Nani ni mtawala wa ulimwengu huu, Mungu au Shetani?

Undava King

JF-Expert Member
Aug 11, 2017
3,205
5,332
Biblia ina andiko la wakati Mungu akimpa Adam mamlaka ya dunia, Adam anashindwa kuitii amri ya Mungu na hatimaye anaishia kumkabidhi mamlaka hayo shetani.

Quran inasema "isipokuwa kwa wajakazi (wafuasi) wangu (shetani) hauna mamlaka yeyote juu yao, isipokuwa kwa wale wanaokufuata(wanaokutii)

Tunaona katika vitabu hivi viwili vya imani kuwa shetani amepewa mamlaka juu ya watu wa Mungu kwa sababu ya dhambi.

Je, maandiko yanasemaje kuhusiana na Mungu kuwa ndiye mmliki au mtawala wa ulimwengu huu.

Yesu anasema "mamlaka yote nimekabidhiwa mimi, mbinguni na duniani" mathayo 28:18

Katika sala ya Bwana ndani ya mathayo 6:13 inaishilia na mstari huu "...kwa kuwa ufalme ni wako na nguvu na utukufu, milele, amina! (Andiko hili limewekwa kwenye mabano katika toleo la biblia ya NASB na limeondolewa katika NIV, RSV na ESV)

Waefeso 1:20-22 inasema "Akamwinua kutoka katika mauti na akamweka mkono wa kulia.....na akaweka kila kitu chini ya miguu yake"

Daniel 4:17, 25, 26, mara tatu inatuambia "Aliye juu zaidi uongoza ufalme wa binadamu na umpa yeyote amtakaye"

2 wakolosai 20:6 inathibitisha "Ewe Mwenyezi Mungu wa baba zetu, je siye Mungu wa mbinguni? Na utawalaye falme zote hata za wapagani? Na katika mkono wako je hakuna nguvu na uwezo, kiasi hakuna hawezae kuhimili?"

Je, maandiko yanasemaje kuhusiana na Shetani kuwa mtawala au mmliki wa ulimwengu huu?

Luka 4:6, Shetani akamjaribu Bwana Yesu jangwani, shetani akamwambia Yesu kuwa ufalme wote wa duniani ni wangu na nampa yeyote yule nimtakaye. (Kumbuka kauli hii ni kinyume na Daniel 4:17,25,26)

Mathayo 4:4 shetani akaahidi kumpa kristo utawala wa dunia kama zawadi ya kumwinamia na kumwabudu.

Tuangalie katika matoleo kadhaa ya biblia tukianza na NIV "Dunia iko chini ya utawala wa mwovu"
Warumi 12:9, NKJV, NASB katika mathayo 5:37 na 6:13, Holman standard, ESV (vitabu vyote vinathibitisha kuwa shetani ndiye "Mtawala wa ulimwengu" Yohana 12:31,14:30 na 16:11)

Yohana 14:30 Sitosema tena mengi nanyi kwa sababu mtawala wa dunia hii anakuja. Yeye hana uwezo juu yangu.

Yohana 12:31-33 "Wakati wa Mungu kutamka hukumu juu ya ulimwengu imetimia, huu ni wakati ambao shetani, MTAWALA WA DUNIA hii, 'ATAPINDULIWA' nami nitakapoinuliwa kutoka ardhini nitawavuta watu wote waje kwangu.

Waefeso 2:1-3 Ninyi mlikuwa mmekufa kwa sababu ya dhambi zenu. Na hata sisi sote tulikuwa kama wao;tuliishi kufuatana na mtindo mbaya wa ulimwengu huu, MKAMTII MTAWALA WA PEPO WENYE NGUVU WA ANGA, pepo ambao hutawala sasa watu wasiomtii Mungu. Na hata sisi sote tulikuwa kama wao;tuliishi kufuatana na tamaa zetu za kidunia na kufanya mambo yale yaliyo ipendeza miili na akili zetu ila dunia, sisi kama vile pia wao, tulistahili ghadhabu ya Mungu.

Waefeso 6:12-13 Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya nyama na damu, bali dhidi ya falme, mamlaka, dhidi ya WAKUU WA GIZA NA MAJESHI YA PEPO WABAYA katika ulimwengu wa kiroho.

Tunaona pia kuwa hata malaika mkuu Mikaeli mamlaka yake haizidi ile ya shetani, Yuda 1:9 kwamba hata ' Mikaeli malaika mkuu, katika ule ubishi na ibilisi juu ya mwili wa musa, Mikaeli akuthubutu kumshitaki kwa kumlahumu bali alisema, Bwana na akukemee.

