Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,476
- 39,995
Kita cha Pili cha Fallujah kule Iraq mwaka 2004 kwa Wamarekani kilikuwa ni mpambano ambao ungeamua matokeo ya vita ya Iraq. Baada ya uvamizi wa Wamarekani katika kumuondoa Sadam Hussein wapiganaji wa Kiiraq walianza mapambano ya mijini (urban warfare) wakitumia mbinu na njia mbalimbali. Hata hivyo, hakuna mpambano mkubwa ambao wapiganaji wale wa Kiiraq walifanikiwa sana kama kuchukua eneo la Fallujah kutoka kwa Wamarekani na washirika wake mapema mwaka 2004 mwezi Aprili.
Mji wa Fallujah ulikuwa ni miongoni mwa miji ambayo ilikuwa imependelewa wakati wa Sadam na wakazi wake wengi walikuwa ni watumishi kwenye vyombo mbalimbali vya usalama. Hata baada ya Wamarekani na Washirika kuingia Fallujah haikuhofiwa sana kuwa na waasi na hivyo vikosi vya wavamizi havikuwa kwa wingi katika mji ule hasa baada ya kuwa na kiongozi wa mji ambaye alionekana anawahusudu Wamarekani.
Matukio kadhaa yaliyowagonganisha wakazi wa Fallujah na askari wa Wamarekani yaliwafikisha pale ambapo watumishi 4 wa kampuni ya Ulinzi ya Blackwater walipouawa na miili yao kuning'inizwa kando yam to Euphrates. Hakukuwa na shaka kwa wataalamu wa Inteligensia kuwa Fallujah ilikuwa imeshikiliwa na wapiganaji wa Kiiraq. Kamandi ya Kijeshi ya Wamarekani wakaamua kuandaa kampeni ya kijeshi ya kwenda kuwaondoa wapiganaji wale na kuleta amani katika Fallujah.
Aprili 1 mwaka 2004 Gen. Mark Kimmit alitangaza nia ya Wamarekani kuhakikisha kuwa Fallujah inatulia. Mipango ya kampeni ya kijeshi ilianza kwa umakini mkubwa. Mwezi Mmoja baadaye (Mei 1, 2004) Wamarekani walijikuta wameshindwa kuleta amani, na mipango yao yote ya kuwatumia Wairaq wenyewe kuleta amani imeshindikana, silaha walizowapatia Wairaq hao zikiangukia mikononi mwa waasi na amri ya kujiondoa (withdraw) kutoka Fallujah ikatolewa na mji wa Fallujah kwa asilimia 100 ukarudi mikononi mwa wapiganaji wa kikundi cha Sheikh Muktadar Al Sadr. Kwa wapiganaji wa Jeshi la Mahdi ulikuwa ni ushindi mwororo. Hata hivyo walijitambua kuwa Wamarekani wangepanga siku nyingine kujaribu tena. Hicho kilikuwa ni kita (battle) cha kwanza cha Fallujah.
Kita cha pili cha Fallujah
Miezi ilipita wakati Wamarekani na Washirika wake pamoja na vikosi vya Kiiraq wakijipanga kuichukua Fallujah. Muda wote Wamarekani wanajipanga wapiganaji wa Al Sadr nao walikuwa wanajipanga kwa kile ambacho tunaweza kukiita ni mpambano wa mwisho (the final confrontation). Siyo lengo langu kuangalia siasa za vita hivyo nzima ya Iraq au kuangalia masuala mengine zaidi ya kuangalia mipango ya kivita tu ya taifa lenye nguvu zaidi linapolazimishwa kupigana mtaa kwa mtaa, nyumba kwa nyumba na wapiganaji wasio na jeshi! Hadi leo hii mpambano wa Fallujah ndio ulikuwa mpambano mkali zaidi wa vita nzima ya Iraq na wanahistoria wa mambo ya kivita wanataja mpambano huo kuwa uliandika upya kitabu cha vita vya mjini (urban warfare).
