Je, Tanzania ina uraia pacha?

Je, Tanzania ina uraia pacha?

Nevergive up

JF-Expert Member
Joined
Dec 24, 2024
Posts
372
Reaction score
574
Wakuu nina swali naomba ufafanuzi. Katika team yetu ya taifa ya mpira wa miguu(taifa starts ) kuna wachezaji wageni, kwa information wengine hawajui kiswahili vizuri na inasemekana wengine walizaliwa nje ila baba au mama ni Mtanzania ila mtoto kazaliwa nje.

Je, hii imekaaje hadi mtoto kuitwa ni Mtanzania hadi kufikia hatua ya kuchezea team ya taifa na ilihali kazaliwa nje?

Je, kuna uraia wa kurithi au uraia pacha? Au serikali imeamua kufumba macho jambo hili?

Je, kama ni kweli why watoto ambao wazazi walizaliwa Tanzania lakini mababu walitoka labda Burundi, Congo, Rwanda n,k wanateseka sana hata kupata documents ni ngumu sana kwa kigezo cha kwamba wao siyo watanzania?.
 
Nini kinaendelea mkuu hapo?
Ninachojua Mimi ni kwamba kwa mujibu wa Sheria ya nchi hii mtu yeyote haruhusiwi kuwa na uraia wa nchi nyingine.

Sasa nadhani hawa wachezaji wanaoichezea timu ya Taifa watakuwa wamepewa uraia wa nchi hii na kwamba hawana uraia wa nchi nyingine japokuwa sina uhakika si unaijua hii nchi?

Kingine ni kwamba ukiwa mtu maarufu kwa mfano msanii mchezaji n.k. inakuwa rahisi sana kupewa uraia wa nchi hii, kwa mfano miaka kadhaa iliyopita mchezaji Kibu Denis alipewa uraia wa Tanzania, kumbuka huyu jamaa wazazi wake walikimbolia Tanzania yeye akiwa na miaka kadhaa.

MUHIMU: Kama hujulikani katika Taifa hili basi utachelewa sana kupata haki yako.

Ni hayo tu mkuu.
 
Ni watanzania kama hawana uraia wala pass za nchi nyingine za walikozaliwa. Lakini, ukweli ni kuwa watu wengi wanazo pass za nchi nyingine na wakati huo wanaendelea kuwa na uraia wa Tanzania. Kuzaliwa nje ya nchi siyo shida.
Kwahiyo kuna ubaguzi baina ya nchi na nchi? Why Burundi,Congo,nk mtu anasakamwa?
 
Ninachojua Mimi ni kwamba kwa mujibu wa Sheria ya nchi hii mtu yeyote haruhusiwi kuwa na uraia wa nchi nyingine.

Sasa nadhani hawa wachezaji wanaoichezea timu ya Taifa watakuwa wamepewa uraia wa nchi hii na kwamba hawana uraia wa nchi nyingine japokuwa sina uhakika si unaijua hii nchi?

Kingine ni kwamba ukiwa mtu maarufu kwa mfano msanii mchezaji n.k. inakuwa rahisi sana kupewa uraia wa nchi hii, kwa mfano miaka kadhaa iliyopita mchezaji Kibu Denis alipewa uraia wa Tanzania, kumbuka huyu jamaa wazazi wake walikimbolia Tanzania yeye akiwa na miaka kadhaa.

MUHIMU: Kama hujulikani katika Taifa hili basi utachelewa sana kupata haki yako.

Ni hayo tu mkuu.
Mkuu huwezi kuzaliwa nchi fulani usiwe na documents za nchi hiyo. Mkuu je umaarufu na haki Tanzania kuna uhusiano gani?
 
Mkuu huwezi kuzaliwa nchi fulani usiwe na documents za nchi hiyo. Mkuu je umaarufu na haki Tanzania kuna uhusiano gani?
Yeah, kama ulizaliwa nje ya Tanzania ukataka kuchukua uraia wa Tanzania Kuna vigezo uanatakiwa kuwa navyo kwa mfano unatakiwa uwe umekaa hapa nchini kwa miakaa kadhaa (nadhani si chini ya miaka mitano), awe na tabia mzuri, n.k.

Katika hii nchi Kuna uhusiano mkubwa sana kati ya umaarufu na haki kwa sababu watu wanatuongoza wako very unprofessional, wanatumia sana hisia katika kufanya mambo, ndiyo maana katika nchi hii utasikia watu wanasema neno 'connection' wakimaanisha kupeana deals kwa kujuana na si kwa kuangalia uwezo.
 
