Je, Una Kipaji cha Utangazaji? Jinsi ya Kujiajiri Utayarishaji na Utangazaji Vipindi Vyako vya TV

Pascal Mayalla

Platinum Member
Sep 22, 2008
50,513
113,638
Wanabodi,

Mimi ni mwandishi wa habari wa kujitegemea, nikitayarisha vipindi vyangu vya TV na Redio na kuvitangaza kupitia vituo mbalimbali vya Televisheni, Redio na kusambaza habari kwenye Magazeti.

Kama una kipaji cha utangazaji, au hata bila kuwa na kipaji wewe lakini unataka kuanzisha production studio yako ya kuandaa vipindi vya Redio na TV, kuna fursa ya kutengeneza pesa, hivyo karibu nitakushauri humu jf bure.

Nakiri kupandisha uzi huu, kufuatia ombi la mwana jf huyu.
Pascal Mayalla Nimekuomba angalau unipe a, b, c za namna ya kuanzisha Kipindi binafsi cha TV Kama NgazkwaNgaz, hususani taratibu na gharama zake, lakini umenitosa mkuu - Najua wewe ni mzoefu wa media
Mkuu Mkaruka, ni kweli swali nililiona nikawa nakusubiria uulize, na hapa nimeliona tena, ila hujauliza, lakini kwa faida ya wengi, haya sasa naumwaga tuu huu mtama hapa jf.

Kuanzisha Kipindi Binafsi cha TV.

1.0 Kwanza uwe na wazo. Program Idea
Wazo au Program Idea ndio ndio utajiri mkubwa kuliko kitu chochote. Wazo ni kipindi kuhusu nini, maudhui ya kipindi, lenoo la kipindi ni nini?. Unataka kuonyesha nini, au watu waone nini?, jee hao watu wakiishaona hicho unachotaka kuonyesha, watapata nini?, habari, elimu, burudani, ushawishi, etc. Jee ni kipindi cha aina gani na kitaendeshwaje?.

2.0 Aina za Vipindi vya TV. Type of TV Program
Kuna aina nyingi za vipindi vya TV.
Kuna TV Documentary, TV Talk Show, TV Reality Show, TV VOX Pop, TV feature, TV Descriptive, TV Exhibition show, Live TV Broadcasting, Special TV Prog, TV Interview Prog. etc.

3.0 Mwendeshaji wa Kipindi/Mtangazaji. TV Presenter, Host, Anchor
Nani atakiendesha kipindi, Mtangazaji, kama ni wewe mwenyewe, jee una kipaji?, una uwezo?, una sauti?, unatazamika? (photogenic)

4.0 Mtayarishaji wa Kipindi /Producer
Nani atakitayarisha kipindi?, nani atakitengeneza kipindi?, yaani producers. Wako watayarishaji wa aina tatu.
4.1 TV Stations-
Vituo vya TV ndio wenye vifaa vyote vya production. Ukipeleka wazo lako kwenye TV yoyote wakiridhia TV hiyo wanaweza kukubali kuwa the producers wa kipindi chako na mkakubaliana kugawana mapato, wao watakitengeneza bure na kukirusha bure, kisha hiyo TV wakulipe wewe, au mgawane mapato.
Advantage: The easiest and the cheapest, unachohitaji wewe ni kuwa tuu na wazo la kipindi hata kama huwezi kutangaza, hiyo TV watakutafutia mtangazaji.
Disadvantage: Wazo linaweza kuibiwa, ama wanaweza kukulalia kwa kulipwa kiduchu, kisha wao ndio wakatengeneza faida.
Copyright ya Kipindi i ya TV Station, hicho lazima kirushwe na TV hiyo tuu wanayokutengenezea.

4.2 Production House/Studio.
Hizi ni makampuni ya production ambayo unapeleka wazo lako, wanakupa gharama za kukutengenezea kipindi chako, unawalipa, yaani unapewa production cost, unalipa wanakutengenezea kipindi chako. Bongo makampuni ya kutengeneza vipindi yako zaidi ya 100.
Advantage: Mkiisha kubaliana bei, kipindi kinakuwa ni mali yako na uko free kukirusha TV yoyote.
Disadvantage: Its an expensive exercise kwa sababu lazima kwanza uwe na fedha za kulipia hiyo production.