Ilikuwa Novemba 8 katika kile kilichoitwa Operesheni Ghadhabu Isiyoonekana (Operation Phantom Fury) ndipo vikosi vya Wamarekani wakiongozwa na Marines walipoanza kuishukia Fallujah. Walitumia nguvu zote walizokuwa nazo, utaalamu wote na mbinu zote za kijeshi. Waingereza walipeleka askari 13000; Wamarekani 6500 na Jeshi la Iraq wapiganaji 1500. Upande wa waasi kulikuwa na wapiganaji kati ya 3000-4000 hivi.
Mwisho wa kita kile yaani Disemba 23, 2004 mambo kadhaa yalikuwa wazi; ilikuwa ni mpambano mkali zaidi ambapo vikosi vya Wamarekani vimewahi kuona tangu Vietnam huku askari wake 95 wakiuawa na 560 wakijeruhiwa. Nguvu ya waasi wote ilivunjwa pale na licha ya majaribio ya vikosi vya waasi kujipanga tena hakukuwa na mafanikio yoyote. Pamoja na majaribio mengine Wamarekani wakawa wamejifunza kupigana mtaa kwa mtaa, na kwa kumzidi adui kwa namna ya kipekee. Tofauti zote za kisiasa au kimtazamo za makamanda wale hazikuwa wazi kwani walijua walichokuwa wanapigania na ni kutoka katika mafunzo ya Fallujah, vita vya Ramadi na maeneo mengine yaliweza kuzuiliwa kuangukia mikononi mwa waasi. Miaka mitatu baadaye Fallujah ikarudishwa kwa utawala wa kiraia wa Wairaq mwishoni mwa 2007.
CHADEMA na Arumeru Mashariki
Kwa maoni yangu hakuna mpambano muhimu sana kwa CHADEMA katika historia yake yote ya kisiasa kama kiti cha Arumeru Mashariki. Nimeandika mahali pengine kwa nini hili ni kweli lakini itoshe kusema hapa kuwa CCM na Serikali yake watapeleka nguvu na uzoefu wao wote. CCM haitaki kushindwa na hautoshindwa kirahisi. Mfanano ninaouzungumzia hapa zaidi ni katika taswira ya kijeshi kati ya Fallujah na Arumeru Mashariki – kwamba sehemu zote mbili maslahi makubwa zaidi yanagombaniwa.
CCM inataka kuonesha kuwa CHADEMA hakina ubavu wa kushinda uchaguzi mdogo na hivyo kina hamu na kiu ya kuendeleza rekodi yake ya kuinyanyasa CDM. CCM inaingia ikiwa na rekodi ya kutisha kabisa – haijalishi ilipatikanaje – ya kuweza kushinda chaguzi karibu nane mfululizo hata katika mazingira ambapo CDM walifikiriwa wangeweza kushinda. Hakuna mahali ambapo CDM walikuwa na harufu ya ushindi kama Igunga lakini matokeo yake tunakumbuka. CDM ikabakia kulalamikia mambo yale yale ambayo ililalamikia kuanzia Kiteto – shahada, polisi, serikali, vyombo vya habari n.k!
Lakini kule Igunga CDM ilikuwa imemsimamisha mgombea ambaye kwa kweli alikuwa anajulikana zaidi na watu wa pale lakini hakuwa na umaarufu na ujiko wa Dr. Peter Kafumu. Kafumu alikuwa amelitaka jimbo la Igunga tangu 1994 na hivyo kwa baadhi ya watu walijua mapema kuwa ni mrithi "halali" wa Rostam Aziz. Lakini vile vile tuliona jinsi ambavyo CCM isingekubali jimbo la Rostam ambaye alikuwa anatajwa kuwa ni kinara wa ufisadi nchini liangukie upinzani kwani itakuwa ni uthibitisho wa wazi wa madai ya watu. Huko Arumeru Mashariki hata hivyo mgombea wa CCM hana sifa hizo – hana uzoefo, hajulikani na hana nafasi ya kutisha ndani ya chama au hata serikalini. Ni mgombea dhaifu zaidi ambaye amesimamishwa na CCM labda katika historia ya uchaguzi wake tangu Uhuru! Inapofika mahali CCM wenyewe wanasema ati wapiga kura wamchague tu "wasiporidhika naye watambadilisha mwaka 2015" maana yake ni kuwa hata wao ndani ya CCM wanajua kuwa wamemsimamisha mtu dhaifu.