Kwahiyo kuna ubaguzi baina ya nchi na nchi? Why Burundi,Congo,nk mtu anasakamwa?

Shida siyo ubaguzi. Idara ya uhamiaji imejaa rushwa na uozo mbaya sana. Kunae watu wana passport hadi za nchi tatu au nne na Tanzania ikiwa mojawapo.
 
Wakuu nina swali naomba ufafanuzi. Katika team yetu ya taifa ya mpira wa miguu(taifa starts )kuna wachezaji wageni kwa information wengine hawajui kiswahili vizuri na inasemekana wengine walizaliwa nje ila baba au mama ni Mtanzania ila mtoto kazaliwa nje.je hii imekaaje hadi mtoto kuitwa ni Mtanzania hadi kufikia hatua ya kuchezea team ya taifa na ilihali kazaliwa nje? Je kuna uraia wa kurithi au uraia pacha? Au serikali imeamua kufumba macho jambo hili? Je kama nikweli why watoto ambao wazazi walizaliwa tz lakini mababu walitoka lbda Burundi,Congo, Rwanda n,k wanateseka sana hata kupata documents ni ngumu sana kwa kigezo cha kwamba wao siyo watanzania?.

Hao wachezaji ni "Watanzania" kwa sababu ya kuwa na vinasaba na Tanzania tokea kwa wazazi wao, hivyo wanapata haki ya kuchagua taifa la kuchezea endapo tu hawajawahi chezea taifa jingine kwenye mashindano ya wakubwa...

Fuatilia sheria za FIFA zinazoelezea uhusiano wa kuchezea taifa fulani na asili ya vinasaba kwa wachezaji waliozaliwa na wazazi wa nchi mbili tofauti, au aliyezaliwa ardhi tofauti na nchi ya ukazi n.k...

Nukuu...
"players must be able to demonstrate a "clear connection" to a country that they had not been born in but wished to represent. This ruling explicitly stated that, in such scenarios, the player must have at least one parent or grandparent who was born in that country, or the player must have been resident in that country for at least two years."
 
Huko ni kutaka mafanikio ya harakaharaka hata kwa kuvunja sheria za nchi. Timu ina mpaka wazungu, machotara, sijui wamezaliwa wapi wale wageni. Nchi itengeneze wachezaji wake iache kudandiadandia vipaji vya nje na kuvipa nafasi timu ya taifa. Haya sasa mbona hawajaleta mafanikio walau timu ifike hatua ya pili? Hiyo ni tamaa kutamani raia wa nje kuja kuchezea timu ya taifa wakati wapo watanzania wenye vipaji ila hawaendelezwi!
 
Kwa ujinga ujinga, rushwa na kupuuzwa kwa sheria za nchi, sitoshangaa hata kidogo kusikia kuna mtanzania ana uraia wa nchi nyingine na bado anao uraia wa Tanzania.
 
Kwa ujinga ujinga, rushwa na kupuuzwa kwa sheria za nchi, sitoshangaa hata kidogo kusikia kuna mtanzania ana uraia wa nchi nyingine na bado anao uraia wa Tanzania.
Inasikitisha sana Mkuu mnyonge anakosa haki yake kuna watu hapo nchini babu zao walitoka nje nyingine kama Burundi kipindi kile cha vita 1972 lkn wajukuu wao hadi leo wanaonekana siyo watanzania hata kupata documents kama nida,passport nitatizo je nchi hii why hivi?
 
Huko ni kutaka mafanikio ya harakaharaka hata kwa kuvunja sheria za nchi. Timu ina mpaka wazungu, machotara, sijui wamezaliwa wapi wale wageni. Nchi itengeneze wachezaji wake iache kudandiadandia vipaji vya nje na kuvipa nafasi timu ya taifa. Haya sasa mbona hawajaleta mafanikio walau timu ifike hatua ya pili? Hiyo ni tamaa kutamani raia wa nje kuja kuchezea timu ya taifa wakati wapo watanzania wenye vipaji ila hawaendelezwi!
Ni bora wahalalishe tu uraia pacha. Mkuu uhamiaji wanasema kuzaliwa Tanzania siyokigezo cha wewe kuwa mtanzania na kuzaliwa nje hii ni kigezo tosha kwamba wewe siyo mtanzania. Nimeona nikashuhudia unakuta mtu Alizaliwa Uganda na wazazi watanzania na ana cheti cha kuzaliwa lkn uhamiaji wanamwambia yeye siyo mtanzania ,je hii imekaaje?
 
