Jeshi la Polisi linachafuliwa na Green Guard wa CCM

Jeshi la Polisi linachafuliwa na Green Guard wa CCM

Quinine

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2010
Posts
24,145
Reaction score
56,411
Matukio ya utekaji, mauaji ya viongozi wa vyama vya upinzani hasa Chadema mengi hutekelezwa na UVCCM (Green Guard) kwa mwamvuli wa jeshi la polisi.

1746596549747.png


Hawa Green Guards 'WENGI' wao ni vijana wa vijiweni wahuni, wavuta bangi wasio na maadili yeyote hutumiwa na Chama cha Mapinduzi kuwaumiza kuwatesa kuwapoteza wanachama wa vyama vya upinzani hasa wanaomkosoa Rais na serikali yake.

Katika matukio tofauti Viongozi wa jeshi la Polisi IGP, RPC, RCO, OCD, Waziri wa Mambo ya ndani kwa kushirikiana na wakuu wa Mikoa na Wilaya hulazimika kuwavalisha UVCCM magwanda kwa shinikizo ili chama kitimize malengo yake.

Viongozi hao wapumbavu kwa kujua au kutokujua husababisha lawama kwa jeshi la polisi huku Chama cha Mapinduzi kikijiweka pembeni na kulichia jeshi la polisi mzigo wa kujitetea.

Siku CCM ikitoka madarakani hawa vijana watakuwa hawana kazi maalum ndio watakaokuwa Interahamwe na M23 ya Tanzania.
 
Acheni kuwapamba hao mgambo wa green guard. Hawana lolote hao. Policcm ndiyo inayohusika kwa kila kitu kupitia kitengo chake cha siri cha kufanya hayo matukio ya kihalifu.
 
Hao wote ni Baba mmoja mama mmoja.

Kazi ya jeshi la Polisi NI kulinda usalama wa raia na mali zake, sasa kama kuna kikundi ambacho kinahatarisha usalama wa raia na mali zake na jeshi la Polisi haiwezi kufanya kitu maana yake ni nini?

Kuna haja gani ya kuwa na jeshi la Polisi kama kuna vikundi vinanguvu kuliko jeshi la Polisi?, ndio maana tunasema wote ni Baba mmoja mama mmoja.
 

Ali Bananga: UVCCM tutalinda Chama, Wanachama na mali za CCM kwa gharama za damu zetu.​

NB. Jeshi la polisi ndilo linalolinda raia na mali zao.
 
Matukio ya utekaji, mauaji ya viongozi wa vyama vya upinzani hasa Chadema mengi hutekelezwa na UVCCM (Green Guard) kwa mwamvuli wa jeshi la polisi.

View attachment 3326621

Hawa Green Guards 'WENGI' wao ni vijana wa vijiweni wahuni, wavuta bangi wasio na maadili yeyote hutumiwa na Chama cha Mapinduzi kuwaumiza kuwatesa kuwapoteza wanachama wa vyama vya upinzani hasa wanaomkosoa Rais na serikali yake.

Katika matukio tofauti Viongozi wa jeshi la Polisi IGP, RPC, RCO, OCD, Waziri wa Mambo ya ndani kwa kushirikiana na wakuu wa Mikoa na Wilaya hulazimika kuwavalisha UVCCM magwanda kwa shinikizo ili chama kitimize malengo yake.

Viongozi hao wapumbavu kwa kujua au kutokujua husababisha lawama kwa jeshi la polisi huku Chama cha Mapinduzi kikijiweka pembeni na kulichia jeshi la polisi mzigo wa kujitetea.

Siku CCM ikitoka madarakani hawa vijana watakuwa hawana kazi maalum ndio watakaokuwa Interahamwe na M23 ya Tanzania.

Kwa taarifa yako, hao Green Guard wengi wao ni Mawakala wa Siri/Askari wa Siri kutoka Polisi na TISS ambao wamewekwa huko kwa ajili ya kutekeleza 'kazi Maalumu.'

Hao ni Mamluki waliiwekwa huko ili kukilinda chama. Kama utakumbuka, kuna Askari Polisi (WP) alikuwepo huko kwenye chama hicho alijifanya kuwa ni Mwandishi wa Habari wa Chama hicho, alifariki katika ajali ya Barabarani na mara moja Jeshi la Polisi lilijitokeza na kumzika mtu huyo kwa kufuata Taratibu zao za kipolisi.

