Sildenafil Citrate
JF-Expert Member
- Jan 29, 2021
- 573
- 2,554
Jeshi la Polisi limeona video hii fupi (clip) ikimwonesha Mtoto aliyefanyiwa vitendo vya ukatili na udhalilishaji na limeanza kuifanyia kazi kuanzia ilipoanza kusambaa ili aliyefanya kitendo hicho cha kinyama kisichokubalika aweze kukamatwa na hatua zingine za kisheria ziweze kufuata.
Mtoto huyu lazima atakuwa na Mama, Babu, Bibi, Shangazi, Mjomba, Majirani na Viongozi wa Serikali za Mitaa.
Tunatoa wito kwa yeyote mwenye taarifa za nani alifanya kitendo hicho au kilifanyikia wapi asisite kutoa taarifa Polisi au kwa Kiongozi yeyote yule ili kufanikisha kukamatwa kwake.
Imetolewa na:
David A. Misime - SACP
Msemaji wa Jeshi la Polisi
Makao Makuu Ndogo ya Polisi
Dar es Salaam, Tanzania
Pia soma: Serikali imchukulie hatua kali za Kisheria huyu aliyemtesa Mtoto kwa staili hii