Jerry Silaa kashindwa kazi?

Mkitafuta uwajibikaji wa viongozi bila uwajibikaji wa wananchi ni kazi bure!

Ama kwa hakika manispaa ya Ilala tumepata hasara, huyu ndiye meya na huu ndio uwezo wake wa kufikiria! amesahau kwamba wananchi wanawajibika kila siku, na ndio hao waliosababisha ongezeko la mapato ya manispaa toka sh.16bilioni hadi sh.26bilioni.

Sasa Jerry, unataka uwajibikaji gani zaidi ya huu wa wananchi kuendelea kuchangia miradi ya maendeleo lakini viongozi mnaishia kufanya ufisadi? Jaribu kutueleza hizi fedha zinazotajwa hapa chini ziko wapi!!?? kama sio wizi wa nguvu za wananchi??


Halafu bila aibu kabisa mtu kama huyu anataka awe mbunge!! Kwa utumishi gani, kwa sifa gani unazoweza kuwaeleza watu wakuchague? kama umeshindwa kuonyesha uwezo wako na kipaji chako ukiwa kama diwani, utaweza kukopa wapi akili ya kuwa mbunge bora??
 

MTM,

Haya tunayoyaeleza hapa ndio ushahidi wa kushindwa kazi kwa jerry, na yeye mwenyewe amethibitisha hilo kwa kuandika mara kadhaa hapa hapa JF.

Tunachokiandika hapa ni ukweli mtupu na hakuna hata chembe ya uongo ama uzushi kama anavyodai. Hatuna sababu yoyote ya kumzushia na ndio maana utaona tangu ameingia kwenye manispaa ya ilala kama meya ni jambo jema kumpima baada ya mwaka mmoja wa kufanya kazi, lakini tunachokishuhudia ni kinyume na matarajio. Na hii ni aibu kwa vijana ambao kila siku tunapiga kelele kwamba tunabaniwa nafasi za kuonyesha uwezo wetu wa utumishi kwa watanzania wenzetu.

Katika hali kama hii ambayo kijana mwenzetu anaapoonekana kupwaya lazima tumweleze ili ajirekebishe na atimize wajibu wake. Hoja zote za msingi zilizotolewa hapa hajaweza kujibu hata moja. Anachofanya ni kuchagua vitu vyepesi ambavyo ni irrelevant na kuvijibu kwa majivuno. Kuna mahali aliwahi kusema manispaa ya ilala ni kubwa kama meli, kwahiyo hawezi kukata kona kirahisi kama mtu anavyoendesha gari.

Katika mazingira kama haya huwezi kutarajia jerry awe ni mtu mwenye vision. Huyu ameridhika tu kuwa meya katika manispaa tajiri nchini, akiwa na umri mdogo lakini output yake kama diwani na kama meya ni minus zero!!
 

Nasikiliza , lakini nashauri ujikite kwenye hoja na uelewa ninachoandika hapa ni muhtasari wa mambo mengi yaliyofanyiwa kazi na yaliyopo kwenye hatua mbalimbali za kutekeleza.
 
Hoja zote za msingi zilizotolewa hapa hajaweza kujibu hata moja. Anachofanya ni kuchagua vitu vyepesi ambavyo ni irrelevant na kuvijibu kwa majivuno

Mfano wa hoja?

 
Ungerudi kwenye hoja ya msingi ya barabara ya mombasa na zahanati ya mongolandege utaaelewa wajibu wa viongozi na wananchi.

 
Hoja zote za msingi zilizotolewa hapa hajaweza kujibu hata moja. Anachofanya ni kuchagua vitu vyepesi ambavyo ni irrelevant na kuvijibu kwa majivuno

Mfano wa hoja?

Kuna hoja zimetolewa na brigedia, usitake kuniambia kwamba hukuziona pamoja na kukusaidia kuzifupisha.