Hao Watu wamepewa Mamlaka na madaraka yote kabisa ya kufanya Kitu chochote kile dhidi ya Mtu yoyote yule ambaye anaonekana kuwa anahatarisha Usalama wa Chama, na huwezi kuona kwamba wanashitakiwa Mahakamani kwa uhalifu wao.
 
Matukio ya utekaji, mauaji ya viongozi wa vyama vya upinzani hasa Chadema mengi hutekelezwa na UVCCM (Green Guard) kwa mwamvuli wa jeshi la polisi.

View attachment 3326621

Hawa Green Guards 'WENGI' wao ni vijana wa vijiweni wahuni, wavuta bangi wasio na maadili yeyote hutumiwa na Chama cha Mapinduzi kuwaumiza kuwatesa kuwapoteza wanachama wa vyama vya upinzani hasa wanaomkosoa Rais na serikali yake.

Katika matukio tofauti Viongozi wa jeshi la Polisi IGP, RPC, RCO, OCD, Waziri wa Mambo ya ndani kwa kushirikiana na wakuu wa Mikoa na Wilaya hulazimika kuwavalisha UVCCM magwanda kwa shinikizo ili chama kitimize malengo yake.

Viongozi hao wapumbavu kwa kujua au kutokujua husababisha lawama kwa jeshi la polisi huku Chama cha Mapinduzi kikijiweka pembeni na kulichia jeshi la polisi mzigo wa kujitetea.

Siku CCM ikitoka madarakani hawa vijana watakuwa hawana kazi maalum ndio watakaokuwa Interahamwe na M23 ya Tanzania.
Polisi wanashirikiana na hao panyaroad UVCCM kuteka na kuua wapinzani, kama siyo washirka wao wangeshawakomesha .
 
Matukio ya utekaji, mauaji ya viongozi wa vyama vya upinzani hasa Chadema mengi hutekelezwa na UVCCM (Green Guard) kwa mwamvuli wa jeshi la polisi.

View attachment 3326621

Hawa Green Guards 'WENGI' wao ni vijana wa vijiweni wahuni, wavuta bangi wasio na maadili yeyote hutumiwa na Chama cha Mapinduzi kuwaumiza kuwatesa kuwapoteza wanachama wa vyama vya upinzani hasa wanaomkosoa Rais na serikali yake.

Katika matukio tofauti Viongozi wa jeshi la Polisi IGP, RPC, RCO, OCD, Waziri wa Mambo ya ndani kwa kushirikiana na wakuu wa Mikoa na Wilaya hulazimika kuwavalisha UVCCM magwanda kwa shinikizo ili chama kitimize malengo yake.

Viongozi hao wapumbavu kwa kujua au kutokujua husababisha lawama kwa jeshi la polisi huku Chama cha Mapinduzi kikijiweka pembeni na kulichia jeshi la polisi mzigo wa kujitetea.

Siku CCM ikitoka madarakani hawa vijana watakuwa hawana kazi maalum ndio watakaokuwa Interahamwe na M23 ya Tanzania.
Hivi yule aliyekuwa mkuu wa wilaya Ubungo Said Yuko wapi? Aliyekuwa anaenda Guest house kusaka dada poa?
 
Hao wote ni Baba mmoja mama mmoja.

Kazi ya jeshi la Polisi NI kulinda usalama wa raia na mali zake, sasa kama kuna kikundi ambacho kinahatarisha usalama wa raia na mali zake na jeshi la Polisi haiwezi kufanya kitu maana yake ni nini?

Kuna haja gani ya kuwa na jeshi la Polisi kama kuna vikundi vinanguvu kuliko jeshi la Polisi?, ndio maana tunasema wote ni Baba mmoja mama mmoja.
Ni kawaida kiongozi au chama kikaa muda mrefu na kupoteza mvuto, hutengeneza vikundi vya kihalifu ili kutisha jamii iliyoichoka kwa minajilkya kulinda madaraka yake. Na mara nyingi vikundi hivi vya kihalifu hushirikiana ama kupewa kinga na vyombo rasmi vya ulinzi na usalama.
 
Watu karibu wote waliotekwa , kuumizwa au kupotezwa kabisa na Wasiojulikana walionywa na hawa UVCCM siku chache kabla ya matukio. Coincidence?
 
Back
Top Bottom