Jeshi nchini Gabon lapindua Serikali ya Ali Bongo

Jeshi nchini Gabon lapindua Serikali ya Ali Bongo

Jeshi nchini Gabon limetangaza kwamba limetekeleza mapinduzi ya serikali katika taifa hilo la Afrika Magharibi.

Wanajeshi wenye vifaru na magari ya kivita wanashika doria katika barabara za mji mkuu Libreville.

Amri ya kutotoka nje imetangazwa.

Tangazo kutoka kwa kundi la vijana wa umri wa makamo linatangazwa na kurudiwa katika kituo cha redio cha serikali nchini humo, ambapo wanasema kumekuwepo na wasiwasi kuhusu uwezo wa Rais Ali Bongo kuongoza nchi hiyo.

Wanakosoa pia viongozi wakuu wa jeshi nchini humo.

Bw Bongo amekuwa nje ya nchi hiyo kwa zaidi ya miezi miwili, akipokea matibabu nchini Morocco kutokana na maradhi ambayo hayajafichuliwa baada yake kuugua akiwa ziarani Saudi Arabia.

Familia ya Bongo imetawala taifa hilo kwa miaka 51 iliyopita, na imetuhumiwa kwa kujilimbikizia mali na utajiri mkubwa kutokana na rasilimali za taifa hilo.


Sent using Jamii Forums mobile app
Hawajapindua bado ila ndiyo wamekamata kituo cha radio cha taifa na baadhi ya maeneo ya nchi.
Ukweli utajulikana in 24 hours time kama wamefanikiwa kudhibiti maeneo muhimu na kuyashinda majeshi loyal kwa Bongo.

Bado mapema sana kuwapa ushindi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
1546851068665.png


Soldiers in Gabon have attempted a coup, announcing the establishment of a "restoration council" after taking over the national radio station.


There were reports of shots being fired in the capital, Libreville, on Monday.


Reading out a statement, the military officers condemned President Ali Bongo who addressed his compatriots last week from Morocco for the first time since reportedly suffering a stroke in October.
A New Year's address by Bongo "reinforced doubts about the president's ability to continue to carry out of the responsibilities of his office", said Lieutenant Kelly Ondo Obiang, leader of the self-declared Patriotic Movement of the Defence and Security Forces of Gabon.


"Once again, one time too many, the wielders of power deceptively continue to instrumentalise the person of Ali Bongo Ondimba, a patient devoid of many of his physical and mental faculties," said Obiang.
Soma zaidi
Chanzo Gabon soldiers seize national radio station in coup attempt
 
Jeshi hilo limeshikilia Kituo cha Redio ya Taifa na kutangaza kushikilia madaraka huku wakieleza kuwa lengo lao ni kurudisha demokrasia nchini humo. Luteni Kelly Ondo Obiang ndiye aliyetangaza mapinduzi hayo na kuongeza kwamba Rais Ali Bongo wa nchi hiyo ameshindwa kufanya majukumu yake ipasavyo ya kuimarisha demokrasia. Rais Bongo anapinduliwa madarakani huku akiwa nchini Morocco, akipatiwa matibabu kwa maradhi ya kiharusi kwa miezi miwili sasa. Rais huyo ambaye aliingia madarakani Oktoba, 2009, akimpokea baba yake, Omar Bongo aliyeitawala nchi hiyo kwa miaka 42. Wanajeshi na vifaru vya jeshi vimeonekana kutawala mitaa ya nji mkuu wa nchi hiyo Libreville.
 
Walevi hatuwazi maendeleo kabisa. Eti nliposikia nchi imepinduliwa na kuna amri ya kutotoka nje nikawaza wananchi sijui watakunywaje balimi na safari lager zao?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom