Je, nimuache huyu msichana?

Je, nimuache huyu msichana?

Wewe ni mpumbavu sana, naona humpendi huyo binti ila kwa kuwa huna akili na hujui unataka nini bado uko nae... Wewe ni JINGA sana. Motherfucker weeee
 
Wakati huna kaz alipokuvumilia yeye hakukuona mkosi ila yeye leo maradhi yamemsibu ndo unamuona mkosi aah mie nyie wanaume mmeshanishinda
 
Napita huku nkitafakari hali ngumu ya maisha inavyozidi kushamiri kuliko mapenzi
 
Yaan aliesema huna akili alipatia kbs. Hv unaanzaje kujisikia vzr kuona mgonjwa anajiburuza chini kwaajili yako. Na wewe ni mbinafsi kwsbb unajiangalia upande wako bila kufikiria mwenzio alikuwa anapata maumivu kiasi gani ktk harakati za kutaka kusimama.
Ningekuwa mm ht makofi ningekuchapa, na wewe ndio utakuwa na nuksi maana hujielewi.
 
Tena hao ndugu zake hyo binti wametumia busara, mwenzio anaumwa anajiburuza kukupikia na ww unakula na vinashuka?! Makubwa jaman mi cjawah kuona tangu na tangu... yani mtu akupnde, akusaidie kifedha na akupe ushaur lkn unamuacha bila kisa kisha unampa sifa ya kuwa na nuksi... masikini binti wa watu... Muache, usizid kumpotezea muda....ataumia lkn yataisha kuliko hayo unayomfanyia sasa hivi...!
 
Mkuu umenisikitisha sana, hata mimi nakwambia hutumii akili, yani unakubali mpenzi wako mwenye matatizo ya miguu akuhudumie pasipo na msaada wako kweli inaingia akilini!!!? wewe ulipaswa kuwa mfariji kwake na mtu wa kwanza kumsaidia kutokana na hali yake, na ukimuacha nakuhakikishia utapata laana na NUKSI kubwa kuliko hiyo unayofikiri ni laana, Mungu sio wa mchezo mchezo.
Jaribu kufikiri ingekuwa wewe ndio umepata huo ulemavu halafu mkeo anasubiri umuandalie chakula na ulemavu wako bila kumsaidia, ungeendelea kumpenda?? lakini huyo binti pamoja na hali yake, tabia yako mbaya bado anakupenda. Mkuu narudia tena tumia akili kuamua na kufikiri. Kiukweli umeniharibia siku yangu kwa huo ukatili unaomfanyia huyo binti mlemavu.
Yani nmemshangaa kweli huyu mtu Mkuu, anajifnya kachukia, kilichimchukiza hpo ni kipi au kuambiwa ukweli.. ye angekuwa hyo ni mdogo wake anatendewa hyo anayomtendea mtoto wa watu angejisikiaje.. kweli kuna viumbe wazito duniani, mimi pia kaniharibia siku..!
 
Natumai we ni kijana mwenzangu. Ushauri wangu kwako. Msichana/ binti/ mmama ambaye yuko radhi kukuvumilia ukishindia na ugali maharage asubuhi kamwe usimwache. Nakuambia kama kijana mwenzangu. Nakumbuka akati nasoma nilimwacha binti wa watu aliye jitolea kwangu bila ata ya sababu maalumu. Kuna muda na mmisi lakini ndo nisha chelewa. Umri wako unakaribia kuoa au ulitakiwa uwe usha oa. Ukiwa na miaka 27 kwa umri huo itakegemea na wewe kama umekwisha vipanga au rah. Huo ni umri ambao angalua uwe n uwezo wa kumvumilia mwanamke kwa maana ndo unajiandaa kuwa baba wa familia. Yangu ni hayo mkuu usiku mwema
 
Naomba nikuulize swali moja tu na unijibu ukweli. Ni hivi Katika kujiburuza buruza kwake wakati anapokuona kwa maana ya kukupokea au kukuandalia chakura wewe reaction yako ilikuwa inakuwaje na hasa mbele za nduguze.
Kwa namna anavyojieleza unywanywa wake atakuwa anacheka mpaka machozi hyu...Mkuu!
 
mkuu inaonekana huyo mwanamke kakupenda na wewe umelijua hilo, ndio maana unamsumbua,
mara kumuacha bila sababuu,mara kumrudia kwa kua amekubembeleza sana na kukulilia na kukuomba msamaha bila kosa lolote. anakusaidia,anakushauri anakuwezesha ukihitaji msaada.

wewe,uliyonayo kichwani ni nuksi pindi upatapo matatizo,kwani matatizo ya miguu yake nuksi ni wewe?!! mbona hajakuacha?!! Mara ndugu zake,kwani unahakika gani kua ndg zako wote wanampenda?!!

