Je, Tanzania bado ni nchi ya Amani?

Je,unadhani huu utulivu uliopo nchini(na kamwe si amani) kwa karibu nusu karne sasa umetusaidia sisi watanzania hasa ukizingatia uchumi tulionao ukilinganisha na maliasili za nchi?

Je,unadhani utulivu huu ni faida kwa mtanzania wa kawaida au ni faida kwa watawala?

Je,unadhani utulivu huu utaendelea kudumu kwa miaka mingine 50?

Kwa mtazamo wako,je utulivu huu ukitoweka wakulaumiwa ni watawala au mtanzania wa kawaida?

Je,si kweli kuwa walioko mstari wa mbele kuhubiri amani ndio hao hao vinara wa kuvuruga amani?

Hivi mlala hoi huwa anachakupoteza amani inapotoweka?

Naombeni majibu.
 
Je,unadhani huu utulivu uliopo nchini(na kamwe si amani) kwa karibu nusu karne sasa umetusaidia sisi watanzania hasa ukizingatia uchumi tulionao ukilinganisha na maliasili za nchi?

Je,unadhani utulivu huu ni faida kwa mtanzania wa kawaida au ni faida kwa watawala?

Je,unadhani utulivu huu utaendelea kudumu kwa miaka mingine 50?

Kwa mtazamo wako,je utulivu huu ukitoweka wakulaumiwa ni watawala au mtanzania wa kawaida?

Je,si kweli kuwa walioko mstari wa mbele kuhubiri amani ndio hao hao vinara wa kuvuruga amani?

Hivi mlala hoi huwa anachakupoteza amani inapotoweka?

Naombeni majibu.


Amani sio swali la kuuliza... utakuwa mpumbavu... JUST LOOK AROUND YOURSELF... Hapo Ulipo ni wangapi wanafika NYUMBANI kwao kwa familia zao salama??? that's what MATTER --- AMANI haipimiki...

Mshukuru JK NYERERE and move on buddy...


c.c
Salary Slip
 
Ni suala tete ukijaribu kutafsiri neno AMANI. Mimi siamini kama kweli tanzania kuna amani ila tanzania kuwa USHWARI wa aina fulani. Nchi imetawaliwa na chama kimoja na kudhibitiwa kwa vyombo vya utawala. Laiti amani ingelikuwepo, tusingekuwa na malumbano ya katiba wala harakati za kutia watu ndani kwa shutuma zisizo fahamika. Amani haipo katika udikteta. Amani itakuwepo pale tutapokuwa na demokrasia ya ukweli, uwazi na "accountability".
 
Amani sio swali la kuuliza... utakuwa mpumbavu... JUST LOOK AROUND YOURSELF... Hapo Ulipo ni wangapi wanafika NYUMBANI kwao kwa familia zao salama??? that's what MATTER --- AMANI haipimiki...

Mshukuru JK NYERERE and move on buddy...


c.c
Salary Slip
Hivi wewe amani na utulivu ni kitu kimoja?

Watanzania wana amani au utulivu?

Katika nchi ambayo madaktari wanagoma na wagonjwa wanakufa kuna amani au utulivu?

Kaika nchi ambayo wafanyakazi wanalalamikia mishahara duni na kodi kubwa kuna amani hapo au ni utulivu tu?

Katika nchi ambayo tofauti ya kipato kati ya masikini na matajiri inakua kila kukicha hapo pana amani au ni utulivu?

Katika nchi ambayo wengine wanalipwa 300,000 kwa siku na mwingine 270,000 kwa mwezi kuna amani hapo au ni utulivu tu?

Je,unaweza kujenga taifa lenye amani kama hakuna haki na usawa?

Hivi huku si kujidanganya tu?
 
Hivi wewe amani na utulivu ni kitu kimoja?

Watanzania wana amani au utulivu?

Katika nchi ambayo madaktari wanagoma na wagonjwa wanakufa kuna amani au utulivu?

