nikamkabidhi na nauli pamoja pesa nyingne ya kutumia kama laki na 20. Wakati natoka kazini nikampgigia simu nikamwambia muandae mtoto tukakae sehemu kidogo tupunguze stress za mwezi mzima,kweli tukakutana lakini kumbe mwenzangu ana yake. Tumekula pale monde kidogo tukaenda zetu kulala mwenzangu kumbe usiku kaamka kachukua pesa yote mfukoni na kwenye simu( namba ya siri anaijua) na pia mm hela hua naivuta toka benk kuja kwenye simu, hakuacha kitu na simu pia kachukua. Mimi hapo niko nakoroma,asubuhi naamka simu siioni,pesa sizioni,kumuuliza yeye anaruka futi mia,nikajiuliza inamaana mimi jana nililewa kisi hiki, nikasema anyways ngoja niende nikarenew line maana najua kwenye line kuna pesa. Kurenew line na kuangalia salio hela hakuna,nikarudi ndani nikaomba statement ya siku nzima,kuangalia mida ya kama saa 7 au 8 usiku hela imetoka kwenye simu yangu imeenda kwake. Nikampigia simu hapokei,mara akapokea nikasema mm sitaki maneno ila naomba hela uliyochukua uirudishe unajua kuna watu wananidai,akasema hela gani? Akakata simu,nikasema huyu hanijui,nikachukua boda kurudi home,kufika maeneo ya home nakuta geti liko wazi,kufika ninapoishi mlango uko wazi,kuingia ndani nimekuta holi.Kasepa na kila kitu kaacha zulia tu, daah sababu ya wenge nikatoka nje kuanza kuuliza watu,majirani wananishanga. Baada ya akili kunikaa sawa nikasema hata nikimpata nitamfanya nini muache aende,nikatulia full stress hata kibaruani sikwenda siku hiyo. Muda wa kodi umebakiza siku kadhaa uishe na hela kakimbia nayo.Nikampigia mzee mwenye nyumba nikamuelezea hali nikamuomba anisogezee muda kama wiki moja ntakua nshamuachia nyumba yake,maana siwezi kuendelea kuishi pale kwa kodi ile na vitu sina ukizingatia ni nyumba flani kubwakubwa kdogo,mzee akanielewa. Niliishi kama digidigi,nalala chini mawazo kibao lakini sikuwahi hata kujaribu kumpigia simu yule mwanamke maana ndo alichokua nategemea. Nikanyuti kimyaa napambana na hali yangu. Kiufupi hakuna nililomkosea la maana na do maana sikutaka kumtafuta. Baada ya wiki moja mara simu inaita kuangalia ni namba yake…….

Inaendelea
 
Nilikua naanza kujiuliza kwamba kweli kuna mwanamke ulouezaa nae bila ugomvi akufanyie matukio hayo. Mwisho ndio nimeona neno "itaendelea" so nikahitimisha kwamba ni Utunzi wa fanani. Hivyo moderator ungeni hii mada na Uzi wa kimasihara
 
Mimi sio mwandishi mzuri tuvumiliane lakini natumaini tutaelewana tu wakuu, ngoja niwape story kidogo ya yaliyonikuta na yanayoendelea kunikuta katika maisha .

Huyu mwanamke mwaka jana kategeshea nimepata mshahara na ilitakiwa tulipe kodi ya nyumba kasepa na hela yote pamoja na kila kitu ndani na vijisenti nilivyokua navyo.

Ilikua hivi nyumba kwa mwezi tunalipa laki na 70 nikamkabidhi ya miezi mitatu, tulikua tumepanga mwezi huohuo asafiri aende mkoa ampeleke mtoto kwa bibi yake,kwahiyo nikamkabidhi na nauli pamoja pesa nyingne ya kutumia kama laki na 20. Wakati natoka kazini nikampgigia simu nikamwambia muandae mtoto tukakae sehemu kidogo tupunguze stress za mwezi mzima,kweli tukakutana lakini kumbe mwenzangu ana yake. Tumekula pale monde kidogo tukaenda zetu kulala mwenzangu kumbe usiku kaamka kachukua pesa yote mfukoni na kwenye simu( namba ya siri anaijua) na pia mm hela hua naivuta toka benk kuja kwenye simu, hakuacha kitu na simu pia kachukua. Mimi hapo niko nakoroma,asubuhi naamka simu siioni,pesa sizioni,kumuuliza yeye anaruka futi mia,nikajiuliza inamaana mimi jana nililewa kisi hiki, nikasema anyways ngoja niende nikarenew line maana najua kwenye line kuna pesa. Kurenew line na kuangalia salio hela hakuna,nikarudi ndani nikaomba statement ya siku nzima,kuangalia mida ya kama saa 7 au 8 usiku hela imetoka kwenye simu yangu imeenda kwake. Nikampigia simu hapokei,mara akapokea nikasema mm sitaki maneno ila naomba hela uliyochukua uirudishe unajua kuna watu wananidai,akasema hela gani? Akakata simu,nikasema huyu hanijui,nikachukua boda kurudi home,kufika maeneo ya home nakuta geti liko wazi,kufika ninapoishi mlango uko wazi,kuingia ndani nimekuta holi.Kasepa na kila kitu kaacha zulia tu, daah sababu ya wenge nikatoka nje kuanza kuuliza watu,majirani wananishanga. Baada ya akili kunikaa sawa nikasema hata nikimpata nitamfanya nini muache aende,nikatulia full stress hata kibaruani sikwenda siku hiyo. Muda wa kodi umebakiza siku kadhaa uishe na hela kakimbia nayo.Nikampigia mzee mwenye nyumba nikamuelezea hali nikamuomba anisogezee muda kama wiki moja ntakua nshamuachia nyumba yake,maana siwezi kuendelea kuishi pale kwa kodi ile na vitu sina ukizingatia ni nyumba flani kubwakubwa kdogo,mzee akanielewa. Niliishi kama digidigi,nalala chini mawazo kibao lakini sikuwahi hata kujaribu kumpigia simu yule mwanamke maana ndo alichokua nategemea. Nikanyuti kimyaa napambana na hali yangu. Kiufupi hakuna nililomkosea la maana na do maana sikutaka kumtafuta. Baada ya wiki moja mara simu inaita kuangalia ni namba yake…….