kiuhalisia hakuna balanced love,na nakuambia ukiendelea na hio tabia ya kumkasirikia pindi yanapotokea matatizo,ipo siku atachoka ataenda zake,hapo ndio utaelewa maana ya mema anayoyafanya juu yako. watu km huyo mwanamke hawpo duniani pengine amebaki huyo tu. ukitoka hapo utawakuta vyura wa mjini utatamani uzirudishe siku nyuma.
 
mkuu inaonekana huyo mwanamke kakupenda na wewe umelijua hilo, ndio maana unamsumbua,
mara kumuacha bila sababuu,mara kumrudia kwa kua amekubembeleza sana na kukulilia na kukuomba msamaha bila kosa lolote. anakusaidia,anakushauri anakuwezesha ukihitaji msaada.

wewe,uliyonayo kichwani ni nuksi pindi upatapo matatizo,kwani matatizo ya miguu yake nuksi ni wewe?!! mbona hajakuacha?!! Mara ndugu zake,kwani unahakika gani kua ndg zako wote wanampenda?!!

kiuhalisia hakuna balanced love,na nakuambia ukiendelea na hio tabia ya kumkasirikia pindi yanapotokea matatizo,ipo siku atachoka ataenda zake,hapo ndio utaelewa maana ya mema anayoyafanya juu yako. watu km huyo mwanamke hawpo duniani pengine amebaki huyo tu. ukitoka hapo utawakuta vyura wa mjini utatamani uzirudishe siku nyuma.
They say u never know what u have until u loose it...
 
Habari ndugu zangu,

Ninakuja kwenu nikiwa na tatizo. Naomba mwenye ushauri wa kujenga anisaidie. Mimi ni kijana mwenye umri wa miaka 27. Nina msichana ambaye ninampenda sana naye sina shaka kuwa ananipenda sana. Toka nikiwa sina kazi, huyu msichana alikuwa bega kwa bega na mimi. Alijitoa sana kwangu. Na mpaka sasa nikiwa na shida, anakuwa mstari wa mbele kunisaidia.

Tatizo lililonifanya nije kwenu kuomba ushauri, ni juu ya ndugu zake. Huyu msichana ni mkubwa na ana ndugu zake watatu, wawili ni vijana mapacha ambao kwa sasa wana umri wa miaka 24.

Kuna kipindi huyu msichana aliwahi kupata matatizo ya mguu. Ni kipindi ambacho kiukweli aliumwa na bado ni kipindi ambacho nilikuwa nimepata kazi na bado nikamuacha. Hakuwa amenikosea bali niliwmona kama nuksi hivi, kwani nilifukuzwa kazi bila sababu za msingi nikiwa bado na huyu binti.

Bado alikuwa mstari wa mbele kunipa ushauri na kunisaidia hata kipesa. Nilipopata kazi nikaona ni kheri kumuacha. Huyu msichana alikuwa akilia kila siku. Aliugulia ugonjwa na bado akaugulia kuachwa nami.

Baada ya binti kuniomba msamaha sana hata kwa kutokuwa na kosa, nikamrudia kwani hata mimi bado nilimpenda.

Baada ya kumrudia binti, tukawa nae karibu. Hakuwa anaweza kutembea kipindi hicho lakini nilipoenda kumsalimia, alijiburuta chini ili kunipokea. Muda mwingine alijiburuta kunitengea chakula au hata kupika huku akitambaa.

Haya yote aliyafanya hata mbele za ndugu zake. Waliona upendo wa binti huyu kwangu. Ikafika kipindi anajilazimisha kunyanyuka kwa ajili yangu. Kumbe akifanya hivyo, anakuwa akijiumiza.

Baada ya kuona hayo, kaka zake wakaanza kunichukia. Mmoja aliniita na kunishutumu kwa maneno makali sana. Kusema ukweli sikupendezwa na kauli zake kwasababu ilikuwa ni kama amenidharau. alinitamkia kuwa situmii akili kabisa.

Ndugu wana jamii, kauli hiyo imeniudhi na hata msichana mwenyewe akinipigia simu nakasirika sana. Natamani kumuacha sababu naogopa kama hivi tu tumeanza kugombana hapo baadaye je, itakuwaje? Sina amani ninapokuwa na msichana huyu. Amenililia sana, ameniomba msamaha sana ila mim moyoni mwangu nina kinyongo kutokana na hizo shutuma.

Ndugu wana jamii, nitakuwa nimekosea kumuacha huyu msichana kweli? Kama ungekuwa wewe ungefanya nini?

Naombeni ushauri wenu.

