Je, Serikali ikinyimwa mkopo wa elimu na Benki ya Dunia kutatokea nini?

MsemajiUkweli

JF-Expert Member
Jul 5, 2012
13,171
23,976
Mimi ninashindwa kuelewa hizi kelele kuhusu uwezekano wa serikali kupatiwa mkopo wa elimu au la na Benki ya Dunia.

Kinachonishangaza zaidi ni kuona jinsi ambavyo baadhi ya viongozi waandamizi wa serikali/CCM wanalumbana na wanaharakati na baadhi ya viongozi wa upinzani hasa Zitto Kabwe kuhusu uhalali wa kupewa mkopo au la!

Nikipongeze sana Chama kikuu cha upinzani (CHADEMA) kwa kukaa kando katika malumbano haya ambayo kwa mtazamo wangu hayana mantiki yoyote katika jamii.

Nadhani CHADEMA wameelewa jinsi ambavyo suala la Mimba za utotoni na kuendelea na masomo linavyohitaji uangalifu mkubwa katika kulipatia ufumbuzi kisiasa. Hata sheria ya ndoa nchini bado ina mabishano mengi kutokana na mila na desturi ambazo bado ni sehemu ya maisha katika jamii nchini.

Ukichunguza utagundua wananchi wengi wanadhani sio vizuri mwanafunzi aliyepata mimba, akajifungua halafu akarudi tena kwenye darasa lenye wanafunzi wasio na watoto na kuendelea na masomo. Haishangazi kuona watu wengi wanapinga kwa sababu wananchi wengi nchini bado ni conservative lakini pia imani za dini zinakataza msichana kupata Mimba kabla ya kuolewa.

Wanaharakati na baadhi ya viongozi wa upinzani hasa Zitto wanaona ni sawa mwanafunzi aliyepata mimba ya utotoni na kujifungua lazima arudi tena kwenye darasa lenye wanafunzi wasio na watoto baada ya kujifungua na kuendelea na masomo.

Ieleweke kuwa moja ya sharti muhimu la kupata mkopo huo ni kuhakikisha wasichana wanapewa kipaumbele katika kupata elimu. Hii ni pamoja na wale ambao watapata mimba za utotoni.

Serikali imesema haiwezi kuruhusu wasichana waliozaa wasome darasa moja na wasichana ambao hawajazaa bali itawajengea shule zao na watasoma kwa miaka 2 badala ya minne kwa elimu ya sekondary (O-level) na kama watafaulu watakutana na wanafunzi wengine A-level.

Thamani ya mkopo ni dola za Kimarekani milioni 500. Hata hivyo, hizi pesa hazitolewi kwa mkupuo bali zitatolewa kidogo kidogo kwa miaka 7. Hii ina maana kuanzia 2020-2026.

Hapa chini ni Jedwali linaloonyesha jinsi ambavyo pesa zitatolewa kama mkopo utakubaliwa.
Screenshot (34).png
Kama Mkopo utatolewa basi kwa mwaka huu wa fedha tutaletewa jumla ya dola za Kimarekani milioni 8.52 tu.

Ni aibu kwa pande zote hasa serikali kulumbana kupata mkopo badala ya kulumbana jinsi ya kukusanya mapato ya ndani na matumizi yake! Huu ni mkopo for God's sake!

Ni bora angalau malumbano haya yangekuwa ni kuhusu msaada (grant) kwa sababu hauna malipo kama ilivyokuwa kwenye Msaada (grant) wa thamani ya dola za kimarekani milioni 500 uliokuwa utolewe na serikali ya Marekani kupitia kitengo cha Millennium Challenge Corp (MCC) ambao ulisitishwa mwaka 2016.

Je, huu mkopo ukitolewa, nani atanufaika na nani hatanufaika?

Je, huu mkopo usipotelewa, nani atanufaika na nani hatanufaika?

Swali la msingi la kujiuliza, Baada ya MCC kusitishwa mwaka 2016 kilitokea nini? Jibu ndilo litatoa jibu la maswali yaliyoko juu.

Haya ndio maswali muhimu ya kujiuliza?
 
Jiulize sababu ya serikali kuomba huo mkopo ilikuwa ni nini? Bila shaka ni bajeti finyu na uwezo mdogo wa serikali kifedha. Huo mkopo usipotoka malengo ya serikali hayatatimia na uzalishaji wa magumbaru kama wewe nchini utaongezeka maradufu. Understand?
 
Jiulize sababu ya serikali kuomba huo mkopo ilikuwa ni nini? Bila shaka ni bajeti finyu na uwezo mdogo wa serikali kifedha. Huo mkopo usipotoka malengo ya serikali hayatatimia na uzalishaji wa magumbaru kama wewe nchini utaongezeka maradufu. Understand?
Kwamba umeandika ''mkopo usipotoka malengo ya serikali yatatimia''.

