Je ni uoga tu au kuna la zaidi?

De Novo kutokana na takwimu kutuonyesha kuwa wanandoa wanaongoza kwa UKIMWi, huoni kama kuna umuhimu wa kubadilika kwa kuweka utaratibu maalumu wa kupima kila baada ya muda flani? Maana slogani za badili tabia naona kama zimegonga mwamba kwa maana kuwa watu wameamua kufanya kuwa ni hulka yetu kumega/gwa nje ya mahusiano yetu ya ndoa wakenya wanasema mpango wa nje!
naungamkono hoja... nadhani haijalishi kama watu wanakaa mbali au karibu... periodic testic ni nzuri hasa kwa watoto na couples wenyewe kwani wanweza kujipanga zaidi na hata kuepusha maabukizi zaidi (kama yapo)

cha maana sasa ni advocacy na uamsho wa ziada watu kukubali kupima. Now the question still lingers; hivi ni kweli kwamba wanaohitaji sensitization ni wanaume pekee?

Je kwanini tusiweke sheria kwamba kupima ni lazma?

Kuna mradi wa PITC (provider initiated testing and counselling)... hapa nadhani tungetilia mkazo kiasi kwamba hata kama unaenda kutibiwa kidonda uwe unapata test; watoto wa nursery wote wapimwe ili kujiandaa kuwalea vizuri na hata wanaotafuta medical clearance nao wapimwe... mwanzo utakua mgumu lakini baada ya 2 years tutazoea tu
 
MJ1, wakati tukifikiria along those lines, unakumbuka kiapo cha ndoa? cha kwanza ni UAMINIFU!

Hivi, utajisikiaje, kwa vile tu umeenda kusoma au mmetengana kwa sabau za kikazi mwenzio anakujia na kukwambia ukapime HIV? maana yake ni kwamba HAKUAMINI...I stand to be corrected...hata aipambe2 vipi kwamba ooh unajua ni hatari, ooh hata JK kapima ...lakini mi nadhani atakuwa ameshakuhisi vibaya. Utajisikiaje kama umekuwa mwaminifu kipindi hicho chote?

na utakapokuja kuniambia tukapime DNA unadhani mie nitajickuiaje?..hii thread ya leo mie nipo nipo tu kama nyanya za nyongeza, kwangu yote mawili magumu.
 
siogopi....
but why nipime wakati
kuchovya chovya sina mpango wa kuacha karibuni????
nitapima nikiwa tayari kwa ndoa....
nimepima last year....but sikurudi kupima tena
after three months....

lengo la kupima ni kama unataka kuacha kutumia condom
mimi hata msichana akiwa bikra natumia condoms

hahaha jibu lako limenivutia
endelea kuwa makini The Boss
ABC naona unazifata vizuri
 
MJ1, wakati tukifikiria along those lines, unakumbuka kiapo cha ndoa? cha kwanza ni UAMINIFU!!

Ni kweli inatupasa kukumbuka kiapo lakini Kaizer reality inaonyesha kuwa wengi hatuzingatii kiapo hiki-otherwise UKIMWI ndoani ungekuwa ni hadithi ya kuisikia tu. Tusifumbie macho reality jamani kisa kiapo. Mimi nawakumbusha uaminifu siku hizi hakuna dunia imebadilika. Nina mifano hai mingi tu ambapo mke/mume amemletea mwenzake huu ugonjwa pamoja na kuwa walikula kiapo.

Hivi, utajisikiaje, kwa vile tu umeenda kusoma au mmetengana kwa sabau za kikazi mwenzio anakujia na kukwambia ukapime HIV? maana yake ni kwamba HAKUAMINI...I stand to be corrected...hata aipambe2 vipi kwamba ooh unajua ni hatari, ooh hata JK kapima ...lakini mi nadhani atakuwa ameshakuhisi vibaya. Utajisikiaje kama umekuwa mwaminifu kipindi hicho chote?!

Sio Ukapime Kaizer- tukapime. Ndio maana nikasema tukishawezakuifanya kuwa utaratibu wa kawaida ndani ya nyumba sidhani kama italeta hisia tofauti. Kumbuka wewe unawezakuwa umejitunza but mie nikateleza so usiniamini kihivyo love kwa ababu kosa likitokea ni la maisha si kuwa unaweza ku-undo.


yeah tulishajiandaa, lakini tulimhonga kwanza MC apeleke mambo chap chap..shangazi tukamweka sawa kabla.....afu mshenga alikuwa na desa la maswali...lol mambo mswano!

hapo Blue I hope Kova hajaiona maana siku hizi yeye ndo TAKUKURU. Am happy kama kila kitu kilikwenda sawa bin sawia
 
MJ1, wakati tukifikiria along those lines, unakumbuka kiapo cha ndoa? cha kwanza ni UAMINIFU!

Hivi, utajisikiaje, kwa vile tu umeenda kusoma au mmetengana kwa sabau za kikazi mwenzio anakujia na kukwambia ukapime HIV? maana yake ni kwamba HAKUAMINI...I stand to be corrected...hata aipambe2 vipi kwamba ooh unajua ni hatari, ooh hata JK kapima ...lakini mi nadhani atakuwa ameshakuhisi vibaya. Utajisikiaje kama umekuwa mwaminifu kipindi hicho chote?

na utakapokuja kuniambia tukapime DNA unadhani mie nitajickuiaje?..hii thread ya leo mie nipo nipo tu kama nyanya za nyongeza, kwangu yote mawili magumu.

ama kweli nyamayao umerudi lol eti nyanya za nyongeza- kama naziona.

Hili ni swali zuri sana kwa kaizer na ndio lililobeba ujumbe mzima wa thread hii- kwa nini iwe rahisi kwa wao kutaka (maana huwa hawaombe wala kushauri) kupima DNA ambayo hata uipambe vipi inatoa ujumbe wa 'mke wangu siamini kama huyu baby ni wangu.'
 
hope uliniwakilisha kwenye sendoff ma luv.....hii nguo c ndio tulicmama nayo altareni cku zile... remember?

yes babe, I remember....ngoja nikdediketia kawimbo leo....

[ame]http://www.youtube.com/watch?v=YjUaWiy_QXc[/ame]
 
hahaha FL1, unadhani hajitambu ki ivyo hadi akatambuliwe na vitambuzi vinavoweza kukutambua vinavyotambua vyenyewe? LOL

Anaweza kuwa hajitambui bwana ..unaweza banjuka mala moja ukaukwaaa na pia inawezekana ukabanjuka more than a million lakini usiukwae
Epuka kuchangia ,Mikasi ,Wembe ,....nk nk
 
ama kweli nyamayao umerudi lol eti nyanya za nyongeza- kama naziona.

Hili ni swali zuri sana kwa kaizer na ndio lililobeba ujumbe mzima wa thread hii- kwa nini iwe rahisi kwa wao kutaka (maana huwa hawaombe wala kushauri) kupima DNA ambayo hata uipambe vipi inatoa ujumbe wa 'mke wangu siamini kama huyu baby ni wangu.'

hapo kwangu ndio tatizo, nitajiuliza mara 100 kwamba ameonaje/hic nini mpaka kafikiria tukafanye hivyo, kwamba haamini watoto anaowalea sio wake? na kwanini haamini wakati mie najua 100% ni wake, bac habari mgongano tu hapo...kuhusu HIV hapa kwangu sio tatizo sana, najiamini na naiamini mienendo yangu, tatizo na yeye anaiamini yake? ukimwambia wazo hilo utaanzishiwa historia.....ndio mana nasema wala cjielewi kwenye hii thread.
 
