Je, Waziri Ndalichako ajiuzulu kuinusuru elimu Tanzania?

ndalichako yuko poa sana, kadhibiti uhuni wote pale necta hata kwenye bodi ya mikopo kulikuwepo na ujanjaujanja mwingi sana lakni sasahiv haupo, mm binafsi naona huyu mama yuko poa.
Mimi nadhani NECTA ndio kuna mfaa , sio huyu katibu wa sasa naona kama amebebeshwa mzigo mzito pale NECTA
 
Ndio maana nakwambia kuwa ulikimbia umande
Mimi silingani elimu na ww hata kidogo jichunge na maneno yako usije fikiri kila mtu ni mbumbumbu kama wewe.
Ni kheri ukapingana hoja kwa hoja weka vigezo vya ubishani wako kuhusu mikopo na wangapi walipata ama wangapi wamekosa ila mihemuko na hisia visikuponze ukapiga piga kelele mitandaoni kama hayawani.
 
Mimi silingani elimu na ww hata kidogo jichunge na maneno yako usije fikiri kila mtu ni mbumbumbu kama wewe.
Ni kheri ukapingana hoja kwa hoja weka vigezo vya ubishani wako kuhusu mikopo na wangapi walipata ama wangapi wamekosa ila mihemuko na hisia visikuponze ukapiga piga kelele mitandaoni kama hayawani.
Sina muda mchafu kama huo
 
Wewe una stress tu za kukosa kazi na kushindwa kukubali ukweli au unataka uwezo wako mdogo uonekane, kwani hayo uliyoyataja kama kuongeza mishahara, kupandisha madaraja,kulipwa uhamisho, mafao kwa wastaafu nk yako kwenye wizara ya elimu tu toka 2015 mwishoni?. Hivi ulikuwa nje ya nchi au ulikuwa sehemu kusiko na radio wala tv kusikia Rais mwenyewe akisitisha yote uliyoyasema kwa madai ya kuhakiki watumishi hewa?. Wewe ungemlaumu Rais na siyo waziri maana tamko hilo ni la rais. Ngoja nikwambie ndg Tembea shule zote za mjini waalimu wa arts wametosha na hata vijijini washaanza kuzidi, halafu siyo kwamba shule zote tz yote hazikuwa na waalimu wa sayansi hao wanaoenda kuziba gepu iliyokuwepo lakini hata kama hatukuwa na mwalimu hata moja wa sayansi nchi nzima huwezi kuajiri tu wakati BUDGET HAITOSHI UTAWALIPA NINI KAKA? unajua maana ya budget kweli?, hii bila shaka ni product ya theofilo au udom au MMU. KAKA BADO NI MAPEMA HEBU FANYA MENGINE UTAKUFA UNALAUMU NA MAJUKUMU YANAONGEZEKA KESHO NA KESHO KUTWA UMEOA, UNA MTOTO SIJUI UTAMWAMBIA OOOH NDALICHAKO NDIYE KATULAZA NJAA. VYETI VYAKO HIVYO NI KAMA MAKARATASI KAMA VINAKUFANYA UENDELEE KULAUMU NDALICHAKO KWA WEWE KUKOSA AJIRA. NAJUA MAUMIVU YA KUKOSA AJIRA MWENYEWE YAMENIPATA ILA SINA MUDA WA KULAUMU NASONGA MBELE BROTHER.
Katika vitu ulivozingua kutaja hivyo vyuo TEOFILO,UDOM,MMU una maana gani apo maana apa ndio tutaona IQ yako ipoje kwamha hiyo product ya hivyo vyuo ipoje na utupe statistics apa nitakuona unajielewa ila bila hvy nawe ni wale wale
 
Ndalichako ni jipu ni mda tuu utasema pale kwenye elimu bora hata angewekwa January Makamba, huyu ndo waziri amebaki anajielewa sana kwenye baraza la mawaziri waliobaki. KWA UFUPI NDALICHAKO matamko yamezidi na hajui hata mipaka yake.Mm najua wizara inayohusika na ajira ni tamisemi hyu ndalichako kuwa kieleele mpaka kuingilia majukumu ya wenzake inakueje. Wameondoa watumishi hewa ila wameshindwa kuajiri watumishi wapya.
Wameondoa wanafunzi hewa wameshindwa kuwapa wanafunzi wengi mikopo ya elimu ya juu.Waziri anatakiwa kuwa mbunifu na sio matamko.
 
nilimuheshimu sana huyu Prof, mpka mwanzo mwa uwaziri wake...

ila kayumba sana na katepeta sana, hata utendaji wao hauna tofauti na Mungai
 
Habari wanajamvi,

Leo nakuja na ushauri wa kumtaka huyu mama aachie ngazi kwani amekuwa akiyumba sana, kwa kutomueleza mkuu uhalisia wa elimu nchini.

Huyu mama kwa mda mchache aliopewa wizara pamoja na uprofesa wake amesababisha mengi katika sekta ya elimu;
>Wanafunzi vyuo kukosa mikopo
>Wanafunzi wanaosoma kwa nje ya nchi kuwanyima mikopo
>Kufuta vyuo bila utafiti maalum na hivyo kuisababishia serikali kukosa kodi
>Kushindwa kuajili walimu
>Baya zaidi jana anasema wakurugenzi wawahamishe walimu walioko mjini
>Tatizo sio kuhamisha, tatizo hawapo, na yeye hamuambii mkuu ukweli kwa kuogopa kutumbuliwa.

