Je, Tanzania bado ni nchi ya Amani?

Mimi nadhani hapa JK anakosea kitu kimoja. Watu wa kuwaonya ni viongozi wa serikali ambao kila siku hukimbilia vyombo vya habari kuzungumza ulevi wao kana kwamba pale ni mahala pa kuuzwa mchemsho..
Ni busara kwa JK kuwaonya viongozi wake kwanza kuheshimu wadhifa waliopewa na kutumia maneno ya busara wanapowakilisha hoja laa sivyo vyombo vya habari vitaendelea kuchimba zaidi kutafuta ukweli wa vita baina ya wahusika..ambao kwa bahati mbaya ni viongozi wetu na toka chama kimoja.

JK Kwake yeye vyombo vya habari vibaya ni vile vinavyofichua maovu ya viongozi,vinavyopambana na rushwa,mafisadi n.k.Hapa wa kulaumiwa ni yeye mwenyewe na kama kutatokea machafuko uko mbeleni mtu wa kulaumiwa ni yeye kwa kukaa kimya na kutochukua hatua kwa maovu yanayofichuliwa na vyombo hivyo vya habari Kama sio vyombo vya habari tusingejua mikataba mibovu Richmund,Buzwagi,bandari,Reli ,Rada,Mereremeta,EPA mpasuko iliomo CCM n.k.Kwa mtu makini kawa mh.Rais JK ningelipenda kabla ya kutamka mambo hayo angelitoa pongezi kwa vyombo vya habari na waandishi wa habari kwa kazi kubwa walio ifanya na waendelea kuifanya kupambana na maovu hayo kabla ya kulaumu.Ndiyo kunavyombo vya habari ambavyo ni vya hao hao mafisadi vinatumika kupakana matope.Najua ni vigumu kwa JK kuvipongeza vyombo vinavyopigana na ufisadi kwa sababu maovu yote vilivyoyafichua JK hajachukua hatua yoyote kuyatatua.Mh JK vyombo vya habari ni kioo cha jamii ni mahala ambapo wewe na viongozi wote mjitazame na mjione mlivyo Kuvunja kioo hicho sio suluhisho.Mfichaficha maradhi kilio kitamfichua!MUNGU IBARIKI TANZANIA.
 
Mimi nadhani hapa JK anakosea kitu kimoja. Watu wa kuwaonya ni viongozi wa serikali ambao kila siku hukimbilia vyombo vya habari kuzungumza ulevi wao kana kwamba pale ni mahala pa kuuzwa mchemsho..
Ni busara kwa JK kuwaonya viongozi wake kwanza kuheshimu wadhifa waliopewa na kutumia maneno ya busara wanapowakilisha hoja laa sivyo vyombo vya habari vitaendelea kuchimba zaidi kutafuta ukweli wa vita baina ya wahusika..ambao kwa bahati mbaya ni viongozi wetu na toka chama kimoja.
.

Mkuu Mkandara.
Nafikiri wapiganaji wetu ndiyo wananongoza kwa kuvitumia vyomba vya habari kwa kupotesha ukweli mwingi sana.

1.Utasikia- mimi mti mkavu hauchimbwi dawa-Majira

2.Nilitaka kuchomwa kisu Jimboni kwangu-Nipashe

3.Sereli-awanyamazisha Lowasa na RA.

4.Mkuu wa mkoa wa mbeya ni mc wa mafisadi na mambo mengi sana.

Ndiyo maana Mwakyembe aliwatukana hao wandishi wa habari.wanakunywa chai ya Bunge ,bila kulipia
 
- Yaani huyu amesahau Mtandao walivyokuwa wanatutisha wakati wanatafuta power 2005, kwamba wasipopata nchi haitakalika na yale magazeti yao kama Tazama, walipowatuma wale viongozi wa zamani kupita nchi nzima wakimchafua Salim haikuwa kuvuruga amani, ila sasa baada ya kuanza kushindwa kuongoza ndio amegundua kuwa waandishi ndio wachawi badala ya kujialumu na uongozi wake mdhoofu?