hapo kwangu ndio tatizo, nitajiuliza mara 100 kwamba ameonaje/hic nini mpaka kafikiria tukafanye hivyo, kwamba haamini watoto anaowalea sio wake? na kwanini haamini wakati mie najua 100% ni wake, bac habari mgongano tu hapo...kuhusu HIV hapa kwangu sio tatizo sana, najiamini na naiamini mienendo yangu, tatizo na yeye anaiamini yake? ukimwambia wazo hilo utaanzishiwa historia.....ndio mana nasema wala cjielewi kwenye hii thread.
Tatizo hapa ukimwuliza atakuuliza if humwamini na atakuuliza if you are cheating sasa sijui ukimjibu you are not atakuamini? Na hata akikuamini does the 'no' means the truth?

ninapokwambia no sijatoka nje ya ndoa yangu, ina maanisha ni kweli sijatoka? kiasi cha wewe kama mume uniamini kihivyo?
 
Ni kweli inatupasa kukumbuka kiapo lakini Kaizer reality inaonyesha kuwa wengi hatuzingatii kiapo hiki-otherwise UKIMWI ndoani ungekuwa ni hadithi ya kuisikia tu. Tusifumbie macho reality jamani kisa kiapo. Mimi nawakumbusha uaminifu siku hizi hakuna dunia imebadilika. Nina mifano hai mingi tu ambapo mke/mume amemletea mwenzake huu ugonjwa pamoja na kuwa walikula kiapo.

Hapo juu nakubaliana na wewe moja kwa moja luv,lakini essense ya sredi tangu mwanzoni haikuwa ivo,,hebu angalia hapa chini,

Sio Ukapime Kaizer- tukapime. Ndio maana nikasema tukishawezakuifanya kuwa utaratibu wa kawaida ndani ya nyumba sidhani kama italeta hisia tofauti. Kumbuka wewe unawezakuwa umejitunza but mie nikateleza so usiniamini kihivyo love kwa ababu kosa likitokea ni la maisha si kuwa unaweza ku-undo.
Sasa hivi mjadala unaweza kuwa balanced kwa maana ya kwamba labda uedit bandiko la mwanzoni kabisa ambalo ni:

hivi inakuwaje ni rahisi kwenu kuwaambia wake zenu mkacheck vinasaba (DNA) kwa watoto wenuat the same time ni ngumu kwenu mkiombwa mkacheck afya zenu (HIV/AIDS/STDs)? hasa pale ambapo kumekuwa na umbali kidogo kati yako na mwenzi wako either due to kika au masomo? (Yaani kama kuna separation ya aina flani)
 
Hivi, utajisikiaje, kwa vile tu umeenda kusoma au mmetengana kwa sabau za kikazi mwenzio anakujia na kukwambia ukapime HIV? maana yake ni kwamba HAKUAMINI...I stand to be corrected...hata aipambe2 vipi kwamba ooh unajua ni hatari, ooh hata JK kapima ...lakini mi nadhani atakuwa ameshakuhisi vibaya. Utajisikiaje kama umekuwa mwaminifu kipindi hicho chote?

na utakapokuja kuniambia tukapime DNA unadhani mie nitajickuiaje?..hii thread ya leo mie nipo nipo tu kama nyanya za nyongeza, kwangu yote mawili magumu.

Ki ukweli sio sahihi kabisa kwa mpenzi wako ambaye mko nae mbali kukuomba ukapime HIV. Yani akikwambia hivyo siku moja jua amekosa imani na wewe!
 
Ki ukweli sio sahihi kabisa kwa mpenzi wako ambaye mko nae mbali kukuomba ukapime HIV. Yani akikwambia hivyo siku moja jua amekosa imani na wewe!
Napata shida kweli hapa hasa nikifikiria risk tunayocheza nayo in the name of UAMINIFU upo ndani ya ndoa!! Mi jamani nikifikiria kukiacha kibaby changu huku nisijue kinalelewaje inaniuma sana unless tuseme sasa tumeamua kuuchukulia ugonjwa huu kama malaria tu kuwa upo na ukiupata its part of life (Sisemi kuwa ukiupata ni kifo la hasha kwani najua kuna wanaoishi hata baada ya kuupata but jamani kama tuna uwezo wa kuzuia kwa nini tusizuie?


