Melki the Storyteller
JF-Expert Member
- May 3, 2022
- 5,701
- 9,779
Mpaka sasa najuta sana kulisikia neno "TANESCO" masikioni mwangu. Basi bhana! Mida ya saa 12 niliwasili hapa Ubungo kwenye hii fly over ya Kijazi, pembezoni mwa jengo la mitambo ya umeme
Nikiwa nimeshikilia zangu kibahasha chenye pea tatu za kyupi mdangio kwa ajili ya mteja aliyehitaji delivery, (nikiwa namngoja) nalishangaa kumuona mwanamke mmoja mzuri sana kuwahi kutokea hapa chini ya jua na peponi kwa ujumla
Alikuwa na umbo la nyigu mwenye upwiru, ngozi ya zambarau, nywele za singa. Pia alikuwa ni mwenye adabu nikiwa na maana ya mwanamke mwenye tako mbudule yaani matikiti kudondokeana
Kwa kuwa nilivalia traki la bluu ambalo kimuonekano unaweza dhania ni ovaroli, nikachekecha kichwa kwa haraka ili nimnase pasi na mashaka. Nikaona wacha nitazame miwaya waya ndani ya lile jengo huku nikijaribu kumakinika sana kana kwamba nasolve hesabu za Dr. Heinstain
Yule mwanamke aliponikaribia nikaamua kumuhamishia attention. Baada ya salamu nikaingizia hoja za "Nilikuwa najaribu kutafakari huo waya, maake ndio unaosafirisha mawasiliano ya umeme Ubungo nzima kuelekea Mbezi mwisho, najitahidi sana siku ya leo umeme usijaribu kuzima hata kidogo. Kwani dada yangu ulikuwa unaelekea wapi labda nikupe kampani?"
Mwanamke wa watu akaamua kuniuliza, "Umesema wewe ni mfanyakazi wa TANESCO?". Nikajua nimekula shavu, nikaongezea nyama nyama "Sio mfanyakazi, mimi ni Mkurugenzi Mfawidhi". Yule mwanamke akanipatia msonyo wa nguvu, akamalizia na neno "TANESCO hiyo kwio". Akaondoka zake
Ni mara mia ningezuga kuwa Gerejian huenda ningeibuka na hiyo mama. Namuomba mama awatandike viboko watumishi wote wa TANESCO kwa dhambi kubwa ya kunikosesha utelezi
Ni hilo tu
Nikiwa nimeshikilia zangu kibahasha chenye pea tatu za kyupi mdangio kwa ajili ya mteja aliyehitaji delivery, (nikiwa namngoja) nalishangaa kumuona mwanamke mmoja mzuri sana kuwahi kutokea hapa chini ya jua na peponi kwa ujumla
Alikuwa na umbo la nyigu mwenye upwiru, ngozi ya zambarau, nywele za singa. Pia alikuwa ni mwenye adabu nikiwa na maana ya mwanamke mwenye tako mbudule yaani matikiti kudondokeana
Kwa kuwa nilivalia traki la bluu ambalo kimuonekano unaweza dhania ni ovaroli, nikachekecha kichwa kwa haraka ili nimnase pasi na mashaka. Nikaona wacha nitazame miwaya waya ndani ya lile jengo huku nikijaribu kumakinika sana kana kwamba nasolve hesabu za Dr. Heinstain
Yule mwanamke aliponikaribia nikaamua kumuhamishia attention. Baada ya salamu nikaingizia hoja za "Nilikuwa najaribu kutafakari huo waya, maake ndio unaosafirisha mawasiliano ya umeme Ubungo nzima kuelekea Mbezi mwisho, najitahidi sana siku ya leo umeme usijaribu kuzima hata kidogo. Kwani dada yangu ulikuwa unaelekea wapi labda nikupe kampani?"
Mwanamke wa watu akaamua kuniuliza, "Umesema wewe ni mfanyakazi wa TANESCO?". Nikajua nimekula shavu, nikaongezea nyama nyama "Sio mfanyakazi, mimi ni Mkurugenzi Mfawidhi". Yule mwanamke akanipatia msonyo wa nguvu, akamalizia na neno "TANESCO hiyo kwio". Akaondoka zake
Ni mara mia ningezuga kuwa Gerejian huenda ningeibuka na hiyo mama. Namuomba mama awatandike viboko watumishi wote wa TANESCO kwa dhambi kubwa ya kunikosesha utelezi
Ni hilo tu