Je, nitumie mbao gani kutengeneza frame za milango na milango bora?

Je, nitumie mbao gani kutengeneza frame za milango na milango bora?

Mninga, mkongo, ni mzuri.
Pia sasahivi kuna mtu wa porini unaitwa mpanganga una ranging nyeusi ama kahawia nimzuri pia ngumu na unakubali vanishi.

Fremu za hiyo miti yote ni 140,000/= na top ni 250,000 single na 350,000/= double.
Habari mkuu. Nimependa hizi bei alafu niko stage hii. Fundi wa wapi huyu anafanya Mkongo/Mninga kwa 140k per fremu.. Pls niungishe
 
Hata kama utaweka frame za chuma lakini huwezi kuruka kuwema frame za mbao plus top zake na bei ya mninga ipo juu kidogo japokuwa wabongo sometimes wahuni wanatumia mbao nyingine kisha wanapaka rangi feki feki kama hujui mbao ndiyo unakuwa umeligwa changa la macho
Mkuu mlango mkubwa na ule wa uani usitumie mbao,weka mlango wa bati gumu tumezoea kuita geti.Usiweke fremu ya mbao wala top ya mbao.Tafuta fundi mzuri geti litapendeza na gharama yake kwa dar ni kiasi cha laki mbili na nusu kwa kila geti.
 
Habari wakuu,natumaini mko poa..

Nina ishu ktk kumalizia kibanda changu, nahitaji frame za milango na milango/top kwa ajili ya milango ya nje miwili mkubwa (double) na mdogo wa kawaida.
Kwa wataalam naomba ushauri

1. Ni mbao zipi zinafaa kwa ajili ya frame na zipi kwa ajili ya milango/top?

2. Je ipi bajeti/bei yake ili nijiandae financially kwa ajili ya hiyo milango miwili mpaka ikamilike.

Kumbuka nina kiasi cha kuunga unga kwa ajili ya hii kazi ili ikamilike nihamie kwangu.
kwa ufupi nahitaji frame na milango mizuri japo iwe na kiwango cha kuridhisha.
Mbao za miti pori..
Mahogany
Mvule nk
 
Back
Top Bottom