Tujenge mazoea ya kupima wapendwa yaani iwe among out life's menu please
 
Kwani wanawake ni wepesi wa kwenda kupimwa virusi? Naombeni takwimu tafadhali....

Hakuna sehemu inayosema kuwa wanawake ni wepesi kupima UKIMWI mimi nimeiweka hivyo kwa kuwa kuna thread ilishawahikurushwa juu ya upimaji wa DNA kwa wenetu na ikaonyesha kuwa wanaume walikuwa so possitive kwenye kupima DNA ndo nikauliza why uwepesi huu usiwe na kwenye VVU/UKIMWI?
 
Hao ni waoga tu,

UKIMWI tukapime wote ili tufanye comparison ya majibu, kama mimi ni -ve naye ni +ve itakuwa ni habari njema tu.

DNA, mnh.
 
Hakuna sehemu inayosema kuwa wanawake ni wepesi kupima UKIMWI mimi nimeiweka hivyo kwa kuwa kuna thread ilishawahikurushwa juu ya upimaji wa DNA kwa wenetu na ikaonyesha kuwa wanaume walikuwa so possitive kwenye kupima DNA ndo nikauliza why uwepesi huu usiwe na kwenye VVU/UKIMWI?

Lakini MwanajamiiOne, kupimwa virusi na kupima dna kuhakikisha kama kweli mtoto ni wako ni vitu viwili tofauti ingawa vyote ni vya muhimu. Hebu jiweke ktk nafasi ya mwanamme ambaye kadanganywa na kubambikiwa mtoto asiye wake halafu akamlea na baadaye kuja kugundua kuwa si wake? Utajisikiaje kama ni wewe? Hakuna mtu ambaye anapenda kutwishwa jukumu ambalo si lake na ni kutokana na udanganyifu wa baadhi ya wanawake ndio maana baadhi ya wanaume wanakuwa wepesi kuomba upimaji wa dna kufanywa ili wahakikishe kweli majukumu yaliyopo mbele yao ni yao kweli. Na hilo halina ubaya wowote na mwanamke kama ana uhakika baba ni nani wala hatabisha wala kusita kwenda kupima. Tunaishi kwenye dunia ya kutokuaminiana siku hizi.
 
Habari ndugu

naombeni tusaidiane kuelewana kina wapwa na binamu kwa sababu - kwa wanaume rahisi kuwaambia wake zenu mkacheck vinasaba (DNA) kwa watoto wenu at the same time ni ngumu kwenu mkiombwa mkacheck afya zenu (HIV/AIDS/STDs)? hasa pale ambapo kumekuwa na umbali kidogo kati yako na mwenzi wako either due to kika au masomo? (Yaani kama kuna separation ya aina flani)

Na kina dada naambiwa nasi tu wagumu kukubali kucheck vinasaba- pamoja na ukimwi

Je mnataka tuamini ule usemi kuwa wanaume hawawezikukaa bila kumega nje?
Na je mnapomega nje huwa hamtumii kinga? Maana kama mnatumia kwa nini mnaogopa sana kucheck afya?

Nisaidieni tafadhali

MJ1,

Kwani inachukuwa muda gani kuambukizwa HIV au kupata mimba nje ya ndoa?

HIV au mimba is a matter of minutes and not hours or days! So kama unawasiwasi na mwenzi wako kiasi hicho inabidi mpime kila siku kabla ya kufanya tendo la ndoa. Believe me, kama ni fisadi wa ngono anaweza kwenda kazini asubuhi akiwa mzima (HIV -ve) lakini akirudi nyumbani jioni ni HIV +ve!
 
Back
Top Bottom