Lowassa tofauti ya CDM kushindwa au kushinda
Licha ya kwamba mgombea wa CCM ni dhaifu hata hivyo hana udhaifu nyuma yake. Anakuja akiwa na silaha zote za CCM na anakuja pamoja na silaha inayosadikiwa kuwa na nguvu kubwa ya fedha na ushawishi yaani Edward Lowassa. Lowassa licha ya kuwa ni mkwe wa Siyoi Sumari vile vile ni mwanasiasa wa Arusha na anamaslahi mbalimbali huko Arumeru. Lowassa kama jemedari wa kisiasa hayuko tayari kushindwa Arumeru Mashariki. Atatumia mbinu mbalimbali na hakuna mbinu ambayo anaitumia vizuri sasa hivi kama vita vya kisaikolojia. Amekuwa kama jinamizi ambalo linatishia kuwa litaibuka wakati wowote!
Ushindi wa CCM Arumeru Mashariki utakuwa ni pigo lisilo na utata kwa CDM. Watu wasifarijiane kwa kuridhishana kwa uongo kuwa CCM ikishinda basi CDM imejitahidi, au imekubalika zaidi au imepata mashabiki zaidi. Kushinda kwa CCM ni kutuma ujumbe kwa wapinzani kuwa hawana mbinu, ujuzi, mikakati wala uwezo wa kuzuia nguvu za CCM. Ni kama unyanyasaji wa aina fulani hivi – CCM imewashinda Kiteto, Biharamulo, Buchosa, Mbeya Vijijini, Tunduru, n.k CCM itaweza kusimama kwa fahari tu kuwa "hawatuwezi" na hakutakuwa na ubishi!
Kushinda kwa CDM upande mwingine kutakuwa ni ushindi mkubwa wa kisaikolojia. Ni sawasawa na kumpiga Goliathi kwa Kombeo. Utakuwa ni ushindi ambao Vietnam iliupata dhidi ya Marekani licha ya kuzidiwa kijeshi kwa kila hali. Utakuwa ni ushindi ambao siyo tu utawapa nguvu CDM lakini utatuma ujumbe pande nyingine za nchi ambapo kutakuwa na chaguzi mbalimbali baadaye kuwa CCM inaweza kubwaga licha ya nguvu nyingi inazoweza kutumia.
Lakini athari kubwa zaidi ya ushindi wa CDM Arumeru Mashariki itakuwa ndani ya CCM. Kutakuwa na kujichunguza kujua ni kwa nini walimsimamisha Siyoi, jinsi gani walifungua kampeni (maneno ya Mkapa) na hata mkakati wa kushindwa kujenga hoja zenye mashiko. Lakini pia kutakuwa na mgogoro wa wazi wa nafasi ya Lowassa ndani ya CCM kwani maoni ya wengi ndani ya CCM ni kuwa Siyoi amepewa nafasi hiyo si kwa sababu ya utii wake kwa chama au kujionesha kuwa ni kiongozi mzuri bali kwa sababu ya Lowassa, mkwewe. Ndio maana wapo wengine tunaoamini kuwa CCM imempa Lowassa kamba Arumeru ajimalize mwenyewe.
Wiki ya CDM kuonesha ina mikakati nje ya mikutano ya hadhara
Wamarekani waliweza kuichukua Fallujah baada ya kugundua kuwa ushindi hauji kwa kuwaangushia mabomu watu huku anayerusha mabomu hayo yuko kwenye meli baharini au mbali angani. Walitambua hakukuwa na ujanja isipokuwa kwenda nyumba kwa nyumba mtaa kwa mtaa na kuchafuka na kupigwa na kulipuliwa. Siku hizi zilizopita tumeona jinsi ambavyo CDM na viongozi wake wakishambuliwa na wakati mwingine wao wenyewe kushambuliana kuelekea mpambano wa Aprili Mosi. NInachokiona ni kuwa Arumeru ni muhimu sana kiasi kwamba wapo watu wanaoweza kusababisha mpambano wa wenyewe kwa wenyewe.
