Hizi hasira ni maisha kupanda au nini?
Hebu tueleze baba mtoto ni nani na yupo wapi?! Je, huyu wa sasa mara ya kwanza alipoanza kubadilika ni jambo gani aliongea ambalo lilikufanya ujue umezingua wapi?!
Kwa kutumia mbinu zangu za kiinteligencia naweza kubaini mambo kadhaa.
1. Wewe una tabia za kuvimbia wanaume wako. Sababu hadi mwanaume anakuachia na mtoto wake basi ni kutokana na kumuonyesha kuwa wewe haubabaishwi na unaweza life bila msaada wake.
2. Wanawake wanaojiunga vikoba wengi huwa ni aina ya wanawake ambao wanauchumi mbovu na wanajitegemea wao wenyewe kusurvive kifedha ingawa wapo kimahusiano na wanaume na wanaishi nyumba. So hii inamaanisha mwanaume ulienae hana msaada kwako baada ya kuanza kuishi nae.
3. Inaonyesha umekuwa aidha ukiwasiliana na baba mtoto kwa siri au wanaume wengine maana tabia za wanawake wa kaliba yako huwa ni kuhaha wakitafuta pesa za marejesho n kimbilio mara nyingi ni mwanaume wa kuzaa nae ambaye utatunga uongo wa aina mbali mbali ili kupata pesa za kukuwezesha marejesho. Hii mwanaume uliye nae sasa ameshtukia na imepelekea kukudharau na kukuona hauna shukurani na haufadhiliki sababu ya kutojali hisia zake.
4. Mara nyingi mwanaume anaekwenda nje kutafuta wanawake na kuja nao ndani au kukuonyesha wazi wazi ana wanawake anao lala nao nje yako kwa makusudi ya kutaka ujue na uumie huwa ni Beta males au wanaume dhaifu ambao huwa tayari kupokea mizigo ya wanaume wenzao waliyoikimbia ili kuprove wao ni wanaume kumbe ndani ni dhaifu na ni kasha tu la mwanaume.
Sasa wewe umejua hilo baada ya kuingia nae ndani na kuishi nae na umemdharau hii imemuumiza na ili kukurudishia anakuonyesha kuwa na yeye nje wapo wanawake wanamtaka na anataka ujue kuwa analala nao ili uumie na ujiskie vibaya sababu wewe umemfedhesha hakubali kuonekana mdhaifu sababu ni mdhaifu.
5. Unaonekana una mahusiano nje ya haya ya sasa aidha kwa namna ya kujitafutia kipato au faraja. Jamaa amejua na ndio anakufanyia visa sababu anakuona wewe na mtoto kuwa ni mzigo na amedhalilishwa kama mwanaume.