Inaendelea
Iendelea
 
Kumekucha series zmeanza siti ya mbele hapa na popcorn

Alafu cjui nani anawapa jeri KE saivi ukigombana nao kidogo wanabeba vitu vyote ndani hii sio kesi ya kwanza kuisikia nyingne nilijionea kwa macho..shida nini??
 
Inaendelea



Nikasema nisipokee nikasema hapana ngoja nipokee maana labda dogo ana tatizo ,nikapokea anaongea dogo. Mwanangu bado alikua hajajua kuongea vizuri lakini nilifurahi kuongea naye japo najua yote hiyo ilikua ni geresha mama mtu ndo alikua anataka kuongea, mara mama mtu kachukua simu. Kauli aliyoongea eti “mbona hututafuti,yaani umekaa kimya hujui mimi nina mwanao”. Dah nikajiuliza hivi nilizaa ni chizi mstaafu afu yaani yeye haoni tatizo wala haya. Nikamwambia nikutafute kwani uliaga.Kiufupi pale sikuona haja ya kuonga naye lolote,nikamwambia we endelea na maisha yako,siku ikawa imeisha hivyo.

Nikapambana nikapata kijihela flani kwa kukopa kazini nikaenda kutafuta chumba kimoja sehemu nyingine,nimehama pale sina godoro wala nini ni vindoo na vibeseni (duh aibu hii).Lakini nikasema nitaanzia hapahapa.Maisha yalikua magumu lakini nikajipiga kifuani na kusema mimi ni mwanaume ntapambana. Lakini yeye simu haziishi kunipigia mara hivi mara vile mara mtoto anakulilia anataka akuone. Nikaendelea kukaza.

Sasa kumbe kipndi kile kakimbia na kila kitu kwangu lengo lake aende kupanga,ni kweli alienda kupanga maeneo flani ya kiswazi akidhani maisha ni mepesi.Alivyoona life sio,maana hata ile buku mbili aliyokua naiona ndogo niliyokua nampa sasahivi kuipata ni mbinde,ndo akaanza kunisumbua na simu zake. Sijui nini kilinikumba nikajikuta nimekubali nionane nae lakini kwa asilimia kubwa nilitaka kumuona mwanangu. Nikakutana nae kachoka huyo hana la kuongea na mm siongei kitu naongea na dogo,mara kasema twende ukapaone nilipopanga,nikataka kugoma lakini nikasema ngoja niende lolote linaweza kutokea kwa gogo nikakosa sehemu ya kuanzia.Kufika pale asee pale ndo nikajua huyu mwanamke hazimo kichwani,kachumba kadogo full uswazi,nikamuuliza hivi wewe mwanamke una akili kweli? Nini kilichokukimbiza kule tulipokua tunaishi vyumba vikubwa tupo ndani ya geti unakuja kuishi humu kwenye stoo? Akanijibu “ Tulikua tunalipa hela nyingi sana na mimi roho ilikua inaniuma kwahiyo nikaamua kuja huku nikijua utanifata,maana kama ningekwambia usingenielewa”.Duh kwahiyo hiyo ndo sabau ya wewe kuondoka? Nilimuuliza,akanijibu ndiyo na pia mapenzi niliona kama yamepungua. Nikamwambia wewe akili huna na sina la kukwambia ila aibu uliyonitia kwa majirani,msoto ambao nimepitia na ninaoendelea kuupitia huwezi kujua ukubwa wake,wewe nendelea na maisha yako ndo life ulilochagua. Nikasema mradi nimepaona mi nasepa zangu. Nimeondoka pale mara kapiga simu anafoka eti ooh nina wanawake ndo wananitia kiburi,eti sijui kama ana mtoto wangu mara sijui nini. Nikasema wewe hueleweki niache kwanza we endelea na drama zako.

Kumbe yeye plan yake ilikua anategemea mimi ntakubali kuishi nae pale,kumbuka kalipa kodi ya miezi mine na hata mwezi ulikua bado tokea ahamie pale.Alivyoona mpango umefeli na mm sieleweki siku hiyohiyo akaita gari akapakia vitu akasepa……



Itaendelea
 
Tujifunze nini sasa hapo?. Kwanza unaoaje mtu anaweza kukukimbia?. Yaani mazingira uliyompatia?. Kama ulimuokota bar sawa,huyo hakuwa mke
Mkuu mwisho wa story ndo utajua kua kuna maamuzi niliyafanya bila kufikiria na ndo yameleta tabu tupu mpaka sasa
 
Nilikua naanza kujiuliza kwamba kweli kuna mwanamke ulouezaa nae bila ugomvi akufanyie matukio hayo. Mwisho ndio nimeona neno "itaendelea" so nikahitimisha kwamba ni Utunzi wa fanani. Hivyo moderator ungeni hii mada na Uzi wa kimasihara
Mkuu hii sio story ya kutunga,ni maisha niliyopitia kiuhalisia
 
Back
Top Bottom