Kuna hoja nimezitoa mimi mwenyewe, kuna hoja zimetolewa na Nguruvi3, kuna hoja zimetolewa na Mkandara, kuna hoja zimetolewa na MTM, Ogah pamoja na wengine kadri ya post inavyojieleza.

Lingekuwa ni jambo la busara ukazijibu, badala ya kuzikwepa na kutafuta vitu vyepesi ambavyo havina uhusiano na maendeleo ya manispaa ya ilala. Usizungumzie hoja za personal affairs, tunataka uzungumzie hoja za maendeleo ya wananchi na huduma za jamii katika manispaa ya ilala!!
 
Ungerudi kwenye hoja ya msingi ya barabara ya mombasa na zahanati ya mongolandege utaaelewa wajibu wa viongozi na wananchi.

Suala la barabara ya mombasa-moshi bar na zahanati ya mongolandegebado hujalijibu lakini pia jitahidi kujibu hoja za mradi ya maji mzambarauni!!
 
Suala la barabara ya mombasa-moshi bar na zahanati ya mongolandegebado hujalijibu lakini pia jitahidi kujibu hoja za mradi ya maji mzambarauni!!
Unajua hata simwelewi Jerry Slaa? nadhani huyu siye ni mtu akjipachika jina la Slaa maana sidhani kama Meya anaweza jibu kipuuzi namna hii..
 
I know they have nothing to do na wananchi wa kawaida zaidi ya kuwafaidisheni wewe na maswaiba zako, ambao ni mafisadi wakubwa
Unaweza kulithibitisha hili na ukiwataja maswaiba?

Serikali ya mtaa madafu
Nimekuwa diwani kwa miaka 6 sasa na ninaheshimu misingi ya utawala bora. Mambo ya mtaa huamuliwa na wana mtaa wenyewe kwenye mikutano yao ya mitaa. Michango, miradi, mapato na matumizi yanafanyika huko. Unaniingizaje kwenye maswala ya serikali ya mtaa wa madafu. Kama hamuafiki hayo myaraise kwenye mkutano wa wananchi. Lakini na sisi tunaangalia uwezekeno wa kuziwezesha ofisi za mitaa maana kwa sasa zipo zinazotoza pesa wananchi kwa kisingizo cha kuendesha ofisi.

Mradibwa majibmzambarauni ulibuniwa na kuendeshwa na MMDO chini ya serikali ya mtaa wa madafu. Naamini kama mwananchi wa madafu unahaki ya kufika ofisini kwa mwenyekiti kupata maelezo.

Viwanja vya kinyerezi
Halmashauri imetwaa eneo la ekari 1600 kwa ajili ya zoezi la upimaji viwanja. Kati ya eneo hilo ekari 800 ni mabonde, barabara na huduma za jamii. Ekari 800 tu ndio zinazofaa kwa viwanja. Tathmini ya fidia imefanyika na viwango ni kati ya 500,000-94m. Kuna mazoea ya viwanja kutolewa burevna serikali au miradi ya viwanja kuwa subsidized na serikali jambo ambalo halifanyiki. mradi huu lazma ujighatamie wenyewe. Swala la kugharamia mradi kwa mkopo ndio miradi yote mikubwa inavyogharamiwa. Gharama ya kuhudumia squatter ni kubwa. Cost of living ya mwananchi wa squatter na wa surveyed area ni tofauti kubwa. Matokeo yake tunakuja kokopa Worldbank kuupgrade slums kama vingunguti. Yawezekana wapo wataoshindwa kumudu difference kati ya fidia na bei ya viwanja, niliomba orodha wananchi wakaopt kwenda mahakamani.


Swala la ubunge wa ukonga nimeshalisema.
Tuna mbunge mzuri mhe. Mwaiposa na kazi yetu kubwa ni kumsaidia kuleta maendeleo. Swala la kukaa Tokyo ndio kazi ya siasa kushiriki makundi ya kijamii. Kwa kuwa mtoa hoja anakuwa Tokyo hawezi kujua ni vijiwe vingapi vya kahawa , tangawizi, camp na mikusanyiko mingine. Unavyofika kwa wanywaji wakati mwengine unanunua bia wakati mwengine hununui. Wala haina impact wala milage yoyote ya kisiasa.