Yesu mwenyewe alimwita shetani 'mtawala wa ulimwengu' Yohana 16:11

Ni wazi kuwa kulingana na maandiko haya, shetani ana mamlaka katika dunia. Na mifumo ya ulimwengu mzima inaendeshwa kulingana na design alizoamua. (Angalia tena, waefeso 2:2)

Ndiyo maana wenye kuiamini hekima toka kwa Mungu wanaonekana kama wajinga na waliopotoka kwa sababu mtizamo wao ni tofauti kabisa na hekima ya kiulimwengu. (1wakorintho 1:21-25)

Shetani utawala juu ya mifumo ya ulimwengu na Biblia inathibitisha hili kwa kukazia "Je hamtambui kuwa rafiki wa dunia ni adui wa Mungu? Yeyote atakaye kuwa rafiki wa dunia ujifanisha mwenyewe kuwa adui wa Mungu (James 4:4)(1 Yohana 2:15) inaamuru" usipende ulimwengu au vitu vyake, endapo mtu atapenda ulimwengu, upendo wa baba hautokuwa nae; kwa sababu adui wa Mungu ni MTAWALA WA ULIMWENGU.

Kama haitoshi katika Quran shetani kuonesha mamlaka na uwezo wake anamwakikishia Allah kuwa "Nitawaendea uso kwa uso, na kwa kutokea nyuma, na kutokea kulia na kwa kutokea kushoto" (I shall approach them head on and from behind and from the right and from the left)

Kulingana na ushahidi wa maandiko matakatifu hayo hapo juu yamhusuyo Mungu na Shetani toka katika pande zote mbili,

1. Wewe kama mwamuzi, toa jibu lako na sababu kuwa nani ni mtawala halisi wa ulimwengu huu?

2. Ikiwa unadhani shetani ndiye mtawala wa ulimwengu, Je ni haki kuishi kinyume nae kwa kutii amri za mamlaka nyingine?

3. Ikiwa unadhani Mungu ndiye mtawala wa ulimwengu, Je ni haki kuendelea kumshtumu shetani aliye ndani ya mamlaka yake?
 
Mkuu wa ulimwengu huu ni shetani , Mungu alimkabidhi kisheria , hata hvyo utawala wake sio kamili sababu si wote wanaomtii shetani na hili ndo linamuumiza kichwa mwamba

Kwahiyo unamaanisha kuwa Mtawala wa awali (Mungu) alimkabidhi mtawala mpya (shetani)ulimwengu autawale lakini hakuridhika kumwachia mamlaka yote ndiyo maana shetani anapata ukinzani toka kwa wafuasi wa Mungu?

Na vipi katika siku ya hukumu kwa sababu shetani ni mshtakiwa unafikiri Mungu atashinda kesi ilihali hata shetani naye kuna namna ameingiliwa/kawekewa vikwazo na Mungu kwenye utawala wake?
 
YESU NDIYE MWENYE MAMLAKA LAKINI SHETANI NDIYE MTAWALA.


MATHAYO 28:18.

18 Yesu akaja kwao, akasema nao, akawaambia, Nimepewa mamlaka yote mbinguni na duniani.

19 Basi, enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa jina la Baba, na Mwana, na Roho Mtakatifu.

20 na kuwafundisha kuyashika yote niliyowaamuru ninyi; na tazama, mimi nipo pamoja nanyi siku zote, hata ukamilifu wa dahari.
Mathayo 28:20

YESU NDIYE MWENYE MAMLAKA LAKINI SHETANI NDIYE MTAWALA
 
Inafikirisha, unaposema ulimwengu huu unamaanisha hii dunia au ulimwengu wa mwili na wa roho kwa ujumla? Je shetani ana nguvu na utawala rohoni au huku duniani? Au kote?

Ana utawala Kote, kiroho na kimwili, ndiye mtawala wa 'Dunia' na ndiye mfalme wa 'Anga', ndiye mtawala wa 'Giza', Kumbukeni vita vyetu si vya damu na nyama bali dhidi ya majeshi ya 'Kiroho' yanayoongozwa na shetani.

Na yeye ndiye fundi aliyedizaini dunia tuionayo na kuipenda kwa maana aipendaye dunia na anasa zake (binadamu kuwa na urafiki na dunia) anamchukiza Mungu, kwa kuwa mtawala wa ulimwengu huu ni adui wa Mungu.
 
Shetani ni mtawala wa Dunia SI ulimwengu, ulimwengu ni dude kubwa ambalo limebeba kadunia sehemu ndogo sana, pia shetani Hana kitu chochote ni mtupu kama binadamu tu akuja na chochote tofauti na nguvu , shetani ni kibaka tu alimpora Adamu hati miliki ya Dunia Kwa uzembe wa adamu ndio maana anaitwa mwizi na muhongo.

Pia sisi wanadamu duniani sio kwetu kwetu ni mbinguni ndio maana sir God anamwona Ibilisi ni lofa tu, ila yesu alikuja kuturudishia Yale mamlaka ambayo tuliporwa na Ibilisi kwa hiyo ukiokoka na kumkiri yesu anakurudishia yote uliyoporwa na ibilisi pia unakuwa na nguvu na mamalaka ya kupambana na ulimwengu wa Giza na hakuna kitu kitakudhuru.

