Je, Sakata la Mbunge Mpina Linaamsha Hitaji la Mgombea Binafsi?

Je, Sakata la Mbunge Mpina Linaamsha Hitaji la Mgombea Binafsi?

Mgeni wa Jiji

JF-Expert Member
Joined
Jul 27, 2017
Posts
10,484
Reaction score
19,987
Habari za muda wana JF

Nimefuatilia kwa muda matukio mbali mbali yanayoendelea kwa sasa nchini kwetu na nimeona niweke uzi huu kujadili athari chanya au hata hasi inayoweza kuletwa na matukio haya. Kwa leo nitajadili suala la kuwepo kwa mgombea binafsi.

Turudi kwenye yaliyojiri kwa siku za hivi karibuni kisiasa.

Katika siku za hivi karibuni, tumeshuhudia maelekezo yanayoelekeza kuenguliwa Mbunge wa Kisesa, Mh. Luhaga Mpina, kwenye mchakato wa kura za maoni ndani ya chama chake cha CCM. Hili si tukio la kwanza kushuhudia mgombea maarufu mfano Askofu Gwajima au kiongozi aliyewahi kushika nafasi ya juu ya uongozi akiondolewa katika hatua za awali za uteuzi wa chama kama ilivyotokea kwa baadhi ya wanasiasa mwaka 2020. Lakini tukio hili linaibua mjadala mpana kuhusu haki ya raia binafsi kushiriki katika uongozi bila kupitia vyama vya siasa. Swali kuu linabaki: je, sakata hili linaamsha tena hitaji la mgombea binafsi?

Tuiangalie kwa kifupi sana historia ya Mgombea Binafsi;

Katika historia ya Tanzania ya kisiasa, suala la mgombea binafsi lilishika kasi zaidi mwaka 2006 baada ya mwanasheria maarufu, Ndugu Christopher Mtikila, kuibua hoja hiyo mahakamani. Mahakama ya Rufaa iliamua kuwa kuzuia mgombea binafsi ni kinyume na Katiba. Hata hivyo, kwa muda mrefu, Tume ya Uchaguzi na serikali zilishikilia msimamo wa kutoiruhusu kwa sababu za kiutendaji na kisiasa.

Muktadha wa Kisasa juu ya hoja ya mgombea binafsi

Katika mazingira ya sasa ya kisiasa, ambapo malalamiko kuhusu mchakato wa ndani wa vyama yameongezeka ikiwemo madai ya upendeleo, rushwa, au kutokuaminika kwa vikao vya maamuzi haya yakiwa kwa vyama vyote vilivyopo. Wananchi wengi wameanza kuhoji iwapo vyama vya siasa bado ni njia pekee ya haki na uwakilishi wa kweli. Sakata la Mh. Mpina linatoa mfano hai wa hali hiyo. Wafuasi wake na baadhi ya wachambuzi wanadai kuwa aliadhibiwa si kwa sababu ya kutokuwa na sifa, bali kwa sababu ya msimamo wake binafsi.

Sasa ni upi umuhimu wa Mgombea Binafsi ili tujadili kama suala hili ni hoja ya msingi kwa sasa nchini kwetu.

Kuwepo kwa mgombea binafsi kunaweza kusaidia:
1. Kuongeza ushindani na uwajibikaji miongoni mwa wanasiasa.
2. Kutoa fursa kwa watu wenye maono lakini wasiokuwa na maslahi ya vyama.
3. Kuzuia ukiritimba wa vyama katika maamuzi ya uwakilishi wa wananchi.

Mbali na umuhimu wake pia hatuwezi kukataa wala kubishania kuwa pia kuna changamoto zinazoweza kuja na uwepo wa mgombea binafsi

Pamoja na faida, mgombea binafsi pia anakabiliwa na changamoto kama:
  • Kukosa mtandao wa kisiasa au kifedha.
  • Kutojulikana kitaifa kama wagombea wa vyama.
  • Changamoto za kisheria na kimfumo kuhusiana na usimamizi wa uchaguzi.

Hitimisho

Kwa kuzingatia matukio mbali mbali ya kisiasa yanayoendelea kutokea ni wazi kuwa mjadala wa mgombea binafsi unazidi kupata nguvu mpya. Je, hii ni dalili kuwa umefika wakati Tanzania kuwa na mfumo unaotoa fursa pana za ushiriki wa kisiasa usiofungwa na makundi au miiko ya vyama?

Wasalimu.

Pascal Mayalla
Mshana Jr
johnthebaptist
Lucas Mwashambwa
 
Mgombea binafsi ni muhimu sana kwa wakati wa sasa.Nje ya hapo uchawa utatamalaki Sana...
 
sasa huyo mgombea binafsi atashinda nchi gani,hii hii Tanzania ambayo tume yote ya uchaguzi inateuliwa na mmoja wa wagombea?

badili swali lako bwana unatusumbua bure tu!
 
  • Thanks
Reactions: Ame
sasa huyo mgombea binafsi atashinda nchi gani,hii hii Tanzania ambayo tume yote ya uchaguzi inateuliwa na mmoja wa wagombea?

badili swali lako bwana unatusumbua bure tu!
Kuna hatua hili litatuvusha
 
Mkuu hili la mgombea binafsi lilifika mpaka Mahahama ya Africa Mashariki na Mtikila alishinda kesi hiyo,,baada ya mahakama ya rufaa ya Tanzania ,chini ya Jaji mkuu Marehemu Augustine Ramadhani tena wakiwa full bench majaji (saba)kushindwa kulitolea maamuzi,akisaidiwa na Profesa Kabudi kwa kofia ya marafiki wa mahakama.
Visingizio vilivyotolewa eti liende bungeni kwa kuwa ni la kisiasa.
Ni Profesa (Marehemu)Jwani Mwaikusa naye aliitwa kama rafiki wa mahakama ndiye aliyelisimamia hilo na kuunga mkono kuwepo kwa mgombea binafsi.
Kiuhalisia hata Mwalimu Nyerere aliwalaumu sana ccm kwa kuzuia haki ya mgombea binafsi, nakumbuka hilo kwenye mkutano wa Mbeya 1995.
Kimsingi ni hitaji la msingi la haki shida ipo kwa vyama vya siasa haswa ccm. Wakiruhusu hilo watashindwa kuwadhibiti watu wenye mawazo tofauti kama kina Mpina na Gwajima etc.
 
Back
Top Bottom