Jenerali Mabeyo(JWTZ): Kuna Viashiria vinavyotishia Usalama wa Nchi. Hatua zinachukuliwa kudhibiti hali hiyo

Ndo tabu ya kuteua watu kikanda na kikabila, inabidi wote waimbe wimbo toka ukurasa mmoja kujibainisha na aliyewateua. Hiki ni kiashiria kimojawapo vinavyotishia usalama na umoja wa nchi:

Hotuba ya Jenerali Venance Mabeyo mkoani Ruvuma kuadhimisha " Maji Maji"


c.c kunguru mjanja moderator
 
Awamu hii mpaka wajeda wanapiga siasa.kwani jukumu la jeshi si nikulinda mipaka ya inchi?,hayo mambo mengine anayozungumzia si nijukumu la polisi.

Alafu kwanini haya matamko yemekuwa yanashabiana sana ktk maudhui kuwausia watu wamuunge mkono bwana mkubwa
 
Unaambiwa huyu ni Rafiki yake Mkubwa Sizonje, hawa ndio wanakula keki ya Taifa

Bahati mbaya wanajeshi wengi ngazi ya chini ni choka mbaya

Mauaji haya ndio amani? watu kukatwa mapanga, watu kuokotwa baharini?

Uhuru wa habari kubinywa? Vyombo vya habari vitafichuaje sasa maana watapotezwa na Wasio julikana?

Risasi kufyatuliwa hadharani kulenga wananchi?

Uchumi kudorora

Mpaka maelfu ya Madokta hawana ajira

Generally kula kimya kimya, Umeshiba...!!!!!!

Waalimu wa chuo kikuu kupelekwa kufundisha primary

Ajira za waaalimu Zero

Kampuni kufungwa na maelfu kupoteza Ajira

TRA kutumia nguvu kubwa kudai kodi isiyo halali?

Demokrasia kubinya...Nani haoni? Labda nyie Mmeshiba mkasinzia

Kura kuibwa mchana kweupe
Hawa ni wanafiki wakubwa. Wao uvunjifu wa amani ni wananchi kudai haki zao.
 
Nadhani CDF Mabeyo asingelizungumzia hili na badala yake hii Kauli angeisema TISS DG Dr. Kipilimba ingeleta maana kubwa na kueleweka na wengi kutokana na umuhimu / unyeti wa hiyo Idara. Najua CDF Mabeyo ameshindwa kuivumilia hii hali hasa kwakuwa hata Yeye nae alikuwa na bado ni mbobezi wa ' Unjagu / Ujasusi ' kwa upande wa huko Umedanini / Jeshini kupitia kule kulikomkomaza CMI.
 
Tangu lini Mabeyo ameanza kufanya kazi za Takukuru, mawaziri, polisi na siasa za kuiunga mkono CCM? Huyu ndiye anataka kutuletea chuki na utengano ktk nchi yetu. Komenti hizi za kisiasa zinazoegenea upande wa CCM zinaweza kuligawanya jeshi na kupelekea utovu wa utenganano jeshini, hivyo kusababisha amani ya nchi kutetereka. Anapohubiri siasa za CCM jeshini asidhani kila mwanajeshi ni mwanaCCM.
Point mkuu, huyu mtu ni wa 11 ktk ile list ya watu hatari nchini
 
WAMETIKISIKA, mambo ni Moto 26 April

Mwambieni Mzee kuwa mambo ni Moto....aitishe mazungumzo ya Mustakabadhi wa Taifa

----WanaCCM wengi wanaunga mkono Maandamano..kimya kimyaaaa


Wewe Generally, tuma wanajeshi wakafyatue risasi...Kila mwanajeshi ataua ndugu yake...Inshallah

Wale wanajeshi wa Mara wataua wa Mtwara, Wa Mbeye wataua wa Mara,,,

Wa Dodoma akauwe Arusha na wa Arusha akauwe Mbeya....

Kuuana Watanzania!!!!!

Acheni Maandamano yawe ya Amani, Ni Haki ya Kidemokrasia

Wananchi wanaandamana kwa Amani....Wewe Mabeyo na Sirro ndio mtavunja amani....
Wachumia tumbo hawa, wamelewa madaraka. Maandamano ni ishara ya Pombe kutokukubalika ndio maana wanataka kuzuia hivi vya usalama wa nchi ni visingizio tu labda usalama wa CCM. Na wakiua wananchi tunawapeleka ICC.
 