Isitoshe kusema tu kuwa binadamu ni kiumbe Cha thamani na kipekee Sana kiasi anapiganiwa na mamlaka kuu mbili za Giza na Nuru sema atatujajua TU thamani tuliyonayo.
 
YESU NDIYE MWENYE MAMLAKA LAKINI SHETANI NDIYE MTAWALA.


MATHAYO 28:18.

18 Yesu akaja kwao, akasema nao, akawaambia, Nimepewa mamlaka yote mbinguni na duniani.

19 Basi, enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa jina la Baba, na Mwana, na Roho Mtakatifu.

20 na kuwafundisha kuyashika yote niliyowaamuru ninyi; na tazama, mimi nipo pamoja nanyi siku zote, hata ukamilifu wa dahari.
Mathayo 28:20

YESU NDIYE MWENYE MAMLAKA LAKINI SHETANI NDIYE MTAWALA
Ninavyeelewa mimi Utawala ni mamlaka na haki ya kuongoza. Sasa inawezekana vipi akawepo mwenye mamlaka ila asiwe ni kiongozi.

Na kama si kiongozi (Yesu) bali ni mwenye mamlaka juu ya vyote kwanini atumii mamlaka yake kuamuru anavyotaka viwe badala yake nae anatafuta wafuasi wakumuunga mkono?
 
Shetani ni mtawala wa Dunia SI ulimwengu, ulimwengu ni dude kubwa ambalo limebeba kadunia sehemu ndogo sana, pia shetani Hana kitu chochote ni mtupu kama binadamu tu akuja na chochote tofauti na nguvu , shetani ni kibaka tu alimpora Adamu hati miliki ya Dunia Kwa uzembe wa adamu ndio maana anaitwa mwizi na muhongo.

Pia sisi wanadamu duniani sio kwetu kwetu ni mbinguni ndio maana sir God anamwona Ibilisi ni lofa tu, ila yesu alikuja kuturudishia Yale mamlaka ambayo tuliporwa na Ibilisi kwa hiyo ukiokoka na kumkiri yesu anakurudishia yote uliyoporwa na ibilisi pia unakuwa na nguvu na mamalaka ya kupambana na ulimwengu wa Giza na hakuna kitu kitakudhuru.

Isitoshe kusema tu kuwa binadamu ni kiumbe Cha thamani na kipekee Sana kiasi anapiganiwa na mamlaka kuu mbili za Giza na Nuru sema atatujajua TU thamani tuliyonayo.

Naomba urudie kusoma uzi utabaini kuwa utawala wa ibilisi hauko tu katika dunia na vitu vyake, bali katika tabaka lote la anga na giza, pamoja na viumbe vya gizani au mapepo ambao wanatambulishwa kama jeshi lenye nguvu linalofuatwa na wale wasiomtii Mungu, hivyo ni mtawala wa ulimwengu kiujumla wake.

Ukienda kucheza kamari au kubeti huku umeweka bondi hati ya nyumba yako mwenyewe na ikatokea umeliwa, je mmiliki mpya wa ile nyumba ataitwa mwizi, tapeli au muongo?

Umesema kwetu ni mbinguni ila tukimkiri Yesu tunarudishiwa mamlaka ambayo tumepokonywa na shetani, ambapo mamlaka yenyewe ni kuitawala dunia. Je, wakati tukipewa mamlaka hayo na Mungu kabla ya kupokonywa na shetani, makazi yetu yalikuwa wapi?
 
Biblia ina andiko la wakati Mungu akimpa Adam mamlaka ya dunia, Adam anashindwa kuitii amri ya Mungu na hatimaye anaishia kumkabidhi mamlaka hayo shetani.

Quran inasema "isipokuwa kwa wajakazi (wafuasi) wangu (shetani) hauna mamlaka yeyote juu yao, isipokuwa kwa wale wanaokufuata(wanaokutii)

Tunaona katika vitabu hivi viwili vya imani kuwa shetani amepewa mamlaka juu ya watu wa Mungu kwa sababu ya dhambi.

Je, maandiko yanasemaje kuhusiana na Mungu kuwa ndiye mmliki au mtawala wa ulimwengu huu.

Yesu anasema "mamlaka yote nimekabidhiwa mimi, mbinguni na duniani" mathayo 28:18

Katika sala ya Bwana ndani ya mathayo 6:13 inaishilia na mstari huu "...kwa kuwa ufalme ni wako na nguvu na utukufu, milele, amina! (Andiko hili limewekwa kwenye mabano katika toleo la biblia ya NASB na limeondolewa katika NIV, RSV na ESV)

Waefeso 1:20-22 inasema "Akamwinua kutoka katika mauti na akamweka mkono wa kulia.....na akaweka kila kitu chini ya miguu yake"

Daniel 4:17, 25, 26, mara tatu inatuambia "Aliye juu zaidi uongoza ufalme wa binadamu na umpa yeyote amtakaye"

2 wakolosai 20:6 inathibitisha "Ewe Mwenyezi Mungu wa baba zetu, je siye Mungu wa mbinguni? Na utawalaye falme zote hata za wapagani? Na katika mkono wako je hakuna nguvu na uwezo, kiasi hakuna hawezae kuhimili?"

