Je, Unafahamu kuwa sio nchi zote husherekea Sikukuu ya Krismasi Desemba 25?

Je, Unafahamu kuwa sio nchi zote husherekea Sikukuu ya Krismasi Desemba 25?

Wont be the same

JF-Expert Member
Joined
Aug 15, 2024
Posts
1,564
Reaction score
2,483
Unafahamu sio nchi zote husherekea Sikukuu ya Krismasi Desemba 25?

Wakristo wengi wa Madhehebu ya 'Orthodox' nchini Urusi, Ulaya ya Mashariki pamoja na nchi zilizopo Mashariki ya Kati husherehekea Krismasi siku ya Januari 7, ambayo kwa Kalenda ya Julian ni sawa na Desemba 25. Huku Kanisa la Kitume la Armenia wao husherehekea Krismasi Januari 6.

Aidha, Nchini Mexico, shamrashamra za Krismasi huanza Desemba 16 ikiwa ni sherehe ya siku tisa inayoenzi safari ya Maria na Yosefu kutoka Nazareti hadi Bethlehemu kabla ya kuzaliwa kwa Yesu.

Pia, Nchini Hispania, msimu wa Krismasi huanza Desemba 8 kupitia maadhimisho ya wiki moja ya Sikukuu ya Mkingiwa Dhambi ya Bikira Maria 'Immaculate Conception'.
 
Asante,kwa taarifa,bokazi wanaumia moyoni kwanini xmass iko inasherekewa duniani kote.

Hakika amezaliwa,azaliwe mioyoni mwetu,ili tuipate amani ya kweli.
 
Back
Top Bottom