Ngongo
JF-Expert Member
- Sep 20, 2008
- 18,921
- 31,161
Wataalamu wengi wa uchumi wanakubaliana kwamba ili nchi ijikwamue/isonge mbele kiuchumi tabaka la kati "middle Class" ni muhimu likawa kubwa.Nimejaribu kujiuliza tabaka la kati linashirikisha watu wa aina gani ?.Je tabaka la kati Tanzania [Middle Class] tangu enzi za Mwl J Nyerere hadi sasa limeongezeka au limepungua ?.
Kwa mujibu wa tafsiri ya WB/IMF tabaka la kati [middle class] ni watu wenye kipato kuanzia u$ 2 mpaka u$ 20[3,000 - 30,000] kwa siku.Tukitumia tafsiri ya WB utakuta wafanyakazi wote wa serekali wenye kupata mshahara kima cha chini wanaangukia kwenye hili kundi[Middle Class].Wafanyabiashara ndogo ndogo eg Mama lishe,wauza mitumba,mboga mboga,matunda na nk wote wanaangukia kwenye kundi la tabaka la kati.
Je pato la tsh 3,000/= kwa siku linakidhi mahitaji muhimu eg milo mitatu kwa siku,usafiri,huduma za afya na elimu kwa watoto ?.Ukijaribu kukokotoa utakuta pato la tsh 3,000/= kwa siku halitoshelezi milo mitatu kwa mtu mmoja na kama mtu huyo atakuwa na watu tegemezi eg mke na watoto hakika hata mlo mmoja utakuwa ni mgogoro mkubwa.
Wataalamu wa uchumi wanapaswa kuangalia upya viwango vya kupima umaskini.Pato la u$ 2 kwa siku ni kiwango kidogo sana ukweli ukiangalia kwa namna yoyote mtu mwenye kipato hiki bado ni masikini sana hana uwezo wa kukidhi mahitaji yake muhimu ya kila siku.Yafaa kiwango cha middle class kipandishwe hadi u$ 10 [tsh 15,000]kwa siku pia suala la utegemezi eg ukubwa wa familia,usafiri na inflation likizingatiwa.
Kwa mujibu wa tafsiri ya WB/IMF tabaka la kati [middle class] ni watu wenye kipato kuanzia u$ 2 mpaka u$ 20[3,000 - 30,000] kwa siku.Tukitumia tafsiri ya WB utakuta wafanyakazi wote wa serekali wenye kupata mshahara kima cha chini wanaangukia kwenye hili kundi[Middle Class].Wafanyabiashara ndogo ndogo eg Mama lishe,wauza mitumba,mboga mboga,matunda na nk wote wanaangukia kwenye kundi la tabaka la kati.
Je pato la tsh 3,000/= kwa siku linakidhi mahitaji muhimu eg milo mitatu kwa siku,usafiri,huduma za afya na elimu kwa watoto ?.Ukijaribu kukokotoa utakuta pato la tsh 3,000/= kwa siku halitoshelezi milo mitatu kwa mtu mmoja na kama mtu huyo atakuwa na watu tegemezi eg mke na watoto hakika hata mlo mmoja utakuwa ni mgogoro mkubwa.
Wataalamu wa uchumi wanapaswa kuangalia upya viwango vya kupima umaskini.Pato la u$ 2 kwa siku ni kiwango kidogo sana ukweli ukiangalia kwa namna yoyote mtu mwenye kipato hiki bado ni masikini sana hana uwezo wa kukidhi mahitaji yake muhimu ya kila siku.Yafaa kiwango cha middle class kipandishwe hadi u$ 10 [tsh 15,000]kwa siku pia suala la utegemezi eg ukubwa wa familia,usafiri na inflation likizingatiwa.