Tunachoomba jiuzulu utuachie wizara yetu iliyokuwa ikiajiri kila mwaka Sayansi na Sanaa, huku mambo yakienda, nyie mmetoa walimu hewa halafu hamuajiri kisha unaendelea kubaki.

Achia ngazi mama, uwaziri sio haki yako ya msingi, hata ukaeje, kwa ulivyovurunda na kaubunge ka kupewa, utaachia tu.

Fadhila zinamwisho.
Hana lolote kabisa huyu Mama
 
Habari wanajamvi,

Leo nakuja na ushauri wa kumtaka huyu mama aachie ngazi kwani amekuwa akiyumba sana, kwa kutomueleza mkuu uhalisia wa elimu nchini.

Huyu mama kwa mda mchache aliopewa wizara pamoja na uprofesa wake amesababisha mengi katika sekta ya elimu;
>Wanafunzi vyuo kukosa mikopo
>Wanafunzi wanaosoma kwa nje ya nchi kuwanyima mikopo
>Kufuta vyuo bila utafiti maalum na hivyo kuisababishia serikali kukosa kodi
>Kushindwa kuajili walimu
>Baya zaidi jana anasema wakurugenzi wawahamishe walimu walioko mjini
>Tatizo sio kuhamisha, tatizo hawapo, na yeye hamuambii mkuu ukweli kwa kuogopa kutumbuliwa.

Tunachoomba jiuzulu utuachie wizara yetu iliyokuwa ikiajiri kila mwaka Sayansi na Sanaa, huku mambo yakienda, nyie mmetoa walimu hewa halafu hamuajiri kisha unaendelea kubaki.

Achia ngazi mama, uwaziri sio haki yako ya msingi, hata ukaeje, kwa ulivyovurunda na kaubunge ka kupewa, utaachia tu.

Fadhila zinamwisho.
Kaleta matatizo makubwa kwenye hii sekta na aliye mteua anamwangalia tuu.
 
Wengine wanamtetea Cjui bibi yao hata kama wakwao kama hafai aachie ngazi kutumbuliwa haiwezikani b'coz anafanya kama mh: anavyotaka.
Pili tuombe hoja ipelekwe bungeni kura ipigwe kumtoa rais hafai kabisa.
 
Aah,,mtajijua na Ndalichako wenu,kwanza si mulimuombea kazi humu......
 
Katika vitu ulivozingua kutaja hivyo vyuo TEOFILO,UDOM,MMU una maana gani apo maana apa ndio tutaona IQ yako ipoje kwamha hiyo product ya hivyo vyuo ipoje na utupe statistics apa nitakuona unajielewa ila bila hvy nawe ni wale wale

Najua kimoja wapo ni chako, ila kwa wale wa UDSM,SUA au hata MZUMBE wanaweza kunielewa at least UDOM imeanza kuwa na hadhi ya chuo kikuu kitaaluma hayo mengine mnatoka hamna kitu kama huyo mwenzako. Argument tu inawaumbua nimebahatika kufanya na baadhi ya products za hivyo vyuo ni sawa na bure.
 
Huyu mimi namuona mwehu pale aliposema kuingia chuo kikuu lazima upitie form six tu, kupitia kwanza diploma haikubaliki. Lo hapa aliniacha na mduazo mpaka leo namuona hafai haswaa, atimue
 
ndalichako yuko poa sana, kadhibiti uhuni wote pale necta hata kwenye bodi ya mikopo kulikuwepo na ujanjaujanja mwingi sana lakni sasahiv haupo, mm binafsi naona huyu mama yuko poa.

Ww kwakuwa ni dereva wake baki unashabikia huo upuuzi. Sasa hivi waalimu hawafundishi wanakaa maofisini wanapiga soga tu. Ila kila mwisho wa mwezi wanachukua mshahara. Nina ushahidi mtoto wangu yupo shule toka tarehe 9 ila mpaka leo kafundishwa somo moja tu tena kiubabaishaji. Ww baki unasifia yeye kudhibiti sijui necta na mikopo wakati huko kote hakuna wanafunzi. Elimu inauwawa yeye huyo Ndalichako watoto wake wanasoma nje huku anachukua mshahara na huduma muhimu kulipiwa na serekali wakati elimu yetu hapa nchini anaiangamiza. Nasubiri mwisho huu wa mwezi nije na madaftari ya mwanangu hapo ofisini aone kinachofundishwa na shule zetu, halafu aangalie madaftari ya watoto wake kama yanakaribiana.
 
ndalichako yuko poa sana, kadhibiti uhuni wote pale necta hata kwenye bodi ya mikopo kulikuwepo na ujanjaujanja mwingi sana lakni sasahiv haupo, mm binafsi naona huyu mama yuko poa.
Kama kadhibiti ukanjaujanja loan board kwann wasipewe wengi sasa?
 
Back
Top Bottom