4.3 Own Production.
Hii ni baada ya kuwa na wazo, una invest kwenye vifaa, unakuwa una own a production yako mwenyewe kama mimi nilivyo na PPR.
Hivyo unatengeneza vipindi mwenyewe na kuamua utavirusha wapi. this is what I do.

Advantage: This is the best option, vipindi unatengeneza mwenyewe kwanza kwa kutafuta sponsor wa kugharimia production cost, na kuvilipia airtime cost, anakulipa wewe, kisha mwenyewe, una produce, unalipia airtime halafu pesa yote inayobakia inakuwa ni pesa yako.

Disadvantage: Its an expensive undertaking, lazima uwe na mtaji wa kununua vifaa na viko expensive, na lazima uwalipe watendakazi, ila sio lazima kuanza na kila kitu, unaweza kuanza na baadhi tuu ya vifaa vya muhimu, halafu vifaa vingine vyote ukakodisha, kila kifaa kinakodishika na gharama ni cheap kukodi kuliko kutumia pruduction house.

5.0 Vifaa vya Production.
Hivi ni vifaa muhimu kuwa navyo as Basic Equipments za Own Production

5.1 Professional Camera angalau 1 kwa kuanzia ila standard good production ni kamera 3 na kuendelea. Simple good camera ni Milioni 2, expensive ni hadi milioni 100
Kadri unavyotumia kamera nzuri, ndivyo kipindi kinakuwa kizuri zaidi. Kamera nzuri kwa Broadcast ya Tanzania ni Sony HDV ila hata SLR (hizi za still kama Canon na Nikon zina video na zinaweza), wenzetu sasa wako kwenye 4K quality, sisi bado tuko kwenye HD.
5.2 Uwe na Mic nzuri 500,000 - 2,000,000 (wireless)
5.3 Taa angalau 2, 100,000-500,000 (kwa kuanzia sio lazima sana mfano mimi vipindi vyangu vingi, navifanya nje kutumia natural light, mwanga wa jua ambao ni bure.
5.4 Editing bench ni computer ya kueditia hata any good laptop can do. Computer zinazoongoza kwa kupiga kazi ya production ni Mac (apple) ila hata Windows za kawaida zinaweza, kinachohitajika ni high specs tuu kwa upande wa graphic card
Apple Macbook Pro ya bei poa used ni 1.5 mkononi
Vifaa vyote vipya na used vinapatikana. Vyote vina faida zake na hasara zake.
Advantage and Disadvantage of New Equipments
Advantage:
Vifaa vipya vina faida moja, vina good quality, vina uhakika na vina guarantee, vitadumu kwa muda mrefu kabla ya kuchoka.
Disadvantage: Vifaa vipya ni kwanza ni ghali, they are expensive lakini pia getting the genuine ones ni changamoto!, vingi ya vifaa vya producton ni famba za kutoka China na Dubai hivyo havidumu.

Advantage and Disadvantage of Used Equipments
Advantage
: Vifaa used, vina faida mbili, kwanza bei yake ni cheap, pili ni vifaa genuine vya ukweli
Disadvantage: Havina guarantee na vingine vimetumika sana hadi kuchoka, hivyo unakaa navyo kidogo tuu vinachoka. technology yake imepitwa na wakati.
Yapo maduka ya vifaa vyote full iliwemo
1-Sony pale Samora.
2. Duka la Deo Filikunjombe pale NSSF Benjamin Mkapa Towers
3. AL Muntazil Mtaa wa Jamhuri.
4. Kuna duka Shoppers
5. Kuna duka Mlimani City
6. Kuna duka Quality Plaza
7. Arusha -Benson
8. Moshi-Bahsgwan
9. Mwanza-Barmedas
10. Dodoma kuna duka la Mchaga fulani Uhindini.

6.0 Gharama za Airtime, Airtime Cost
Ukifanikiwa kuanzisha studio yako na kutengeneza kipindi, ili kirushwe lazima kufanyike mambo matatu yafuatayo
6.1 Kipindi Kinunuliwe na TV Station.
Ukiishatengeneza kipindi chako, unawauzia TV Station, wao wanakupipa kiasi unachotaka na kukirusha kipindi, mapato yote ya kipindi chako ni mali ya TV Station.
Advantage: Kazi yako ni kuzalisha tuum yaani unauza kipaji, unakama fungu lako kwa ulaini.
Disadvantage: TV zetu zinatubania sana, watakulipa pesa mbuzi kisha wao ndio watazimake, ila TV za hapa wako radhi kulipia mamilioni kununua vipindi vya nje kuliko vya ndani.

6.2 Kipindi kirushwe bure na TV Stations Mgawane Mapato Co-production
Ukiisha tengeneza kipindi chako, unakipeleka TV Station kuomba kirushwe bure, kikipata wadhamini, mnagawana 50/50 na TV Stations
Advantage: Wewe unaingia ghara za kutayarisha tuu, halafu unaingiza fedha za udhamini.
Disadvantage: Ukitokea udhamini mnene, unawafaidisha TV Stations bure.

6.3 Ukirushe kwa Gharama zako.
Ukiisha tengeneza kipindi chako, unakilipia fully kukirusha kwenye TV Station
Advantage: Ukilipia kipindi, unaamua kitoke TV ngapi, unawalipa TV airtime yao wanakurushia, fedha zote ulizopata zinakuwa zako.
Disadvantage:You have to be good kupata mdhamini mzuri atakayelipa pesa za production, airtime na faida ukabaki.

Rates za Kurusha kipindi cha 30 min.
The cheapest ni TBC -TZS 2,000,000
The highest ni ITV -TZS 5,000,000
TV nyingine zote zina range hapo katikati

Ushauri kama huu niliwahi kuutoa kwa JF
Vipindi Maalum vya JF kwenye TV: Naomba Maoni Yako!
Thanks.

Pascal
Update
Mkuu Abtali Mwerevu, kitu muhimu kuliko vyote kama nilivyoeleza ni kuwa na idea, wazo, that is where money lies!.

Baada ya wazo, ndipo kinakuja kipaji, ukiwa na wazo, hata kama huna kipaji, unaliuza wazo lako, kwenye TV Stations, then wao ndio watatafuta hao wenye vipaji kuendesha kipindi chako.

Baada ya kutambua kipaji, ndipo sasa unakitafutia elimu ya utangazaji. Elimu ni kitu kinachofundishika, ila kipaji ni kitu ambacho mtu anazaliwa nacho, kikiendelezwa kwenye the right direction ndipo kinatengeneza pesa.

Vyuo vya uandishi wa habari, kila siku vinawapika mamia ya waandishi na watangazi, ila only wenye vipaji, ndio they make it kwenye fani, wakati mitaani kuna wenye vipaji kibao, ambao hawakubahatika kupata elimu ya utangazaji, mwisho wa siku vipaji vyao vinaishia kujifia bure!.

Paskali
Wanabodi huu ni msimu wa Saba Saba. Nimejitolea kutangaza fursa za utangazaji kwa Watanzania wenye vipaji vya Utangazaji. Kama unajihisi una kipaji cha Utangazaji wa Redio na TV, mimi nimejitolea kufanya screening bure kule kwenye viwanja vya Saba Saba. Unachotakiwa kufanya ni kuwa na Kiingilio chako kwenye Saba Saba. Zoezi la Screening litafanyika Siku ya Jumamosi Tarehe 8/7/2017 kuanzia saa 8:00 mchana ndani ya ofisi za PPR ambazo ziko ndani ya viwanja vya Maonyesho.

Paskali
 
Kwa Tsh 5,000,000 kwa 30 mins kuna uwezekezano kweli wa kuhimili pesa yote hiyo kwa mdhamini mmoja, ambayo ni zaidi ya 20,000,000Tsh kwa mwezi

Cc Pascal Mayalla
Wenye kuweza kuhimili budget hiyo ni mashirika makubwa tuu ndio yenye vipindi weekly 52 programs kwa mwaka kwenye 4 tv stations.

Ukiandika good program idea, sponsor anaweza kutoa hadi 50 m kwa mwezi.

Mimi wakati wa Saba Saba, narusha 10 programs za 30 minutes kwa muda wa siku 10, kwenye Vituo 7 vya TV na vyote navilipia. Pesa sio tatizo, taasisi zote zimetenga budget.

ITV, TBC, STAR TV, CHANNEL TEN, CLOUDS TV, AZAM TV na ZBC

Paskali
 
Paschal,

Ahsante kwa elimu hii.

Mimi nilikua najiuliza, makampuni (tv stations/redios) wanapata wapi fedha , leo ndio nimepata jibu.


Kwahio vijana wale wa ze comedy na orijino comedy, au hata wale wa startv,

Kwa makadirio wanakunja ngapi?
 