Huyu anatetea tumbo lake tu, amani imevunjwa na serikali iliyopo ni amani ipi anaongelea..!?

Kumbe kabila la wasukumu halifai kabisa kuongoza sekta yoyote hawana maana kabisa, halina kabisa damu ya uongozi.

Shame on you Mabeyo.
Nyerere hakuwa mjinga, tutasikia Na kuona mengi. Ukiona huyasikii au huyaoni basi ujue zamu yako imefika.
 
Ni vema kama kweli Mkuu wa majeshi ana nia ya dhati na amani ya Tanzania aanze na hao wasiojulikana wanaotuulia watanzania wenzetu, wasiotaka mawazo mbadala lakini wanaobagua watanzania kwa itikadi zao. Tanzania ya leo tunafahamu maovu yanayofanyika lakini kama walipa kodi tunajua haki yetu.
 
Kuhusu viashiria vya uvunjifu wa amani ningependa pia awe mshauri kwa mkubwa amweleze hali halisi ya wananchi kuwa wamechoka kuzibwa midomo na pia kumkumbusha yaliyomo kwenye waraka wa maaskofu wa kikatoliki,hata akina Kakobe.

Yanatakiwa yafanyiwe kazi na upande wa Serikali kwa kurudi nyuma na kujipanga kwa mustakabali wa nchi yetu.

Mbuyu ulianza kama mchicha hakuna kuangalia upande mmoja tu tuangalie na staili ya uongozi wa awamu hii ni wazi watu watabanwa sana lakini lazima pumzi itoke hivyo utokaji wa pumzi unaweza kuleta madhara makubwa sana.hata kama hawana bunduki.

Unaweza kuona visa vya Tunisia na egypt wananchi hawakuwa na silaha hata moja lakini kwa umoja wao baada ya kudharauliwa sana walijikuta wako wamoja hata wanajeshi walisitisha kuwapiga wananchi wakaugeukia uongozi na madikteta wakasalimu nguvu ya umma.
 
ushaur aliotoa mkuu wa majeshi ni mzur sana, lakin yatupasa tusiangalie tu hali hii upande mmoja inabidi tuangalie kwa jicho la pili ili tuweze kuijengea heshima MAMA TANZANIA, kwa kwel hapa tz kwa sasa hali si shwar kabisa ivyo yatupasa tuangalie nn chanzo cha tatizo kisha tukemeee sana lakin tukisema tuangalie upande fln tu " tutakuwa bado hatujajenga nchi sababu hii nchi sasa hv hata hatujui tuna practice utamadun wa nchi gan yaan hali si shwari kabisa nchi iko ovyo ovyo
 
Kuhusu viashiria vya uvunjifu wa amani ningependa pia awe mshauri kwa mkubwa amweleze hali halisi ya wananchi kuwa wamechoka kuzibwa midomo na pia kumkumbusha yaliyomo kwenye waraka wa maaskofu wa kikatoliki,hata akina Kakobe.yanatakiwa yafanyiwe kazi na upande wa serikali kwa kurudi nyuma na kujipanga kwa mustakabali wa nchi yetu.mbuyu ulianza kama mchicha hakuna kuangalia upande mmoja tu tuangalie na staili ya uongozi wa awamu hii ni wazi watu watabanwa sana lakini lazima pumzi itoke hivyo utokaji wa pumzi unaweza kuleta madhara makubwa sana.hata kama hawana bunduki. unaweza kuona visa vya Tunisia na egypt wananchi hawakuwa na silaha hata moja lakini kwa umoja wao baada ya kudharauliwa sana walijikuta wako wamoja hata wanajeshi walisitisha kuwapiga wananchi wakaugeukia uongozi na madikteta wakasalimu nguvu ya umma.
Mabeyo mwenyewe mda wake wa kustaafu ulishafika anatembelea miaka ya kuazima kwa Mtukufu, Huyo mkuu wa majeshi ( CDF) kwanza hana Mvuto pia Asikari wengi wa JWTZ hawampendi kutokana na kuwanyima mikopo na stahiki nyingi ambazo walikuwa wakizipata kipindi cha Gen mwamunyange, hivyo endapo atatoa Amri Jwtz kuwapiga wananchi huenda wasitekeleze Amri zake kwani wanaamini utawala huu uking’oka na yeye Mabeyo atakwenda na huo Upepo wapate CDF mpya ambaye atajali masilahi ya Asikari.
 
Back
Top Bottom