Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 360,602
- 830,350
Inaweza kuwa mshangao kwa wengi kuwa sasa nataka kufundisha uchawi live.. La hasha! Hili sio lengo langu kuu. Lengo langu hapa ni;
1. Kuondoa yale mawazo potofu na mgando kuwa unapozungumzia ushirikina basi wewe hujasoma hujui na unaamini vitu ambavyo havipo.
2. Kuondoa dhana ya kuwa uchawi uko Africa na waafrika ndio waabudu uchawi wakubwa.
3.Uchawi na ushirikina ni aina ya sayansi mbinu mahesabu na viashiria vya mambo ya kawaida kabisa.
Wakati sisi tukiaminishwa na wazungu kuwa uchawi ni kitu kibaya na cha kishamba kabisa, wao wameendelea na utafiti juu ya uchawi huku kukiwa na maandiko makongamano vyuo na hata miradi mbalimbali ya uchawi na ushirikina.
Sasa hivi ukihitaji kujifunza uchawi huhitaji kwenda mbali bali kwenye simu yako tayari kuna apps nyingi tu zinazofundisha hayo mambo.
Kama u mpenzi wa kujifunza mambo mapya na udadisi wa yale yasiyojulikana na wengine, waweza ingia huko na kupata mengi, LAKINI jifunze kwa nia ya kufahamu na si kutenda.
Fahamu kila utendalo lakini usitende kila unalofahamu..