Kwa mantiki yako ya kijinga waliomba mkopo ili malengo ya serikali yasitimie?

Kumbuka ujinga ni bora kuliko upumbavu kwa sababu upumbavu ni sifa kama ufupi na urefu lakini ujinga huondoka kama utapata elimu zaidi!
 
Likely huu mkopo tutanyimwa ama tutacheleweshewa maana tayari bank imesitisha mchakato wa kujadili hilo jambo.

Hela ya mcc ilipositishwa aliefaidi ni viongozi wa ccm maana wao ndio waliiba kura zanzibar na wala hawakuumia kuhusu hilo kwa sababu ni faida kwao huku watanzabia tukitaabika.
 
Likely huu mkopo tutanyimwa ama tutacheleweshewa maana tayari bank imesitisha mchakato wa kujadilo hilo jambo.
Tukiukosa Ccm itakosa hela za kampeni

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Likely huu mkopo tutanyimwa ama tutacheleweshewa maana tayari bank imesitisha mchakato wa kujadilo hilo jambo.
Nadhani serikali itanyimwa!
 
Kwamba umeandika ''mkopo usipotoka malengo ya serikali yatatimia''.

Kwa mantiki yako ya kijinga waliomba mkopo ili malengo ya serikali yasitimie?

Kumbuka ujinga ni bora kuliko upumbavu kwa sababu upumbavu ni sifa kama ufupi na urefu lakini ujinga huondoka kama utapata elimu zaidi!
Hakuna mahali nimeandika 'mkopo usipotoka malengo ya serikali yatatimia'. Hakuna! Ukiitwa gumbaru usitoe povu, ni halali yako kabisa.
 
Hakuna mahali nimeandika 'mkopo usipotoka malengo ya serikali yatatimia'. Hakuna! Ukiitwa gumbaru usitoe povu, ni halali yako kabisa.

Uzuri ni kwamba baada ya zile comment zako mbili nimejua ninajadiliana na kiumbe wa aina gani!
 
Siasa zimebadilika sana. Wanasiasa waliozoea siasa za kwenda kinyume na serikali kwenye kila kitu hawachanganui vizuri mambo.

Kuna mengine ni mtego, ukiyashupalia wananchi hawakuelewi kabisa. Mfano hai ni hili la Elimu, Miundombinu na lile la Ndege. Mwishowe unaonekana mpinga maendeleo.

Politics is all about optics.
 
Mimi ninashindwa kuelewa hizi kelele kuhusu uwezekano wa serikali kupatiwa mkopo wa elimu au la na Benki ya Dunia.

Kinachonishangaza zaidi ni kuona jinsi ambavyo baadhi ya viongozi waandamizi wa serikali/CCM wanalumbana na wanaharakati na baadhi ya viongozi wa upinzani hasa Zitto Kabwe kuhusu uhalali wa kupewa mkopo au la!

Nikipongeze sana Chama kikuu cha upinzani (CHADEMA) kwa kukaa kando katika malumbano haya ambayo kwa mtazamo wangu hayana mantiki yoyote katika jamii.

Nadhani CHADEMA wameelewa jinsi ambavyo suala la Mimba za utotoni na kuendelea na masomo linavyohitaji uangalifu mkubwa katika kulipatia ufumbuzi kisiasa.

Ukichunguza utagundua wananchi wengi wanadhani sio vizuri mwanafunzi aliyepata mimba, akajifungua halafu akarudi tena kwenye darasa lenye wanafunzi wasio na watoto na kuendelea na masomo. Haishangazi kuona watu wengi wanapinga kwa sababu wananchi wengi nchini bado ni conservative lakini pia imani za dini zinakataza msichana kupata Mimba kabla ya kuolewa.

Wanaharakati na baadhi ya viongozi wa upinzani hasa Zitto wanaona ni sawa mwanafunzi aliyepata mimba ya utotoni na kujifungua lazima arudi tena kwenye darasa lenye wanafunzi wasio na watoto baada ya kujifungua na kuendelea na masomo.

Ieleweke kuwa moja ya sharti muhimu la kupata mkopo huo ni kuhakikisha wasichana wanapewa kipaumbele katika kupata elimu. Hii ni pamoja na wale ambao watapata mimba za utotoni.

Serikali imesema haiwezi kuruhusu wasichana waliozaa wasome darasa moja na wasichana ambao hawajazaa bali itawajengea shule zao na watasoma kwa miaka 2 badala ya minne kwa elimu ya sekondary (O-level) na kama watafaulu watakutana na wanafunzi wengine A-level.

Thamani ya mkopo ni dola za Kimarekani milioni 500. Hata hivyo, hizi pesa hazitolewi kwa mkupuo bali zitatolewa kidogo kidogo kwa miaka 7. Hii ina maana kuanzia 2020-2026.

