Kiranga
Platinum Member
- Jan 29, 2009
- 85,695
- 145,396
Je, wanaharakati wana haki ya kuzuia wengine wasipige kura?
Tuna siku chache kabla ya uchaguzi mkuu wa 2025. Uchaguzi huu umegubikwa lindi la kukosa uhalali pengine kuliko uchaguzi mwingine wowote Tanzania.
Hata mgombea wa CCM ameshutumiwa na mpaka kufunguliwa kesi kuwa kajipitisha bila kufuata utaratibu.
CHADEMA imesusia uchaguzi. Mgombea wa ACT Wazalendo kazuiwa kushiriki, ingawa kuna wanaosema kafanya makosa mwenyewe. Wagombea wengi, hata ndani ya CCM wamekatwa bila sababu za kueleweka.
Kuna watu wengi wanalalamika kuwa uchaguzi hauna uhalali, tume ya uchaguzi inachaguliwa mwenyekiti na rais anayegombea urais pia katika uchaguzi, na matatizo mengine mengi ya kikatiba na kiuendeshaji.
Hivyo, wanaharakati wengi wanataka kuandamana siku ya uchaguzi tarehe 29 October. Hiyo ni haki yao ya kikatiba.
Lakini, wengine wanakwenda mbali zaidi, wanataka kufanya civil disobedience kuzuia wengine wasifanye uchaguzi. Hawa si tu wanataka kuandamana, bali pia wanataka kuzuia uchaguzi hata kwa kutumia fujo na nguvu.
Wanasema huu si uchaguzi, ni uchafuzi, ni maigizo, ni figisu tupu. Hivyo, wana haki ya kuuvuruga usifanyike.
Lakini, kuna watu wameamua kushiriki kwenye uchaguzi huu. Kwa kujua na kukubali huu si uchaguzi ni uchafuzi, au kwa kutokujua na hata kukataa habari hiyo inayopinga uhalali wa uchaguzi.
Na wao wanasema wana haki yao kushiriki uchaguzi huo, na wana haki ya kufanya uamuzi binafsi kwamba uchaguzi huu ni halali au si halali, waachwe waitumie haki yao. Demokrasia si kulazimishana, ni watu wote kupata uhuru wa kufanya maamuzi wanayoona ni sahihi.
Hili ni swali muhimu na gumu kifalsafa.
Kuna wanaharakati wanasema wana haki ya kuvuruga uchaguzi usio halali.
Kuna wapiga kura wanasema haki yao ya kuamua kupiga kura iheshimiwe.
Haki hizi mbili zinaonekana kugongana.
Tunapitaje hapa kwa usalama bila kuvunjia kundi moja la wanaharakati haki yao ya civil disobedience kuvuruga uchaguzi, lakini pia tusiwavunjie watu walioamua kupiga kura?
Na kama hatuwezi ku maintain haki zote, haki ipi inaipiku nyingine? Kwa sababu gani?
Naomba mazungumzo ya kidhahania zaidi, yajikite kwenye sababu za kifalsafa Zaidi, kimantiki, kuliko kuwa na mjadala wa kisasa wenye hisia zaidi.
Tuna siku chache kabla ya uchaguzi mkuu wa 2025. Uchaguzi huu umegubikwa lindi la kukosa uhalali pengine kuliko uchaguzi mwingine wowote Tanzania.
Hata mgombea wa CCM ameshutumiwa na mpaka kufunguliwa kesi kuwa kajipitisha bila kufuata utaratibu.
CHADEMA imesusia uchaguzi. Mgombea wa ACT Wazalendo kazuiwa kushiriki, ingawa kuna wanaosema kafanya makosa mwenyewe. Wagombea wengi, hata ndani ya CCM wamekatwa bila sababu za kueleweka.
Kuna watu wengi wanalalamika kuwa uchaguzi hauna uhalali, tume ya uchaguzi inachaguliwa mwenyekiti na rais anayegombea urais pia katika uchaguzi, na matatizo mengine mengi ya kikatiba na kiuendeshaji.
Hivyo, wanaharakati wengi wanataka kuandamana siku ya uchaguzi tarehe 29 October. Hiyo ni haki yao ya kikatiba.
Lakini, wengine wanakwenda mbali zaidi, wanataka kufanya civil disobedience kuzuia wengine wasifanye uchaguzi. Hawa si tu wanataka kuandamana, bali pia wanataka kuzuia uchaguzi hata kwa kutumia fujo na nguvu.
Wanasema huu si uchaguzi, ni uchafuzi, ni maigizo, ni figisu tupu. Hivyo, wana haki ya kuuvuruga usifanyike.
Lakini, kuna watu wameamua kushiriki kwenye uchaguzi huu. Kwa kujua na kukubali huu si uchaguzi ni uchafuzi, au kwa kutokujua na hata kukataa habari hiyo inayopinga uhalali wa uchaguzi.
Na wao wanasema wana haki yao kushiriki uchaguzi huo, na wana haki ya kufanya uamuzi binafsi kwamba uchaguzi huu ni halali au si halali, waachwe waitumie haki yao. Demokrasia si kulazimishana, ni watu wote kupata uhuru wa kufanya maamuzi wanayoona ni sahihi.
Hili ni swali muhimu na gumu kifalsafa.
Kuna wanaharakati wanasema wana haki ya kuvuruga uchaguzi usio halali.
Kuna wapiga kura wanasema haki yao ya kuamua kupiga kura iheshimiwe.
Haki hizi mbili zinaonekana kugongana.
Tunapitaje hapa kwa usalama bila kuvunjia kundi moja la wanaharakati haki yao ya civil disobedience kuvuruga uchaguzi, lakini pia tusiwavunjie watu walioamua kupiga kura?
Na kama hatuwezi ku maintain haki zote, haki ipi inaipiku nyingine? Kwa sababu gani?
Naomba mazungumzo ya kidhahania zaidi, yajikite kwenye sababu za kifalsafa Zaidi, kimantiki, kuliko kuwa na mjadala wa kisasa wenye hisia zaidi.