Nijenge msingi kwanza! Rais Obama aliwahi kusema Africa inahitaji Strong institution tu kujikomboa. Kwa maneno mengine Taasis imara hususan za Dola.
Nije kwenye mada. Ukiwasikiliza Wahenga na simulizi zao na hata ndugu Polepole miezi ya karibuni utagundua kuwa katika uchaguzi wa kwanza wa vyama vingi mwaka 1995 ndani ya CCM baada tu ya mfumo wa vyama vingi kurejeshwa aliibuka mgombea mwenye nguvu ndani ya Chama aliyeitwa Bwana Jakaya Kikwete. Huyu alipambana na Bwana Benjamin Mkapa (Chaguo la Nyerere) kwa karibu kabisa.
Kutokana na kukosekana kwa Taasis Imara labda ilibidi Nyerere atumie ukubwa wake kumzima Kikwete. Nafikiri hapa ndipo kosa lilipofanyika. Nyerere alipaswa kuwaacha vijana wachuane na atakayeshinda ashinde wakadhibitiwe na Taasis imara huko mbele ya safari.
Kitendo Cha Nyerere kuingilia mchakato na kuchagua upande huku yeye akiwa Baba Taifa kiliacha chuki na uhasama wa kisiasa kati ya watoto wake wawili Kikwete na Mkapa (Huo ni ubinadamu kisaikolojia).
Ukiendelea na simulizi hizo za wahenga utagundua kuwa Kikwete hata kama alichukizwa aliamua kufuata mifumo ya kidemokrasia na kisiasa kuendelea mapambano yake. Ndipo likaibuka neno mtandao. Rostam Aziz alitetea vizuri dhana ya mtandao. Ni kama vile MAGA ya Sasa ya Rais Donald Trump.
Mtandao ulimwezesha Kikwete kushinda uchaguzi uliofuata baada ya Mkapa kumaliza awamu yake ya pili na Kikwete akawa Rais.
Kikwete alianza kuharibu kwa lengo la kujilinda kwa kuwaingiza wanamtandao na siasa zao kwenye Taasis za Dola. Kukaanza mambo ya unanijua Mimi nani!?
Kikwete akaweka mapandikizi hadi kwenye vyama vya upinzani hivyo siasa yetu ikaingia unafiki, Hila, gilba, na Sanaa. Ikawa kila chombo cha wapinzani wa Kikwete Cha wapinzani wake kupumulia kikawa na mamluki wanaolipwa pesa kwa mlango wa nyuma kuwa snitch wapinzani wa Kikwete.
Mambo ya nchi yakaanza kupelekwa kwa kujuana na nchi ikaanza kutoka kwenye kufanya kazi kimfumo na ki haki. Vikaanzishwa vyuo mpaka vya online. Kama unatakiwa unaambiwa katafute cheti tu ulete hata kama hukukaa darasani tutakupigania utachukua nafasi nzuri. PhD uchwara na degree uchwara zikaibuka nyingi na watu wakalamba vyeo.
Alipokuja Magufuli ambaye ni timu Mkapa/Nyerere na ambaye kisiasa na kwa kufuata mifumo kama kungekuwa na kura za wanachama au kampeni za primary Magufuli asingetoboa dhidi ya Lowassa, hili likatonesha majeraha ya zamani.
Wanamtandao wakawa optimistic na positive kuwa muda wa siasa za kujipanga umefika. Wakaanza harakati za mapema, lakini Magufuli ama kwa mawazo yake au kwa kushauriwa na Mkapa au yoyote akaanza kutumia nguvu na amri zake binafsi badala ya mifumo, Taasis na Sheria. Wanamtandao walipotaka kuutumia upinzani wa Tanzania kusukuma ajenda zao Magufuli akaushughulia upinzani. Badala ya siasa kuendeshwa kama vilabu vya mpira ikaanza kuendeshwa kama Dini au kiapo. Ikafika hatua hata kumtembelea mgonjwa wa chama kingine mtu anaogopa.
Utawala wa Magufuli ukambananga Kikwete huku Mkapa akishuhudia. Matokeo yake kibinadamu JK akaweka kisasi na kuanza harakati zake za kuwa KINYAGO NILICHOKICHONGA mwenyewe hakiwezi kunitisha. JK akawa akipata nafasi ya kuongea anarusha makombora.
Binafsi naamini tofauti za kisiasa na kirafiki kati ya Kikwete na Mkapa ziliongezeka sana kipindi cha Magufuli. Alipokufa Mkapa basi Magufuli alibaki bila mtu mwenye nguvu juu yake kama Mkapa alivyobaki bila Nyerere kwenye uongozi wake.