Mayalla Naomba kufahamu kwako wewe kama mwanahabari mwenye uzoefu katika mambo ya habari unaweza vipi kumsaidia mtu mwenye uwezo na elimu ya uandishi wa habari ?.

Licha ya hilo ili mtu awe mwanahabari mzuri anatakiwa awe na nini (kwenye ufahamu wake) je unaweza kumsaidia mtu kuwa na aina ya utangazaji ambao sio wake yaani wa kutengeneza?.

Mtangazaji mzuri ni yupi,yule mwenye kipaji asie na elimu au mwenye elimu asiye na kipaji?

Nitafurahi kama nitapata hayo majibu.
 
Paschal,

Ahsante kwa elimu hii.

Mimi nilikua najiuliza, makampuni (tv stations/redios) wanapata wapi fedha , leo ndio nimepata jibu.


Kwahio vijana wale wa ze comedy na orijino comedy, au hata wale wa startv,

Kwa makadirio wanakunja ngapi?
Television za Tanzania zinawanyonya sana hawa watu, Wote hao wanaweza kuwa wameajiriwa tu na hizo stations na wanalipwa mishahara
 
Wenye kuweza kuhimili budget hiyo ni mashirika makubwa tuu ndio yenye vipindi weekly 52 programs kwa mwaka kwenye 4 tv stations.

Ukiandika good program idea, sponsor anaweza kutoa hadi 50 m kwa mwezi.

Mimi wakati wa Saba Saba, narusha 10 programs za 30 minutes kwa muda wa siku 10, kwenye Vituo 7 vya TV na vyote navilipia. Pesa sio tatizo, taasisi zote zimetenga budget.

ITV, TBC, STAR TV, CHANNEL TEN, CLOUDS TV, AZAM TV na ZBC

Paskali
Kwani Mkuu Pascal Mayalla huwa unakuwa busy sana "throughout the year" au ni kipindi cha 7-7 tu, hakuna uwezekano wowote tukaaongea hata kwa baadaye ili tuone namna ya kulipush hili suala langu. Kama utakuwa na muda nijulishe ili nikutafute tuongee ( ingawa siyo karibuni ) baada ya kuliandikia proposal na kupata usajili au kama una ushauri mwingine pia niko tayari kusikiliza
 
mkuu unamaanisha kipaji cha utangazaji au elimu ya utangazaji?
Mkuu Abtali Mwerevu, kitu muhimu kuliko vyote kama nilivyoeleza ni kuwa na idea, wazo, that is where money lies!.

Baada ya wazo, ndipo kinakuja kipaji, ukiwa na wazo, hata kama huna kipaji, unaliuza wazo lako, kwenye TV Stations, then wao ndio watatafuta hao wenye vipaji kuendesha kipindi chako.

Baada ya kutambua kipaji, ndipo sasa unakitafutia elimu ya utangazaji. Elimu ni kitu kinachofundishika, ila kipaji ni kitu ambacho mtu anazaliwa nacho, kikiendelezwa kwenye the right direction ndipo kinatengeneza pesa.

Vyuo vya uandishi wa habari, kila siku vinawapika mamia ya waandishi na watangazi, ila only wenye vipaji, ndio they make it kwenye fani, wakati mitaani kuna wenye vipaji kibao, ambao hawakubahatika kupata elimu ya utangazaji, mwisho wa siku vipaji vyao vinaishia kujifia bure!.

Paskali
 
Wenye kuweza kuhimili budget hiyo ni mashirika makubwa tuu ndio yenye vipindi weekly 52 programs kwa mwaka kwenye 4 tv stations.

Ukiandika good program idea, sponsor anaweza kutoa hadi 50 m kwa mwezi.

Mimi wakati wa Saba Saba, narusha 10 programs za 30 minutes kwa muda wa siku 10, kwenye Vituo 7 vya TV na vyote navilipia. Pesa sio tatizo, taasisi zote zimetenga budget.

ITV, TBC, STAR TV, CHANNEL TEN, CLOUDS TV, AZAM TV na ZBC

Paskali
sabasaba ikifika nitakutafuta jirani nikushikie hata taa
 
Mayalla Naomba kufahamu kwako wewe kama mwanahabari mwenye uzoefu katika mambo ya habari unaweza vipi kumsaidia mtu mwenye uwezo na elimu ya uandishi wa habari ?.
Mkuu Rafaeli wa Ureno, kwanza kuwa na elimu ya uandishi wa habari ni jambo moja, na kuwa na uwezo, ni jambo jingine. Kazi ya elimu ni kukujengea uwezo, yaani ukielimika, unakuwa umejenga uwezo, ila kazi zinazohitaji kipaji cha ziada kama utangazaji, elimu pekee haiwezi kukufanya ukawa mtangazaji mzuri kama wewe mwenyewe huna uwezo huo, ndio maana unakuta kuna wasomi wazuri tuu kwenye fani, lakini katika utekelezaji ni mabomu tuu, na kuna watu wazuri mitaani wenye uwezo, lakini hawajengewa uwezo wa kielimu.

Namna pekee ya kujipima kama una uwezo, ni wakati wa field, unakwenda kwenye TV Station, Redio au Magazetini kufanyiwa majaribio, wenye uwezo, wanajulikana na wanachukuliwa!
Licha ya hilo ili mtu awe mwanahabari mzuri anatakiwa awe na nini (kwenye ufahamu wake) je unaweza kumsaidia mtu kuwa na aina ya utangazaji ambao sio wake yaani wa kutengeneza?.
Ili mtu awe mwanahabari mzuri, anatakiwa na pua, yenye uwezo mkubwa wa kunusa habari (nose for news). Hii nose for news ni shauku ya kupata habari, na kujua habari, ni kama umbea fulani, lakini tofauti ya habari na umbeya, habari ni shauku ya kuihabarisha jamii, na umbeya ni shauku ya kujua tuu mambo ya watu na kuyasambaza. Hiyo shauku ndio kipaji chenyewe, baada ya kuwa nacho, sasa ndio unakwenda shule ya habari kufundishwa namna ya kukitumia.
Mtangazaji mzuri ni yupi,yule mwenye kipaji asie na elimu au mwenye elimu asiye na kipaji?.
Mtangazaji mzuri ni yule mwenye kipaji na asiye na elimu, kwa sababu ukiishakuwa na kipaji, elimu inaweza kupatikana popote, kuanzia on job training kupata elimu kwa uzoefu tuu, lakini ukiwa na elimu tuu, lakini hauna kipaji, kipaji ni kitu ambacho hakifundishiki, ila kama ni mtu unayeupenda sana utangazaji, hata kama hauna kipaji, kupitia elimu, utafundishwa mpaka utakuwa mtangazaji wa kawaida, ila hautakuwa mtangazaji mzuri, ndio maana vituo vyote vya redio na TV, vina watangazaji wa kawaida na watangazaji wazuri, unapokuwa mtangazaji mzuri, unalipa, ndio maana kila uchao, vituo vinaibiana watangazaji wazuri, na hutakaa usikie mtangazaji wa kawaida ameibiwa!. The same applied kwa waandishi wazuri.
Paskali
 
sabasaba ikifika nitakutafuta jirani nikushikie hata taa
Bahati mbaya matangazo yote ya Saba Saba ni outdoor hayahitaji taa, ila hata ukinibebea betri tuu ya kamera, inalipa!, kuna sura zingine ukiandamana nazo, zina mvuto wa bahati!, si unashuhudia jinsi chama chetu kilivyo dorora siku za hivi karibuni, laki baada tuu ya kuingia sura mvuto, mara ghafla kimeng'aa, hata wasiokwendaga mpirani, sasa wamekwenda!, usifanya masikhaa na sura za mvuto!. Tena sisi wenye njaa, tunakula tuu kwa macho na tunashiba!.

Paskali
 
Mkuu Paskali naomba uni PM namba yako au naomba uni text kwenye namba yangu 0657-955825 nina jambo la msingi nahitaji kushea nawe idea.
 
Mkuu mayalaa nimekupata ninawazo la sport program hapa i will see big boss naiman pesa ipoo
 
Pascal naomba kuuliza japo ni nje kidogo!
Hivi hizi kampuni mama za TV zenye kumiliki matangazo Kama Star times, Ting nk je ninaweza kuwatumia wao nikamiliki station yangu ya TV ambapo wao wanakuwa wamiliki wa mitambo yao ya broadcast na Mimi nakuwa na studio yangu ya production? Kumbuka mfano TBC1, TBC2 je ingekuwepo TBC3,4,5 nk uendeshaji wao sii wanategemea production room tofauti lkn broadcast er ni mmoja? Naamini umenielewa!!
 
Back
Top Bottom