Kindeena
JF-Expert Member
- Sep 27, 2017
- 9,258
- 16,264
Asante upo vizuri mkuuKuna baadhi ya miti ya matunda ina mizizi korofi sana. Mmoja wapo ni parachichi. Hasa hizi parachichi za asili. Pia kuna mti unajulikana kama grevilia(uchagani miti hii imejaa sana). Mizizi ya grevilia inajua sana kujipenyeza. Hii miti miwili usipande kabisa karibu na nyumba.
Mwembe wacha angalau mita 7 hadi 10 kutoka ukutani. Ukiachana na suala la mizizi pia matawi yake hujiachia sana kadri mti unavyozidi kukua.
Fenesi nao huwa unakua mkubwa sana. Huu panda shambani huko.
Jamii yote ya michungwa(chungwa, ndimu, chenza, limao). Kuanzia mita 4 hadi 7 toka usawa wa ukuta haisumbui.
Topetope, komamanga, nayo yote umbali kama wa michungwa tu bila kusahau mapera.
Stafeli huwa inarefuka sana. Zambarau pia weka shamba huko huu unakuaga mkubwa mno.
Mtanisahihisha kama kuna sehemu nimekosea