Kazi kubwa ya viongozi wa CDM ni kujua ni wakati gani kujibizana ndani kwa ndani na binafsi nitafurahi nikiona viongozi makini wakikaa kimya kushambuliana na kutoingia kwenye mtego wa kuondoa macho yao kwenye zawadi. CDM wakianza tu kuzungumzia mambo mengine nje ya ushindi wa Arumeru Mashariki na sehemu nyingine wiki hii watapoteza nafasi hii adhimu kwao na kama nilivyosema mahali pengine ni lazima VIONGOZI WOTE WA KITAIFA wajiuzulu.
Kutokuelewa uzito wa nafasi hii ya kihistoria ambayo kama Fallujah kwa Wamarekani ni kutoelewa historia vizuri. Ninaamini kabisa safari ya CDM 2015 inaanzia Arumeru Mashariki. Wakishindwa Arumeru Mashariki nafasi yao kwenda 2015 itakuwa ni ile ile ya kutaka kukubalika zaidi, kupata wabunge wengi na kugombea nafasi za kugombea badala ya kutaka kushinda. CDM itapimwa na inapaswa kupimwa siyo kwa idadi ya watu wanaonesha alama ya V au wanaovaa rangi za chama au wanaokitetea mitaani. CDM itapimwa na kwa haki kabisa inapaswa kupimwa kwa kushinda uchaguzi. Sasa hivi rekodi yao kwenye chaguzi ndogo ni mbaya na ya kusikitisha.
Wakijipanga kivita, wanaweza kubadilisha hilo.
Harufu ya ushindi inanukia, lakini ni harufu iliyochanganyika na damu. Ipo ya adui, na ipo ya marafiki. Haya ni mapambano na yeyote ambaye hatambui hili ni watu wasiostahili kwenda mstari wa mbele. Wanaotaka kwenda mstari wa mbele wawe tayari kupigana na adui; hakuna soga, hakuna kuchekeana, hakuna kudekeana na kubembelezana. It's a war out there – win or resign! Hakuna lolote ambalo CCM inafanya Arumeru ambalo CDM walikuwa hawalijui so there is no excuse for defeat; NONE WHATSOVER.
It's as simple as that. CCM hawatawarahisishia kazi hiyo na kwa haki kabisa ni lazima CCM wajitahidi kuhakikisha CDM haishindi – wanaodhani CCM itabania halafu itaachia kiulaini wanaota ! Ndio tofauti kati ya vita na ngoma.
I believe while CCM will more other opportunities to make a stand for CHADEMA it is in Arumeru East where it will and must make its FINAL STAND.
Niandikie: mwanakijiji@jamiiforums.com
Mji wa Fallujah ulikuwa ni miongoni mwa miji ambayo ilikuwa imependelewa wakati wa Sadam na wakazi wake wengi walikuwa ni watumishi kwenye vyombo mbalimbali vya usalama. Hata baada ya Wamarekani na Washirika kuingia Fallujah haikuhofiwa sana kuwa na waasi na hivyo vikosi vya wavamizi havikuwa kwa wingi katika mji ule hasa baada ya kuwa na kiongozi wa mji ambaye alionekana anawahusudu Wamarekani.
Matukio kadhaa yaliyowagonganisha wakazi wa Fallujah na askari wa Wamarekani yaliwafikisha pale ambapo watumishi 4 wa kampuni ya Ulinzi ya Blackwater walipouawa na miili yao kuning'inizwa kando yam to Euphrates. Hakukuwa na shaka kwa wataalamu wa Inteligensia kuwa Fallujah ilikuwa imeshikiliwa na wapiganaji wa Kiiraq. Kamandi ya Kijeshi ya Wamarekani wakaamua kuandaa kampeni ya kijeshi ya kwenda kuwaondoa wapiganaji wale na kuleta amani katika Fallujah.
Aprili 1 mwaka 2004 Gen. Mark Kimmit alitangaza nia ya Wamarekani kuhakikisha kuwa Fallujah inatulia. Mipango ya kampeni ya kijeshi ilianza kwa umakini mkubwa. Mwezi Mmoja baadaye (Mei 1, 2004) Wamarekani walijikuta wameshindwa kuleta amani, na mipango yao yote ya kuwatumia Wairaq wenyewe kuleta amani imeshindikana, silaha walizowapatia Wairaq hao zikiangukia mikononi mwa waasi na amri ya kujiondoa (withdraw) kutoka Fallujah ikatolewa na mji wa Fallujah kwa asilimia 100 ukarudi mikononi mwa wapiganaji wa kikundi cha Sheikh Muktadar Al Sadr. Kwa wapiganaji wa Jeshi la Mahdi ulikuwa ni ushindi mwororo. Hata hivyo walijitambua kuwa Wamarekani wangepanga siku nyingine kujaribu tena. Hicho kilikuwa ni kita (battle) cha kwanza cha Fallujah.