QUOTE=Brigedia;3101011]JERRY SLAA NA MIKAKATI YAKE YA KUTAFUTA UBUNGE JIMBO LA UKONGA 2015:
Siku zote kiongozi bora wa uma ni yule anayekubali kukosolewa na kujisahisha pale inapobidi ili kuboresha ufanisi wa kazi yake. Jerry utake usitake kwenye hili lazima tukukosoe kwa facts, wewe umekuwa diwani katika kata ya ukonga kwa muda mrefu na hiki ni kipindi chako cha pili ambapo awamu ya kwanza ulikuwa naibu meya na sasa ni meya kamili lakini hakuna chochote kile cha maana ulichokifanya pamoja na mbunge wako wa awali Makongoro Mahanga na sasa Mama Eugene Mwaiposa ambaye amekuwa kama mbunge wa viti maalum na si wa jimbo. Sihitaji kuzungumzia takwimu ulizozitoa humu ndani because I know they have nothing to do na wananchi wa kawaida zaidi ya kuwafaidisheni wewe na maswaiba zako, ambao ni mafisadi wakubwa. Hatuyafanyi haya kwa kukukomoa bali tunakukumbusha wajibu wako. Naomba niweke record sawa humu JF ili watanzania waelewe haya tunayoyazungumza wananchi wenzako wa Ukonga:


Suala la huduma za serikali za mitaa Ukonga:
Hii ni changamoto kubwa ya kwanza ambayo inakela sana wananchi wa Ukonga na maeneo mengine ya Manispaa ya Ilala. Katika maeneo yote Wenyeviti wa serikali za mitaa ya Ukonga ambao wote ni maswaiba wako wazuri unaowatumia kukupigia kampeni za kuusaka ubunge 2015, wamejifanya miungu watu na wanataka waabudiwe na wamekuwa wafujaji wazuri wa fedha za uma. Mathalani rafiki yako mkubwa ndugu Alfred Kipondya, mwenyekiti wa mtaa wa Madafu ambaye ni kinara wa kuwachangisha wanachi michango isiyokuwa na kichwa wala miguu. Mmekuwa mkishirikiana nae kula pesa za miradi mbalimbali ya uma kama huu wa maji Mzambarauni kama ambavyo nimeelekeza hapo chini. Hali kadhalika unatueleza mmeongeza magari ya kuzoa taka ya municipal council ilihali wewe na Kipondya mnaendelea kuwachangisha wananchi kila kaya 3,000Tshs fedha ambazo zinaingia katika kampuni yenu binafsi, na hili ninakuombeni acheni mara moja mkija kwetu na wafungulia mbwa. Mbaya zaidi umekuwa ukiwashinikiza wenyeviti pamoja na watendaji wa serikaliza mitaa wakusanye 2,00Tshs kwa kila mtu anayekwenda kwa ajili ya kusainiwa document yoyote ile, ili muulize vizuri swaiba wako Kipondya hatokaa anisahau pale aliponiomba hela kwa ajili ya kunisainia document hukuakitaka kunipa risiti ya cash book yenye muhuli wa serikali ya mitaa. Wananchi huwa tunajiuliza Ilala Municipal Council kwenye hayo makusanyo mnayokusanya si kuna fedha mnazorudisha zitumike katika ofisi zetu za kata pamoja na serikali za mitaa, zinafanya kazi gani?? Jamani mbona hamtuonei huruma? Gharama za maisha zimepanda acheni kutunyonya sana.