Kaika nchi ambayo wafanyakazi wanalalamikia mishahara duni na kodi kubwa kuna amani hapo au ni utulivu tu?

Katika nchi ambayo tofauti ya kipato kati ya masikini na matajiri inakua kila kukicha hapo pana amani au ni utulivu?

Katika nchi ambayo wengine wanalipwa 300,000 kwa siku na mwingine 270,000 kwa mwezi kuna amani hapo au ni utulivu tu?

Je,unaweza kujenga taifa lenye amani kama hakuna haki na usawa?

Hivi huku si kujidanganya tu?

Amani na Utulivu ????

amani ni nini na utulivu ni nini jamani ???
 
KUHUSU AMANI TANZANIA..

SOURCE: GLOBAL PEACE INDEX REPORT

Tanzania imeporomoka kutoka nafasi ya 55 kufikia nafasi ya 59 Kati ya nchi 162 kwa Amani Duniani.

Tanzania inatajwa kuwa ni nchi ya 6 Afrika kwa Amani.

Hata hivyo Tanzania inatajwa kua ni nchi ya Kwanza kwa Amani Afrika Mashariki.
 
Amid the Covid-19 pandemic, I am trying to find anwers and hence the search of what 'has transpired' similary as to " wahenga walisema" since "we dare talk openly" I thought I should bring back some of the un answered questions and some question that may have answers now...
I came across this thread and my thinking is its relevance in this trying times to our Nation.
I have posed a question recently..."is this pandemic political?
Why I asked? Kuna baadhi wanaotumia jangamizi hili tauni kuchafua hali ya kisiasa? Je...amani tuliyonayo inatuunganisha kupambana na tauni hili?
The subject matter sums it all
Amani,
Mungu ibariki Tanzania
Mungu ibariki Afrika
Mchana mwema!
 
Je, nchi yetu bado ni nchi ya amani?


Tanzania no longer heaven of peace?


IBRAHIM JOHN
Dar es Salaam
ThisDay

WHEN I read our dailies with headings like RC shoots a daladala driver to death; Tanzanian ambassador steals 2bn/-; BoT made false payment of 133bn/-; Tanzania pays 152m/- daily for a fake Richmond power deal; Zanzibar in everlasting political crisis; Overpriced radar from Britain; Controversial Presidential jet; Demolition of houses; Fake TICTS deal; Buzwagi, Kiwira, Tangold, Meremeta, Reception parties for corrupt leaders, and the list goes on and on - I get convinced that there is a very thin line between insanity and whatever we call peace here in the once heaven of peace.

If peace exists in our nation, then this makes me wonder if peace is really a good philosophy of life! I think we are missing something, somewhere. We do need to seriously re-examine ourselves. Someone once said: You should examine yourself daily. If you find faults, you should correct them. When you find none, you should try even harder. Our problem is that we quit examining ourselves many years ago. So we see no fault. We dont even know the last time we experienced peace as a people. Its time we examined ourselves as a nation.

Otherwise I would suggest we get into the Guinness world Book of Records for becoming the first nation in the whole wide world to have co-existence of injustice and peace.

I, however, think that its just confusion of words. What we call peace is the absence of war, which is not necessarily peace, for peace is not a relationship of nations. It is a condition of mind. By the way Im not sure if the Wanchari have stopped fighting the Wakira in Tarime!

But since we need peace I think we need to work for it. Dr Martin Luther King, Jr. was quoted as saying, Those who love peace must learn to organize as well as those who love war. We as Tanzanians need to be honest to ourselves. We need to organize ourselves as peace-loving people as well as war-lovers.

Pope Paul VI said If you want peace, you must work for justice. Justice is our biggest challenge. We need to work for it. But because of lack of functional law enforcement system we need to work even harder for justice and organize ourselves better.