Hapa chini ni Jedwali linaloonyesha jinsi ambavyo pesa zitatolewa kama mkopo utakubaliwa.
View attachment 1337756
Kama Mkopo utatolewa basi kwa mwaka huu wa fedha tutaletewa jumla ya dola za Kimarekani milioni 8.52 tu.

Ni aibu kwa pande zote hasa serikali kulumbana kupata mkopo badala ya kulumbana jinsi ya kukusanya mapato ya ndani na matumizi yake! Huu ni mkopo for God's sake!

Ni bora angalau malumbano haya yangekuwa ni kuhusu msaada (grant) kwa sababu hauna malipo kama ilivyokuwa kwenye Msaada (grant) wa thamani ya dola za kimarekani milioni 500 uliokuwa utolewe na serikali ya Marekani kupitia kitengo cha Millennium Challenge Corp (MCC) ambao ulisitishwa mwaka 2016.

Cha kujiuliza, Baada ya MCC kusitishwa mwaka 2016 kilitokea nini? Nani alinufaika na nani hakunufaika?

Je, huu mkopo ukitolewa, nani atanufaika na nani hatanufaika?

Je, huu mkopo usipotelewa, nani atanufaika na nani hatanufaika?

Haya ndio maswali muhimu ya kujiuliza?
WB wasipotoa mkopo na kujiondoa kabisa ita set precedence ifuatayo:

- UN itaiweka nchi kwenye microscopic observation
- EU/US zitakaza zaidi na possibly kukata kabisa
- development partners waliokuwa wanasaidia kidogo kidogo watakata kabisa
- kimbilio letu China ndiyo hivyo tena - coronavirus!
- CCM tunaweza tusirudi madarakani October 2020, or else TZ itakuwa ni modern version of Zimbabwe
- civil unrest (God forbid!!)
 
MsemajiUkweli ,

..kuna tatizo.

..na tatizo ni watoto kupata mimba mashuleni.

..serikali, ccm, wapinzani, na wadau, walipaswa kukaa pamoja na KUZUNGUMZA ili kupata mbinu muafaka za kupambana na tatizo la watoto kupata mimba.

..hata WB wasipotoa mkopo na tukalazimika kugharamia elimu kwa fedha za ndani bado tatizo la watoto kupata mimba litahitaji kutatuliwa.

..Napendekeza suala hili liangaliwe kwa mapana yake.

..Tusisahau kwamba hawa ni watoto. Kuwa na uwezo wa kupachika au kushika mimba haimaanishi kwamba mhusika ni mtu mzima.

..Kuna umri ambao watoto hupitia changamoto ya miili yao kubadilika. Lazima tuwaandae kupambana na hali hiyo.

..Kuna umri ambao watoto hujaribu mambo mbalimbali na kufanya makosa mengi. Kwa mfano wako wanaojaribu sigara, pombe, udokozi, mapenzi, etc etc. Watoto wanahitaji kuongozwa vizuri ktk umri huo.

..Binafsi nashauri viongozi wetu na wadau wakae pamoja na kushauriana kuhusu suala hili.
 
MsemajiUkweli ,

..kuna tatizo.

..na tatizo ni watoto kupata mimba mashuleni.

..serikali, ccm, wapinzani, na wadau, walipaswa kukaa pamoja na KUZUNGUMZA ili kupata mbinu muafaka za kupambana na tatizo la watoto kupata mimba.

..hata WB wasipotoa mkopo na tukalazimika kugharamia elimu kwa fedha za ndani bado tatizo la watoto kupata mimba litahitaji kutatuliwa.

..Napendekeza suala hili liangaliwe kwa mapana yake.

..Tusisahau kwamba hawa ni watoto. Kuwa na uwezo wa kupachika au kushika mimba haimaanishi kwamba mhusika ni mtu mzima.

..Kuna umri ambao watoto hupitia changamoto ya miili yao kubadilika. Lazima tuwaandae kupambana na hali hiyo.

..Kuna umri ambao watoto hujaribu mambo mbalimbali na kufanya makosa mengi. Kwa mfano wako wanaojaribu sigara, pombe, udokozi, mapenzi, etc etc. Watoto wanahitaji kuongozwa vizuri ktk umri huo.

