Je, ni salama kwa kiongozi mkuu wa nchi kufanyiwa dhihaka?

we naweee.. ndo kujipendekeza auuuu.. unajifanya ZOMBI
ila yeye anapowambia nyie kuwa KATeRERO NYIE... KISONONO NYIEE.... MAAFA NYIE... UKIMWI NYIEEE.... dhihaka hii unaiona ni sawa au tukubali tu kuwa jamaa ni kichaa mgonjwa fresh ??
Kwa hiyo akiongea namna hiyo ndio tiketi ya mimi na wewe kumtukana yeye binafsi?. Ameongelea nyiee hakusema wewe au yule.
 
Ivi mtu akikwambia yeye ni KICHAA unaelewaje?

NB: Tumia akili kabla hujanijibu.
Inategemea na mazingira ya mtu kusema hivyo. Anamaanisha wakati mwingine kushughulika na watanzania unahitaji kuwa roho ngumu ya kufanya maamuzi pasipo kumtazama mtu usoni.

Unafanya maamuzi bila ya kusikiliza maoni au mawazo ya kundi la watu, kwa faida ya wengi kuliko hao wachache ambao lazima watakukosoa.
 
Inategemea na mazingira ya mtu kusema hivyo. Anamaanisha wakati mwingine kushughulika na watanzania unahitaji kuwa roho ngumu ya kufanya maamuzi pasipo kumtazama mtu usoni.

Unafanya maamuzi bila ya kusikiliza maoni au mawazo ya kundi la watu, kwa faida ya wengi kuliko hao wachache ambao lazima watakukosoa.
hayo mazingira basi ndo hayohyo tumeyatumia kujibu msikasirike tu
 
tuepuke matusi.N

atoa taadhari kwa wote,ni muhimu kuzingatia.kwa kuwa Mh Rais ni mtiwa mafuta kwa Bwana ni kosa na dhambi kwa Mungu kumnenea mabaya,kumtukana hata kumtweza,yeyote anayefanya hayo atakutana na mkono wa Mungu aliyemweka pale. Awe ni mdhaifu au awe na tatizo lolote hatupaswai kumnenea mabaya wala kumnyoshea kidole.unapofanya hivyo actually unamfanyia Mungu aliyeruhusu awepo hapo.
HIVI MTIWA MAFUTA WA BWANA ANARUHUSIWA KUJITUKUNA NA KUJINENEA MABAYA KWA KUJIITA KICHAA
 
Katika jamii yeyote ya watu wanaoheshimu utu na kustarabika.Jamii ya watu wanaopenda watoto wao wawe watu wa heshimu,ni lazima kujenga desturi ya kuheshimiana.kuna tabia inaanza kujengeka ya baadhi yetu kudhani kuwa unapomtukana kiongozi unapata sifa,lakini swali la kujiuliza ikiwa ungekuwa wewe ndio unafanyiwa hivyo ungefurahi.

Nchi zetu hizi zinaongozwa na wanadamu ambao si wakamilifu,kama tutaamua tu kuangalia mabaya ya viongozi wetu tutayaona lakini je hakuna mazuri yanayoweza kutufanya tuone umuhimu wa kuwaheshimu.maandiko matakatifu yanatuonya kuwaheshimu viongozi wetu kwa sababu wamewekwa na Mungu kwa makusudi yake mwenyewe.

Magufuli alipokwenda kuchukua form ya kuomba kugombea Urais wengi wetu tulimchukulia tu kama msindikizaji LAKINI MUNGU alimchagua ndio awe kiongozi wetu.

Ombi langu kwenu wote tunapaswa kumheshimu na kumsaidia ili atuongoze mpaka muda wake utakapokwisha.Kumbukeni anaweza akawa amekosea kwa mtizamo wako lakini kwa maslahi mapana ya nchi anapaswa kuungwa mkono.

Magufuli anajenga Reli ambayo itakuwepo kwa miaka mingi ijayo,si kwa manufaa yake bali kwa manufaa ya nchi,Magufuli anajenga miundombinu mikubwa ya kuzalisha umeme ambayo itakuwepo miaka mingi hata baada ya yeye kuondoka lakini kwa ajili ya nchi.Pale ambapo tunahisi Mh amekosea ni vyema kutumia lugha ya staha na heshima.tuepuke matusi.N

atoa taadhari kwa wote,ni muhimu kuzingatia.kwa kuwa Mh Rais ni mtiwa mafuta kwa Bwana ni kosa na dhambi kwa Mungu kumnenea mabaya,kumtukana hata kumtweza,yeyote anayefanya hayo atakutana na mkono wa Mungu aliyemweka pale. Awe ni mdhaifu au awe na tatizo lolote hatupaswai kumnenea mabaya wala kumnyoshea kidole.unapofanya hivyo actually unamfanyia Mungu aliyeruhusu awepo hapo.

Adhabu yake huwa mbaya inakwenda mpaka kizazi cha nne.ONYO JIEPUSHENI NA DHAMBI HIYO YA KUMNENEA MABAYA MPAKWA MAFUTA WA BWANA.
Kwanza Mungu hakupiga kura tusidanganyane
Pili ni kweli sio sahihi kumdhihaki kiongozi au hata mtu yoyote haijalishi anakosea au yupo sahihi
Tatu mjue namna yakutofautisha dhihaka na kukosolewa viongozi wetu ukimkosoa anachukulia ni kumtusi au kumdhihaki
Nne na mwisho usipojiheshimu hautaheshimika hata ukitumia mamlaka yako uliyonayo na unapokataa kumsikiliza mtu au kumnyima nafasi yakuongea tegemea kutukanwa tu haijalishi ww ni nani?
 
we naweee.. ndo kujipendekeza auuuu.. unajifanya ZOMBI
ila yeye anapowambia nyie kuwa KATeRERO NYIE... KISONONO NYIEE.... MAAFA NYIE... UKIMWI NYIEEE.... dhihaka hii unaiona ni sawa au tukubali tu kuwa jamaa ni kichaa mgonjwa fresh ??
Tatizo hawa wenzetu wanamtetea sana mtu kama ameamua kuifundisha jamii inabidi awe refa yaani azungumzie pande zote mbili lakin yy ameshaonesha kama mkubwa huwa hakosei bado anahitaji tumuelewe
 
Sina sababu ya kujipendekeza na wala hakuna haja ila nimetoa taadhari.hivi kule kwenu baba akisema neno ambalo unahisi amekosea unafanyaje. Unamtukana au unatafuta namna bora ya kumweleza
Ulisikia wapi baba anachaguliwa kwa kura?
Au ulisikia wapi familia inaongozwa kwa katiba?
Au ulisikia wapi mtoto anakua baba na baba anakua mtoto?

Kama tunakosoana kwa mujibu wa katiba haina ubaya maana tunalijenga taifa moja. Mambo ya kuwavika utukufu watu, ndio maana mpaka leo tu watumwa
 
Sina sababu ya kujipendekeza na wala hakuna haja ila nimetoa taadhari.hivi kule kwenu baba akisema neno ambalo unahisi amekosea unafanyaje. Unamtukana au unatafuta namna bora ya kumweleza
Ulichotakiwa nikuzungumzia pande zote mbili sio kusema huyo baba hajakosea na baba ni mtu mzima na yupo na mtoto hii kesi ni tofauti kwenye siasa wote ni watu wazima tofauti vyeo tu so mfano wako hauendani nq uhalisia huo
 
Back
Top Bottom