Kwani wewe unavyojua ibilisi historia yake ikoje?? Au unabisha bisha hovyo vitu usivyovijua?
Ibilisi ni jini ambaye alikuwa akiishi na malaika
sasa maswali yangu ndio nikayapanga kama ifuatavyo
1)Wazazi wake ni nani na nani?
2)Ndugu zake ni akina nani?
3)Anatokea katika aina/koo ipi ya majini?
4)Uzao wake ulianzaje anzaje?
5)Kama ikiwa binadamu wa kwanza kuumbwa alikuwa Adamu, je jini wa kwanza kuumbwa ni nani?
Wakuu, Ibilisi ni jina kila linapotajwa linachanganya watu sana na hasa pale linapofungamana na majina kama Malaika na Majini na Nabii Adam as,.
Kwani wewe unavyojua ibilisi historia yake ikoje?? Au unabisha bisha hovyo vitu usivyovijua?
Ibilisi ni jini ambaye alikuwa akiishi na malaika
sasa maswali yangu ndio nikayapanga kama ifuatavyo
1)Wazazi wake ni nani na nani?
2)Ndugu zake ni akina nani?
3)Anatokea katika aina/koo ipi ya majini?
4)Uzao wake ulianzaje anzaje?
5)Kama ikiwa binadamu wa kwanza kuumbwa alikuwa Adamu, je jini wa kwanza kuumbwa ni nani?
Kumekuwepo na mkanganyiko mkubwa hasa kati ya majina haya Ibilisi, Shetani Jini na malaika.
Tuanze na Ibilisi, neno hili pamoja na hayo mengine yana asili ya lugha ya kiarabu (au asili ya lugha za Semitic).ukifungua kamusi la lugha ya kiarabu W. Lane, tunakuta mzizi wa neno Ibiliis (إبليس) ni Iblis (إبلس ikiwa na maana zifuatazo (tafsiri):-
(1) Mazuri au mema yake yameshuka au kupungua.
(2) Ameacha matumaini au amekata tamaa ya rehema za Mungu.
(3) Amevunjika moyo katika imani na ni muombolezaji.
(4) Alitahayari na hakuweza kuona njia yake.
(5) Alikuwa au alishikwa na ukimya kutokana na huzuni au kukata tamaa.
(6) Alikatwa kauli au kunyamazishwa katika hoja.
(7) Hakuweza kufanya safari yake.
(8) Alizuiwa kufikia haja yake.
Hizo ndizo tafsiri za mzizi wa neno Ibiliis, kwa muktadha huo, kama neno hilo litachukuliwa katika msingi wa dini basi linakukuwa na maana za kisifa (attributive name), yaani ni Yule ambaye mwenye sifa za kutokuwa na wema na aliyeachwa na butwaa njiani na mwenye kukata tamaa na rehema za Mungu.
Ibilisi anahusiana katika kisa kimoja na Nabii Adamu katika (Qur'an),pia ukisoma unakuta Ibliis alikuwa Jini, hapa shida nyingine inaibuka, je, Jini ni kitu gani?, kama ilivyokuwa katika neno Ibliis, Jini ni neno la kiarabu au (Semitic) lenye maana ya kitu kidichoonekana kwa macho ya kawaida (nakef eyes) na katika hali hiyo kitu chochote kikipewa jina hilo lazima kitakuwa na sifa ya kutoonekana kirahisi na hata baadhi ya watu katika jamii wamepewa sifa ya jini kwa sababu tu hawaonekani, hawapatikani au hawachangamani na jamii kirahisi na hata wataalamu wakubwa wa fani fulani katika taaluma nao kisifa wanaitwa majini (Genious), pia wadudu wadogo sana kama Bakteria, virusi,Amoeba,paramecium,nk wote hao wanaitwa majini kwa kiarabu,pia majoka na wanyama wanaoishi katika misitu minene ambako ni shida kwa watu kufika nao pia wanaitwa majini.
Kuna visa vimezoeleka kwamba ile hali inayowakumba akina mama na akina Dada wanapokuwa katika hali fulani katika miili yao eti, ni majini!!, hali ile inaitwa kitaalamu Hysteria na wala si kitu kinachoitwa jini kinatoka mahali fulani na kumuingia kichwani mtu.
Nabii Adamu alikuwa mtu wa kwanza kupokea ufunuo kutoka kwa Mungu na Ibiliis aliambiwa amsaidie (kumtii) katika kazi ya Mungu naye akakataa kwa sababu alikuwa na majivuno kwa sababu yeye alikuwa ni jini yaani mtu mkubwa basi Mungu akamlaani kwa kukosa utii.
Hivyo Ibiliis anatoa taswira ya Maibilisi wengi ambao walipatikana na wataopatikana katika kupinga kazi za Manabii.
Mkuu Hance Mtanashati, kwa kufupi hiyo ndiyo falsafa ya Ibiliis na sio vinginevyo nadhani maswali yako nitakuwa nimekujibu ukisoma kwa makini hayo maelezo.