Zak Malang
JF-Expert Member
- Dec 30, 2008
- 5,404
- 234
Wanajamvi nauliza hivi: Jee, ingekuwa ni wafuasi qwa Chadema ndiyo wamevunja uzio (ribbon) iliyowekwa na polisi pale kidongo Chekundu na kuingia uwanjani, ingekuwaje?
Jee sasa hivi Chadema si ingekuwa tayari imefutwa? Polisi lazima wangeingilia na kutmbeza virungu na risasi, watu wangekufa na kulaumiwa CDM kwa "kutotii amri halali' ya polisi.
Hivi katika mikusanyiko na maandamano ni Chadema pekee ndiyo inatakiwa kutii "amri halali' ya polisi?
Hadi lini polisi wataendelea kutiwa vidole machoni namna hii na kukaa kimya, lakini huwa tayari, hata kuleta FFU kutoka mikoa mingine, kuhakikisha CDM wanatii 'amri halali" kutoka kwao?
Kuna unafiki mkubwa hapa. Kuna bvaadhi ya viongozi hao wa dini wamewahi kutoa matamko ya kuilaani CDM 'kwa kutotii amri halali ya polisi" wakati kunaibuka virugu polisi wakiingilia mikutano yao.