Otherwise Im really afraid of the future of this nation. And until we get a capable partial law enforcement system, I suggest we be creative. I suggest we adopt George Carlins idea of using signs. He said there are a lot of signs for minor offences and infractions. And they seem to work pretty well.

When people read signs like "Thank you for not smoking"; "Please wait in line" etc they do just that.

Why then dont we have signs that say Murder Strictly Prohibited; or No Raping People and something like Thank you for not conducting business in the State House. Signs are good. Im sure we can use those for a while until we have a good law enforcement system.

mailto: ijwerrema@ijwerrema.info

Kwani.kuna vita wapi mpaka pasiwe na amani?
Mnatembea mpausiku kucha bila kusikia risasi bado unauliza?
 
Kesaboso...
Vita unayofikiri wewe haipo. Usikurupuke. Naelewa ukurupukaji, kwani nami huwa nafanya hivyo, kwa kujua au kwa ujinga. Vyote hivi ni "kukurupuka"
Vita ya COVID-19 ipo.
Amani
 
Wanabodi..
Natumai mnaendelea vizuri na kushiriki kikamilifu kwenye zoezi la upigaji kura sambamba na kuwachagua viongozi wetu wapya kwa kipindi cha miaka mitano ijayo.

Nimeamua niandike uzi huu na kwa kuazima mashairi yanayopatikana kwenye wimbo wa kwaya ya AICT MAKONGORO VIJANA CHOIR.

Vijana hawa waliimba huu wimbo ambao ukiusikiliza na kuutafakari vizuri unasadifu kinachoendelea muda huu kwenye zoezi zima la uchaguzi.

Kama mjuavyo,ndani ya zoezi la uchaguzi ndipo mataifa ya nnje yasiyo na nia njema na Tanzania yanapotumia chance (nafasi) kama hii kuvuruga Amani,Umoja na Mshikamano wa Kitaifa.

Naungana na Mamlaka zilizochukua jukumu la kuzima Huduma ya Internet toka juzi na kudhibiti mitandao ya kijamii kama tweeter,Whatsapp,Telegram,Facebook n.k

Inafahamika toka uchaguzi uliopita wa mwaka 2015, mitandao ya kijamii imetumika sana katika kutaka kuvuruga Umoja,Mshikamano na Amani ya nchi.

Tumeona ma-champion wa mtandaoni kina Kigogo na wengineo ambao wametumia mitandao hii kuchochea vurugu kwa kigezo cha kuwahabarisha wananchi.

Kwa namna moja hawa watu walifikia hatua hata ya kuandaa maandamano kwa kutumia mitandao ya kijamii huku wao wakiwa mbali na Tanzania.

Kwa kuangalia mapema kwenye uchaguzi huu unaona kabisa kulikua na uchochezi wa makusudi wa kuvuruga amani na kuchochea vurugu hasa kwenye kipindi hiki cha uchaguzi.

Tumeona ndugu Amsterdam anavyokesha kuandika maandiko na waraka kuhusu uchaguzi wakati haumuhusu,tumeona vibaraka wengi hata wa hapa Tanzania wakitumia mitandao hii hii kuchochea vurugu na chuki kati ya wananchi na serikali yao.

Tanzania kuwa na amani miaka yote mpaka kuitwa "Kisiwa cha Amani" hili haliwafuhishi mabeberu na watu wasioitakia mapenzi mema hii nchi .

Mpaka Serikali kupitia mamlaka zake imeamua kufikia maamuzi ya kuzima huduma hii ya internet ni dhahiri inapenda welfare' (ustawi) wa raia wake hasa kipindi hiki.

Kumbuka siku moja inatosha kabisa kuipoteza Amani..lakini miaka ,miezi itapotea ili KUITAFUTA Amani.

Vikao na vikao vitakaa kuitafuta hii Amani.

Kweli Tupoteze Amani yetu kwa ajili ya uchaguzi wa siku moja??

