Je, unajua hata Ariel Sharon, kiongozi wa Israel, aliwahi itwa "bulldozer" na "lion of the God" kutokana na matendo yake?

Salary Slip

JF-Expert Member
Apr 3, 2012
47,014
144,372
Huyu aliwahi kuwa waziri mkuu wa Israel kati ya mwaka 2001 na 2006 kabla ya kulazimika kuondolewa madarakani baada ya kuugua kiharusi(stroke) mwezi March mwaka 2006.

Kwa kifupi, huyu bwana alipendwa sana na wayahudi mpaka wakampa hayo majina lakini alichukiwa sana na waarabu hasa kwa jinsi alivyokuwa akiwatendea wapalestina.

Huyu bwana mwaka 1982 wakati huo akiwa Waziri wa Ulinzi wa Israel, alifumbia macho mauji ya wakimbizi wa kipalestina huko Lebanoni ambapo wapalestina kati ya 800 mpaka 1200 waliuwawa na Wakiristo huku majeshi ya Israel yakitazama tu.

Hata hivyo, sijui ndio nguvu ya karma, kwani bwana huyu alikuja kuugua kiharusi na kusababisha awe kwenye "coma"kwa kipindi cha miaka 8 kuanzia January 2006 mpaka January 11, 2014 alipooaga dunia.

Kwa vyovyote vile itakavyotasiriwa,watawala dunia kote wana somo la kujifunza hapa kuwa hata wao wanaweza kupata mateso kama binadamu wengine waliowaumiza katika tawala zao na pengine kupata tabu na mateso makali zaidi ya yale waliyoyasabisha kwa binadamu wenzao.

Ni habari ya kusikitisha, kuhuzunisha na kuumiza sana ila bado tunapaswa kuitafakari kwa mapana yake maana huenda kuna somo kwa sisi ambao bado tuko hai hasa kwa wenzetu wenye madaraka katika hii dunia.
 
Hunaga off? Leo sikukuu ila bado unaenda ofisini(kupost jf), au Leo unavizia overtime? mboye atakubali kulipa Leo?
 
Hata hivyo,sijui ndio nguvu ya karma,kwani bwana huyu alikuja kuugua kiharusi na kusababisha awe kwenye "coma"kwa kipindi cha miaka 8 kuanzia January 2006 mpaka January 11,2014 alipooaga dunia
Hapana. Kilichopelekea kupata hiyo coma ni uamuzi wake wa kuwaondoa waisrael ktk mji wa Jerusalem alipokuwa waziri mkuu. Maana yake alikubaliana na matakwa ya wapalestina wakati huo yakichagizwa na Mahamoud Abbas (a.k.a Aboumazam). Hii iliwaudhi sana waisrael.
 
Hapana. Kilichopelekea kupata hiyo coma ni uamuzi wake wa kuwaondoa waisrael ktk mji wa Jerusalem alipokuwa waziri mkuu. Maana yake alikubaliana na matakwa ya wapalestina wakati huo yakichagizwa na Mahamoud Abbas (a.k.a Aboumazam). Hii iliwaudhi sana waisrael.
Ukosahihi sana Mkuu.
 
Sikia bwana salary,hakuna mtu duniani!hakuna hata mmoja ambaye hana madaraka ya kiutawala. Sawa? Mungu ametuumba tutawale sema tunatofautiana maeneo ya kutawala.Wengine familia,wengine vikundi,wengine,na wengine na wengine.hata kaka anatawala wadogo zake. Kwa maana hiyo hili lituhusu Mimi na wewe.
 
Reasoning ya Kipumbavu. Hayatollah,Papa n.k wapo ambao wamekufa kwa magonjwa kama hayo na zaidi. Kufa kila mtu atakufa kwa style yake.
 
Back
Top Bottom