Je, maandiko yanasemaje kuhusiana na Shetani kuwa mtawala au mmliki wa ulimwengu huu?

Luka 4:6, Shetani akamjaribu Bwana Yesu jangwani, shetani akamwambia Yesu kuwa ufalme wote wa duniani ni wangu na nampa yeyote yule nimtakaye. (Kumbuka kauli hii ni kinyume na Daniel 4:17,25,26)

Mathayo 4:4 shetani akaahidi kumpa kristo utawala wa dunia kama zawadi ya kumwinamia na kumwabudu.

Tuangalie katika matoleo kadhaa ya biblia tukianza na NIV "Dunia iko chini ya utawala wa mwovu"
Warumi 12:9, NKJV, NASB katika mathayo 5:37 na 6:13, Holman standard, ESV (vitabu vyote vinathibitisha kuwa shetani ndiye "Mtawala wa ulimwengu" Yohana 12:31,14:30 na 16:11)

Yohana 14:30 Sitosema tena mengi nanyi kwa sababu mtawala wa dunia hii anakuja. Yeye hana uwezo juu yangu.

Yohana 12:31-33 "Wakati wa Mungu kutamka hukumu juu ya ulimwengu imetimia, huu ni wakati ambao shetani, MTAWALA WA DUNIA hii, 'ATAPINDULIWA' nami nitakapoinuliwa kutoka ardhini nitawavuta watu wote waje kwangu.

Waefeso 2:1-3 Ninyi mlikuwa mmekufa kwa sababu ya dhambi zenu. Na hata sisi sote tulikuwa kama wao;tuliishi kufuatana na mtindo mbaya wa ulimwengu huu, MKAMTII MTAWALA WA PEPO WENYE NGUVU WA ANGA, pepo ambao hutawala sasa watu wasiomtii Mungu. Na hata sisi sote tulikuwa kama wao;tuliishi kufuatana na tamaa zetu za kidunia na kufanya mambo yale yaliyo ipendeza miili na akili zetu ila dunia, sisi kama vile pia wao, tulistahili ghadhabu ya Mungu.

Waefeso 6:12-13 Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya nyama na damu, bali dhidi ya falme, mamlaka, dhidi ya WAKUU WA GIZA NA MAJESHI YA PEPO WABAYA katika ulimwengu wa kiroho.

Tunaona pia kuwa hata malaika mkuu Mikaeli mamlaka yake haizidi ile ya shetani, Yuda 1:9 kwamba hata ' Mikaeli malaika mkuu, katika ule ubishi na ibilisi juu ya mwili wa musa, Mikaeli akuthubutu kumshitaki kwa kumlahumu bali alisema, Bwana na akukemee.

Yesu mwenyewe alimwita shetani 'mtawala wa ulimwengu' Yohana 16:11

Ni wazi kuwa kulingana na maandiko haya, shetani ana mamlaka katika dunia. Na mifumo ya ulimwengu mzima inaendeshwa kulingana na design alizoamua. (Angalia tena, waefeso 2:2)

Ndiyo maana wenye kuiamini hekima toka kwa Mungu wanaonekana kama wajinga na waliopotoka kwa sababu mtizamo wao ni tofauti kabisa na hekima ya kiulimwengu. (1wakorintho 1:21-25)

Shetani utawala juu ya mifumo ya ulimwengu na Biblia inathibitisha hili kwa kukazia "Je hamtambui kuwa rafiki wa dunia ni adui wa Mungu? Yeyote atakaye kuwa rafiki wa dunia ujifanisha mwenyewe kuwa adui wa Mungu (James 4:4)(1 Yohana 2:15) inaamuru" usipende ulimwengu au vitu vyake, endapo mtu atapenda ulimwengu, upendo wa baba hautokuwa nae; kwa sababu adui wa Mungu ni MTAWALA WA ULIMWENGU.

Kama haitoshi katika Quran shetani kuonesha mamlaka na uwezo wake anamwakikishia Allah kuwa "Nitawaendea uso kwa uso, na kwa kutokea nyuma, na kutokea kulia na kwa kutokea kushoto" (I shall approach them head on and from behind and from the right and from the left)

Kulingana na ushahidi wa maandiko matakatifu hayo hapo juu yamhusuyo Mungu na Shetani toka katika pande zote mbili,