Tuipoteze Amani yetu na tumwage damu kwa ajili ya Mitandao ya kijamii na Propaganda za chuki toka kwa wasioipendea mema Tanzania??

Kwa hili naungana na serikali katika kusitisha huduma hii ya Internet na ni Uamuzi mzuri katika suala zima la kuitunza Amani..

Jamani,vuruga kwengine lakini usivuruge Amani.

Chezea kwengine lakini Usichezee Amani.

Na watanzania hatuko tayari na hatutakua tayari kuona Amani yetu ikitikiswa na watu wasiotakia mema kama akina Amsterdam.

Najua wengine watasema wamepata hasara kwenye biashara zao au kwenye mambo yao mengine sababu tu huduma hii imesitishwa lakini wakumbuke kama Amani ikiondoka hawataweza fanya hizo biashara zao .

Amani ndo kila kitu na hongera sana Serikali na mamlaka zake kwa kuweka mbele utaifa na kuilinda Amani yetu kwenye kipindi hiki ambacho Mataifa mengi watataka kuivuruga Tanzania.

Lakini hawataweza ivuruga Tanzania maana asilimia 90 ya namna ya kuivuruga Tanzania ni kupitia mitandao ya kijamii ambayo imedhibitiwa hivyo imekula kwao.

Amani yetu tuilinde,Maana kuipoteza Amani ni Rahisi sana na ni Vigumu kuirudisha Amani...

Chezea Pengine lakini usichezee Amani,Vuruga kwengine lakini usivuruge Amani.

Uchaguzi mwema na MUNGU ibariki Tanzania.

Kwa maoni au ushauri :
godjohn8@gmail.com
 
Wanabodi..
Natumai mnaendelea vizuri na kushiriki kikamilifu kwenye zoezi la upigaji kura sambamba na kuwachagua viongozi wetu wapya kwa kipindi cha miaka mitano ijayo.

Nimeamua niandike uzi huu na kwa kuazima mashairi yanayopatikana kwenye wimbo wa kwaya ya AICT MAKONGORO VIJANA CHOIR.

Vijana hawa waliimba huu wimbo ambao ukiusikiliza na kuutafakari vizuri unasadifu kinachoendelea muda huu kwenye zoezi zima la uchaguzi.

Kama mjuavyo,ndani ya zoezi la uchaguzi ndipo mataifa ya nnje yasiyo na nia njema na Tanzania yanapotumia chance (nafasi) kama hii kuvuruga Amani,Umoja na Mshikamano wa Kitaifa.

Naungana na Mamlaka zilizochukua jukumu la kuzima Huduma ya Internet toka juzi na kudhibiti mitandao ya kijamii kama tweeter,Whatsapp,Telegram,Facebook n.k

Inafahamika toka uchaguzi uliopita wa mwaka 2015, mitandao ya kijamii imetumika sana katika kutaka kuvuruga Umoja,Mshikamano na Amani ya nchi.

Tumeona ma-champion wa mtandaoni kina Kigogo na wengineo ambao wametumia mitandao hii kuchochea vurugu kwa kigezo cha kuwahabarisha wananchi.

Kwa namna moja hawa watu walifikia hatua hata ya kuandaa maandamano kwa kutumia mitandao ya kijamii huku wao wakiwa mbali na Tanzania.

Kwa kuangalia mapema kwenye uchaguzi huu unaona kabisa kulikua na uchochezi wa makusudi wa kuvuruga amani na kuchochea vurugu hasa kwenye kipindi hiki cha uchaguzi.

Tumeona ndugu Amsterdam anavyokesha kuandika maandiko na waraka kuhusu uchaguzi wakati haumuhusu,tumeona vibaraka wengi hata wa hapa Tanzania wakitumia mitandao hii hii kuchochea vurugu na chuki kati ya wananchi na serikali yao.

