trachomatis
JF-Expert Member
- Jun 7, 2011
- 3,758
- 736
Wanafunzi wa shule ya sekondari Ndanda,iliyoko wilaya ya Masasi, wamefukuzwa shuleni jana. Hii ni pamoja na wanafunzi wa kidato cha sita! Sababu kubwa ni baadhi ya wanafunzi wa imani ya dini ya Kiislamu kutotimiziwa ahadi ya kujengewa nyumba yao ya ibada kwa muda mrefu sasa. Chanzo kinasema ilifikia hata 'parade' za 'assembly' asubuhi,wanafunzi wa imani hiyo,kuanza kujitenga na wenzao! Habari zaidi tutaendelea kujuzana..