Kilichofuata hadi kufikia mwaka 2020 Magufuli akabakia mwenyewe ila akafunga mianya yoyote ya kisiasa ya kumng'oa au kumpinga. Wapinzani wake ndani ya CCM akawafukuza uanachama na vijana wake wakamkweza mno huku nae akimshambulia Kikwete ambaye alikuwa ni senior kwake na mwenye kujua siasa kuliko yeye maana alianza mapambano tangu na Nyerere wakati Magufuli akiwa mwalimu huko.
Katika harakati za Kikwete na timu yake kujipanga ndipo likaibuka neno WATOTO WA MJINI. Hawa wanajua kila mtu ni wazoefu wa mtaa na Dunia. Wanajua uchawi, uongo, gilba, Hila, wema, subira, fitina n.k wapo fit idara zote. Unavyotaka wewe na wao wanataka hivyo hivyo.
Alipofariki Magufuli wakati watu wanafikiria namna ya kupindua meza Makamu akatangaza msiba juu kwa juu.
Baada Samia kushika madaraka lile kundi la Nyerere na Mkapa na baadae Magufuli likaanza kulilia uhuru wa siasa ambao liliwanyima Wanamtandao. Wanamtandao nao wakaamua kuacha mifumo ya siasa na Sheria na kuamua kuwaendesha waliojiita Wazalendo kibabe kibabe kama na wao walivyokuwa wanawafanyia.
Walitekwa nao wakawateka, waliuliwa nao wakaamua kuwaua. Walizuiwa kuandamana nao wakawazuia, walicheza na Taasis na Sheria ili kukandamiza nao wakafanyiwa hivyo hivyo.
Mwisho wa picha Wazalendo pumzi ikawaishia wakaamua kutengeneza chaos. Siasa lazimishi matokeo yake ndio hayaaa wamekufa na waliokuwamo na wasiokuwamo.
Nafikiri haya yametokea kama namna ya Mungu kuwakumbusha wagombanao na washindanao wapatane maana wamekuja kufa wajukuu kisa ugomvi wa akina babu.
Kikwete umeshinda na wewe ndio Babu uliyebakia. Waachie wajukuu nchi yenye amani na upendo usifuate nyayo za JK mwenzako Nyerere kuachia watoto ugomvi.
Turudishe Taasis imara. Kutunishiana misuli hadi Balozi tumempoteza pamoja na wanasiasa wengi chipukizi wa upinzani
Nije kwenye mada. Ukiwasikiliza Wahenga na simulizi zao na hata ndugu Polepole miezi ya karibuni utagundua kuwa katika uchaguzi wa kwanza wa vyama vingi mwaka 1995 ndani ya CCM baada tu ya mfumo wa vyama vingi kurejeshwa aliibuka mgombea mwenye nguvu ndani ya Chama aliyeitwa Bwana Jakaya Kikwete. Huyu alipambana na Bwana Benjamin Mkapa (Chaguo la Nyerere) kwa karibu kabisa.
Kutokana na kukosekana kwa Taasis Imara labda ilibidi Nyerere atumie ukubwa wake kumzima Kikwete. Nafikiri hapa ndipo kosa lilipofanyika. Nyerere alipaswa kuwaacha vijana wachuane na atakayeshinda ashinde wakadhibitiwe na Taasis imara huko mbele ya safari.
Kitendo Cha Nyerere kuingilia mchakato na kuchagua upande huku yeye akiwa Baba Taifa kiliacha chuki na uhasama wa kisiasa kati ya watoto wake wawili Kikwete na Mkapa (Huo ni ubinadamu kisaikolojia).
Ukiendelea na simulizi hizo za wahenga utagundua kuwa Kikwete hata kama alichukizwa aliamua kufuata mifumo ya kidemokrasia na kisiasa kuendelea mapambano yake. Ndipo likaibuka neno mtandao. Rostam Aziz alitetea vizuri dhana ya mtandao. Ni kama vile MAGA ya Sasa ya Rais Donald Trump.
Mtandao ulimwezesha Kikwete kushinda uchaguzi uliofuata baada ya Mkapa kumaliza awamu yake ya pili na Kikwete akawa Rais.
Kikwete alianza kuharibu kwa lengo la kujilinda kwa kuwaingiza wanamtandao na siasa zao kwenye Taasis za Dola. Kukaanza mambo ya unanijua Mimi nani!?
Kikwete akaweka mapandikizi hadi kwenye vyama vya upinzani hivyo siasa yetu ikaingia unafiki, Hila, gilba, na Sanaa. Ikawa kila chombo cha wapinzani wa Kikwete Cha wapinzani wake kupumulia kikawa na mamluki wanaolipwa pesa kwa mlango wa nyuma kuwa snitch wapinzani wa Kikwete.