- Nchi ikishakuwa na vacuum katika uongozi wa juu, then ni rukhsa kwa anybody kujiingilia na kuwa a decision maker, walianza kina Pengo na waraka, mafisadi na NEC, sasa imekua sadakarawe,

- Anayehatarisha amani ni yeye na uongozi wake mdhooofu, ajiangalie yeye kwanza then wasaidizi wake wote! Wa-Tanzania tulijkiongoza under Mwinyi for ten years, hatuwezi kushindwa sasa, kama hawezi aachie ngazi uhuru wa waandishi ulikuwepo kabla yeye hajaingia na yeye ameutumia kwa 100% kupata urais, na utaendelea kuwepo!

Anyways, later wakuu Spika yuko intown tukapate dataz huko!

Respect.

FMEs!
 
The telltale totalitarian tone, tampering and twiddling with tools of Tiananmen, taunts Tanzanians to see the highhanded henchman Hammurabi decreeing daily doses of draconian derelictions.

Kikwete hata anapoweza kuwa na pointi, anaibungle katika his standard four delivery, and in politics, the delivery is part of the message.
 
Vyombo vya habari na waandishi huwa ni vizuri unapovitumia kama ngazi kufanikisha malengo yako ya kisiasa, na waandishi wanakuwa ni marafiki zako wakubwa, kwa kula nas kunywa nao huku ukiwafungashia vile vibrown envelopes, lakini vyombo hivyo hivyo vinapokuja kukushukia kwa maroroso unayoyafanya, ndipo vinageuka mwiba na waandishi wanageuka maadui wako.

Lazima tukubali to take the bitter with the seeter kwenye tasnia ya habari.
 
- Spika yuko intown tukapate dataz huko!

Respect.

FMEs!

Nimemuona kwenye picha na Na Mabalozi Palham na Mahiga, naamini atawaeleza jinsi RA anavyofanyiza hadi yeye kujikuta amekalia kuti kavu, masikini JK kwa RA haambiwi kitu, hata ile almanusura ya Sitta kwenye NEC, sio kwa sababu wanampenda sana, bali wanalinda tuu chama kisimeguke. Pesa! kweli shetani!.
 
Alichoeleza Mh JK ni kuwa waandishi wachunge maadili ya uandishi na kuacha ushabiki.
 
Alichoeleza Mh JK ni kuwa waandishi wachunge maadili ya uandishi na kuacha ushabiki.

Mkuki mtamu kwa nguruwe,

Alivyowatumia kina Nchimbi kumpaka matope Salim grossly wakati wa campaign alikuwa anajali maadili ya uandishi?
 
Alichoeleza Mh JK ni kuwa waandishi wachunge maadili ya uandishi na kuacha ushabiki.
Sasa hivi ndio amelijua hilo? Mambo haya ya kuchafuana na kuandika uzushi kayaanzisha yeye mwenyewe na mtandao wake 2005. Yanamrudia anaanza mikwara, ameanzisha ugonjwa ambao yeye hana tiba yake.
 
Atoe mfano wa hizo habari zinazohatarisha amani ya nchi. Kama magazeti yanaandika kuhusu ufisadi halafu yeye anaona yanahatarisha amani ya nchi, basi we have a very serious problem! Anachotakiwa kufanya yeye ni kuchukua hatua dhidi ya mafisadi badala ya kuendelea kucheka nao. Na hii itam-cost vibaya sana.
 
Hapa mimi naona kuna mpango au mkakati wa kushughulikia magazeti yanayoiumbua serikali ya JK. Na it seems is so close. Hivyo basi muheshimiwa najaribu kufore-neutralize the issue ili wakianza utekelezaji aje aseme niliwaambia.......wht a cheap shot! Dd some one said raia mwema somewhere in here??????? smells like it!
 
Hakuna wanahabari wanaovuruga amani, ila amani inavurugwa na mafisadi ambao wanawanunua wanahabari ili waandike yale wao wanataka yaandikwe.

JK ukitaka kulinda amana washughulikie mafisadi na amani itakuwepo tena ya kudumu.
 
- Ukiona panafuka moshi ujue chini kuna moto, Rais ajifunze kutoka kwa kina Obama, na hapa JF yaani hoja hujibiwa kwa hoja,

- Waandishi wetu huwa wanaandika hoja hata kama finyu, sasa na yeye ajibu hoja zao moja after another sio kuleta hivi viroja vya kutishia media nzima kwa sababu ya kushindwa kwake kujibu hoja zao,

Mheshimiwa Rais, please jibu hoja zao na hoja zijibiwe kwa hoja, sio vitisho na viroja!

Respect.


FMEs!
 
