MsemajiUkweli
JF-Expert Member
- Jul 5, 2012
- 13,171
- 23,976
Mimi ninashindwa kuelewa hizi kelele kuhusu uwezekano wa serikali kupatiwa mkopo wa elimu au la na Benki ya Dunia.
Kinachonishangaza zaidi ni kuona jinsi ambavyo baadhi ya viongozi waandamizi wa serikali/CCM wanalumbana na wanaharakati na baadhi ya viongozi wa upinzani hasa Zitto Kabwe kuhusu uhalali wa kupewa mkopo au la!
Nikipongeze sana Chama kikuu cha upinzani (CHADEMA) kwa kukaa kando katika malumbano haya ambayo kwa mtazamo wangu hayana mantiki yoyote katika jamii.
Nadhani CHADEMA wameelewa jinsi ambavyo suala la Mimba za utotoni na kuendelea na masomo linavyohitaji uangalifu mkubwa katika kulipatia ufumbuzi kisiasa. Hata sheria ya ndoa nchini bado ina mabishano mengi kutokana na mila na desturi ambazo bado ni sehemu ya maisha katika jamii nchini.
Ukichunguza utagundua wananchi wengi wanadhani sio vizuri mwanafunzi aliyepata mimba, akajifungua halafu akarudi tena kwenye darasa lenye wanafunzi wasio na watoto na kuendelea na masomo. Haishangazi kuona watu wengi wanapinga kwa sababu wananchi wengi nchini bado ni conservative lakini pia imani za dini zinakataza msichana kupata Mimba kabla ya kuolewa.
Wanaharakati na baadhi ya viongozi wa upinzani hasa Zitto wanaona ni sawa mwanafunzi aliyepata mimba ya utotoni na kujifungua lazima arudi tena kwenye darasa lenye wanafunzi wasio na watoto baada ya kujifungua na kuendelea na masomo.
Ieleweke kuwa moja ya sharti muhimu la kupata mkopo huo ni kuhakikisha wasichana wanapewa kipaumbele katika kupata elimu. Hii ni pamoja na wale ambao watapata mimba za utotoni.
Serikali imesema haiwezi kuruhusu wasichana waliozaa wasome darasa moja na wasichana ambao hawajazaa bali itawajengea shule zao na watasoma kwa miaka 2 badala ya minne kwa elimu ya sekondary (O-level) na kama watafaulu watakutana na wanafunzi wengine A-level.
Thamani ya mkopo ni dola za Kimarekani milioni 500. Hata hivyo, hizi pesa hazitolewi kwa mkupuo bali zitatolewa kidogo kidogo kwa miaka 7. Hii ina maana kuanzia 2020-2026.
Ni aibu kwa pande zote hasa serikali kulumbana kupata mkopo badala ya kulumbana jinsi ya kukusanya mapato ya ndani na matumizi yake! Huu ni mkopo for God's sake!
Ni bora angalau malumbano haya yangekuwa ni kuhusu msaada (grant) kwa sababu hauna malipo kama ilivyokuwa kwenye Msaada (grant) wa thamani ya dola za kimarekani milioni 500 uliokuwa utolewe na serikali ya Marekani kupitia kitengo cha Millennium Challenge Corp (MCC) ambao ulisitishwa mwaka 2016.
Je, huu mkopo ukitolewa, nani atanufaika na nani hatanufaika?
Je, huu mkopo usipotelewa, nani atanufaika na nani hatanufaika?
Swali la msingi la kujiuliza, Baada ya MCC kusitishwa mwaka 2016 kilitokea nini? Jibu ndilo litatoa jibu la maswali yaliyoko juu.
Haya ndio maswali muhimu ya kujiuliza?
Kinachonishangaza zaidi ni kuona jinsi ambavyo baadhi ya viongozi waandamizi wa serikali/CCM wanalumbana na wanaharakati na baadhi ya viongozi wa upinzani hasa Zitto Kabwe kuhusu uhalali wa kupewa mkopo au la!
Nikipongeze sana Chama kikuu cha upinzani (CHADEMA) kwa kukaa kando katika malumbano haya ambayo kwa mtazamo wangu hayana mantiki yoyote katika jamii.
Nadhani CHADEMA wameelewa jinsi ambavyo suala la Mimba za utotoni na kuendelea na masomo linavyohitaji uangalifu mkubwa katika kulipatia ufumbuzi kisiasa. Hata sheria ya ndoa nchini bado ina mabishano mengi kutokana na mila na desturi ambazo bado ni sehemu ya maisha katika jamii nchini.
Ukichunguza utagundua wananchi wengi wanadhani sio vizuri mwanafunzi aliyepata mimba, akajifungua halafu akarudi tena kwenye darasa lenye wanafunzi wasio na watoto na kuendelea na masomo. Haishangazi kuona watu wengi wanapinga kwa sababu wananchi wengi nchini bado ni conservative lakini pia imani za dini zinakataza msichana kupata Mimba kabla ya kuolewa.
Wanaharakati na baadhi ya viongozi wa upinzani hasa Zitto wanaona ni sawa mwanafunzi aliyepata mimba ya utotoni na kujifungua lazima arudi tena kwenye darasa lenye wanafunzi wasio na watoto baada ya kujifungua na kuendelea na masomo.
Ieleweke kuwa moja ya sharti muhimu la kupata mkopo huo ni kuhakikisha wasichana wanapewa kipaumbele katika kupata elimu. Hii ni pamoja na wale ambao watapata mimba za utotoni.
Serikali imesema haiwezi kuruhusu wasichana waliozaa wasome darasa moja na wasichana ambao hawajazaa bali itawajengea shule zao na watasoma kwa miaka 2 badala ya minne kwa elimu ya sekondary (O-level) na kama watafaulu watakutana na wanafunzi wengine A-level.
Thamani ya mkopo ni dola za Kimarekani milioni 500. Hata hivyo, hizi pesa hazitolewi kwa mkupuo bali zitatolewa kidogo kidogo kwa miaka 7. Hii ina maana kuanzia 2020-2026.
Hapa chini ni Jedwali linaloonyesha jinsi ambavyo pesa zitatolewa kama mkopo utakubaliwa.
Kama Mkopo utatolewa basi kwa mwaka huu wa fedha tutaletewa jumla ya dola za Kimarekani milioni 8.52 tu.Ni aibu kwa pande zote hasa serikali kulumbana kupata mkopo badala ya kulumbana jinsi ya kukusanya mapato ya ndani na matumizi yake! Huu ni mkopo for God's sake!
Ni bora angalau malumbano haya yangekuwa ni kuhusu msaada (grant) kwa sababu hauna malipo kama ilivyokuwa kwenye Msaada (grant) wa thamani ya dola za kimarekani milioni 500 uliokuwa utolewe na serikali ya Marekani kupitia kitengo cha Millennium Challenge Corp (MCC) ambao ulisitishwa mwaka 2016.
Je, huu mkopo ukitolewa, nani atanufaika na nani hatanufaika?
Je, huu mkopo usipotelewa, nani atanufaika na nani hatanufaika?
Swali la msingi la kujiuliza, Baada ya MCC kusitishwa mwaka 2016 kilitokea nini? Jibu ndilo litatoa jibu la maswali yaliyoko juu.
Haya ndio maswali muhimu ya kujiuliza?