1. Wewe kama mwamuzi, toa jibu lako na sababu kuwa nani ni mtawala halisi wa ulimwengu huu?

2. Ikiwa unadhani shetani ndiye mtawala wa ulimwengu, Je ni haki kuishi kinyume nae kwa kutii amri za mamlaka nyingine?

3. Ikiwa unadhani Mungu ndiye mtawala wa ulimwengu, Je ni haki kuendelea kumshtumu shetani aliye ndani ya mamlaka yake?
Katika kumbukumbu zangu, hakuna verse Mungu anamkabidhi Shetani kuwa mtawala wa Dunia hii. Ulimwengu inatumika kwa Maana ya Jamii ya Kibinadamu. NB Mungu alileta gharika baada ya kuona Ulimwengu. 2pet3:6 yasema Ulimwengu wa wakati huo (wa Nuhu) uliangamia kwa gharika. Biblia kweli inamtaja Shetani kuwa Mtawala wa Ulimwengu huu (John 16:11) hata inaenda mbali zaidi kusema Shetani ni mungu wa Ulimwengu huu (wanadamu). Ilitokeaje Wanadamu tukajiweka chini ya utawala wa Shetani???
Yote yalianzia Bustani ya Eden. Adam na Hawa walipewa uhuru na Mungu uliokuwa na sharti Moja tu la kutokula matunda ya mti uliokuwa katikati ya Bustani. Kiujumla Mungu alichotaka Toka kwao ni UTII. Walipokutana na Shetani, wao wakaona Yale wanayoambiwa na Shetani ndiyo ya kweli na yakuyafuata. Kiufupi wakaamua kumtii Shetani na kumukaidi Mungu. Mfano wa hicho kilichotokea ni pale wazazi baada ya kumlea mtoto wao katika maadili yote na kumpa kilakitu anachohitaji, siku mtoto huyo atakawakaidi na badala yake kuamua kumsikiliza mtu wa mbali, wazazi waweza sema basi nenda UKAISHI NA HUYO UNAYEMTII. Hicho ndicho kilichotokea kwa Adamu na Hawa. Mungu aliwafukuza Toka Bustani ya Eden na akawekwa Malaika mwenye upanga kulinda wasirudi nyumbani kwake Mwanzo 3:24
Lakini Mungu ni mwenye UPENDO.mapema kabisa akatangaza unabii Mw.3:15 namna atakavyomtumia Mwanae Mpedwa Yesu kumuangamiza Shetani na Kizazi chale. Kuanzia hapo unabii wote ulielekeza kwa Yesu na jinsi atakavyo wakomboa wanadamu. Kwa kiufupi Yesu atatumia Mamlaka yake ya Kifalme kumuangamiza Shetani na wafuasi wake na baada ya hapo ndyo ataanza kuwarudishia wanadamu mazingira Bora kama Yale ya Bustani ya Eden.
Ndyo maana maandiko yanaonyesha kuwa katika miaka ya baadae baada ya yeye kufa na kufufuka ndipo anapewa Mamlaka Waebrania 1:13 " Kaa kuume kwa Mkono wangu mpaka nitakapowaweka Maadui zako chini ya miguu Yako. Mlolongo mzima wa jinsi Yesu atakavyo shughulika na Maadui zake na wa Mungu unaelezewa katika 1Kor. 15:24-28 katika mistari hiyo inaonyesha pia kuwa Yesu ndiye atakaye ondoa JANGA LA KIFO kwa wanadamu.
Kitabu Cha UFUNUO ndicho Cha mwisho. Kinafunua makubwa mawili
1. Ufunuo 11:15 hatimaye Ufalme wa Ulimwengu umewekwa chini ya Yesu
2. Ufunuo 21:3 "Hema la Mungu liko pamoja na Wanadamu naye atakaa pamoja nao, nao (wanadamu) watakuwa watu wake naye atafuta kila chozi, na hawatakuwa na maombolezo tena na WALA KIFO HAKITAKUWAPO TENA.
tafadhali angalieni huu mtiririko ulivyokuwa consistent. NB kwenye Qur'an huwezi pata majibu haya Wala hii consistence.
 
Katika kumbukumbu zangu, hakuna verse Mungu anamkabidhi Shetani kuwa mtawala wa Dunia hii. Ulimwengu inatumika kwa Maana ya Jamii ya Kibinadamu. NB Mungu alileta gharika baada ya kuona Ulimwengu. 2pet3:6 yasema Ulimwengu wa wakati huo (wa Nuhu) uliangamia kwa gharika. Biblia kweli inamtaja Shetani kuwa Mtawala wa Ulimwengu huu (John 16:11) hata inaenda mbali zaidi kusema Shetani ni mungu wa Ulimwengu huu (wanadamu). Ilitokeaje Wanadamu tukajiweka chini ya utawala wa Shetani???
Yote yalianzia Bustani ya Eden. Adam na Hawa walipewa uhuru na Mungu uliokuwa na sharti Moja tu la kutokula matunda ya mti uliokuwa katikati ya Bustani. Kiujumla Mungu alichotaka Toka kwao ni UTII. Walipokutana na Shetani, wao wakaona Yale wanayoambiwa na Shetani ndiyo ya kweli na yakuyafuata. Kiufupi wakaamua kumtii Shetani na kumukaidi Mungu. Mfano wa hicho kilichotokea ni pale wazazi baada ya kumlea mtoto wao katika maadili yote na kumpa kilakitu anachohitaji, siku mtoto huyo atakawakaidi na badala yake kuamua kumsikiliza mtu wa mbali, wazazi waweza sema basi nenda UKAISHI NA HUYO UNAYEMTII. Hicho ndicho kilichotokea kwa Adamu na Hawa. Mungu aliwafukuza Toka Bustani ya Eden na akawekwa Malaika mwenye upanga kulinda wasirudi nyumbani kwake Mwanzo 3:24
Lakini Mungu ni mwenye UPENDO.mapema kabisa akatangaza unabii Mw.3:15 namna atakavyomtumia Mwanae Mpedwa Yesu kumuangamiza Shetani na Kizazi chale. Kuanzia hapo unabii wote ulielekeza kwa Yesu na jinsi atakavyo wakomboa wanadamu. Kwa kiufupi Yesu atatumia Mamlaka yake ya Kifalme kumuangamiza Shetani na wafuasi wake na baada ya hapo ndyo ataanza kuwarudishia wanadamu mazingira Bora kama Yale ya Bustani ya Eden.
Ndyo maana maandiko yanaonyesha kuwa katika miaka ya baadae baada ya yeye kufa na kufufuka ndipo anapewa Mamlaka Waebrania 1:13 " Kaa kuume kwa Mkono wangu mpaka nitakapowaweka Maadui zako chini ya miguu Yako. Mlolongo mzima wa jinsi Yesu atakavyo shughulika na Maadui zake na wa Mungu unaelezewa katika 1Kor. 15:24-28 katika mistari hiyo inaonyesha pia kuwa Yesu ndiye atakaye ondoa JANGA LA KIFO kwa wanadamu.
Kitabu Cha UFUNUO ndicho Cha mwisho. Kinafunua makubwa mawili
1. Ufunuo 11:15 hatimaye Ufalme wa Ulimwengu umewekwa chini ya Yesu
2. Ufunuo 21:3 "Hema la Mungu liko pamoja na Wanadamu naye atakaa pamoja nao, nao (wanadamu) watakuwa watu wake naye atafuta kila chozi, na hawatakuwa na maombolezo tena na WALA KIFO HAKITAKUWAPO TENA.
tafadhali angalieni huu mtiririko ulivyokuwa consistent. NB kwenye Qur'an huwezi pata majibu haya Wala hii consistence.
Umeeleza vema kabisa , nami nitaongeza kitu baadae hivi ,naomba nikumbushwe maana app yangu huwa haioneshi notifications za post nilizotembelea so mada nyingi nakuwa sipati rejea

Sent from my TECNO KG5j using JamiiForums mobile app
 
Biblia ina andiko la wakati Mungu akimpa Adam mamlaka ya dunia, Adam anashindwa kuitii amri ya Mungu na hatimaye anaishia kumkabidhi mamlaka hayo shetani.

Quran inasema "isipokuwa kwa wajakazi (wafuasi) wangu (shetani) hauna mamlaka yeyote juu yao, isipokuwa kwa wale wanaokufuata(wanaokutii)

Tunaona katika vitabu hivi viwili vya imani kuwa shetani amepewa mamlaka juu ya watu wa Mungu kwa sababu ya dhambi.

Je, maandiko yanasemaje kuhusiana na Mungu kuwa ndiye mmliki au mtawala wa ulimwengu huu.

Yesu anasema "mamlaka yote nimekabidhiwa mimi, mbinguni na duniani" mathayo 28:18

Katika sala ya Bwana ndani ya mathayo 6:13 inaishilia na mstari huu "...kwa kuwa ufalme ni wako na nguvu na utukufu, milele, amina! (Andiko hili limewekwa kwenye mabano katika toleo la biblia ya NASB na limeondolewa katika NIV, RSV na ESV)

Waefeso 1:20-22 inasema "Akamwinua kutoka katika mauti na akamweka mkono wa kulia.....na akaweka kila kitu chini ya miguu yake"

Daniel 4:17, 25, 26, mara tatu inatuambia "Aliye juu zaidi uongoza ufalme wa binadamu na umpa yeyote amtakaye"

2 wakolosai 20:6 inathibitisha "Ewe Mwenyezi Mungu wa baba zetu, je siye Mungu wa mbinguni? Na utawalaye falme zote hata za wapagani? Na katika mkono wako je hakuna nguvu na uwezo, kiasi hakuna hawezae kuhimili?"

Je, maandiko yanasemaje kuhusiana na Shetani kuwa mtawala au mmliki wa ulimwengu huu?

Luka 4:6, Shetani akamjaribu Bwana Yesu jangwani, shetani akamwambia Yesu kuwa ufalme wote wa duniani ni wangu na nampa yeyote yule nimtakaye. (Kumbuka kauli hii ni kinyume na Daniel 4:17,25,26)

Mathayo 4:4 shetani akaahidi kumpa kristo utawala wa dunia kama zawadi ya kumwinamia na kumwabudu.