Utanzania wao umekuja kivipi mkuu na wakati wamezaliwa nje?
Wazazi wao watanzania.
Kasome vizuri sheria.
Ipo hivi, ili uwe raia wa Tanzania lazima uzaliwe na raia wa Tanzania.
Siyo alzima uzaliwe ardhi ya Tanzania.
Pia unaweza kuomba uraia na hapa shariti uukane uraia wa nchi yako ya kuzaliwa.
Kama umezaliwa Tanzania na wazazi siyo raia wa Tanzania basi wewe siyo raia wa Tanzania.
Ipo hivyo kwa sheria zetu.
Ndiyo maana wahamiaji na wakombozi wakizaa watoto Tanzania bado watoto wao siyo raia wa Tanzania.
Kumbuka sheria hizi za uraia au uhamiaji zinatofautia kati ya nchi moja na nyingine.
Kwa Marekani ukizaliwa nchini kwao tu una sifa ya uraia wa Marekani hata Kama wazazi wako siyo raia wa Marekani. Nadhani England ipo vivyo hivyo.
 
Hao wachezaji ni "Watanzania" kwa sababu ya kuwa na vinasaba na Tanzania tokea kwa wazazi wao, hivyo wanapata haki ya kuchagua taifa la kuchezea endapo tu hawajawahi chezea taifa jingine kwenye mashindano ya wakubwa...

Fuatilia sheria za FIFA zinazoelezea uhusiano wa kuchezea taifa fulani na asili ya vinasaba kwa wachezaji waliozaliwa na wazazi wa nchi mbili tofauti, au aliyezaliwa ardhi tofauti na nchi ya ukazi n.k...

Nukuu...
"players must be able to demonstrate a "clear connection" to a country that they had not been born in but wished to represent. This ruling explicitly stated that, in such scenarios, the player must have at least one parent or grandparent who was born in that country, or the player must have been resident in that country for at least two years."
Hiyo nisheria ya FIFA,je sheria ya nchi inasemaje? Mkuu usiongee tu hivi unajua kama kuna watu wanateseka kwa jambo hili?
Yeah, kama ulizaliwa nje ya Tanzania ukataka kuchukua uraia wa Tanzania Kuna vigezo uanatakiwa kuwa navyo kwa mfano unatakiwa uwe umekaa hapa nchini kwa miakaa kadhaa (nadhani si chini ya miaka mitano), awe na tabia mzuri, n.k.

Katika hii nchi Kuna uhusiano mkubwa sana kati ya umaarufu na haki kwa sababu watu wanatuongoza wako very unprofessional, wanatumia sana hisia katika kufanya mambo, ndiyo maana katika nchi hii utasikia watu wanasema neno 'connection' wakimaanisha kupeana deals kwa kujuana na si kwa kuangalia uwezo.
Je kama ulizaliwa Tanzania na babu zako walitoka nje wewe utakuwa wa nchi gani?
 
Wakuu nina swali naomba ufafanuzi. Katika team yetu ya taifa ya mpira wa miguu(taifa starts ) kuna wachezaji wageni, kwa information wengine hawajui kiswahili vizuri na inasemekana wengine walizaliwa nje ila baba au mama ni Mtanzania ila mtoto kazaliwa nje.

Je, hii imekaaje hadi mtoto kuitwa ni Mtanzania hadi kufikia hatua ya kuchezea team ya taifa na ilihali kazaliwa nje?

Je, kuna uraia wa kurithi au uraia pacha? Au serikali imeamua kufumba macho jambo hili?

Je, kama ni kweli why watoto ambao wazazi walizaliwa Tanzania lakini mababu walitoka labda Burundi, Congo, Rwanda n,k wanateseka sana hata kupata documents ni ngumu sana kwa kigezo cha kwamba wao siyo watanzania?.
Ngoja nimwambie kijana wangu wa kidato cha pili aje akujibu hili swali dogo kabisa linalokushinda. Inaonekana wakati wenzako wanasoma uraia ulikuwa busy na manati kuwinda ndege na kucheka kamari huku ukivizia wenzako wakitoka muongozane wote ili ionekane na wewe ulikuwa shule.
 
Back
Top Bottom