Suala la Mgogoro wa Ardhi Kinyerezi:
Halmashauri ya Ilala imepitisha mpango wa upimaji wa viwanja kwenye maeneo ambayo watu wanaishi kule kinyerezi, ambapo mmewaambia wananchi wachangie gharama za upimaji ambapo katika kila square metre moja wanatakiwa kuchangia shilingi 1500. Ukishindwa kulipia gharama kwa ajili ya upimaji unanyang’anywa eneo na unalipwa fidia. Na unajua fika kesi iko mahakamani ambapo wananchi wanapinga gharama ya uchangiaji na hali kadhalika mnajua fika kabisa hata kama mtu akishindwa kulipa gharama za upimaji, gharama za ufidiaji haziendani kabisa na gharama ahalisi za ardhi. Mwanasheria wako wa manispaa ya Ilala aliieleza mahakama kuu mbele ya Judge Shangwa kwamba fedha hizo mnazotaka kuwalipa wananchi mmezikopa bank. So mnataka hizo interest ndio wananchi wawasaidie kulipa?? Huu ni mradi ambao una harufu ya ufisadi na wewe unahusika moja kwa moja kwenye hili pamoja na maswaiba zako.


Mradi wa maji Ukonga Mzambarauni:
Mh mstaiki meya Jerry Slaa hili linaniuma sana kwani lina nigusa sana na watu wa Ukonga hawatokaa walisahau milele katika kipindi chao chote cha maisha yao hapa Duniani. Wananchi wote walichangishwa shilingi 5,000 Tshs kwa kila kaya kwa ajili ya mradi huu tena uchangiaji huo ulikuwa ni wa lazima kwa ajili ya kuondoa shida ya maji, na mkawaambia wananchi mtawasambazia mabomba kuanzia pale mzambarauini kwenda sehemu zingine mbalimbali kama Madafu,Mombasa, Gongo la Mboto, Mwisho wa Lami, mpaka Mazizini. Hivi huwa ukipita pale Mzambarauni roho huwa haikuumi kuona mmekula pesa za wananchi na huduma hakunailiyopatikana?? Muogopeni mwenyezi mungu tendeni haki panapostahili.

Mkakati wako wa kuusaka Ubunge Jimbo La Ukonga-2015:
Hongera sana kwa kushiriki kikamilifu kupigania kupatikana kwa jimbo la Ukonga ambalo linaongozwa na very weak candidate Mh Eugene Mwaiposa,ambaye anafahamu kuwa hiki ndiyo kipindi chake cha mwisho na hatorudi tena kwenye nafasi hiyo. Kwa hili naomba nikupongeze kwa kuona umuhimu wa kuwa na jimbo letu la Ukonga, dhana ambayo tuliamini itasaidia kutuletea maendeleo eneo letu la Ukonga, lakini hali imekuwa tofauti kabisa zaidi ya kuwa chaka la watu kuvuna pesa. Nashukuru umekili kuwa kama kugombea ungegombea 2010 kwani ulikuwa moja ya waasisi wa kupatikana kwa jimbo. Lakini ukweli wenyewe wa hili uko moyoni mwako, na ninajua dhamira yako inakusuta kwenye hili. Chanzo cha wewe kutogombea ubunge 2015 kinafahamika wazi kwa wale tunaofutailia. Mshauri wako mkubwa siku zote amekuwa ni mzee wetu mpendwa Balozi Patrick Tsere (Kipenzi cha vijana) ambaye ulifanya nae kazi akiwa kama DC wa Ilala na wewe ukiwa kama naibu Mstaiki meya. Unafahamu vizuri jinsi ambavyo walikuwa hawaelewani na mstaiki meya wa wakati huo na sababu kubwa ilikuwa ni uelewa pamoja na elimu ndogo aliyonayo mheshimiwa huyo kwa hiyo walikuwa wakipishana mzee Tsere muda wote. Hali iliyopelekea Mzee Tsere kukutumia wewe zaidi kwenye masuala mengi, hili unaweza ukabisha ila likowazi ulisafiri sana kwenda ziara za nje kwa sababu hiyo tu. Ili fika mahali mambo yakawa hayaendi kwa ajili ya mgogoro huo,ndipo Mh Rasi alipoona amsimamishe kazi Tsere na baadaye kumpangia nafasi ya ubalozi Malawi (rejea maneno ya Mh Raisi siku anamwapisha Tsere Ikulu). Na ni mzee Tsere aliyekushauri usubiri kwanza usiingie kwenye ubunge uongoze Ilala Municipal Council. Sasa mikakati yako ya kuusaka ubunge wa jimbo la Ukonga umeizindua katika ma Bar mbalimbali na kijiwe chako kikubwa cha kukusanya taarifa ni Mangi Bar (Tokyo) ,chini ya swaiba wako mkubwa na tapeli namba moja Saidi Dezo. Hutopata kula za Ukonga kwa kuwanywesha watu bia ndugu yetu, chapa kazi tukuvalue kwa uadilifu na uwajibikaji wako. Majuzi ulikuwa Kampala International University-KIU,kwa ajili ya mkakati huoo na umemwaga hela ukiamini vijana wanakupenda la hasha yawezekana hizo ni ndoto za buriani. Umri wako ulionao bado ni mdogo, weweni kijana mwenzetu cha kushangaza umekuwa na lugha za kejeli hali kadhalika dharau kubwa watu, hasa vijana unatuona tuko kijiweni. La hasha yawezekana sasa tukawa hatuna cha kukusaidia ila japo salamu tutakuona kiongozi wetu unatujali. Umediriki kuanza kuchangisha fedha kwenye mitandao na sehemu mbalimbali (ushaidi tunao) kwa ajili ya mambo mbalimbali ya Jimbo la Ukonga lakini badala ya kutimiza lengo la uchangishaji huo badala yake umekuwa ukiyafanya hayo mambo kisiasa. Haya yote yana mwisho wake ndugu yetu tunakuomba utimize wajibu wako kama ambavyo tulikupa ridhaa ya kutuwakilisha.

