Mzalendo Uchwara
JF-Expert Member
- Jan 26, 2020
- 3,702
- 11,635
Tangu kuasisiwa kwake mwaka 1964, mauungano wa Tanganyika na Zanzibar umeonekana wazi kugubikwa na ujanja ujanja mwingi.
Ni jambo lililo wazi kabisa kuwa waasisi wa muungano walikua na malengo yasiyofanana, mwalimu Nyerere alidhamiria kuwepo na muungano kamili chini ya serikali moja huku mzee Karume yeye alitaka kuutumia muungano kuhodhi mamlaka kule Zanzibar baada ya mapinduzi kisha auvue kama koti linalobana mambo yakikaa sawa.
Inaonekana mwalimu alimzidi kete Karume kwasababu tokea mwaka 1964 hadi 1984 kulikowepo na juhudi za wazi za kimkakati za kudhoofisha mamlaka ya Zanzibar huku akizidi kuiunganisha nchi.
Baada tu ya muungano, nchi yetu mpya iliitwa 'The united republic of Tanganyika and Zanzibar'. Na kwenye hati za muungano kulikua na mambo 11 (sio 9 kama baadhi ya watu wanavyo dai) yakiyo ainishwa kuwa ni mambo ya muungano ambayo ni;
Kuvunjika kwa taasisi za EAC kama bank na mahakama ya rufani pamoja na kuvunjika kwa jumuiya yenyewe kulitoa nafasi adimu sana ya kuongeza mambo yaliyokuwa EAC kuwa ya muungano. Kwa mujibu wa katiba ya JMT ya sasa, orodha ya mambo ya muungano ina mambo yafuatayo ya ziada;
Ukizingatia kwamba tulikuwa kwenye mfumo wa chama kimoja, basi kwa mara ya kwanza ilipatikana 'mechanism' madhubuti ya kumdhibiti rais wa Zanzibar na serikali yake kupitia vikao vya chama.
Umuhimu wa kete hii ulionekana kipindi cha mchafuko wa hali ya hewa Zanzibar mwaka 1983/1984 ambapo rais wa Zanzibar wa wakati huo ndugu Aboud Jumbe 'alifukuzwa kazi' na CCM. Yaani rais wa Zanzibar anaweza akaitwa Dodoma kwenye vikao vya kawaida kisha akavuliwa uanachama wake na kupotesa sifa ya kuwa rais, akarudi nyumbani akiwa mwananchi wa kawaida tu.
Baada ya mwalimu kung'atuka, na baadaye kuanzishwa kwa mfumo wa vyama vingi, tumejikuta tunakumbana na changamoto ambazo hatukuwahi kuzitegemea hapo awali.
Kwa mfano, nini kitatokea iwapo vyama viwili tofauti vitashinda uchaguzi wa Zanzibar na ule wa Jamhuri ya Muungano? Tutaweza vipi kumfunga speed governor rais wa Zanzibar na serikali yake kupitia mgongo wa chama ikiwa rais wa JMT anatoka chama tofauti?
Nikiri kuwa nimeona jitihada kupitia ACT kwa kumuweka Maalim Seif katikati ya wadau wa dola lakini mkakati wa namna hii unaweza kufanya kazi as long as CCM imeshikilia madaraka ya JMT. Pia hili sio suluhisho la kudumu.
Lakini kikubwa zaidi, ni wazi kuwa ule mkakati wa mwalimu uliishia 1985 alipo ng'atuka, kuanzia hapo hadi leo Zanzibar wamekua wajanja zaidi, na inaonekana kama sasa ni wao wenye mkakati wa kulivua koti la muungano.
Mifano michache ya jinsi Zanzibar ilivyo anza kujiimarisha ni kama;
1. Kuimarisha taasisi zake, ni trend inayoendele sasa huko viziwani. Japo tunaweza kusema hili linafanyika ili kuongeza ufanisi wa utendaji wa SMZ, lakini ndivyo inavyopunguza utegemezi wa SMZ kwa SJMT.
2. Wimbo wa taifa na bendera ya tifa la Zanzibar, mwaka 2005 Zanzibar ilipitisha sheria iliyorejesha bendera yake na wimbo wake wa taifa. Kwa maana hiyo wazanzibari wanafundishwa utii, heshima na uzalendo kwa Zanzibar.