To be honest akili yako inamchukia sababu ya matatizo yake huyo mwanamke ila sio kwa shutma..kama humpendi achana nae tends kwa utapopendwa..ila angalia ucje rudi kuomba ushauri namna ya kumrudia uyo nuksi wako.
 
Habari ndugu zangu,

Ninakuja kwenu nikiwa na tatizo. Naomba mwenye ushauri wa kujenga anisaidie. Mimi ni kijana mwenye umri wa miaka 27. Nina msichana ambaye ninampenda sana naye sina shaka kuwa ananipenda sana. Toka nikiwa sina kazi, huyu msichana alikuwa bega kwa bega na mimi. Alijitoa sana kwangu. Na mpaka sasa nikiwa na shida, anakuwa mstari wa mbele kunisaidia.

Tatizo lililonifanya nije kwenu kuomba ushauri, ni juu ya ndugu zake. Huyu msichana ni mkubwa na ana ndugu zake watatu, wawili ni vijana mapacha ambao kwa sasa wana umri wa miaka 24.

Kuna kipindi huyu msichana aliwahi kupata matatizo ya mguu. Ni kipindi ambacho kiukweli aliumwa na bado ni kipindi ambacho nilikuwa nimepata kazi na bado nikamuacha. Hakuwa amenikosea bali niliwmona kama nuksi hivi, kwani nilifukuzwa kazi bila sababu za msingi nikiwa bado na huyu binti.

Bado alikuwa mstari wa mbele kunipa ushauri na kunisaidia hata kipesa. Nilipopata kazi nikaona ni kheri kumuacha. Huyu msichana alikuwa akilia kila siku. Aliugulia ugonjwa na bado akaugulia kuachwa nami.

Baada ya binti kuniomba msamaha sana hata kwa kutokuwa na kosa, nikamrudia kwani hata mimi bado nilimpenda.

Baada ya kumrudia binti, tukawa nae karibu. Hakuwa anaweza kutembea kipindi hicho lakini nilipoenda kumsalimia, alijiburuta chini ili kunipokea. Muda mwingine alijiburuta kunitengea chakula au hata kupika huku akitambaa.

Haya yote aliyafanya hata mbele za ndugu zake. Waliona upendo wa binti huyu kwangu. Ikafika kipindi anajilazimisha kunyanyuka kwa ajili yangu. Kumbe akifanya hivyo, anakuwa akijiumiza.

Baada ya kuona hayo, kaka zake wakaanza kunichukia. Mmoja aliniita na kunishutumu kwa maneno makali sana. Kusema ukweli sikupendezwa na kauli zake kwasababu ilikuwa ni kama amenidharau. alinitamkia kuwa situmii akili kabisa.

Ndugu wana jamii, kauli hiyo imeniudhi na hata msichana mwenyewe akinipigia simu nakasirika sana. Natamani kumuacha sababu naogopa kama hivi tu tumeanza kugombana hapo baadaye je, itakuwaje? Sina amani ninapokuwa na msichana huyu. Amenililia sana, ameniomba msamaha sana ila mim moyoni mwangu nina kinyongo kutokana na hizo shutuma.

Ndugu wana jamii, nitakuwa nimekosea kumuacha huyu msichana kweli? Kama ungekuwa wewe ungefanya nini?

Naombeni ushauri wenu.
Hii uzi naona watu wamekomenti
Kwa mihasira, wengine kejeli,
Wengine masihara,

Hapa sina la kusema
Wacha nipite tu mkuu...
Maoni ushayapata kwa wadau mbalimbali.

 
Kama umeshamchoka sema au hiyo hali alokua nayo umeona itakua stress kwako pia sio mbaya ukamuacha
ila kumbuka asowaka ana Mungu,na mwenyezi mungu hakupi kilema akakosesha mwendo, leo ndio maneno ya kaka zake
yanakuchefua leo ndio kawa Nuksi? haya nenda kaka usije kuchelewa lakini kumbuka mwenyezi mungu ni wawatu wote
atasimama huyo kwa uwezo wa mungu na huenda kuondoka kwako wewe kwenye maisha yake ndio mwanzo ya furaha
yake...
 
Unaoa binti na siyo kaka zake. Labda kama una sababu nyingine.
 
Tatizo lako kubwa unaogopa kumwacha mwenzio wakati akiwa na matatizo unafikiria jamii itakufikiriaje
 
Pole sana pole sana. Huyo dada anakupenda sana ila kama unahis humpendi utamtesa muache alie sasa hivi Mungu aje amfute badae. Umemuita nuksi umekosea umuombe msamaha maana huyo unaewaza atakuwa baraka anaweza kuwa nuksi mara mbili zaid
 
Back
Top Bottom