Tuangalie katika matoleo kadhaa ya biblia tukianza na NIV "Dunia iko chini ya utawala wa mwovu"
Warumi 12:9, NKJV, NASB katika mathayo 5:37 na 6:13, Holman standard, ESV (vitabu vyote vinathibitisha kuwa shetani ndiye "Mtawala wa ulimwengu" Yohana 12:31,14:30 na 16:11)

Yohana 14:30 Sitosema tena mengi nanyi kwa sababu mtawala wa dunia hii anakuja. Yeye hana uwezo juu yangu.

Yohana 12:31-33 "Wakati wa Mungu kutamka hukumu juu ya ulimwengu imetimia, huu ni wakati ambao shetani, MTAWALA WA DUNIA hii, 'ATAPINDULIWA' nami nitakapoinuliwa kutoka ardhini nitawavuta watu wote waje kwangu.

Waefeso 2:1-3 Ninyi mlikuwa mmekufa kwa sababu ya dhambi zenu. Na hata sisi sote tulikuwa kama wao;tuliishi kufuatana na mtindo mbaya wa ulimwengu huu, MKAMTII MTAWALA WA PEPO WENYE NGUVU WA ANGA, pepo ambao hutawala sasa watu wasiomtii Mungu. Na hata sisi sote tulikuwa kama wao;tuliishi kufuatana na tamaa zetu za kidunia na kufanya mambo yale yaliyo ipendeza miili na akili zetu ila dunia, sisi kama vile pia wao, tulistahili ghadhabu ya Mungu.

Waefeso 6:12-13 Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya nyama na damu, bali dhidi ya falme, mamlaka, dhidi ya WAKUU WA GIZA NA MAJESHI YA PEPO WABAYA katika ulimwengu wa kiroho.

Tunaona pia kuwa hata malaika mkuu Mikaeli mamlaka yake haizidi ile ya shetani, Yuda 1:9 kwamba hata ' Mikaeli malaika mkuu, katika ule ubishi na ibilisi juu ya mwili wa musa, Mikaeli akuthubutu kumshitaki kwa kumlahumu bali alisema, Bwana na akukemee.

Yesu mwenyewe alimwita shetani 'mtawala wa ulimwengu' Yohana 16:11

Ni wazi kuwa kulingana na maandiko haya, shetani ana mamlaka katika dunia. Na mifumo ya ulimwengu mzima inaendeshwa kulingana na design alizoamua. (Angalia tena, waefeso 2:2)

Ndiyo maana wenye kuiamini hekima toka kwa Mungu wanaonekana kama wajinga na waliopotoka kwa sababu mtizamo wao ni tofauti kabisa na hekima ya kiulimwengu. (1wakorintho 1:21-25)

Shetani utawala juu ya mifumo ya ulimwengu na Biblia inathibitisha hili kwa kukazia "Je hamtambui kuwa rafiki wa dunia ni adui wa Mungu? Yeyote atakaye kuwa rafiki wa dunia ujifanisha mwenyewe kuwa adui wa Mungu (James 4:4)(1 Yohana 2:15) inaamuru" usipende ulimwengu au vitu vyake, endapo mtu atapenda ulimwengu, upendo wa baba hautokuwa nae; kwa sababu adui wa Mungu ni MTAWALA WA ULIMWENGU.

Kama haitoshi katika Quran shetani kuonesha mamlaka na uwezo wake anamwakikishia Allah kuwa "Nitawaendea uso kwa uso, na kwa kutokea nyuma, na kutokea kulia na kwa kutokea kushoto" (I shall approach them head on and from behind and from the right and from the left)

Kulingana na ushahidi wa maandiko matakatifu hayo hapo juu yamhusuyo Mungu na Shetani toka katika pande zote mbili,

1. Wewe kama mwamuzi, toa jibu lako na sababu kuwa nani ni mtawala halisi wa ulimwengu huu?

2. Ikiwa unadhani shetani ndiye mtawala wa ulimwengu, Je ni haki kuishi kinyume nae kwa kutii amri za mamlaka nyingine?

3. Ikiwa unadhani Mungu ndiye mtawala wa ulimwengu, Je ni haki kuendelea kumshtumu shetani aliye ndani ya mamlaka yake?
Mtawala wa ulimwengu huu ni Bin Adam! Yeye ndiye huamua kufanya kazi na Mungu au shetani.
 
Mtawala wa ulimwengu huu ni Bin Adam! Yeye ndiye huamua kufanya kazi na Mungu au shetani.
Umesoma bandiko lote na bado unakanusha bila kuja na sura au aya inayotetea dai lako.

Ni rahisi kusema yeye ndiye uamua lakini kiuhalisia bin Adam ndiye upangiwa cha kufanya kwa kuwa anatawaliwa/anasukumwa na nguvu zote mbili Allah na Shetani ambazo si nguvu zilizopaswa kuwepo duniani kukinzana juu ya bin Adam kwa maana utawala huu kiuhalisia haukuwa wakwao.
 