Asante
Brigedia[/QUOTE]
 
Hukusoma hii!

Wakati unangoja tujenge barabara ya mombasa, kama hauna jambo binafsi, waseme na waliojenga road reserve na wanakimbilia mahakamani na kutaka billions za compansation as if hiyo barabara haitawanufaisha wao.

Kama unakaa Mongolandege sema tukuteue ujumbe wa kamati ya usimamizi ya zahanati ambayo hata hivyo vifaa vikienda na wewe na wananchi wenzako badala ya kusimamia physically mkasimamia humu JF na mkaningoja mimi, mtaandika volume.

Suala la barabara ya mombasa-moshi bar na zahanati ya mongolandegebado hujalijibu lakini pia jitahidi kujibu hoja za mradi ya maji mzambarauni!!
 
Majuzi ulikuwa Kampala International University-KIU,kwa ajili ya mkakati huoo na umemwaga hela ukiamini vijana wanakupenda la hasha yawezekana hizo ni ndoto za buriani

Hivi unahitaji PHD kujua mwanafunzi wa. 1st year KIU anamaliza 2013 max 2014 na uchaguzi ni 2015!!!!!

[/QUOTE]
 
Mh. Jerry Silaa, hongera kwa kazi unayofanya na vile vile kujaribu kujibu hoja humu JF.

Watanzania kwa ujumla wetu tunakabiliwa na tatizo sugu la kupenda sana kulalamika na kujifanya wajuaji wa kila kitu. Yaani sisi, kitu chochote kwetu kimefanywa vibaya sana lakini hatupendi kuangalia kiini cha vitu. Malalamiko mengi yanatakiwa yaende kwa madiwani wa maeneo yao, ili muwabane vizuri na wao wakienda kwenye baraza la madiwani watetee maeneo yao. Sasa malalamiko yote yanapokuja huku juu kwa Meya, inakuwa counter productive.

CCM ni kweli imeleta matatizo mengi sana viongozi wa serikali asilimia kubwa nao hawajui wajibu wao, yaani mtu akichaguliwa basi party nazo zinafanywa kumpongeza, sababu kwa watanzania wadhifa maana yake ni kuula, sio kutumikia wananchi.

