Jeshi la Kuezeka

Jeshi la Kuezeka

Kuna kajumba ka kupangisha nimekajenga sehemu. Nyumba hii ni vyumba vitatu vya kulala,sebule,jiko na vyoo viwil kama kawaida.
Sasa wakati wa kuezeka kama kawaida nilivyozoea najua ni kazi ya siku 3-5. Fundi alienijengea akaniambia ana watu wake wa kuezeka wanaezeka kwa siku moja tu yaani wanakuja asubuhi 0600 jioni 1800 wanakabidhi kazi! Nikamuuliza mara mbili mbili akaniambia wanaweza ma kazi ni kiwango.
Akaniunganisha na hawa mafundi. Wakanipa list ya material na wakasema wanaweza kulala site ili waanze saa 0600 nikawaambia site hairuhusu kulala au kutumza vifaa basibwakasema watakuja asubuhi.
Asubuhi wakafika pale saa 0600 mpaka vifaa kufika site wakaanza kazi 0800. Mimi nilifika site around 1600 hivi na nilikuta wanamalizia kuweka mabati sehemu iliobaki kama robo tu ya nyumba nzima. Na kazi ilikuwa kiwango cha juu. Kufika 1830 wamemaliza na wakasema kama vifaa vingewahi ningekuta kazi imeisha. Kwa kweli nilishazoea kuezeka ni kazi ya siku tatu na kuendelea. Nyumba ilitumia mabati 95, mbao 2*2 100pcs na 2*4 150pcs. Mafundi walikuwa 8. Wote mafundi hakuna kibarua.
View attachment 3588379
Nyumba nzuri namimi nitakuja kumiliki nyumba
 
😀😀😀 huwa tunasema 'kuna fasheni acha zinipite tu' Hapo ningeweka dirisha moja ingebidi liwe kubwa sana ukuta mpana. Madirisha mawili yanavutia zaidi.
Ishu ya dirisha kuwa kubwa n maamuzi tuu, Tia dirisha moja size ya kati hapo katikati, unatullia
 
Back
Top Bottom