Elisha Chuma
JF-Expert Member
- Jul 22, 2013
- 282
- 275
Hivi karibuni nilipata safari za kutembelea mikoa tofauti tofauti hapa nchini Tanzania, lakini pia nilipata fursa ya kubadilishana mawazo na watu wa kada na makundi mbalimbali, usafiri wangu wa kuniwahisha mahali mara nyingi nilitumia pikipiki ama jina maarufu boda boda, kitu kilichonifikirisha sana ilikuwa mawazo na mlengo wa taifa huko mbele miaka 15 hadi 20 ijayo, taifa tutakuwa wapi?
Biashara ya boda boda imekuwa mkombozi wa vijana wengi kwa sasa na imekuwa ni kama mtu akipunguza machaguzi kwenye maisha anatafuta boda anakuwa dreva boda na anaendelea na maisha, lakini nilichogundua boda boda ni mradi unao ua ubunifu na mipango ya maisha ya vijana wengi kwa sasa, vijana wengi wanaoendesha boda boda malengo yao yameishia kwenye bodaboda na hesabu zake. Ndoto zao nyingi zinakufa kwa sababu tu anaendesha bodaboda na inamruhusu kupata Tshs 5000 - 10,000/= ya kwake kwa sikuu basi anakuwa anabweteka na pia inakuwa rahisi sana kwake.
Asilimia kubwa ya wanaoendesha bodaboda ndoto zao hazikuwa kuendesha bodaboda lakini baada ya kupata upenyo mwepesi wa kuendesha maisha wanaua ndoto zao na kupambana na huu upenyo, nikapata swali kwa sasa nchi nzima biashara ya boda imeshamiri na inakuwa kwa kasi, kama nchi tunamipango ya kuendelea kuwa kwenye uchumi wa kati lakini kujivuta hadi uchumi wa juu hii lazima iende na nguvu kazi pamoja na kujituma, lakini hata mipango ya familia ni kuongeza kipato na kuwa kipato kilichosimama, sasa nikajiuliza kwa asili na muonekano wa biashara hii ya bodaboda baada ya miaka 15 au 20 nchi itakuwa wapi? iwapo biashara ya boda boda ikiendelea kuwa ndio kimbilio la vijana wakichelewa kupata ajira?
Sitaki kugusia sana kuhusu matendo na tabia zinazoonyeshwa na madreva boda, ambazo zinachangiwa na umri wao, mazingira na elimu duni ya matumizi ya fedha na mkumbo wa eneo ila nnachokiwazia ni tukiendelea kuua malengo na ndoto nyingi kila mwaka kwa kisingizio cha ajira kuwa ngumu ama kuchelewa tutakuwa na taifa gani miaka 20 ijayo na je, hizo ndoto zilizokufa nani atakuja kuzifanyia kazi? ama tunaawachia wageni ndio wazifanye na kisha wazawa tubaki tunawahudumia wageni kwa kazi zao?
Hili jambo limeniwazisha mambo mengi sana kwa mustakabali wa nchi na familia kwa ujumla, tunahitaji kubadilisha mawazo na fikra kuhusu biashara hii ni kweli inatusaidia kuvusha kutoka sehemu moja kwenda nyingine kwa haraka lakini tunapoteza nguvu kazi kubwa ambayo tunaihitaji kama taifa na familia, kutimiza malengo makubwa ukiwa na biashara ya bodaboda sio suala dogo lakini waajiriwa wake ndio nguvu kazi ya leo na kesho?
Bodaboda ni Dream killer ambae anaonekana mkombozi kwa sasa. Tuamke, njia bora nadhani hawa vijana waanze kupokea mafunzo ya kujitambua kabla ya kupewa hizi bodaboda ili tuanze kubadilisha vituo vya boda kutoka kuwa genge hadi kuwa VTC vijana wawe na uongozi ambao utasimamia mienendo na afya za akili zao ikiwa inamaanisha kuwa na semina na warsha za madreva boda nyingi za kuwajenga kihisia na akili ili wajitambue nafasi zao na uhusika wao kwenye jamii na familia kwa ujumla isiwe tu kwa sababu ya kukosa ajira bali iwe ni daraja la kijana na ndoto zake.
