tweenty4seven
JF-Expert Member
- Sep 21, 2013
- 15,672
- 19,187
Huwezi kua na kichwa kikubwa ukawa na akili,hiki kichwa kimejaa topeeeNimesoma kitu kinachoitwa TAARIFA KWA UMMA iliyotolewa na Tume ya Taifa ya uchaguzi, iliyosainiwa na Mkurugenzi wake Dkt Mahera, tarehe 27/11/2020, naomba maswali yafuatayo uyajibu Dkt Mahera:-
1. Katika taarifa yako kwa Umma umedai kuwa ulipokea majina hayo ya wabunge wa viti maalum, toka kwa Katibu Mkuu wa Chadema, John Mnyika, tarehe 19/11/2020, je taarifa hiyo ilikuwaje iwe na jina la Nasrat Hanje, ambaye alitolewa gerezani rumande, usiku wa tarehe 23/11/2020 kwa amri ya DPP, Biswalo Mganga, ambako Jeshi lenu la Polisi lilimbambikia kesi ya kukusanyika bila kibali na kutompa dhamana pasipo halali, ambapo alikaa rumande kwa siku 133?
2. Tunakuomba Mkurugenzi wa uchaguzi, Dkt Mahera uutangazie Ulimwengu "kama ubavu huo utakuwa nao" kuwa kauli tuliyosikia kutoka kwa Katibu Mkuu wa Chadema aliyoitoa kwenye kikao na waandishi wa habari hapo tarehe 25/11/2020 kuwa form zenu za Tume ya uchaguzi, alikuwa nazo ofisini kwake zikiwa hazijajazwa hata kidogo na kuwa form hizo hazijatumwa kwenye Tume yenu ya uchaguzi, kuwa ilikuwa ni kauli ya uwongo?
3. Iweje Bunge la Jamhuri la Muungano, chini ya Spika wake Job Ndugai na Katibu wake, Kigaigai, wakiuke kanuni zake yenyewe na kuwaapisha "kisiri siri" tena kwenye eneo nje ya Bunge wabunge hao wa viti maalum, wakati kanuni zinawataka ni LAZIMA tendo hilo lifanyike rasmi ndani ya Jengo la Bunge, kwa kuwa tendo hilo siyo la unyago, ambalo lingehitaji usiri mkubwa?
4. Iweje Spika wa Bunge, Job Ndugai anukuliwe kwa kutoa taarifa kuwa Bunge lake litawalinda kwa gharama zozote wabunge hao wa viti maalum wa Chadema, kama ambaye anajua kuwa uapishwaji wao ulikuwa batili?
5. Iweje Mkurugenzi wa uchaguzi Dkt Mahera usitoe taarifa hiyo nyeti mapema, hadi ungojee sakata hilo la wabunge wa viti maalum wa Chadema, li-trend sana kwenye social media na usubiri chama kikuu cha upiinzani nchini Chadema, kiitishe kikao chao cha dharura cha Kamati Kuu ya Chama chao kuwajadili hao ambao mmewahalalisha kuwa wabunge wateule wa viti maalum?
Kama Dkt Mahera amethubutu kutupa taarifa za uongo kuhusiana na suala la kuapishwa kwa wabunge wa viti maalum wa Chadema, tunawezaje kumuamini kwa taarifa aliyotupa ya matokeo ya uchaguzi mkuu uliopita, ambayo kwa mujibu wake kuwa Rais Magufuli alipata ushindi wa kishindo wa zaidi ya kura milioni 12 ambayo ni zaidi ya asilimia 84 ya kura zote zilizopigwa nchini?
Naomba hayo maswali machache unijibie Mkurugenzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Dkt Mahera ili kuondoa huu utata mkubwa uliogubika zoezi hili zima la kuwaapisha hao wabunge wa viti maalum wa Chadema.