Sasa hivi wizara zote ziko chini ya makaritibu wakuu.Magari yote yamesharudishwa parking pamoja na nyumba za serikali.EL nadhani atabaki kwenye historia kama PM aliejiuzuru kwa scandal;
John Malecela atabaki kama PM alietimliwa na mzee Ruksa 1994 na Msuya kumalizia ungwe ya pili ya mzee Ruksa 1994-95.
Bila shaka kama atakosa uteuzi toka kwa muajiri wake ambae ni Rais wa JMT, bila shaka ataingia kwenye record ya kutumika miaka mitano kama Joseph Sinde Warioba 1985-90.
Ikitokea akateuliwa tena na kuthibitishwa na Bunge, ataingia kwenye record kama ya Sumaye kuwa PM back to back au Mizengo Pinda aliemalizia awamu ya kwanza ya JK na kuaminiwa kwa awamu ya pili.
Kila la kheri wale wote wenye bahati ya kuchagiliwa kuwa wabunge.maana wana equal chance ya kuteuliwa. PM Majaliwa ana chance kubwa kwa uchapa kazi wake kwenye awamu ya kwanza ya Rais wa JMT.
Siasa ni ajira ngumu aisee.sababu hakuna waziri aliyemaliza muda wake mwenye uhakika wa kurudi ofisini tena kwa 100%.Ijapo wengine wana asilimia kubwa mfano Kabudi.