Je, ni sahihi kuoa binti kutoka family friend?

Je, ni sahihi kuoa binti kutoka family friend?

Youbettersleep

JF-Expert Member
Joined
May 3, 2019
Posts
944
Reaction score
1,628
NAULIZA JE NI SAHIHI MIMI KUOA BINTI KUTOKA KWA FAMILIA YENYE UKARIBU NASI?

Wajomba na mamshangazi habari ya Asubuhi, naomba niende moja kwa moja...!!

Mimi nimezaliwa na Kuishi Dar ila nina asili ya Mwanza, familia yangu imekuwa na uhusiano mkubwa na familia flani tangu mwaka 2010 yaan zinafahamiana na kuheshimiana sana sababu pia ni Wasukuma (si mnajua wasukuma wakikutana hugeuza urafiki hadi undugu)

Mama wa ile familia ninamuita Aunt au Mama na vijana wake ni marafiki zangu tangu 2010 tumeishi

KISANGA.....!!
2020 Nilianza mahusiano na binti 1 wa familia ile na tunapendana sana na ahadi mingi za kuoana na tayari tumeshafanya uchafu woteee na baadhi ya wanafamilia wake wanajua mahusiano yetu ila bado yule mama yake tu hajui.


MSAADA.

NAULIZA JE NI SAHIHI MIMI KUOA PALE AU NITAKUWA NIMESHUSHA URAFIKI WA FAMILIA ZETU?
 
Wazazi wenu waliwaweka karibu wakijua kabisa mtatamaniana na mwisho kupendana kabisa.Usikae ukidhani watashtuka au kushangaa.Watakushangaa wewe utakayeshangaa.Ni mtego laini wa muda mrefu.
Acha niishi na hii comment.....Dec nilipanga kumaliza mchezo 2026 nimuweke ndani tu ila uoga ukanijaa
 
Back
Top Bottom