Tatizo kubwa la serikali ya TZ ni ukusanyaji mapato. Meya wa Ilala amejua wazi kuwa bila kuremove leakages za mapato, hakuna mipango sio ya barabara, zahanati, uchafu, maji wala nini inaweza kufanywa kwa ufanisi. So solution No.1, Increase revenue. Hapa Mkuu Meya nakupa pongezi, lakini mapato yanatakiwa yazidi with min. 100 bln kwa mwaka, na mimi nadhani ukijikita kwenye swala la tax za nyumba especially za jijini Dar, mapato yatakuwa yakutosha.

Sasa baada ya mapato kuongezwa, suala la pili kabla hata ya kuanza mipango ya kuboresha vitu, ni kuondoa mianya yote ya rushwa na wizi kwenye miradi, hapa najua kazi itakuwa ngumu.

Then, mkuu ndio mipango ianze rasmi ya maji, barabara, zahanati, mashule n.k

Kwangu mimi uko kwenye right track, 2010-2015, ndio kwanza mwaka mmoja umepita. Nadhani by 2014, ndio results zitaanza kuonekana, kwa hiyo ndugu yangu Meya, nakutakia mafanikio mema, ila zingatia sana results zionekane wazi especially by 2014, 2 yrs from now.
 
Asante Moelex


QUOTE=Moelex23;3104416]Mh. Jerry Slaa, hongera kwa kazi unayofanya na vile vile kujaribu kujibu hoja humu JF.

Watanzania kwa ujumla wetu tunakabiliwa na tatizo sugu la kupenda sana kulalamika na kujifanya wajuaji wa kila kitu. Yaani sisi, kitu chochote kwetu kimefanywa vibaya sana lakini hatupendi kuangalia kiini cha vitu. Malalamiko mengi yanatakiwa yaende kwa madiwani wa maeneo yao, ili muwabane vizuri na wao wakienda kwenye baraza la madiwani watetee maeneo yao. Sasa malalamiko yote yanapokuja huku juu kwa Meya, inakuwa counter productive.

CCM ni kweli imeleta matatizo mengi sana viongozi wa serikali asilimia kubwa nao hawajui wajibu wao, yaani mtu akichaguliwa basi party nazo zinafanywa kumpongeza, sababu kwa watanzania wadhifa maana yake ni kuula, sio kutumikia wananchi.

Tatizo kubwa la serikali ya TZ ni ukusanyaji mapato. Meya wa Ilala amejua wazi kuwa bila kuremove leakages za mapato, hakuna mipango sio ya barabara, zahanati, uchafu, maji wala nini inaweza kufanywa kwa ufanisi. So solution No.1, Increase revenue. Hapa Mkuu Meya nakupa pongezi, lakini mapato yanatakiwa yazidi with min. 100 bln kwa mwaka, na mimi nadhani ukijikita kwenye swala la tax za nyumba especially za jijini Dar, mapato yatakuwa yakutosha.

Sasa baada ya mapato kuongezwa, suala la pili kabla hata ya kuanza mipango ya kuboresha vitu, ni kuondoa mianya yote ya rushwa na wizi kwenye miradi, hapa najua kazi itakuwa ngumu.

Then, mkuu ndio mipango ianze rasmi ya maji, barabara, zahanati, mashule n.k

Kwangu mimi uko kwenye right track, 2010-2015, ndio kwanza mwaka mmoja umepita. Nadhani by 2014, ndio results zitaanza kuonekana, kwa hiyo ndugu yangu Meya, nakutakia mafanikio mema, ila zingatia sana results zionekane wazi especially by 2014, 2 yrs from now.[/QUOTE]
 
Jerry... what is your vision kwa watu wako?? na strategies zako ni zipi ili tukuunge mkono?
 