Mambo ya nchi yakaanza kupelekwa kwa kujuana na nchi ikaanza kutoka kwenye kufanya kazi kimfumo na ki haki. Vikaanzishwa vyuo mpaka vya online. Kama unatakiwa unaambiwa katafute cheti tu ulete hata kama hukukaa darasani tutakupigania utachukua nafasi nzuri. PhD uchwara na degree uchwara zikaibuka nyingi na watu wakalamba vyeo.
Alipokuja Magufuli ambaye ni timu Mkapa/Nyerere na ambaye kisiasa na kwa kufuata mifumo kama kungekuwa na kura za wanachama au kampeni za primary Magufuli asingetoboa dhidi ya Lowassa, hili likatonesha majeraha ya zamani.
Wanamtandao wakawa optimistic na positive kuwa muda wa siasa za kujipanga umefika. Wakaanza harakati za mapema, lakini Magufuli ama kwa mawazo yake au kwa kushauriwa na Mkapa au yoyote akaanza kutumia nguvu na amri zake binafsi badala ya mifumo, Taasis na Sheria. Wanamtandao walipotaka kuutumia upinzani wa Tanzania kusukuma ajenda zao Magufuli akaushughulia upinzani. Badala ya siasa kuendeshwa kama vilabu vya mpira ikaanza kuendeshwa kama Dini au kiapo. Ikafika hatua hata kumtembelea mgonjwa wa chama kingine mtu anaogopa.
Utawala wa Magufuli ukambananga Kikwete huku Mkapa akishuhudia. Matokeo yake kibinadamu JK akaweka kisasi na kuanza harakati zake za kuwa KINYAGO NILICHOKICHONGA mwenyewe hakiwezi kunitisha. JK akawa akipata nafasi ya kuongea anarusha makombora.
Binafsi naamini tofauti za kisiasa na kirafiki kati ya Kikwete na Mkapa ziliongezeka sana kipindi cha Magufuli. Alipokufa Mkapa basi Magufuli alibaki bila mtu mwenye nguvu juu yake kama Mkapa alivyobaki bila Nyerere kwenye uongozi wake.
Kilichofuata hadi kufikia mwaka 2020 Magufuli akabakia mwenyewe ila akafunga mianya yoyote ya kisiasa ya kumng'oa au kumpinga. Wapinzani wake ndani ya CCM akawafukuza uanachama na vijana wake wakamkweza mno huku nae akimshambulia Kikwete ambaye alikuwa ni senior kwake na mwenye kujua siasa kuliko yeye maana alianza mapambano tangu na Nyerere wakati Magufuli akiwa mwalimu huko.
Katika harakati za Kikwete na timu yake kujipanga ndipo likaibuka neno WATOTO WA MJINI. Hawa wanajua kila mtu ni wazoefu wa mtaa na Dunia. Wanajua uchawi, uongo, gilba, Hila, wema, subira, fitina n.k wapo fit idara zote. Unavyotaka wewe na wao wanataka hivyo hivyo.
Alipofariki Magufuli wakati watu wanafikiria namna ya kupindua meza Makamu akatangaza msiba juu kwa juu.
Baada Samia kushika madaraka lile kundi la Nyerere na Mkapa na baadae Magufuli likaanza kulilia uhuru wa siasa ambao liliwanyima Wanamtandao. Wanamtandao nao wakaamua kuacha mifumo ya siasa na Sheria na kuamua kuwaendesha waliojiita Wazalendo kibabe kibabe kama na wao walivyokuwa wanawafanyia.
Walitekwa nao wakawateka, waliuliwa nao wakaamua kuwaua. Walizuiwa kuandamana nao wakawazuia, walicheza na Taasis na Sheria ili kukandamiza nao wakafanyiwa hivyo hivyo.
Mwisho wa picha Wazalendo pumzi ikawaishia wakaamua kutengeneza chaos. Siasa lazimishi matokeo yake ndio hayaaa wamekufa na waliokuwamo na wasiokuwamo.
Nafikiri haya yametokea kama namna ya Mungu kuwakumbusha wagombanao na washindanao wapatane maana wamekuja kufa wajukuu kisa ugomvi wa akina babu.
Kikwete umeshinda na wewe ndio Babu uliyebakia. Waachie wajukuu nchi yenye amani na upendo usifuate nyayo za JK mwenzako Nyerere kuachia watoto ugomvi.
Turudishe Taasis imara. Kutunishiana misuli hadi Balozi tumempoteza pamoja na wanasiasa wengi chipukizi wa upinzani