Imeandikwa na Mwandishi Maalum,
Rome, Italia;
Tarehe: 18th November 2009
Habari Leo

RAIS Jakaya Kikwete amerudia kuvionya vyombo vya habari nchini visitumie uhuru wao kuvuruga amani na kuvunja umoja wa kitaifa.

Rais Kikwete amesema, endapo vitafanya hivyo Serikali haiwezi kuviacha,vitashughilikiwa.

Sanjari na onyo hilo, Rais Kikwete amesema, Serikali itaendelea kulea na kudumisha uhuru wa vyombo vya habari.

Lakini Rais Kikwete amesema,vyombo vya habari lazima vijirekebishe,vitimize wajibu ambao ni sehemu muhimu ya uhuru huo wa habari.

“Kama nilivyowaambia pale Musoma majuzi wakati wa kuadhimisha miaka 10 ya kifo cha Mwalimu Nyerere, huu hauwezi kuwa uhuru wa kuvunja taifa, uhuru wa kugawa watu, uhuru wa kuchochea maasi na ugomvi kati ya dini mbalimbali, kati ya makabila, kati ya watu wenye rangi mbalimbali”

Alisema “Baadhi ya vyombo vyetu havina wajibu kabisa. Vinachochea maasi ya kuvunja nchi na kuleta mfarakano kati ya watu wetu. Vinajaribu kugawa watu wetu, kugawa mataifa yetu na kusababisha maafa makubwa. Hatuwezi kuvumilia vyombo vya habari vya namna hiyo vinavyotumia uhuru kuleta balaa kwa watu.”


Alafu January Makamba na Zitto wanasema kuwa raisi anaruhusu uhuru wa habari. Kikwete sio mvumilivu ila ni kwa vile alikuwa anataka kusafiri nchi za ulaya na marekani basi akaamua kuachia kidogo. Sasa hivi ziara zake zimeanza kupungua unaona haya yote yakitokea.
 
RAIS Jakaya Kikwete amerudia kuvionya vyombo vya habari nchini visitumie uhuru wao kuvuruga amani na kuvunja umoja wa kitaifa.

Rais Kikwete amesema, endapo vitafanya hivyo Serikali haiwezi kuviacha,vitashughilikiwa.

Sanjari na onyo hilo, Rais Kikwete amesema, Serikali itaendelea kulea na kudumisha uhuru wa vyombo vya habari.

Lakini Rais Kikwete amesema,vyombo vya habari lazima vijirekebishe,vitimize wajibu ambao ni sehemu muhimu ya uhuru huo wa habari.

“Kama nilivyowaambia pale Musoma majuzi wakati wa kuadhimisha miaka 10 ya kifo cha Mwalimu Nyerere, huu hauwezi kuwa uhuru wa kuvunja taifa, uhuru wa kugawa watu, uhuru wa kuchochea maasi na ugomvi kati ya dini mbalimbali, kati ya makabila, kati ya watu wenye rangi mbalimbali”

Alisema “Baadhi ya vyombo vyetu havina wajibu kabisa. Vinachochea maasi ya kuvunja nchi na kuleta mfarakano kati ya watu wetu. Vinajaribu kugawa watu wetu, kugawa mataifa yetu na kusababisha maafa makubwa. Hatuwezi kuvumilia vyombo vya habari vya namna hiyo vinavyotumia uhuru kuleta balaa kwa watu.”
http://www.habarileo.co.tz/kitaifa/?n=4449
 
Wapenzi wana jamii,
Mimi binafsi sielewi kabisa dhana hii ya amani.
watu huzungumzia amani lakini sijui uwepo wa amani unapimwaje.
Kwa mfano kisiasa mataifa mengi husema Nchi ya Tanzania ni nchi ya amani.
Hivi kipimo cha amani ni kipi?
Je amani sii kitu ambacho kiko ndani ya moyo wa mtu?Amani huletwa na Mungu au mazingira?
Mtu binafsi si ndo anapaswa kujua kama ana amani au la?
Au kipimo cha amani ni kipi?
 
Pole Asha,
Nakuona kama mgeni japo hujabisha hodi, ila nikutie moyo kuwa mada yako ni nzuri sana.
Mimi sina jibu kwa sasa ila nikuhakikishie kwamba hapa JF (jamii forum) utapata majibu.Mimi mwenyewe nimesaidiwa sana hapa.Changia hoja za watu pia.
Kaa mkao wa kula Asha.
 
Back
Top Bottom