Tanzania kuwa na amani miaka yote mpaka kuitwa "Kisiwa cha Amani" hili haliwafuhishi mabeberu na watu wasioitakia mapenzi mema hii nchi .

Mpaka Serikali kupitia mamlaka zake imeamua kufikia maamuzi ya kuzima huduma hii ya internet ni dhahiri inapenda welfare' (ustawi) wa raia wake hasa kipindi hiki.

Kumbuka siku moja inatosha kabisa kuipoteza Amani..lakini miaka ,miezi itapotea ili KUITAFUTA Amani.

Vikao na vikao vitakaa kuitafuta hii Amani.

Kweli Tupoteze Amani yetu kwa ajili ya uchaguzi wa siku moja??

Tuipoteze Amani yetu na tumwage damu kwa ajili ya Mitandao ya kijamii na Propaganda za chuki toka kwa wasioipendea mema Tanzania??

Kwa hili naungana na serikali katika kusitisha huduma hii ya Internet na ni Uamuzi mzuri katika suala zima la kuitunza Amani..

Jamani,vuruga kwengine lakini usivuruge Amani.

Chezea kwengine lakini Usichezee Amani.

Na watanzania hatuko tayari na hatutakua tayari kuona Amani yetu ikitikiswa na watu wasiotakia mema kama akina Amsterdam.

Najua wengine watasema wamepata hasara kwenye biashara zao au kwenye mambo yao mengine sababu tu huduma hii imesitishwa lakini wakumbuke kama Amani ikiondoka hawataweza fanya hizo biashara zao .

Amani ndo kila kitu na hongera sana Serikali na mamlaka zake kwa kuweka mbele utaifa na kuilinda Amani yetu kwenye kipindi hiki ambacho Mataifa mengi watataka kuivuruga Tanzania.

Lakini hawataweza ivuruga Tanzania maana asilimia 90 ya namna ya kuivuruga Tanzania ni kupitia mitandao ya kijamii ambayo imedhibitiwa hivyo imekula kwao.

Amani yetu tuilinde,Maana kuipoteza Amani ni Rahisi sana na ni Vigumu kuirudisha Amani...

Chezea Pengine lakini usichezee Amani,Vuruga kwengine lakini usivuruge Amani.

Uchaguzi mwema na MUNGU ibariki Tanzania.

Kwa maoni au ushauri :
godjohn8@gmail.com
Huu mwandiko ni wa Polepole a.k.a Mzee kijana
 
Nitajie Nchi mojawapo hapa duniani ambayo wananchi wake walivuruga amani kwa makusudi tu?!! Bila sababu!! Siku zote viongozi wa serikali ndio uwa wanavuruga amani kwa kuminya haki!! Pasipo na haki hakuna amani!!
Nchi nyingi zinazo heshimu haki demokrasia na uhuru wa watu, uwezi kusikia wananchi wanalalamika!! Viongozi hasa hawa ngozi nyeusi wanahubiri amani uku wanaua wananchi wasio na hatia!! Halafu wanasema mtunze amani!!! Wakati wenyewe wameshindwa kulinda uhai wa binadamu wenzao kisa utamu wa madaraka!! Biblia ina sema akitawala Kiongozi wa haki Nchi ustawi!! Akitawala Kiongozi mbaya wananchi unyong'onyea na kufa!! Miaka mitano maisha ya watanzania yamekuwa ya hofu kuu!! Watu wako magerezani bila kusikilizwa!! Watu wametekwa!! Watu wamepotea hawajulikani walipo!! Watu wameuawa na kufungwa kwenye viroba!! Watu wamepotea risasi na kujeruhiwa bila sababu!! Iyo yote ni kazi ya shetani!! Halafu unasikia mawakala wa shetani wanakuja wanasema msivuruge amani uku yana mabomu na damu mikononi!!! Unaua waafrika na watanzania wenzako ili uzidi kutawala!!! Tuwaogope mawakala wa sheitwani!!
 
Back
Top Bottom