The Father of All
JF-Expert Member
- Feb 26, 2012
- 10,959
- 13,425
Najua wengi wanafuatilia tukio chafu na la hovyo la kutekwa Humphrey Polepole mwanaCCM kindakindaki aliyeibuliwa na Magufuli.
Hata hivyo, kuna mambo ya kujiuliza. Je, ni kweli kuwa Polepole alikuwa akiishi Tanzania tangu alipojiuzulu ubalozi? Je, licha ya kuwa zoba, alijiamini nini wakati alikuwa akitia kitumbua cha wenzake mchanga?
Je, japo kuteka ni mchezo wa CCM, inakuwaje wanapoanza kutekana hata kuuana wenyewe? Je, kwa ukondoo wetu, kama Polepole atauawa, kuna lolote la maana litatokea au mambo yataishia hapo?
Je, kwanini serikali yetu sikivu na 'inayojali utu' imeshikwa na kigugumizi? Je, kweli waliomteka ni watu wa serikali au maadui zake ili kukinukisha?
Je, nani watafaidika na kuondolewa Polepole? Je, Polepole alikuwa anajua hatari ya mambo aliyokuwa akifichua?
Hata hivyo, kuna mambo ya kujiuliza. Je, ni kweli kuwa Polepole alikuwa akiishi Tanzania tangu alipojiuzulu ubalozi? Je, licha ya kuwa zoba, alijiamini nini wakati alikuwa akitia kitumbua cha wenzake mchanga?
Je, japo kuteka ni mchezo wa CCM, inakuwaje wanapoanza kutekana hata kuuana wenyewe? Je, kwa ukondoo wetu, kama Polepole atauawa, kuna lolote la maana litatokea au mambo yataishia hapo?
Je, kwanini serikali yetu sikivu na 'inayojali utu' imeshikwa na kigugumizi? Je, kweli waliomteka ni watu wa serikali au maadui zake ili kukinukisha?
Je, nani watafaidika na kuondolewa Polepole? Je, Polepole alikuwa anajua hatari ya mambo aliyokuwa akifichua?