..Binafsi nashauri viongozi wetu na wadau wakae pamoja na kushauriana kuhusu suala hili.
JokaKuu siasa chafu ndiyo inaongoza. Kwanini? Kwani tangu zamani wakati wa Nyerere wasichana waliokuwa wanapata mimba walikuwa wanaruhusiwa kuendelea na masoma kama kawaida? Mbona mimi najua wasichana wengi tu waliozaa wakiwa shuleni kipindi cha awamu ya kwanza na walifukuzwa shule na wakatumia njia nyingine kuendelea na masomo baada ya kujifungua? Tena bora siku hizi kuna alternative nyingi lakini kipindi kile kusoma tena wakati umeshfukuzwa shule ilikuwa ngumu. Hata upimaji wa mimba mashuleni ulikuwepo, tena sana tu. Zitto na hawa wanaharakati wengine wote wamesomea kwenye haya mazingara! Kwanini leo waibuke na kusema serikali haiwatendei haki? Hapa wametumia hasira zao kwa awamu ya tano kupinga kitu ambacho siyo kigeni! Kama ulivyosema hata mimi nakubali hili suala linahita utafiti wa kina na wa kulishughulikia ni sisi wenyewe. Hata kama serikali itakubalina na wanachotaka benki ya dunia, bila sisi kama nchi kufanya ulichosema tunaweza kujikuta tumekuza zaidi hili tatizo.
 
JokaKuu siasa chafu ndiyo inaongoza. Kwanini? Kwani tangu zamani wakati wa Nyerere wasichana waliokuwa wanapata mimba walikuwa wanaruhusiwa kuendelea na masoma kama kawaida? Mbona mimi najua wasichana wengi tu waliozaa wakiwa shuleni kipindi cha awamu ya kwanza na walifukuzwa shule na wakatumia njia nyingine kuendelea na masomo baada ya kujifungua? Tena bora siku hizi kuna alternative nyingi lakini kipindi kile kusoma tena wakati umeshfukuzwa shule ilikuwa ngumu. Hata upimaji wa mimba mashuleni ulikuwepo, tena sana tu. Zitto na hawa wanaharakati wengine wote wamesomea kwenye haya mazingara! Kwanini leo waibuke na kusema serikali haiwatendei haki? Hapa wametumia hasira zao kwa awamu ya tano kupinga kitu ambacho siyo kigeni! Kama ulivyosema hata mimi nakubali hili suala linahita utafiti wa kina na wa kulishughulikia ni sisi wenyewe. Hata kama serikali itakubalina na wanachotaka benki ya dunia, bila sisi kama nchi kufanya ulichosema tunaweza kujikuta tumekuza zaidi hili tatizo.

..Magufuli ndiyo aliyeibua suala hili, baada ya kulitolea kauli ngumu ktk mkutano wa hadhara.

..Sheria dhidi ya wanaopata mimba ni kali, lakini tatizo halielekei kupungua. Je, tufanye nini ili mimba zipungue badala ya kuongeza?

..Halafu naona focus iko ktk kuadhibu watoto wa kike. Kwanini hakuna usawa ktk kutoa adhabu kwa wavulana wanaojaza mimba wanafunzi wenzao?
 
Mbona wagumu kuelewa ninyi? Sawa ilikuwa hivyo, ulimi uliponza kichwa. Awamu ya 5 imwkuwa na maneno mengi ya kutafuta misifa bila kutafakari kwanza unatoa Nini mdomoni, kwa Nani na impact yake Ni Nini. Kwani miaka yote iliyopita watoto walikuwa wanafukuzwa wa mimba, lakini initiative binafsi wanarudi shuleni Mambo yanaendelea. Kilichofanya awamu hii kuropoka hadharani ilikuwa kutafuta misifa au? Ina Sasa imeshakuwa Soo. Inabidi Sasa hiyo awamu iliyotamka hayo hadharani iyengue kauli hizo, yaani Sasa irasmishe watiwa mimba kurudi shureni bila masharyi, hakuna namna Tena vinginevyo mkopo no
 
Labda kama kweli wamenusa matumizi tofauti ya huu mkopo.
Vinginevyo hizi kelele hazieleweki.
Wanaopata mimba ni asilimia chache sana ya wasichana lakini wasichana wengi hawaendelei kielimu kwa sababu ya mazingira ya shule zetu.
Na si hilo tu, kuna issue pia za kisheria na kijamii msichana akipewa mimba akiwa shuleni wanakuwa disturbed kwa hicho kipindi chote, kuwarudisha tu shuleni haitakuwa jibu.

Kama hoja ni mahitaji maalum,
wenzetu walemavu kwenye suala la elimu wanapitia uzoefu mgumu sana. Wengine huko sekondari wanachanganywa hata hawaelewi. Kama tunajali sana kutobagua elimu, je hili nalo limezingatiwa?

Kama hoja ya matumizi fedha hizi kwa ajili ya kampeni za kisiasa, hili laweza kuwa muhimu kuzingatiwa maana CCM wana uzoefu wa kutumia pesa bila taratibu haswa kipindi cha kampeni. Rejea EPA na ESCROW.

Mi naona hivyo, kelele zisizo na mwelekeo wenye kuleta tija pande zote na mwishoe naamini hayo kuna vitu tunafichwa. Na kama tunafichwa na huu ni mkopo WB wabaki na pesa zao.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom