Kwani hakuna uwezekano wa kufanya hivi wakitaka kujenga Fly Over?

Ghazwat

JF-Expert Member
Oct 4, 2015
23,718
66,262
20040abc39d7fd4dbf91e1c25603297a.jpg
7e0909f842b75bf605a462b89b31fd66.jpg


Baada ya Rais kutembelea miradi miwili ya ujenzi wa Barabara za Juu maeneo ya Tazara na Ubungo, Rais aliagiza kuwa Makao Makuu ya Shirika la Umeme Nchini (TANESCO) lililopo eneo la Ubungo sambamba na jengo la Wizara ya Maji yawekwe alama X tayari kwa kubomolewa kupisha ujenzi wa mradi huo.

Sipingani na Rais yuko sawa katika amri ya kubomoa, ila hoja yangu hakuna uwezekano kufanya kama picha zinavyoonyesha hapa? Maana nijuavyo ni kwamba unajenga Fly Over kuepusha msongamano wa magari wakati huo huo shughuli zingine kama za Ofisi au Kibiashara zikiendelea maeneo hayo. Au hata Ulaya nako wanabomoa majengo wakitaka kujenga Fly Over, Au Ubungo Interchange?

Nawasilisha

==========
Mdau Mwingine
Jengo la Tanesco pale Ubungo limejengwa kwa fedha nyingi kwa mabilioni na ni fedha za wananchi masikini wa Taifa hili.

Ni kweli mradi wa Fly over ni wa muhimu na ni maendeleo kwa nchi lakini unapoleta maendeleo hupaswi kukurupuka na kuharibu vile vya thamani ulivyokuwa navyo awali.

Huo utakuwa ulimbukeni na kukurupuka. Nani kasema Fly over lazima inyooke? Kuliko kuvunja jengo la bilioni kadhaa, zingetumika milioni kadhaa kupata mshauri elekezi kutengeneza mchoro wa kukwepesha barabara kwa juu kwa hiyo section isiyozidi hata mita mia moja.

Kuliko kuvunja jengo kama majigambo wakati ni hasara. Mbona wenzetu wanaweza kufanya hivyo? Wataalamu wa kufanya hivyo wapo, tusipende wataalamu rahisi wa kubomoa. Oneni mbona hawa wameweza?
 
unataka watu wakose dili la kubomoa,, ushauri wako ni mzuri sana
20040abc39d7fd4dbf91e1c25603297a.jpg
7e0909f842b75bf605a462b89b31fd66.jpg
Baada ya Rais kutembelea miradi miwili ya ujenzi wa Barabara za Juu maeneo ya Tazara na Ubungo, Rais aliagiza kuwa Makao Makuu ya Shirika la Umeme Nchini TANESCO lililopo eneo la Ubungo sambamba na jengo la Wizara ya Maji yawekwe alama X tayari kwa kubomolewa kupisha ujenzi wa mradi huo.

Sipingani na Rais, ila hoja yangu hakuna uwezekano kufanya kama picha zinavyoonyesha hapa? Maana nijuavyo ni kwamba unajenga Fly Over kuepusha msongamano wa magari wakati huo huo shughuli zingine kama za Ofisi au Kibiashara zikiendelea maeneo hayo. Au hata Ulaya nako wanabomoa majengo wakitaka kujenga Fly Over, Au Ubungo Interchange?

Nawasilisha
 
Inawezekana mkuu ila ina depend na budget uliyonayo
Hiyo budget ya kujenga jengo jipya je?, vipi kuhusu kuhamisha hiyo mitambo? Hakutakuwa na katizo la umeme kipindi cha kubomoa na kuhamisha plant? Hasara za kiuchumi na kijamii zitakazotokana na katizo la umeme (kama litakuwepo)? Waangalie vyema/upya cost benefit analysis.
 
Mumempa jina la Bulldozer, hata kwenye habari za BBC zinapomzungumzia lazima zimpe sifa hii ya Bulldozer. Sasa anafanya kile Bulldozer linachoweza kufanya. Wengine wanamwita kichwa cha pasi, pasi kazi yake ni kunyoosha tu na watu wananyooka sasa. Mkitaka apunguze kasi mwiteni Povu la soda, tena fanta halivuki ata chupa....
 
Hiyo budget ya kujenga jengo jipya je?, vipi kuhusu kuhamisha hiyo mitambo? Hakutakuwa na katizo la umeme kipindi cha kubomoa na kuhamisha plant? Hasara za kiuchumi na kijamii zitakazotokana na katizo la umeme (kama litakuwepo)? Waangalie vyema/upya cost benefit analysis.
Aisee hii kitu inasumbua mno wakati ikianza..
 
Hiyo budget ya kujenga jengo jipya je?, vipi kuhusu kuhamisha hiyo mitambo? Hakutakuwa na katizo la umeme kipindi cha kubomoa na kuhamisha plant? Hasara za kiuchumi na kijamii zitakazotokana na katizo la umeme (kama litakuwepo)? Waangalie vyema/upya cost benefit analysis.
But who told u mitambo itahamishwa?
 
Mumempa jina la Bulldozer, hata kwenye habari za BBC zinapomzungumzia lazima zimpe sifa hii ya Bulldozer. Sasa anafanya kile Bulldozer linachoweza kufanya. Wengine wanamwita kichwa cha pasi, pasi kazi yake ni kunyoosha tu na watu wananyooka sasa. Mkitaka apunguze kasi mwiteni Povu la soda, tena fanta halivuki ata chupa....
HAHAHA
Imebidi nicheke kwa herufi kubwa jamani JF kuna mambo
 
Back
Top Bottom