Lyambalyetu
JF-Expert Member
- Apr 6, 2021
- 265
- 240
Mie kila pakikucha huwa ninakumbuka ile aliyosema ananunua treni. Bahati mbaya siku hiyo nikiwa ninasubiria kwenye foleni pale alipokuwa akihubiria nikasikia ahadi hiyo. Seriously ilinibidi nipaki gari pembeni nikasikiliza mahubiri yake mpaka mwisho na nikahudhuria tena kama mara tatu hivi, sikuona mrejesho wa hiyo ahadi basi nikakoma kwenda kwenye mahubiri yake.
Nikasikitika sana kuwa hadhira ile huwa hairuhusiwi kumwuuliza Askofu kupata mrejesho wa ahadi zilizotolewa wakati statements za kimahubiri zikitamkwa!
Wewe mwenzangu ni ahadi gani ya Gwajima umewahi isikia na kisha ikatekelezwa kwa vitendo?
Tuchangie kwa hoja tafadhali.
Nikasikitika sana kuwa hadhira ile huwa hairuhusiwi kumwuuliza Askofu kupata mrejesho wa ahadi zilizotolewa wakati statements za kimahubiri zikitamkwa!
Wewe mwenzangu ni ahadi gani ya Gwajima umewahi isikia na kisha ikatekelezwa kwa vitendo?
Tuchangie kwa hoja tafadhali.