3. Maboresho ya vikosi maalum huko Zanzibar mf. KMKM na JKU. Japokuwa baadhi ya vikosi hivi vina historia ndefu kutokea idara ya usalama Zanzibar hadi jeshi la wanamaji Zanzibar, lakini uwepo wake kwa sasa na jinsi vinavyozidi kuboreshwa ni wazi kuwa wanajiandaa siku wakiwa huru wawe na majeshi yaliyo kamilika. Ukisoma majukumu ya KMKM yako wazi kabisa kuwa ni kulinda mipaka ya Zanzibar.
4. Maboresho ya katiba ya Zanzibar. Pengine hili ndio kubwa kuliko yote, Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984 ilikua inasema 'Zanzibar ni sehemu ya Jumhuri ya Muungano wa Tanzania', lakini baada ya marekebisho makubwa kwa sasa inafungua kwa kusema 'Zanzibar ni Nchi ambayo eneo la mipaka yake ni eneo lote la Visiwa vya Unguja na Pemba pamoja na Visiwa vidogo vilivyoizunguka na bahari yake ambayo kabla ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ikiitwa Jamhuri ya Watu wa Zanzibar'.
Tena katiba hii inamtambua Rais wa Zanzibar kama amiri jeshi mkuu wa vikosi maalum vya Zanzibar na kumpa mamlaka ya kuanzisha vikosi vipya kulingana na mahitaji.
Sasa basi, kwa maslahi mapana ya uhai wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzani tutalazimika kuyajadili haya siku moja kwa ukweli na uwazi hata kama ni mambo yenye ukakasi.
Kinyume na hapo basi wanamikakati inabidi mkazitafute plan za mwalimu kisha mumshauri mwenyekiti aendelee pale alipokua ameishia mwalimu. Walau kufikia 2064 tuwe na serikali moja.
Kinyume na hapo tutajikuta tunakwama njia panda hususani kwenye hili la vyama vingi, hauwezi kuiba uchaguzi kila siku, kuna siku watu watachoka itakua patashika na unaweza kuwa mwisho wa muungano.
Ni jambo lililo wazi kabisa kuwa waasisi wa muungano walikua na malengo yasiyofanana, mwalimu Nyerere alidhamiria kuwepo na muungano kamili chini ya serikali moja huku mzee Karume yeye alitaka kuutumia muungano kuhodhi mamlaka kule Zanzibar baada ya mapinduzi kisha auvue kama koti linalobana mambo yakikaa sawa.
Inaonekana mwalimu alimzidi kete Karume kwasababu tokea mwaka 1964 hadi 1984 kulikowepo na juhudi za wazi za kimkakati za kudhoofisha mamlaka ya Zanzibar huku akizidi kuiunganisha nchi.
Baada tu ya muungano, nchi yetu mpya iliitwa 'The united republic of Tanganyika and Zanzibar'. Na kwenye hati za muungano kulikua na mambo 11 (sio 9 kama baadhi ya watu wanavyo dai) yakiyo ainishwa kuwa ni mambo ya muungano ambayo ni;
- Katiba na serikali ya Jamuhuri ya Muungano
- Mambo ya nchi za nje
- Ulinzi
- Polisi
- Mamlaka juu ya mambo ya hali ya hatari
- Uraia
- Uhamiaji
- Mikopo na biashara ya nchi za nje
- Utumishi katika serikali ya jamuhuri ya muungano
- Kodi (income, cooperate, customs and exercise)
- Bandari, mambo yanayohusu usafiri wa anga, posta na simu
Kuvunjika kwa taasisi za EAC kama bank na mahakama ya rufani pamoja na kuvunjika kwa jumuiya yenyewe kulitoa nafasi adimu sana ya kuongeza mambo yaliyokuwa EAC kuwa ya muungano. Kwa mujibu wa katiba ya JMT ya sasa, orodha ya mambo ya muungano ina mambo yafuatayo ya ziada;
- Sarafu, fedha, mabenki na fedha za kigeni
- Leseni za viwanda na takwimu
- Elimu ya juu
- Maliasili ya mafuta na gesi asilia
- Baraza la taifa la mitihani
- Usafiri na usafirishaji wa anga
- Utafiti
- hali ya hewa
- Takwimu
- Mahakama ya rufani ya JMT
- Uandikishaji wa vyama vya siasa
- Usalama (imeongezwa kwenye ulinzi)
Ukizingatia kwamba tulikuwa kwenye mfumo wa chama kimoja, basi kwa mara ya kwanza ilipatikana 'mechanism' madhubuti ya kumdhibiti rais wa Zanzibar na serikali yake kupitia vikao vya chama.