Kita cha pili cha Fallujah
Miezi ilipita wakati Wamarekani na Washirika wake pamoja na vikosi vya Kiiraq wakijipanga kuichukua Fallujah. Muda wote Wamarekani wanajipanga wapiganaji wa Al Sadr nao walikuwa wanajipanga kwa kile ambacho tunaweza kukiita ni mpambano wa mwisho (the final confrontation). Siyo lengo langu kuangalia siasa za vita hivyo nzima ya Iraq au kuangalia masuala mengine zaidi ya kuangalia mipango ya kivita tu ya taifa lenye nguvu zaidi linapolazimishwa kupigana mtaa kwa mtaa, nyumba kwa nyumba na wapiganaji wasio na jeshi! Hadi leo hii mpambano wa Fallujah ndio ulikuwa mpambano mkali zaidi wa vita nzima ya Iraq na wanahistoria wa mambo ya kivita wanataja mpambano huo kuwa uliandika upya kitabu cha vita vya mjini (urban warfare).
Ilikuwa Novemba 8 katika kile kilichoitwa Operesheni Ghadhabu Isiyoonekana (Operation Phantom Fury) ndipo vikosi vya Wamarekani wakiongozwa na Marines walipoanza kuishukia Fallujah. Walitumia nguvu zote walizokuwa nazo, utaalamu wote na mbinu zote za kijeshi. Waingereza walipeleka askari 13000; Wamarekani 6500 na Jeshi la Iraq wapiganaji 1500. Upande wa waasi kulikuwa na wapiganaji kati ya 3000-4000 hivi.
Mwisho wa kita kile yaani Disemba 23, 2004 mambo kadhaa yalikuwa wazi; ilikuwa ni mpambano mkali zaidi ambapo vikosi vya Wamarekani vimewahi kuona tangu Vietnam huku askari wake 95 wakiuawa na 560 wakijeruhiwa. Nguvu ya waasi wote ilivunjwa pale na licha ya majaribio ya vikosi vya waasi kujipanga tena hakukuwa na mafanikio yoyote. Pamoja na majaribio mengine Wamarekani wakawa wamejifunza kupigana mtaa kwa mtaa, na kwa kumzidi adui kwa namna ya kipekee. Tofauti zote za kisiasa au kimtazamo za makamanda wale hazikuwa wazi kwani walijua walichokuwa wanapigania na ni kutoka katika mafunzo ya Fallujah, vita vya Ramadi na maeneo mengine yaliweza kuzuiliwa kuangukia mikononi mwa waasi. Miaka mitatu baadaye Fallujah ikarudishwa kwa utawala wa kiraia wa Wairaq mwishoni mwa 2007.
CHADEMA na Arumeru Mashariki
Kwa maoni yangu hakuna mpambano muhimu sana kwa CHADEMA katika historia yake yote ya kisiasa kama kiti cha Arumeru Mashariki. Nimeandika mahali pengine kwa nini hili ni kweli lakini itoshe kusema hapa kuwa CCM na Serikali yake watapeleka nguvu na uzoefu wao wote. CCM haitaki kushindwa na hautoshindwa kirahisi. Mfanano ninaouzungumzia hapa zaidi ni katika taswira ya kijeshi kati ya Fallujah na Arumeru Mashariki – kwamba sehemu zote mbili maslahi makubwa zaidi yanagombaniwa.
