Mhaya
JF-Expert Member
- Aug 20, 2023
- 1,658
- 4,866
Jeshi la Israel kupitia ukurasa wao wa mtandao wa X wameweza kukanusha taarifa juu ya shambulio la kombora lililoangukia Hospitali huko mjini Gaza na kuua zaidi ya watu 500 na kujeruhi wengine kadhaa.
Jeshi hilo limesema, shambulio hilo halikufanywa na Israel bali ni kundi la Kigaidi lenye mlengo wa kidini wa kiislamu baada ya kujaribu kurusha kombora kwenda Israel lakini kombora hilo likashindwa kupata muelekeo na kuangukia eneo la hospitali lililokuwa na mamia ya watu wakiwa wamejihifadhi kukwepa Vita huku likiua wengi na kujeruhi wengine.
Hata hivyo mpaka sasa hakuna taarifa rasmi ya kukanusha au kukubali iliyotoka upande wa HAMAS juu ya tukio hilo. Jeshi la Israel limekuja na taarifa hiyo ya kukanusha baada ya watu kuanza kutuhumu jeshi hilo la IDF (Israel Defensive Force) kufanya shambulio hilo. Mpaka sasa watu wanasubiri taarifa rasmi kutoka HAMAS juu ya kuhusika na shambulio hilo.
Jeshi hilo limesema, shambulio hilo halikufanywa na Israel bali ni kundi la Kigaidi lenye mlengo wa kidini wa kiislamu baada ya kujaribu kurusha kombora kwenda Israel lakini kombora hilo likashindwa kupata muelekeo na kuangukia eneo la hospitali lililokuwa na mamia ya watu wakiwa wamejihifadhi kukwepa Vita huku likiua wengi na kujeruhi wengine.
Hata hivyo mpaka sasa hakuna taarifa rasmi ya kukanusha au kukubali iliyotoka upande wa HAMAS juu ya tukio hilo. Jeshi la Israel limekuja na taarifa hiyo ya kukanusha baada ya watu kuanza kutuhumu jeshi hilo la IDF (Israel Defensive Force) kufanya shambulio hilo. Mpaka sasa watu wanasubiri taarifa rasmi kutoka HAMAS juu ya kuhusika na shambulio hilo.