Reactions: Mbu
mimi nakaa karibu na masika bar..au moshi bar..mheshimiwa jibu swali bara bara ya moshi bar-mombasa vipi?
 
jaribu kuwa makini wakati una quote post ili tukuelewe vizuri.
 
Mkuu naona ile falsafz ya 'hakuna kulala hadi kieleweke' imekuingia sana. Ila baba kelele za chura hazimkatazi ng'ombe kunywa maji, sasa mjadala huu hautajibiwa tena na Silaa. Semeni mnavyoweza kashfuni mnavyotaka, Mungu ni shahidi wa yote yaliyofanyika chini ya uongozi makini wa Silaa, na hizo bia kunywa tu kwa kuwa naona wewe kwako ni zaidi ya ukweli na dhumuni lako ni kupambana gizani, nakushauri nenda ofisini kwa Silaa kapate maelezo, kuishia kubwabwaja humu JF hakusaidii, umeya ushaenda kwa Silaa na wala makerere na vihelehele vyako havisumbui, naona umeelimishwa sana hutaki kuelewa.

Enyi mods, naomba mfute thread hii tuna mengi ya msingi tunataka kujadili.
Pangu Pakavu,

 
Moelex23,
Mawazo yako ni mazuri sana, hasa kwenye revenue collection na kuziba mianya upotevu wa fedha za umma.

Lakini ni vizuri ukakumbuka kwamba Jerry ni kiongozi wetu manispaa ya ilala, ni diwani wa gongolamboto. Anayo majukumu kwa wapigakura wake na wananchi wa manispaa kwa ujumla.

Kama mapato yameongezeka lakini huduma za jamii bado ziko duni, ulitegemea tumchekee? Tumpigie makofi? Tukimhoji unasema tunalalamika? Are you serious?
Sisi ndio tunaoishi ukonga, ndio tunaojua adha za barabara ya mombasa-moshibar, ndio tunaojua adha ya maji pamoja na kuchangia mradi wa maji, ndio tunaojua adha ya zahanati ya mongolandege, sisi ndio tunaojua adha ya barabara ya mombasa-mongolandege, sisi ndio tunaojua adha ya barabara ya pugu-majohe.

Moelex23 watu tunafanya kazi kwa nguvu zote ili kujikwamua kimaendeleo. Tunalipa kodi ili serikali iweze kuitumia vizuri kutoa huduma kwa wananchi wake. Hatuna shida na kiongozi anayefurahia posho, mshahara na gari kubwa pasipo kutekeleza wajibu wake kikamilifu!
 

Mkuu usimkatishe Jerry au kumpotosha

the boy has done marvel kwa kuja kujibu hoja and kwa kiasi fulani amejitahidi ingawa kuna challenge ya emotions kuwa high... which is common

Nasikitika sana unasema watu wanabwabwaja... FYI, Jerry akisimama hapa hadi july tu atakua ameshamaliza maswali yote yanayohusu jimbo na wilaya yake for the rest of his tenure!! JF is a very useful tool ya kutathmini chochote, hizo challenges za maneno yasiyofaa zipo hadi kwa wake/waume zetu majumbani na ndio maana bible na mashafu wanasisitiza wisdom na uvumilivu

Ushauri
Upambe wako kwa Jerry haumjengi ila unamfanya awe na mawazo vimini kama wewe (unless wewe mwenyewe ndio jerry
KUbwabwaja ni relative word, maana ukiniuliza mie ntasema Jerry amejibu hoja ila wewe umebwabwaja tu kama mvuta bange kwa hii post


Just view the glass as half full we ndugu yangu
 

Tumia ID yako ya kawaida utasomeka tu.
Mbona una kiherehere sana kama panya buku!? Mjadala ufungwe kwa kushindwa kujibu hoja?
Kama unadhani ''kubwabwaja'' hapa JF haisaidii kitu, mbona jerry amekuja kujieleza hapa!

FYI Jerry atahojiwa tu, iwe JF, Mtaani ama FB.
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…