Naanza kwa Surprise. Surprise yenyewe ni wimbo. Je, wimbo huu unakukumbusha wapi? Baadaye nitamwaga story za enzi hizo. Keep in touch.
Nyimbo za wakati huo, zilikuwa na mafunzo mengi sana. Kuna wimbo mmoja ulioimbwa na vijana jazz uliitwa " ilikuwa lift" Katika wimbo huo......inaonesha jamaa alichanganyikiwa baada ya kumuona mke wake yuko na jamaa mwingine kwenye gari la mkewe........Soma mashairi ya wimbo huo ufaidi mambo ya zama hizo. Je, unakukumbusha nini?
ILIKUA NI LIFTI TU
Haikua jambo baya kwangu
Kwa yule kijana kumpatia lifti
Kama unavyohamu yapata wiki ya tatu
Gari langu lina matatizo ya kuzimikazimika ooo Mume wangu eee
Kutoka nyumbani Oyster Bay kufika Salender
Gari langu lilinizimikia eeee
Yule kijana alinisaidia kusukuma Mume wangu eee ooo ooooo oooooo
Kilichonishangaza sio lifti Mama Watoto
Ni tabasamu na vicheko mlivyokuanavyo ndani ya gari
Nilichanganyikiwa midomo ilianza kunicheza
Mithili ya mtu aliyemeza kipande cha moto Mama watoto