Jeshi la Polisi ukaguzi wenu ni ovyo stand ya mabasi Mbeya

Kahtan Ahmed

JF-Expert Member
Aug 24, 2011
755
468
Yani mmesahau kuwa abiria huwa wanaondoka na timetable, mmechelewesha abiria kituoni sababu ya ukaguzi?

Mbona mnapenda kufanya yenu tu ndio yaelekee ila hamjali mambo ya wengine, mlishindwaje kukagua gari usiku muache asubuhi na mapema gari ziondoke kwa ratiba.

Kweli ni haki kucheleweshewa safari sababu ya ukaguzi? Hamjui ratiba?
 
Kilitokea siku moja nimepanda rungwe express pale nane nane wakatuweka sana sijui wanakagua nini. Tulikaa saa nzima na nusu ndo tukaondoka. Dereva alikua kakosa sana raha
 
Cha kushangaza tumeruhusiwa kisha tumefika njiani gari imerudishwa tena stand
 
Waswahili tuna matatatizo, Yani wanapambana kuhakikisha unasafiri salama lakini unaona wanakuchelewesha.

Likienda kuwachinja mnaanza kulaumu polisi hawafanyi kazi yao ya ukaguzi, speed nk.

Kufanya ukaguzi usiku ni ngumu kwasababu magari mengi huwa yako kwenye yard za wamiliki yakifanyiwa service Kwa ajili ya kugeuza kesho yake.
 
Hii ni kwa usalama wako! Kawia ufike kijana na Operation hii ni mwezi mzima nchi nzima!
Yani mmesahau kuwa abiria huwa wanaondoka na timetable, mmechelewesha abiria kituoni sababu ya ukaguzi?

Mbona mnapenda kufanya yenu tu ndio yaelekee ila hamjali mambo ya wengine, mlishindwaje kukagua gari usiku muache asubuhi na mapema gari ziondoke kwa ratiba.

Kweli ni haki kucheleweshewa safari sababu ya ukaguzi? Hamjui ratiba?
 
Back
Top Bottom