Elisha Chuma.
Biashara ya boda boda imekuwa mkombozi wa vijana wengi kwa sasa na imekuwa ni kama mtu akipunguza machaguzi kwenye maisha anatafuta boda anakuwa dreva boda na anaendelea na maisha, lakini nilichogundua boda boda ni mradi unao ua ubunifu na mipango ya maisha ya vijana wengi kwa sasa, vijana wengi wanaoendesha boda boda malengo yao yameishia kwenye bodaboda na hesabu zake. Ndoto zao nyingi zinakufa kwa sababu tu anaendesha bodaboda na inamruhusu kupata Tshs 5000 - 10,000/= ya kwake kwa sikuu basi anakuwa anabweteka na pia inakuwa rahisi sana kwake.
Asilimia kubwa ya wanaoendesha bodaboda ndoto zao hazikuwa kuendesha bodaboda lakini baada ya kupata upenyo mwepesi wa kuendesha maisha wanaua ndoto zao na kupambana na huu upenyo, nikapata swali kwa sasa nchi nzima biashara ya boda imeshamiri na inakuwa kwa kasi, kama nchi tunamipango ya kuendelea kuwa kwenye uchumi wa kati lakini kujivuta hadi uchumi wa juu hii lazima iende na nguvu kazi pamoja na kujituma, lakini hata mipango ya familia ni kuongeza kipato na kuwa kipato kilichosimama, sasa nikajiuliza kwa asili na muonekano wa biashara hii ya bodaboda baada ya miaka 15 au 20 nchi itakuwa wapi? iwapo biashara ya boda boda ikiendelea kuwa ndio kimbilio la vijana wakichelewa kupata ajira?
Sitaki kugusia sana kuhusu matendo na tabia zinazoonyeshwa na madreva boda, ambazo zinachangiwa na umri wao, mazingira na elimu duni ya matumizi ya fedha na mkumbo wa eneo ila nnachokiwazia ni tukiendelea kuua malengo na ndoto nyingi kila mwaka kwa kisingizio cha ajira kuwa ngumu ama kuchelewa tutakuwa na taifa gani miaka 20 ijayo na je, hizo ndoto zilizokufa nani atakuja kuzifanyia kazi? ama tunaawachia wageni ndio wazifanye na kisha wazawa tubaki tunawahudumia wageni kwa kazi zao?
Hili jambo limeniwazisha mambo mengi sana kwa mustakabali wa nchi na familia kwa ujumla, tunahitaji kubadilisha mawazo na fikra kuhusu biashara hii ni kweli inatusaidia kuvusha kutoka sehemu moja kwenda nyingine kwa haraka lakini tunapoteza nguvu kazi kubwa ambayo tunaihitaji kama taifa na familia, kutimiza malengo makubwa ukiwa na biashara ya bodaboda sio suala dogo lakini waajiriwa wake ndio nguvu kazi ya leo na kesho?
Bodaboda ni Dream killer ambae anaonekana mkombozi kwa sasa. Tuamke, njia bora nadhani hawa vijana waanze kupokea mafunzo ya kujitambua kabla ya kupewa hizi bodaboda ili tuanze kubadilisha vituo vya boda kutoka kuwa genge hadi kuwa VTC vijana wawe na uongozi ambao utasimamia mienendo na afya za akili zao ikiwa inamaanisha kuwa na semina na warsha za madreva boda nyingi za kuwajenga kihisia na akili ili wajitambue nafasi zao na uhusika wao kwenye jamii na familia kwa ujumla isiwe tu kwa sababu ya kukosa ajira bali iwe ni daraja la kijana na ndoto zake.
Elisha Chuma.