"Katika kumbukumbu zangu, hakuna verse Mungu anamkabidhi Shetani kuwa mtawala wa Dunia hii..."

"...Biblia kweli inamtaja Shetani kuwa Mtawala wa Ulimwengu huu (John 16:11) hata inaenda mbali zaidi kusema Shetani ni mungu wa Ulimwengu huu (wanadamu)..."

Swali ni je, hao binadamu (ulimwengu) wanaotawaliwa na shetani wanaishi angani au duniani?

"..Mungu aliwafukuza Toka Bustani ya Eden na akawekwa Malaika mwenye upanga kulinda wasirudi nyumbani kwake..." Mwanzo 3:24

Kulingana na kifungu hiki hapa inaonekana binadamu mwanzo hakuwa mkazi wa dunia bali aliishi na Mungu?

Au Mungu na Binadamu wote ni wakazi wa dunia ila mmoja anaishi Eden pasipofikika na binadamu sababu ya ulinzi mkali na mwingine anaishi katika dunia iliyolaaniwa?

Na kama dunia ni nyumbani kwa Mungu iweje iitwe ni miliki ya Adam? Ikiwa anaetoa amri na mwongozo wa kufuatwa ni Mungu?

Waebrania 1:13 " Kaa kuume kwa Mkono wangu mpaka nitakapowaweka Maadui zako chini ya miguu Yako.

Je, anayeahidiwa hapa ni Yesu au binadamu?

Kati ya Yesu na binadamu nani ni mtawala wa dunia?

Ikiwa shetani alitukosea sisi kwanini Mungu asitupiganie sisi dhidi ya maadui zetu na kuturudishia utawala wetu tuliopokonywa, mbona anampambania Yesu hili amkabidhi mamlaka yote ya mbinguni (anga) na ardhini (duniani)?

Ufunuo 11:15 "hatimaye Ufalme wa Ulimwengu umewekwa chini ya Yesu.."

Kwahiyo utawala wa ulimwengu kamwe haukuumbwa kwa ajili ya binadamu au upo kushindaniwa?

Au binadamu ni kiumbe dhaifu kiasi kwamba lazima awe chini ya utawala wa Yesu au shetani?

Je, baadae binadamu akija kuasi chini ya utawala mpya wa Yesu nini kitatokea?
 
Umesoma bandiko lote na bado unakanusha bila kuja na sura au aya inayotetea dai lako.

Ni rahisi kusema yeye ndiye uamua lakini kiuhalisia bin Adam ndiye upangiwa cha kufanya kwa kuwa anatawaliwa/anasukumwa na nguvu zote mbili Allah na Shetani ambazo si nguvu zilizopaswa kuwepo duniani kukinzana juu ya bin Adam kwa maana utawala huu kiuhalisia haukuwa wakwao.
Nikuambie jambo maishani mwako? Umeumbwa na kupewa akili na uhuru. Acha kufikiri kuwa Biblia au Quran vimeandikwa na Mungu moja kwa moja. Kuna mambo mazuri katika vitabu hivi ila sio kila kweli imeandikwa humo. Mungu hawezi kujichanganya hata siku moja, wanaojichanganya ni bin Adam. Mtawala wa Dunia hii ni bin Adam. Ukipenda maandiko basi soma Kitabu cha Mwanzo kuanzia sura ya kwanza utagundua hilo pia. Maandiko lakini changanya na zako…
 
Nikuambie jambo maishani mwako? Umeumbwa na kupewa akili na uhuru. Acha kufikiri kuwa Biblia au Quran vimeandikwa na Mungu moja kwa moja. Kuna mambo mazuri katika vitabu hivi ila sio kila kweli imeandikwa humo. Mungu hawezi kujichanganya hata siku moja, wanaojichanganya ni bin Adam. Mtawala wa Dunia hii ni bin Adam. Ukipenda maandiko basi soma Kitabu cha Mwanzo kuanzia sura ya kwanza utagundua hilo pia. Maandiko lakini changanya na zako…
Kama ndiyo hivyo maandiko nayo hayahaminiki, what if nikifikiri kivingine kuwa hamna aliyeniumba wala kunipa akili au uhuru nilionao na hata hayo maandiko ni mambo ya wanadamu tu, je nitakuwa sawa?
 
Kama ndiyo hivyo maandiko nayo hayahaminiki, what if nikifikiri kivingine kuwa hamna aliyeniumba wala kunipa akili au uhuru nilionao na hata hayo maandiko ni mambo ya wanadamu tu, je nitakuwa sawa?
Ipo nguvu ya uumbaji (Mungu) ambaye amempa mwanadamu uhuru wa kuyatawala maisha yake. Maandiko yana sehemu ndogo tu ya ukweli wote hivyo kuwa mwangalifu unavyoyachukulia.
 
Back
Top Bottom