CCM inataka kuonesha kuwa CHADEMA hakina ubavu wa kushinda uchaguzi mdogo na hivyo kina hamu na kiu ya kuendeleza rekodi yake ya kuinyanyasa CDM. CCM inaingia ikiwa na rekodi ya kutisha kabisa – haijalishi ilipatikanaje – ya kuweza kushinda chaguzi karibu nane mfululizo hata katika mazingira ambapo CDM walifikiriwa wangeweza kushinda. Hakuna mahali ambapo CDM walikuwa na harufu ya ushindi kama Igunga lakini matokeo yake tunakumbuka. CDM ikabakia kulalamikia mambo yale yale ambayo ililalamikia kuanzia Kiteto – shahada, polisi, serikali, vyombo vya habari n.k!
Lakini kule Igunga CDM ilikuwa imemsimamisha mgombea ambaye kwa kweli alikuwa anajulikana zaidi na watu wa pale lakini hakuwa na umaarufu na ujiko wa Dr. Peter Kafumu. Kafumu alikuwa amelitaka jimbo la Igunga tangu 1994 na hivyo kwa baadhi ya watu walijua mapema kuwa ni mrithi "halali" wa Rostam Aziz. Lakini vile vile tuliona jinsi ambavyo CCM isingekubali jimbo la Rostam ambaye alikuwa anatajwa kuwa ni kinara wa ufisadi nchini liangukie upinzani kwani itakuwa ni uthibitisho wa wazi wa madai ya watu. Huko Arumeru Mashariki hata hivyo mgombea wa CCM hana sifa hizo – hana uzoefo, hajulikani na hana nafasi ya kutisha ndani ya chama au hata serikalini. Ni mgombea dhaifu zaidi ambaye amesimamishwa na CCM labda katika historia ya uchaguzi wake tangu Uhuru! Inapofika mahali CCM wenyewe wanasema ati wapiga kura wamchague tu "wasiporidhika naye watambadilisha mwaka 2015" maana yake ni kuwa hata wao ndani ya CCM wanajua kuwa wamemsimamisha mtu dhaifu.
Lowassa tofauti ya CDM kushindwa au kushinda
Licha ya kwamba mgombea wa CCM ni dhaifu hata hivyo hana udhaifu nyuma yake. Anakuja akiwa na silaha zote za CCM na anakuja pamoja na silaha inayosadikiwa kuwa na nguvu kubwa ya fedha na ushawishi yaani Edward Lowassa. Lowassa licha ya kuwa ni mkwe wa Siyoi Sumari vile vile ni mwanasiasa wa Arusha na anamaslahi mbalimbali huko Arumeru. Lowassa kama jemedari wa kisiasa hayuko tayari kushindwa Arumeru Mashariki. Atatumia mbinu mbalimbali na hakuna mbinu ambayo anaitumia vizuri sasa hivi kama vita vya kisaikolojia. Amekuwa kama jinamizi ambalo linatishia kuwa litaibuka wakati wowote!
Ushindi wa CCM Arumeru Mashariki utakuwa ni pigo lisilo na utata kwa CDM. Watu wasifarijiane kwa kuridhishana kwa uongo kuwa CCM ikishinda basi CDM imejitahidi, au imekubalika zaidi au imepata mashabiki zaidi. Kushinda kwa CCM ni kutuma ujumbe kwa wapinzani kuwa hawana mbinu, ujuzi, mikakati wala uwezo wa kuzuia nguvu za CCM. Ni kama unyanyasaji wa aina fulani hivi – CCM imewashinda Kiteto, Biharamulo, Buchosa, Mbeya Vijijini, Tunduru, n.k CCM itaweza kusimama kwa fahari tu kuwa "hawatuwezi" na hakutakuwa na ubishi!
Kushinda kwa CDM upande mwingine kutakuwa ni ushindi mkubwa wa kisaikolojia. Ni sawasawa na kumpiga Goliathi kwa Kombeo. Utakuwa ni ushindi ambao Vietnam iliupata dhidi ya Marekani licha ya kuzidiwa kijeshi kwa kila hali. Utakuwa ni ushindi ambao siyo tu utawapa nguvu CDM lakini utatuma ujumbe pande nyingine za nchi ambapo kutakuwa na chaguzi mbalimbali baadaye kuwa CCM inaweza kubwaga licha ya nguvu nyingi inazoweza kutumia.
