Mkuu ukisoma Mwanzo 3 yote utaona ni tamaa na uzembe wa binadamu wenyewe tuu kwani Adamu alishaambiwa asile hilo tunda hata kabla ya Hawa kuumbwa toka ubavuni mwake. Soma Mwanzo 2:16-17 "Mwenyezi-Mungu alimwamuru mwanaume huyo, waweza kula matunda ya mti wowote katika bustani lakini matunda ya mti wa ujuzi wa mema usile, maana siku utakapokula matunda ya mti huo hakika utakufa"
Kwa hiyo kwa mujibu wa huo mstari hapo Adamu alikua keshaonywa hata kabla ya kuumbwa kwa Hawa.
Sasa mkuu nani mjinga? nani mwenye makosa? Mungu au Adamu?
...Adamu ndie mwenye makosa kwa sababu hakutii amri ya Mungu badala yake alisikiliza alichoambiwa na Hawa. Soma Mwanzo 3:11-12 "Mwenyezi-Mungu akamwuliza nani aliyekuambia uko uchi? Je umekula tunda la mti nililokuamuru usile? Huyo mwanaume akajibu mwanamke uliyenipa akae pamoja nami ndiye aliyenipa tunda la mti huo nami nikala"
Sasa mkuu unaanzaje kumlaumu Mungu wakati ni makosa ya Adamu? Tena Adamu ndie mpuuzi kwa sababu alimsikiliza mwanamke badala ya kumsikiliza Mungu wake, so mwanamke kwake alikua ni zaidi ya Mungu! dharau ilioje????
Na uzuri Hawa nae alikua anajua matunda ya mti fulani Mungu kakataza yasiliwe soma Mwanzo 3:2-3
Sasa mkuu kwa kifupi tuko hapa tulipo sababu ya uasi wa binadamu toka mwanzo!
Haya yote yanayotokea hayana budi kutokea. Mungu ni mwema siku zote, binadamu sababu ya tamaa zetu na kutoshika maandiko ndivyo vinatuponza. Ni lazima tujue uwepo wa Mungu, watu wengi wasiposhuhudia matendo makuu ya Mungu huwa hawaamini kwamba Mungu yupo.
Yes bado anatupenda ndio maana alimtoa mwanae wa pekee/Yesu aje kutukomboa lakini pamoja na yote hayo hamna kitu bado binadamu wanazidi kuasi. Soma vitabu vya Daniel na Ufunuo ujue hatma ya huu ulimwengu. Na ni lazima unabii utimie hata Yesu alikuja kutimiza unabii na kutukomboa toka kifungoni mwa shetani.
Nawashangaa sana watu mnaokaa hapa na kuanza kumshushia lawama Mungu wakati ni matokeo ya uasi wetu toka mwanzo.
Huu ndio ukweli.
Hata wanaotengeneza vyombo vya kutumia kama mashine au magari, kuna menu za vyombo hivyo, jinsi ya kuvitumia na kuvitunza.
Binadamu pia ana menu yake inayomwelekeza jinsi ya kujitumia na kuishi.
Mungu kupitia maandiko matakatifu ameeleza kila kitu kuhusu Binadamu aliye muumba, aishi vipi na jirani, ale nini, avae nini, afanye nini, asifanye nini ili aishi vizuri na kujitunza afya yake imavyopasika.
Mambo hayo yako wazi kabisa kwa mfano imeandikwa, usiue, usizini, mpende jirani yako, usiibe, NK.
Sasa wewe unazini na mke wa mtu, au unaiba au unaua, watu wanakukamata wanakuua kwa kukuchinja au kukuchoma moto au kwa kipigo, halafu unaanza kumlaumu Mungu eti haja kulinda.
Unaanza kimsingizia Mungu eti ameumba dunia yenye machafuko ya vita na kadhalika kadhalika.
Umeambiwa kabisa usipotii Neno la Mungu hakika utakufa, sasa kwanini lawama.
Neno la Mungu ndio afya na ulinzi wenyewe.
Amri ambazo Mungu ameziweka ili tuzifuate, zimewekwa kwa manufaa yetu wenyewe ili tustawi hapa duniani na kufurahia maisha.
Tusipo zifuata basi tukubali madhara yatakayotupata, chanzo ni sisi wenyewe.
Ndio maana mtu akipigwa kwa kufumaniwa haendi kushtaki popote, anajua amestahili adhabu hiyo.
Wajibu wa kufanya Wema au Ubaya upo mikononi mwetu.