Umuhimu wa kete hii ulionekana kipindi cha mchafuko wa hali ya hewa Zanzibar mwaka 1983/1984 ambapo rais wa Zanzibar wa wakati huo ndugu Aboud Jumbe 'alifukuzwa kazi' na CCM. Yaani rais wa Zanzibar anaweza akaitwa Dodoma kwenye vikao vya kawaida kisha akavuliwa uanachama wake na kupotesa sifa ya kuwa rais, akarudi nyumbani akiwa mwananchi wa kawaida tu.
Baada ya mwalimu kung'atuka, na baadaye kuanzishwa kwa mfumo wa vyama vingi, tumejikuta tunakumbana na changamoto ambazo hatukuwahi kuzitegemea hapo awali.
Kwa mfano, nini kitatokea iwapo vyama viwili tofauti vitashinda uchaguzi wa Zanzibar na ule wa Jamhuri ya Muungano? Tutaweza vipi kumfunga speed governor rais wa Zanzibar na serikali yake kupitia mgongo wa chama ikiwa rais wa JMT anatoka chama tofauti?
Nikiri kuwa nimeona jitihada kupitia ACT kwa kumuweka Maalim Seif katikati ya wadau wa dola lakini mkakati wa namna hii unaweza kufanya kazi as long as CCM imeshikilia madaraka ya JMT. Pia hili sio suluhisho la kudumu.
Lakini kikubwa zaidi, ni wazi kuwa ule mkakati wa mwalimu uliishia 1985 alipo ng'atuka, kuanzia hapo hadi leo Zanzibar wamekua wajanja zaidi, na inaonekana kama sasa ni wao wenye mkakati wa kulivua koti la muungano.
Mifano michache ya jinsi Zanzibar ilivyo anza kujiimarisha ni kama;
1. Kuimarisha taasisi zake, ni trend inayoendele sasa huko viziwani. Japo tunaweza kusema hili linafanyika ili kuongeza ufanisi wa utendaji wa SMZ, lakini ndivyo inavyopunguza utegemezi wa SMZ kwa SJMT.
2. Wimbo wa taifa na bendera ya tifa la Zanzibar, mwaka 2005 Zanzibar ilipitisha sheria iliyorejesha bendera yake na wimbo wake wa taifa. Kwa maana hiyo wazanzibari wanafundishwa utii, heshima na uzalendo kwa Zanzibar.
3. Maboresho ya vikosi maalum huko Zanzibar mf. KMKM na JKU. Japokuwa baadhi ya vikosi hivi vina historia ndefu kutokea idara ya usalama Zanzibar hadi jeshi la wanamaji Zanzibar, lakini uwepo wake kwa sasa na jinsi vinavyozidi kuboreshwa ni wazi kuwa wanajiandaa siku wakiwa huru wawe na majeshi yaliyo kamilika. Ukisoma majukumu ya KMKM yako wazi kabisa kuwa ni kulinda mipaka ya Zanzibar.
4. Maboresho ya katiba ya Zanzibar. Pengine hili ndio kubwa kuliko yote, Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984 ilikua inasema 'Zanzibar ni sehemu ya Jumhuri ya Muungano wa Tanzania', lakini baada ya marekebisho makubwa kwa sasa inafungua kwa kusema 'Zanzibar ni Nchi ambayo eneo la mipaka yake ni eneo lote la Visiwa vya Unguja na Pemba pamoja na Visiwa vidogo vilivyoizunguka na bahari yake ambayo kabla ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ikiitwa Jamhuri ya Watu wa Zanzibar'.
Tena katiba hii inamtambua Rais wa Zanzibar kama amiri jeshi mkuu wa vikosi maalum vya Zanzibar na kumpa mamlaka ya kuanzisha vikosi vipya kulingana na mahitaji.
Sasa basi, kwa maslahi mapana ya uhai wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzani tutalazimika kuyajadili haya siku moja kwa ukweli na uwazi hata kama ni mambo yenye ukakasi.
Kinyume na hapo basi wanamikakati inabidi mkazitafute plan za mwalimu kisha mumshauri mwenyekiti aendelee pale alipokua ameishia mwalimu. Walau kufikia 2064 tuwe na serikali moja.
Kinyume na hapo tutajikuta tunakwama njia panda hususani kwenye hili la vyama vingi, hauwezi kuiba uchaguzi kila siku, kuna siku watu watachoka itakua patashika na unaweza kuwa mwisho wa muungano.