Lakini athari kubwa zaidi ya ushindi wa CDM Arumeru Mashariki itakuwa ndani ya CCM. Kutakuwa na kujichunguza kujua ni kwa nini walimsimamisha Siyoi, jinsi gani walifungua kampeni (maneno ya Mkapa) na hata mkakati wa kushindwa kujenga hoja zenye mashiko. Lakini pia kutakuwa na mgogoro wa wazi wa nafasi ya Lowassa ndani ya CCM kwani maoni ya wengi ndani ya CCM ni kuwa Siyoi amepewa nafasi hiyo si kwa sababu ya utii wake kwa chama au kujionesha kuwa ni kiongozi mzuri bali kwa sababu ya Lowassa, mkwewe. Ndio maana wapo wengine tunaoamini kuwa CCM imempa Lowassa kamba Arumeru ajimalize mwenyewe.
Wiki ya CDM kuonesha ina mikakati nje ya mikutano ya hadhara
Wamarekani waliweza kuichukua Fallujah baada ya kugundua kuwa ushindi hauji kwa kuwaangushia mabomu watu huku anayerusha mabomu hayo yuko kwenye meli baharini au mbali angani. Walitambua hakukuwa na ujanja isipokuwa kwenda nyumba kwa nyumba mtaa kwa mtaa na kuchafuka na kupigwa na kulipuliwa. Siku hizi zilizopita tumeona jinsi ambavyo CDM na viongozi wake wakishambuliwa na wakati mwingine wao wenyewe kushambuliana kuelekea mpambano wa Aprili Mosi. NInachokiona ni kuwa Arumeru ni muhimu sana kiasi kwamba wapo watu wanaoweza kusababisha mpambano wa wenyewe kwa wenyewe.
Kazi kubwa ya viongozi wa CDM ni kujua ni wakati gani kujibizana ndani kwa ndani na binafsi nitafurahi nikiona viongozi makini wakikaa kimya kushambuliana na kutoingia kwenye mtego wa kuondoa macho yao kwenye zawadi. CDM wakianza tu kuzungumzia mambo mengine nje ya ushindi wa Arumeru Mashariki na sehemu nyingine wiki hii watapoteza nafasi hii adhimu kwao na kama nilivyosema mahali pengine ni lazima VIONGOZI WOTE WA KITAIFA wajiuzulu.
Kutokuelewa uzito wa nafasi hii ya kihistoria ambayo kama Fallujah kwa Wamarekani ni kutoelewa historia vizuri. Ninaamini kabisa safari ya CDM 2015 inaanzia Arumeru Mashariki. Wakishindwa Arumeru Mashariki nafasi yao kwenda 2015 itakuwa ni ile ile ya kutaka kukubalika zaidi, kupata wabunge wengi na kugombea nafasi za kugombea badala ya kutaka kushinda. CDM itapimwa na inapaswa kupimwa siyo kwa idadi ya watu wanaonesha alama ya V au wanaovaa rangi za chama au wanaokitetea mitaani. CDM itapimwa na kwa haki kabisa inapaswa kupimwa kwa kushinda uchaguzi. Sasa hivi rekodi yao kwenye chaguzi ndogo ni mbaya na ya kusikitisha.
Wakijipanga kivita, wanaweza kubadilisha hilo.
Harufu ya ushindi inanukia, lakini ni harufu iliyochanganyika na damu. Ipo ya adui, na ipo ya marafiki. Haya ni mapambano na yeyote ambaye hatambui hili ni watu wasiostahili kwenda mstari wa mbele. Wanaotaka kwenda mstari wa mbele wawe tayari kupigana na adui; hakuna soga, hakuna kuchekeana, hakuna kudekeana na kubembelezana. It's a war out there – win or resign! Hakuna lolote ambalo CCM inafanya Arumeru ambalo CDM walikuwa hawalijui so there is no excuse for defeat; NONE WHATSOVER.
It's as simple as that. CCM hawatawarahisishia kazi hiyo na kwa haki kabisa ni lazima CCM wajitahidi kuhakikisha CDM haishindi – wanaodhani CCM itabania halafu itaachia kiulaini wanaota ! Ndio tofauti kati ya vita na ngoma.
I believe while CCM will more other opportunities to make a stand for CHADEMA it is in Arumeru East where it will and must make its FINAL STAND.
Niandikie: mwanakijiji@jamiiforums.com